Chief Isike
JF-Expert Member
- Jan 17, 2010
- 445
- 462
Wakuu tangu jana nimeona ITV wameanzisha kipindi kizuri tu, ambacho nafikiri watakuwa wanaonesha vipande vya hotuba tamu za Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Lakini kuna kosa kubwa la kimantiki na kiufundi katika utangulizi unaosomwa na Deo Rweyunga kabla kipande hichi cha hotuba maarufu ya "Nyufa" haijaenda hewani.
Rweyunga anasema Mwalimu alisema nini juu ya UTAWALA BORA!!!!!! Hakuna kitu kama hicho katika kinywa cha Mwalimu Nyerere, nimemsikiliza na kumsoma sana mara kadhaa, hakuna mahali Baba wa Taifa alikuwa anatumia neno UTAWALA BORA. Mara zote alisisitiza UONGOZI BORA. Kuna maana kubwa sana katika utofauti wa maneno hayo. UTAWALA vs UONGOZI. Halafu the first one ni moja ya maneno yanayotokana na DONORS IMPOSITION, ambayo kwa kweli yameshatuathiri sana nasi tunayaimba kwa nguvu zetu zote. Kama tunavyoimba sawa na walivyokuwa wakiimba MAKABURU; RULE OF LAW, bila kuhoji ARE THOSE LAWS FAIR...ABLE TO MAKE JUSTICE PREVAIL AND GIVES HOPES TO WANANCHI, AS THE TWO (JUSTICE and HOPES) are the cornerstone for peace and stability in where.
Naweka nukuu ya Mwalimu Nyerere juu ya UONGOZI BORA na si utawala bora. Nukuu inatoka Azimio la Arusha juu ya mambo muhimu kwa sisi kuendelea, WATU, ARDHI, SIASA SAFI NA UONGOZI BORA , ingawa pia neno hilo amelirudia mara nyingi sana katika maneno yake. Ni vyema Watanzania tuimbe na kusisitiza uongozi bora si kinyume chake;
"(d) Uongozi Bora:
TANU inatambua umuhimu wa kuwa na Uongozi Bora. Tatizo lililopo
ni ukosefu wa mipango maalum ya kuwafundisha Viongozi na kwa
hiyo Ofisi Kuu ya TANU ni budi itengeneze utaratibu maalum kuhusu
mafundisho ya Viongozi tangu wa Taifa zima hadi Mabalozi ili
waielewe siasa yetu na mipango ya uchumi. Viongozi ni lazima wawe
mfano mzuri kwa wananchi kwa maisha yao na vitendo vyao pia."
Tunaweza kujadili. Si vyema kueneza uongo huo na sumu ya watu kutambua utawala bora bora badala ya uongozi bora.
Rweyunga anasema Mwalimu alisema nini juu ya UTAWALA BORA!!!!!! Hakuna kitu kama hicho katika kinywa cha Mwalimu Nyerere, nimemsikiliza na kumsoma sana mara kadhaa, hakuna mahali Baba wa Taifa alikuwa anatumia neno UTAWALA BORA. Mara zote alisisitiza UONGOZI BORA. Kuna maana kubwa sana katika utofauti wa maneno hayo. UTAWALA vs UONGOZI. Halafu the first one ni moja ya maneno yanayotokana na DONORS IMPOSITION, ambayo kwa kweli yameshatuathiri sana nasi tunayaimba kwa nguvu zetu zote. Kama tunavyoimba sawa na walivyokuwa wakiimba MAKABURU; RULE OF LAW, bila kuhoji ARE THOSE LAWS FAIR...ABLE TO MAKE JUSTICE PREVAIL AND GIVES HOPES TO WANANCHI, AS THE TWO (JUSTICE and HOPES) are the cornerstone for peace and stability in where.
Naweka nukuu ya Mwalimu Nyerere juu ya UONGOZI BORA na si utawala bora. Nukuu inatoka Azimio la Arusha juu ya mambo muhimu kwa sisi kuendelea, WATU, ARDHI, SIASA SAFI NA UONGOZI BORA , ingawa pia neno hilo amelirudia mara nyingi sana katika maneno yake. Ni vyema Watanzania tuimbe na kusisitiza uongozi bora si kinyume chake;
"(d) Uongozi Bora:
TANU inatambua umuhimu wa kuwa na Uongozi Bora. Tatizo lililopo
ni ukosefu wa mipango maalum ya kuwafundisha Viongozi na kwa
hiyo Ofisi Kuu ya TANU ni budi itengeneze utaratibu maalum kuhusu
mafundisho ya Viongozi tangu wa Taifa zima hadi Mabalozi ili
waielewe siasa yetu na mipango ya uchumi. Viongozi ni lazima wawe
mfano mzuri kwa wananchi kwa maisha yao na vitendo vyao pia."
Tunaweza kujadili. Si vyema kueneza uongo huo na sumu ya watu kutambua utawala bora bora badala ya uongozi bora.