Nshonzi
JF-Expert Member
- Jul 19, 2016
- 3,046
- 1,867
Wacheni kumpa mtu umaarufu wa bure,hivi walper ni nani hapa tanzania bwana?Mwigizaji wa filamu nchini Tanzania Jackline Wolper aliyekuwa aki muunga mkono Edward Lowassa katika uchaguzi Mkuu 2015, alitangaza kujiunga na CCM rasmi jana.
Wolper alikaribishwa na mwenyekiti aliyemaliza muda wake Dkt Jakaya Kikwete baada ya kutangaza kujiunga na CCM.
Kitendo hicho kilifanyika katika Mkutano Mkuu Maalum wa CCM uliofanyika jana Julai 23, mkoani Dodoma.
Je Wolper kujiunga na CCM ni kwa mapenzi ya dhati au ni kafata ulaji?
Kwanini akajitangaze kwenye mkutano mkuu wa CCM??
Sipati mantiki ya yeye kujitangaza kwa mkutano ambao lengo kuu halikua lile..
Nawasilisha mada..