Israel to help Zanzibar improve agriculture

Ndugu Nguruvi3 na Mzee Mwanakijiji

Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni bomu.
Ni mazingaombwe yasiyo na majibu ya mkato( kiini macho)

Kauli zenu zitaungwa mkono na wasomaji wengi, pia kupandisha mizuka wengi lakini bado hatuzungumzii mazingaombwe ya Muungano. Mimi nafikiri huwa tanafanya kwa makusudi ili kutengeneza chuki au kuamsha jazba kwa wanaofata mkumbo tu.

Hiki kijarida ,gonga link http://www.kituochakatiba.org/index2.php?option=com_docman&task=doc_view&gid=1208&Itemid=27 kinajaribu kuelezea utata na ugumu wa Muungano wa baadhi ya mambo kama ulivyo Muungano wa TZ na mahusiano ya kimataifa. Ni vyema kukisoma chote lakini kwa muktadha wa mliyoyaandika anzia uk 94 kwenda mbele.

Na baada ya kukisoma bado tutakuwa na ujasiri wa kuamsha mizuka ya wanajf?
Nonda, nimesoma hicho kijarida. Nimekisoma na kufanya fikra kama mimi na kile nikijuacho. Hii ni tofauti na wewe uliyesoma na kumeza kila kitu.
Ukisoma kwa umakini utadhani ni watu wameandika, nenda uk 94 utaona ni maoni binafsi ya mtu yanayoweza kuegemea upande anaoutaka.

Utashangaa kusikia Wzbar wanalalmikia adha za muungano, ni mwiko kwao kuongelea faida za muungano ambazo ni nyingi sana na hivyo ndivyo mwandishi wa Kijarida alivyozivia akili za Wenzetu. Majuzi wakati wa kauli ya kibaguzi ya mwarabu Jusa, tulianza kampeni dhidi ya Wzbar waishio bara na inaendelea kuhusu ajira, ardhi n.k. Kelele zimekwisha zikionyesha umuhimu wa muungano kwao.

Kilichokuwa kinawatia kiburi ni tetesi za mafuta, sasa yapo Uganda na Kenya. Kiburi kwisha

Zbar ifanye ifanyavyo bado bara ni sehemu muhimu sana ya uchumi wake. Siyo Israel wala Oman. Ukweli huu unauma na hakuna mzbar anayeweza kuuongelea. Bara wakiweka kauzibe Zbar itaumia sana.
Hili linakuja ni suala la muda tu.

Maswali ni haya:
Nyerere amepeleka ukristo Zbar, sasa Waisrael ambao ni wajomba wa damu wa Yesu wataleta nini?

Katika mambo 11 Zbar inayodai ni ya muungano, mambo ya nje ni mojawapo. Seif Idd amefanya hivyo?
 
Nonda, nimesoma hicho kijarida. Nimekisoma na kufanya fikra kama mimi na kile nikijuacho. Hii ni tofauti na wewe uliyesoma na kumeza kila kitu.
Ukisoma kwa umakini utadhani ni watu wameandika, nenda uk 94 utaona ni maoni binafsi ya mtu yanayoweza kuegemea upande anaoutaka.

Utashangaa kusikia Wzbar wanalalmikia adha za muungano, ni mwiko kwao kuongelea faida za muungano ambazo ni nyingi sana na hivyo ndivyo mwandishi wa Kijarida alivyozivia akili za Wenzetu. Majuzi wakati wa kauli ya kibaguzi ya mwarabu Jusa, tulianza kampeni dhidi ya Wzbar waishio bara na inaendelea kuhusu ajira, ardhi n.k. Kelele zimekwisha zikionyesha umuhimu wa muungano kwao.


Maswali ni haya:
Nyerere amepeleka ukristo Zbar, sasa Waisrael ambao ni wajomba wa damu wa Yesu wataleta nini?

Katika mambo 11 Zbar inayodai ni ya muungano, mambo ya nje ni mojawapo. Seif Idd amefanya hivyo?

Nguruvi3

Vipi umefikia hitimisho kuwa mimi nimesoma na kumeza kila kitu?

Ni wazi kuwa kama umekisoma hiko kijarida basi ulikuwa umeshaweka msimamo wako tokea mwanzo.
Kama umekisoma na bila kuweka msimamo basi hapa utaona utata na ugumu wa kimgawanyo wa madaraka na kiutendaji "Suala lenye tatizo kubwa, hata hivyo, ni suala la uwakilishi wa Zanzibar katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhusu mambo yasiyokuwa ya Muungano.
Hoja ya Zanzibar ina mambo mengi. Inatolewa hoja kuwa serikali ya Muungano haina uwezo wa kuiwakilisha Zanzibar kwa misingi
ya mgawanyo wa kazi kuhusiana na mambo ya Muungano na yale yasiyokuwa ya Muungano.
Tatizo, kwa mujibu wa Zanzibar si suala la kutokuwa na madaraka tu kwa upande wa serikali ya Muungano juu ya mambo yasiyokuwa ya Muungano ndani ya Jumuiya ya Afrika Masharaki. Tatizo kubwa zaidi ni kwamba miongoni mwa masuala 18 yaliyoshughulikiwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki 4 tu ndiyo mambo ya Muungano.
Shughuli nyingi za Jumuiya ya Afrika Mashariki ni za mambo yasiyokuwa ya Muungano ambayo yapo ndani ya madaraka ya Zanzibar. Ikiwa haya, kwa kweli, yatachukuliwa na serikali ya Muungano, hiyo ni kuivua zaidi Zanzibar uwezo wake wa kisheria ambao unachukuliwa na serikali ya Mungano ambayo inashughulikia mambo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, na kuiwacha Zanzibar bila ya chochote. Kwa maneno mingine, ni namna ya chini kwa chini ya kuanzisha Muungano wa serikali moja kwa kupitia Jumuiya ya Afrika Mashariki..... uk 99, 100-"

Kwa mfano hoja hiyo hapo juu kama wewe Mkuu Nguruvi3 umekabidhiwa Wizara ya mambo ya nje, ungewakilisha vipi maslahi ya Zanzibar ambayo yanajikita katika mambo ambayo si ya muungano?

Je kama mambo 18 ya EAC ni manne tu,4 ndio mambo ya Muungano. Bado tunaendelea kusema au kujidanganya kuwa Tanzania ni nchi moja? Muungano madudu!

Hebu pata muda ujiulize nchi zinazounganisha baadhi ya mambo na kubakisha baadhi ya mambo katika mamlaka yake, kweli unapata muungano wa nchi moja? Kama unaamini katika kiini/ viini macho basi hilo linawezekana!

Hapa anaesoma na kumeza tu ni mimi pekee au na wewe itabidi tukuingize kundini?

Ndugu Nguruvi3 unapomlaumu Jusa na ubaguzi wa kidini na wewe kushabikia kauli ya Nyerere na kupeleka ukristo Zanzibar au wayahudi na ujomba na yesu...hapa unajitofautisha vipi wewe na Jusa?

Jusa ni mwarabu?

Nimeulizia hili kwa wanaomfahamu huyu kijana na kupata jibu kuwa ana asili ya uhindi(uasia) lakini sio uarabu.

Kama kweli umekisoma kijarida mkuu ni wazi hujazichambua hoja zinazoibuliwa humo.

Kawaida ya binadamu inaonesha kuwa kulalamika ni rahisi kuliko kusifia faida apatazo mtu. Waache walalamike lakini sisi tuwatendee haki pale penye msingi wa madai yao.

Nilisikia kauli ya CHADEMA karibuni wakisema wanataka Zanzibar wapate haki zao kama wakati ule alipokuwepo Karume. Nikiiona pale nilipoisoma kauli hii nitakubandikia source. Ni wazi wao pia wanaona Muungano unavyoendeshwa leo una kasoro nyingi tu.
 
Waliosoma Israel enzi hizo 1963- 1967 si hawa akina Mwema, wote wamestaafu.
Matatizo ya vyombo vya ulinzi yalianza pale vikosi vyake viipo geuzwa matawi ya CCM.

Eti mkuu wa kikosi ni mwenyekiti wa Tawi !!!??
Si mwenyekiti wa Tawi kwa kuchaguliwa ni by default.
Huu ndo upuuzi ilio zaa ujinga wote ndani ya Polisi JWTZ na UWT.
Jeshini hakuna demokrasia, jeshi lenye demokrasia siku zote ni jeshi ndembendembe la walegevu wa maungo na akili

Eti walifunza polisi wengi ndo hawa polisiccm.Sitaki hata kusikia huu upuuzi.Kama madini hatujaweza kumanage ya tufaidishe ije kuwa kilimo
 
Back
Top Bottom