WOWOWO
JF-Expert Member
- Aug 3, 2011
- 590
- 430
Wakuu Salama?
Kuna suala leo limenitatiza sana ingawa limekuwa likijotekeza mara kwa mara katika mazingira fulani fulani
Habari kubwa kwenye magazeti almost yote ya leo ni Juu ya Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt. Slaa kugoma kuhojiwa na Jeshi la Polisi kwa kile alichoeleza kuwa hana imani na Jeshi hilo kwani limekalia taarifa nyingi za uchunguzi ikiwemo ile ya kutegewa kinasa sauti chumbani kwake kule Dodoma.
Aidha, habari hiyo ambayo inauza magazeti yote ya leo imeambatana na maamuzi mbalimbali ya kamati kuu ya CHADEMA iliyoketi kwa siku mbili.
Nimejaribu kufuatilia vipindi vya udondozi wa magazet kwenye TV na Radio kuanzia Star TV, RFA, Magic FM na Channel 10 kote wamesoma habari hiyo kubwa nchini. Maajabu ITV na Radio One kwenye vipindi vyao vya udondozi wa magazeti hawajasoma kabisa habari hiyo na mara zote watangazaji wamekuwa wakiudanganya umma kuwa, habari iliyopamba magazeti yote ni ile ya Rais wa Jumuiya ya madaktari kufikishwa mahakamani.
Kinachokera zaidi, Mwandishi anasoma; nanukuu "Katika Gazeti la Tanzania Daima habari kubwa iliyopamba ukurasa wa mbele ni ile isemayo MADIWANI 22 WA CCM MISUNGWI WAJIORODHESHA KUHAMIA CHADEMA" wakati habari kubwa ni ya Dkt. Slaa.
Aidha, taarifa za habari za jana kwenye TV stations zote hakukuwa na habari hiyo ya CDM isipokuwa Channel ten pekee. Niliikodolea macho ITV bila mafanikio.
My Take
-Hivi ITV/Radio One kuna nini hadi kwa makusudi wanaudanganya umma juu ya habari kubwa kwenye magazeti ya leo?
-Kuna tatizo kati ya ITV/Radio One na CHADEMA?
-Inakuwaje mhariri/mwandishi anaruhusu upotoshaji na upindishaji wa ukweli makusudi?
Nawasilisha...
Kuna suala leo limenitatiza sana ingawa limekuwa likijotekeza mara kwa mara katika mazingira fulani fulani
Habari kubwa kwenye magazeti almost yote ya leo ni Juu ya Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt. Slaa kugoma kuhojiwa na Jeshi la Polisi kwa kile alichoeleza kuwa hana imani na Jeshi hilo kwani limekalia taarifa nyingi za uchunguzi ikiwemo ile ya kutegewa kinasa sauti chumbani kwake kule Dodoma.
Aidha, habari hiyo ambayo inauza magazeti yote ya leo imeambatana na maamuzi mbalimbali ya kamati kuu ya CHADEMA iliyoketi kwa siku mbili.
Nimejaribu kufuatilia vipindi vya udondozi wa magazet kwenye TV na Radio kuanzia Star TV, RFA, Magic FM na Channel 10 kote wamesoma habari hiyo kubwa nchini. Maajabu ITV na Radio One kwenye vipindi vyao vya udondozi wa magazeti hawajasoma kabisa habari hiyo na mara zote watangazaji wamekuwa wakiudanganya umma kuwa, habari iliyopamba magazeti yote ni ile ya Rais wa Jumuiya ya madaktari kufikishwa mahakamani.
Kinachokera zaidi, Mwandishi anasoma; nanukuu "Katika Gazeti la Tanzania Daima habari kubwa iliyopamba ukurasa wa mbele ni ile isemayo MADIWANI 22 WA CCM MISUNGWI WAJIORODHESHA KUHAMIA CHADEMA" wakati habari kubwa ni ya Dkt. Slaa.
Aidha, taarifa za habari za jana kwenye TV stations zote hakukuwa na habari hiyo ya CDM isipokuwa Channel ten pekee. Niliikodolea macho ITV bila mafanikio.
My Take
-Hivi ITV/Radio One kuna nini hadi kwa makusudi wanaudanganya umma juu ya habari kubwa kwenye magazeti ya leo?
-Kuna tatizo kati ya ITV/Radio One na CHADEMA?
-Inakuwaje mhariri/mwandishi anaruhusu upotoshaji na upindishaji wa ukweli makusudi?
Nawasilisha...