Ivi ntaweza kweli kuishi maisha ya chuo kwa kiasi hki cha pesa?

We kwann una wasiwasi hazitakuyosha? Whats ur budget and expected expenses mpaka uone hazitoshi?
Plus maisha ni kujiongeza..ukiona hazitoshi piga mishe mjini hapa usije na jembe akili yako tu. Ila mishe halali maana bw. Polisi atakushughulikia.
Usimwogopeshe mtoto wa watu Mentor. Acha afike afanye matanuzi na akimaliza hela atatulia na kupiga kitabu
 
Last edited by a moderator:
kama unaona haitoshi,pale afrika sana sinza kuna kiwanja kinaitwa ambience,nite fln nenda kajitege unaweza kupata za kuongezea za kukukidhi kimaisha,mbona wanazuoni wengi tu tunawaona pale na tunawabeba ili kuwafadhili,njoo tu
 
Mkuu kwangu inatosha mbona mimi natumia laki moja tu ila rb mpango mzima na suala la tea kushoto but budget inategemeana na mtu
 
mbona unasurvive fresh tu. RB 1000x2=2000,usafiri shato 600,maji ya kudownload,chai 500,vocha 500 ;total 3600/- STAREHE 1400/- jumla 5000/-
Bajeti iko poa. Hebu tujuze hapo kwenye bold: Ni maji gani hayo mkuu.
 
mbona unasurvive fresh tu. RB 1000x2=2000,usafiri shato 600,maji ya kudownload,chai 500,vocha 500 ;total 3600/- STAREHE 1400/- jumla 5000/-

Ndugu yangu hela ya chumba iko wapi hapa??na kutolea copy madesa??dogo ataishia kula mikate na soda moja siku nzima huyu..we ngoja atumiwe hiyo pocket change aone mjini patakuwaje hapa..plus dingi hana habari na ada hapo..atakuwa anafanya kazi ya kufagia pale kwa mkandara..atajuuuuta!
 
Wakuu,ebu nishaurini kidogo hapa,mimi kikweli ckuapply mkopo kule heslb kutokana na sababu ninazozijua mwenyewe,sasa ishu iko hvi,mshua kanambia atakua ananitumia tsh 150000 kila mwisho wa mwezi kama pesa ya kula na matumizi mengne madogo madogo hapo chuo,naomba mnipe ushauri jaman,ntaweza kweli kusurvive kila mwezi kwa pesa hyo na ukizngatia maisha yenyewe ni ya udsm,maana nackia maisha ya hapo dar sio mchezo?

Je, kabla hujajiunga na chuo ulikuwa unapata pesa kama hizo? Kama jibu ni kwamba ulikuwa hupati na sasa unaanza maisha ya chuo unabahati sana kupata kwani nimeona wengine hizo umekuwa mtaji wa ujasirimali halafu we unaongelea kutotosha wakati huko sekondari hukuwa na benefit kama hiyo. Maisha ya chuo si starehe, ni kitabu na unachoangalia tumbo kupata shibe, hizi za kununulia cooler ya vinywaji na mengineyo unayoyajua mwenyewe nenda kuwinda sungura kule mbuga ya mikumi.
 
Ndugu yangu hela ya chumba iko wapi hapa??na kutolea copy madesa??dogo ataishia kula mikate na soda moja siku nzima huyu..we ngoja atumiwe hiyo pocket change aone mjini patakuwaje hapa..plus dingi hana habari na ada hapo..atakuwa anafanya kazi ya kufagia pale kwa mkandara..atajuuuuta!

Mimi nilizoea kufaidi mihogo ambayo ni gharama nafuu na shibe inashindisha siku, sasa hiyo mikate na sota inayokupa nguvu ya saa moja si ndio maana analalamikia pesa kutomtosha? Priority ukiona ni elimu hizo zinatosha na kubaki.
 
Mkuu kwangu inatosha mbona mimi natumia laki moja tu ila rb mpango mzima na suala la tea kushoto but budget inategemeana na mtu

Watu wana familia wanaishia kipato cha laki moja halafu we ikushinde, nini tatizo? Kama hazitoshi waambie wazazi wako wakuongezee.

Majuu kama unapata mkopo kama huo ujue utapewa kwa utaratibu ufuatao.
  • Tuition hupelekwa chuoni moja kwa moja
  • Posho kama waishi chuoni basi ujue imehesabiwa kabisa lunch ya chuoni kwa kiwango cha kawaida tu kishushio juice, chai au maji.
  • Nyumba ya kupanga basi pesa hulipwa moja kwa moja kwa real estate.

Kwa malalamiko yako ni uswahili wa kwetu, lakini angekuwa mzungu angechangamkia kwani kwao hiyo ni ziada isiyo ya kawaida.
 
We kwann una wasiwasi hazitakuyosha? Whats ur budget and expected expenses mpaka uone hazitoshi?
Plus maisha ni kujiongeza..ukiona hazitoshi piga mishe mjini hapa usije na jembe akili yako tu. Ila mishe halali maana bw. Polisi atakushughulikia.

kweli mjini akili yako usije na jembe
 
Last edited by a moderator:
pesa nyingi sana iyo kama huna anasa.........kuna supu plain 300 na chapati zako 3 kwa almost 7000........ukinywa supu saa tano asubuhi na izo chapati inatosha kabisa kuitafuta jioni utakapo kula 1000 wali nyama........+ 500 vocha na 500 maji kwa siku utakuwa umekata 3000 tu.....
 
kwenye 600/= weka shato pori na sahii ni safe wale jamaa ubungo siwameondolewa?
 
Kwa mtazamo wangu ukipiga moyo konde na kujua ulichokifuata pale na kuweka kando utakavyovikuta maisha yatasonga na kumaliza kwakutegemea hicho hicho kiasi
 
Sidhani kama huu ushauri niwakuzingatiwa maana upatapo nafasi kama hiyo na kuichezea utakuja kuijutia mapema mno

Kuna waliotoboa siri moja ambayo tunapoangalia bajeti hii hatuangalii huduma ya ku-downloard ambayo ina maana nyingi, na hawa ndio wanaoinufaisha sana mitandao na mikonga mingi ya mitandao, kwani bajeti kubwa zaidi ni huko kuliko masuala muhimu wanayohitaji yaliyowapeleka chuoni. Fanya utafiti wapambe wakubwa wa facebook ni hawa vijana wa sekondari na vyuo, je bajet za kopo zilifikiriwa na huduma za mitandao?

Nyuo kadhaa vinalalamika kuwa wana lab lakini wanafunzi wengi hawapendi kuzitumia kwa sababu ya restriction ya downloard za mambo yao.
 
Wakuu,ebu nishaurini kidogo hapa,mimi kikweli ckuapply mkopo kule heslb kutokana na sababu ninazozijua mwenyewe,sasa ishu iko hvi,mshua kanambia atakua ananitumia tsh 150000 kila mwisho wa mwezi kama pesa ya kula na matumizi mengne madogo madogo hapo chuo,naomba mnipe ushauri jaman,ntaweza kweli kusurvive kila mwezi kwa pesa hyo na ukizngatia maisha yenyewe ni ya udsm,maana nackia maisha ya hapo dar sio mchezo?

Nikujibu kama ifuatavyo:
Wakati wengi wa kipato cha chini ambao wengi wao huanzia na laki moja na wanaweza kuyamudu maisha, wakati we huna anayekutegemea ila ni kupiga kitabu tu, kama utafikiria kwamba mchumia juani hulia kivulini unaweza kukubaliana nami kuwa kwa mahitaji muhimu na ya lazima inatosha na kubaki ziada ya kurudufia material.

Mimi wakati mwingine nilipokuwa chuo tulikuwa tuna share baadhi ya mambo, mimi nikirudufu leo, tunashea na rafiki yangu ambaye yeye atarudufu kesho. Kuna ubaya gani wakati ukifiki nikishahitimu nitafanya nitakavyo?

Yakhe, achana na ziada ya viyoyozi, fridge, na vinginevyo vya kuwastarehesha marafiki wakike kwani si wakati wake, asiyekubali urafiki kwa vile tu huna virutubisho hivyo ni mtafutaji.
 
kama unaona haitoshi,pale afrika sana sinza kuna kiwanja kinaitwa ambience,nite fln nenda kajitege unaweza kupata za kuongezea za kukukidhi kimaisha,mbona wanazuoni wengi tu tunawaona pale na tunawabeba ili kuwafadhili,njoo tu
Samahani,ivi angekuwa dada yako ungemshauri ivi?huyu yuko serious
 
Back
Top Bottom