Itakuaje akipatikana mbadala wa TANESCO?

sijui nini

JF-Expert Member
Sep 29, 2010
2,553
1,285
Mara nyingi nimekuwa nikijiuliza juu ya jambo hili kwamba endapo itatokea siku imeibuka kampuni nyingine inataka kusambaza umeme itakuaje juu ya haya yafuatayo:
  1. Unafkiri ni njia gani itatumika bila kuingiliana kabisa na Tanesco katika swala lolote hasa usambazaji wa umeme huo (mfano: kutumia nguzo zao au itumike njia nyingine kama wireless?)
  2. Je, TANESCO watakubali nguzo zao zitumike kushare kwa kusambazia umeme bila masharti magumu endapo njia ya wireless itashidikana?
  3. Kama TANESCO wakikataa kushare nguzo zao, unafkiri na hiyo kampuni ikiamua kuweka nguzo zake nchi nzima itakuaje? (mfano jiji kama Dar kuanza kuongeza tena nguzo za umeme na hizo nyaya huko juu zitapitaje?)
  4. Na endapo TANESCO watakubali nguzo zao zitumike unafkiri huu usumbufu wao (ukiritimba) hautawaboa hiyo kampuni nyingine na kushindwa kufanya kazi yake vizuri?
  5. We unafkiria nini endapo litatokea shirika / kampuni nyingine inataka kuzalisha na kusambaza umeme Tanzania!!
NAWAKILISHA!!
 
Back
Top Bottom