ITV wanarusha tangazo moja matata sana,kwakweli limeni-impress sana.Ni tangazo ambalo ni extract kutoka kwenye hotuba mbalimbali za baba wa taifa mwalimu Julius Nyerere.Katika extract hiyo, mwalimu anamshanga jamaa aliyefurahi kupata kipande cha chupa kwa kudanganywa kwamba ndiyo alimasi,na tapeli akachukua alimasi halisi.Katika hali isiyokuwa ya kawaida, yule jamaa aliyechukua kipande cha chupa, ambae mwalimu alimwita zuzu,aliendelea kushangilia kana kwamba ndiye kapata alimasi.Nalipenda tangazo hili kwa vile linaeleza hali halisi tunayopitia hivi sasa. ITV naomba mlitangaze tangazo hili mara kwa mara, labda litasaidia kwa kiasi fulani.