Kidudu Mtu
Member
- Nov 7, 2009
- 64
- 0
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji mstaafu, Lewis Makame (pichani), amesema hivi sasa inajadili majukumu ya kuandaa uchaguzi mkuu wa mwakani, uweze kufanyika kwa uwazi, uhuru na haki kwenye mazingira ya usalama na utulivu zaidi.
Jaji Makame alisema miongoni mwa wadau katika zoezi la uchaguzi ni vyombo vya ulinzi na usalama ambavyo vitahakikisha utulivu unakuwepo.
Pia, alitaka polisi kutokuwa la itikadi kwenye utendaji wake na kutokuwa mashabiki wa kisiasa.
"Kama mnavyojua kwa mujibu wa ibara ya 147(3) na (4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 ni marufuku kwa mwanajeshi yeyote kujiunga na chama cha siasa, alisisitiza
Alisema kuendesha uchaguzi wa kidemokrasia ni lazima pawepo sheria, kanuni na taratibu zinazoelezwa na kuwekwa wazi ili wadau wote wanaoshiriki waweze kuzifahamu na kushiriki kikamilifu.
CHANZO: NIPASHE
............................................................................
Huwa nashindwa kuelewa hawa wasomi na wazoefu inakuwaje wasiwe na uwezo wa kutafakari na kusaidia katika masuala muhimu kwa mustakabali wa taifa, au ili mradi wao wanapata mlo wao wa kila siku inatosha! Inawezekana kwa kuwa wanapewa nyadhifa baada ya "kustaafu", kwao vyeo hivi vinakuwa ni fadhila na si dhamana.
Inawezekana vipi kuwepo na uchaguzi huru wakati:
Jaji Makame alisema miongoni mwa wadau katika zoezi la uchaguzi ni vyombo vya ulinzi na usalama ambavyo vitahakikisha utulivu unakuwepo.
Pia, alitaka polisi kutokuwa la itikadi kwenye utendaji wake na kutokuwa mashabiki wa kisiasa.
"Kama mnavyojua kwa mujibu wa ibara ya 147(3) na (4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 ni marufuku kwa mwanajeshi yeyote kujiunga na chama cha siasa, alisisitiza
Alisema kuendesha uchaguzi wa kidemokrasia ni lazima pawepo sheria, kanuni na taratibu zinazoelezwa na kuwekwa wazi ili wadau wote wanaoshiriki waweze kuzifahamu na kushiriki kikamilifu.
CHANZO: NIPASHE
............................................................................
Huwa nashindwa kuelewa hawa wasomi na wazoefu inakuwaje wasiwe na uwezo wa kutafakari na kusaidia katika masuala muhimu kwa mustakabali wa taifa, au ili mradi wao wanapata mlo wao wa kila siku inatosha! Inawezekana kwa kuwa wanapewa nyadhifa baada ya "kustaafu", kwao vyeo hivi vinakuwa ni fadhila na si dhamana.
Inawezekana vipi kuwepo na uchaguzi huru wakati:
- Hakuna tume huru ya uchaguzi
- Hakuna mazingira sawa ya ushindani kati ya wagombea na vyama
- Katiba inaipa mamlaka ya juu zaidi tume ya uchaguzi kuweza kuamua nani awe Rais
- .....
- ....nk...nk