J.K Usilisuke Baraza La Mawaziri Nashauri Unyoe ili Ziote upya Kwa ufanisi

simon james

JF-Expert Member
Apr 1, 2012
283
140
Kwa udhaifu huu wa J.k ni dhahiri kuwa CHADEMA imeshaikamata dola kabla ya 2015. Ni dhahiri na mwenye tafakuri hana haja ya kuuliza zaidi kwani waswahili husema mwenye macho haambiwi Tazama. Sina haja ya kurejea matukio mengi yaliyopita ila mambo tunayo ya sadiki hivi sasa yanaonyesha kuwa CHADEMA ndiyo inayo ongoza nchi. Ikumbukwe CC Ya CHADEMA ilipo tangaza kufanya maandamano nchi nzima mapema 2010 baada ya uchaguzi mkuu kushinikiza uandikwaji wa Katiba mpya ndipo J.K akaridhia na kutangaza kuanza mchakato wa katiba mpya. Hata hivyo baada ya mswada wa mabadiliko ya katiba kupitishwa na wabunge wa CCM Nakusainiwa na J.K licha ya mapungufu yaliyofanya CDM Kususia na hatimaye kutangaza kuwa CHADEMA watazunguka nchi nzima ndipo J.K Aliridhia mswada urejee tena Bungeni kwa mara ya kwanza. Hivijuzi baada ya CHADEMA kutangaza kuitisha kamati kuu ya dharura kutoa tamko kali kuhusu ufisadi ulioelezwa na CAG J.K Amekuwa mwoga na kuitisha Cc ya Chama Chake ijumaa kabla ya CC ya CHADEMA Jumamosi tar 28/04/2012 kwakuogopa kimbunga kinachokuja amekubali kusuka baraza la mawaziri.Hongera sana CHADEMA kwa kuuonyesha Uma wawa Tz kuwa sera na hoja zenu zinatekelezeka. Zungukeni sasa vijijini kuweka matawi kwani mnakubalika. Na mshauri J.K asilisuke baraza la mawaziri bali alinyoe kabisa ili nywele ziote upya
 
Back
Top Bottom