ITV na "Morbid Curiosity", Very Unprofessional!

Napenda kumshukuru aliyeandika mada hii na kuwezesha kuchambuliwa kwa ufasaha na ufanisi mkubwa kutoka kwa wachangiaji. Tatizo langu kubwa ni lugha iliyotumika, hivi ni kweli wote waliotumia maneno ya Kiingereza walikosa tafsiri yake kwa Kiswahili? Au ndiyo ufisadi mwingine ndani ya Taifa katika matumizi ya lugha? Angalia sana unapokuwa mkosoaji kwani huenda nawe unahitaji kukosolewa ila hujijui. Tuache mawazo potofu ya kwamba ili ujulikane kuwa umesoma na kuelimika lazima utumie maneno ya Kiingereza katika maongezi yako. Wafaransa, Wajerumani, Wajapani, Warusi, Wachina n.k nao watasemaje? Tuelimike na tubadilike.
Mkuu Sly, kwanza samahani kwa kuchanganya lugha, kiukweli kuna baadhi ya maneno ukitumia lugha halisi ya maneno yenyewe ambayo ni professional vocabulary yake yanaeleweka kwa urahisi zaidi kwa lugha ya kutoholewa kuliko tafsiri rasmi ya Kiswahili. Kuna kutumia Kiswahili Sanifu na Kiswahili Fasaha. Kiswahili Sanifu ni ile lugha rasmi kwa mujibu wa kamusi, na Kiswahili Fasaha ni ile lugha ya kueleweka sio lazima iwe sanifu. Kuna maneno mengi tuu ni rahisi kuyatumia kwenye Kiswahili Fasaha kuliko Kiswahili Sanifu!
Mfano
KIswahili Fasaha Kiswahili Sanifu
1. Friji - Jokofu
2. Mail - Barua Pepe
3. Dekoda - Kingamuzi
4. Dokta - Tabibu
5. John - Yohana
6. James - Yakobo
7. DC - Mkuu wa Wilaya
8. Vocha - Kadi Ongezeko la salio
9. TV - Luninga
10. SMS - Ujumbe Mfupi wa ...

Hiyo ni mifano michache ya maneno ya Kiingereza ambayo ni rahisi zaidi kutumika kwenye lugha fasaha lakini sio sanifu.

Ila pia kuna maneno ya kitaaluma ambayo bado hayana Kiswahili rasmi mfano " Morbid Curiosity" mengine mengi tuu yapo na yameshatoholewa hivyo hivyo kugeuka Kiswahili sanifu.
1. Secretariat
2. Oganaizesheni
3. Operesheni
4. Faulo
5. Shuti
6. Blog, FB na tweeter
7. Goli
8. Ligi
9. Jaji
10. Muziki

Na mwisho kuna maneno makali ukiyatumia kwa Kiingereza yanapungiua ukali kuliko ukiyatumia kwa Kiswahili mfano neno "very unprofessional', ukilitimia kwa kiswahili lina sound kama unamtukana!.
1. Shit ni M..vi
2. Fool ni Mpu...vu
3. Mad ni Kichaa
4. Insane ni Mwenda wazimu
5. Thick ni punguani
6. Homo ni Hani....
7. Gay ni Wase....
8. Sex ni Kut....
7. Sleep together ni Kula..na
8. Gold Digger ni wachunaji
9. Back ni Nyu...
10. Game ni mambo fulani

Kwa vile jf ni social media kama fb na tweeter hivyo matumizi yoyote ya kuchanganya lugha kwa madhumuni ya kufupisha, kueleweka kwa urahisi na kupunguza makali ni ruksa!.
 
Nakubaliana na wewe Pasco
Kitendo walichofanya ITV ni kinyume na miiko ya taaluma yao
OTIS
 
Last edited by a moderator:
Nakubaliana na wewe Pasco
Kitendo walichofanya ITV ni kinyume na miiko ya taaluma yao OTIS
Mkuu OTIS, ni kinyume cha taalum only if walio zionyesha hizo picha wanajua miiko ya hiyo taaluma, kwa kawaida ITV huwa inafuata taaluma kwa wale wakongwe ambao ni wana taaluma kweli kweli ila inaelekea kuna new recruitment ya hivi karibuni kutoka kitaa, sasa ili kuonyesha wao sio waoga, unapiga mpaka close up shot ya sura na mdomo wa mtu aliyekufa kwa kunyongwa ili kuwaonyesha watazamaji how does the face look like!. Yeye mpigaji picha zile na mtumiaji wanejiridhisha kuwa kwa vile rule number 1 ya mwana habari ni kusema ukweli au kuonyesha ukweli, wao wametimiza jukumu lao kwa sababu ule ndio ukweli wenyewe!, concern yangu ni kwa ITV ina timu kubwa tena wenye weledi wa hali ya juu kuliona hili, walikuwa wapi?.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu OTIS, ni kinyume cha taalum only if walio zionyesha hizo picha wanajua miiko ya hiyo taaluma, kwa kawaida ITV huwa inafuata taaluma kwa wale wakongwe ambao ni wana taaluma kweli kweli ila inaelekea kuna new recruitment ya hivi karibuni kutoka kitaa, sasa ili kuonyesha wao sio waoga, unapiga mpaka close up shot ya sura na mdomo wa mtu aliyekufa kwa kunyongwa ili kuwaonyesha watazamaji how does the face look like!. Yeye mpigaji picha zile na mtumiaji wanejiridhisha kuwa kwa vile rule number 1 ya mwana habari ni kusema ukweli au kuonyesha ukweli, wao wametimiza jukumu lao kwa sababu ule ndio ukweli wenyewe!, concern yangu ni kwa ITV ina timu kubwa tena wenye weledi wa hali ya juu kuliona hili, walikuwa wapi?.
Pasco,,
asante sana kwa kuanzisha hiii thread. Hili tatizo la kuonyesha picha/video kama maua ya waridi linazidi kukua siku hadi siku. Na hasa kwenye blogs na forums ndio usiseme tena. Kuna mashindano ya ku-upload graphic contents. Hivi hamna sheria zinazowalinda waathirika. kwa mfano, case kama hii ya ITV kuonyesha huyo marehemu aliyejinyonga? Mimi sio mtaalam wa sheria naomba yeyote mwenye kujua atueleweshe.
 
Nashukuru kwa uzi wako, natumai bwana mayala siku chache zijazo utakuja na uzi mfano wa huu, kucriticize TBC na uongo wao wa kichama
Wewe si iendelee kusikiliza ukweli na uhakika kutoka TBC au ianzishe ya kwako kwakuwa unajiona ni nguli kuliko nguli wa BBC.
Haikosoi TBC hata mara moja anaikosoa BBC.
Heeeee! eti BBC!!! Yaani watu hawaoni fyongo, uzushi na upotoshaji wa TBC ya Ayoub wanaona ya London
''Ondoa kibanzi kwenye jicho lako ndipo uondoe boriti .....''
JokaKuu
Uwezo wako ni wakukosoa TBC tu... Huko pengine sio level yako... Kwanza mabeberu ni wakina nani?
P
 
Back
Top Bottom