Its My Wedding Annivesary

Hongera sana mkuu, Mola awawezeshe mzeeke wote kwa amani, upendo na uvumilivu!..

Asante Belinda,

Tuombe Mungu atujalie heri na uzima.
Babu na bibi are still together basi wanapendeza wenyewe wanavyofuatana kama kumbikumbi
 
Kiongozi pongezi sana kwa kutimiza miaka 11 ya ndoa na my wife wako.

Wakati mwingine tukikutana na watu mlio na uzoefu wa kiwango hicho inakuwa ni chachu kwetu.

Mimi ndo nakamata miaka mitatu sasa, naomba Mungu aniwezeshe na kunijaalia ili siku moja nifikie hapo ulipo, nadhani siku hiyo nitakukumbuka Realman.

Kwa kweli niwatakie maisha marefu zaidi ya yenye furaha zaidi.

Naomba leo umwagie maji mengi zaidi kwa niaba ya JF!!

Mwita anafurahi kwa uko thabiti na mwenye malengo.

MMU ni jukwaa la aina yake tunajifunza stadi za maisha.


Leo ntamwagia maji kisha namwambia "Kwa Hisani ya Jamii Forums".
 
Nafikiri wengi wakifikia miaka hiyo wanaleta mazoea kwemye ndoa wanaanza kupunguza care flaniflani hivi na mwanamke anakuwa bize sana na malezi ya watoto kuliko mumewe majukumu pia nayo yanaongezeka pia, sasa hapo usipoangalia vizuri mwanaume anaanza kuwa na company ya marafiki mbalimbali ambao wana tabia tofautitofauti hapo ndipo inapoanza kasheshe.

Jamani tuloko kwenye mahusiano tupate elimu hii, Gaga unachosema nimekishudia kwa watu ninaowafahamu kila mmoja anamlaum mwenzake.

Kwenye hilo la company nadhani ndo mzizi wenyewe maana birds of same feathers....

Halafu jamii imejikita zaidi ktk kumfunza binti kuwa mke bora wakati wanaume twajifunza mambo ya ndoa ndani ya ndoa.

Asante kwa kushea ukweli huu!!
 
Hongera zenu RMn na wifi..mimi ndio naingia tenth month, ndoa si rahisi bwana yataka moyo! Ulikofika tuombe mungu nasi tufike. Kiss wifi kwa hisani ya warembo wote JF.
 
Hongera zenu RMn na wifi..mimi ndio naingia tenth month, ndoa si rahisi bwana yataka moyo! Ulikofika tuombe mungu nasi tufike. Kiss wifi kwa hisani ya warembo wote JF.

Shishi and all ladies in here are just wonderful!!!

10months hupelekea mwaka, kisha miaka hupelekea muongo 1. Wala usihofu maana kwa msaada wa Mungu mtafikia destiny zenu

Ila kwa hisani yenu leo wifi amepata kiss za ziada!
 
....hongera sana Realman na mkeo miaka 11 si haba kwenye ndoa. Kama usemavyo ndoa tamu bana mkielewana.....nikija kufikia hiyo miaka 11 ya ndoa my little boy atakuwa big boy. Uwiii!! Naona mbali kweli kweli maana ndio kwanza nina 1 year na mwezi hivi.
 
Sina la nyongeza ila nawatakia maisha mema na kila jema liwe nawe na familia nzima :first::first:
 
....hongera sana Realman na mkeo miaka 11 si haba kwenye ndoa. Kama usemavyo ndoa tamu bana mkielewana.....nikija kufikia hiyo miaka 11 ya ndoa my little boy atakuwa big boy. Uwiii!! Naona mbali kweli kweli maana ndio kwanza nina 1 year na mwezi hivi.

Pretty,

Nakushukuru sana.
Wala usitie shaka hiyo 11 yrs si mbali maana ukifika hapo jiandae na changamoto ya huyo boy maana utakuwa na wanaume wawili ndani nyumba.

With prayers naamini Mungu atatuvusha
 
Hongera sana RealMan its good to hear the way you love and treat your wife keep it up and keep it rolling, your wife must be very happy to have a man like you in her life, hapo ni mapendo kwa kwenda mbele.

Yes must be the woman of your life and I believe no other can ever take that place SAFI SANA!!
 
Duh hongera sana mkuu, miaka 11 sio mchezo na unaonyesha unafurahia sana ndoa yako.

Kumbe mwanzo wa maisha ya ndoa ni mgumu?? halafu kwa vile hamjazoea matatizo basi kila katatizo mtu anatafuta msaada wa nje hasa kwa wachungaji na wadhamini wa ndoa, nimejifunza kitu hapo kwenu.

Umenifurahisha sana kuonyesha ukomavu wewe na mkeo.

Nawatakia maisha mema na ya raha. Wanao Mungu akukuzie.
 
Hongera na karibu kwenye chama cha ndoa zinazodumu. Nawaombea muje kuwafurahia wajukuu zenu mkiwa pamoja.
 
Jamani RealMan natumaini sijakosea leo ni aniversari yako.

Hongera sana kama nimepatia!

Tujuze siku ya leo iko vipi kwako na kwa mupenzi wako, siku ya leo umesherekea vipi?
 
Jamani RealMan natumaini sijakosea leo ni aniversari yako.

Hongera sana kama nimepatia!

Tujuze siku ya leo iko vipi kwako na kwa mupenzi wako, siku ya leo umesherekea vipi?

Missy asante,

Kwa masaa ya Tanzania it is tomorrow Feb 5th. We'll be doing our 12th year and its just like yesterday.
Tutapata muda wa pamoja as family then of course a special evening away from home for the two of us.

So far tunamshukuru Mungu
 
Wow RealMa, you must be Mr. Man kwa unavyo mjali wie wako!

Hongera sana kaka, kwa kweli wachache sana wako na mapenzi kama yenu!

Tell us what did you get her this time around. :A S wink: ili wengine wajifunze kutoka kwako.

BIG UP BRO!!
 
Wana JF nimeona nisikae kimya bila kuwajuza wema wa Mungu kwangu.

Najua wengine mtakuwa mmevaa kijani/njano kusherekea "chama chetu cha mapinduziiii chajenga nchi" (itikia ni wimbo) huku wengine (pengine) mmevaa nguo nyeusi kuashiria maombolezo kitaifa.

Leo ninatimiza miaka 11 toka nimekula kiapo cha kuishi (kama mume na mke) na huyu mdada.
Tulikutana 1994 na ndoa ikafungwa miaka 6 baadae
Ndani ya miaka hii 11 Mungu kanijalia kuwa baba wa boy-10 na girl-7 na ukiwaangalia ni dhahiri hakunichakachua labda awe amechakachua na mdogo wangu, hahaahahaaa!!!

Ni miaka ya kuishi na mwanamke ambaye alichukua nafasi ya mama na dada yangu katika maisha.

Miaka 11 imenifundisha nisimwamini kila mtu ninaposigana na mke wangu. Nakumbuka in our early years niliwahi kushare na mchungaji juu ya tofauti zangu na mke wangu only for the pastor to use my story in his preaching the next sunday. Siku hizi nayasovu mwenyewe tu, no outsiders!

Miaka 11 ya kutambua kwamba vitu vidogo sana (thanks, sorry, karibu, darling..) vinajenga uhusiano na vitu vidogo pia huwasha moto.

Jamani wakati mwenzenu nashereheka 11 years kuna experience zipi (nzuri/mbaya/vituko) umewahi pitia kwenye mahusiano yako.

Karibuni tuzungumze!!!!!!!!!!!!!!!!

kwa kweli ongereni mnatutia moyo tunaoenda kuingia
 
Realman na Mama Realman hongereni sana kwa kutimiza miaka 11 katika ndoa. kwa kweli mnatupa moyo sie ambao tunaelekea huko. Mbarikiwe sana na upendo udumu milele
 
Back
Top Bottom