Jaden Smith aendelea kusimangwa kwa kuvaa nguo za kike

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
BAADA ya kushambuliwa sana kwenye mitandao ya kijamii kutokana na aina ya mavazi yake, msanii wa muziki na filamu, Jaden Smith, amesema ataendelea kuvaa nguo yoyote atakayoona inampendeza.

Msanii huyo anashambuliwa kutokana na kuvaa nguo za kike, lakini aliwajibu wanaomkashifu kwa nguo hizo kwa madai kwamba anaendelea kuvaa nguo hizo kutokana na mwili wake ulivyo.

“Akili yangu inanituma kuvaa nguo zitakazonipendeza mwilini na kunikaa, hivyo siwezi kuwasikiliza watu wanachotaka juu ya mavazi yangu.

“Hakuna nguo zilizoandikwa kuwa ni za kiume ama za kike, hivyo unaweza kuvaa kama itakuwa inakupendeza, haya ni maisha yangu hakuna wa kuniingilia,” aliandikwa Jaden kwenye akaunti yake ya twitter.


Chanzo: Mtanzania
 
Hivi vitoto vya wanamuziki na wasanii maarufu huwa vimevurugwa na umaarufu wa wazazi wao toka vikiwa vidogo. Si ajabu kakakuambia kuwa ni kashoga tayari.
 
1458134079470.jpg
1458134103312.jpg
1458134117486.jpg
 
Back
Top Bottom