Iringa yavuka wastani ukatili wa kingono

EMT

Platinum Member
Jan 13, 2010
14,483
15,308
IDADI ya watu wanaoripoti kunyanyaswa kijinsia wilayani Iringa mkoani Iringa imeongezeka huku ukatili wa kingono ukiwa kwa asilimia 29 juu ya wastani wa kitaifa wa asilimia 20. Watu 219 wakiwemo watoto 11 na wanaume 51 wameripoti makosa ya kunyanyaswa kijinsia kati ya Oktoba mwaka jana na Machi mwaka huu, mengi yakiwa ya kingono na kipigo.

Matukio hayo yameripotiwa kwenye Taasisi ya Maendeleo ya Wanawake na Watoto wa Vijijini (Tarwoc) kupitia kituo chake cha Family Drop in Centre cha mjini Iringa. Meneja Mradi wa kituo hicho, Amani Nduhise alisema juzi kuwa ili kurahisisha kazi yao, mradi wao wa kupambana na unyanyasaji wa kijinsia unafanya kazi kwa karibu na Polisi, Mahakama na Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake na Watoto.

Alisema ili kurahisisha upatikaji wa taarifa sahihi, mradi wao umepata mabalozi wa kujitolea kutoka katika kila kata watakaokuwa na wajibu wa kufuatilia matukio ya unyanyasaji wa kijinsia katika maeneo yote ya kata zao.

Alisema wakati mradi huo unafanya kazi katika kata zote 16 za Manispaa ya Iringa, Iringa vijijini kata zilizoingizwa katika mradi huo ni Ifunda, Mseke, Kihorogota na Kising’a. Kwa mujibu wa Nduhise, mabalozi 20 watakaofanya kazi katika kata hizo watapewa mafunzo ya kuwawezesha kushiriki kukabiliana na vitendo vyote vya unyanyasaji.

Meneja Utawala na Fedha wa mradi huo, Beatus Magoti alisema katika mafunzo hayo mabalozi hao watafanya kazi ya usuluhishi na utetezi na kuziwasilisha taarifa za vitendo hivyo katika ngazi za uongozi na mradi kabla ya kufikishwa kwenye vyombo vya Dola kama kutakuwa na haja.

HabariLeo | Iringa yavuka wastani ukatili wa kingono
 
Watoto wa Iringa hawa jui kuringa.

Ukiomba K unapewa bado ya moto moto sio mpaa ipowe :cool2:
 
IDADI ya watu wanaoripoti kunyanyaswa kijinsia wilayani Iringa mkoani Iringa imeongezeka huku ukatili wa kingono ukiwa kwa asilimia 29 juu ya wastani wa kitaifa wa asilimia 20. Watu 219 wakiwemo watoto 11 na wanaume 51 wameripoti makosa ya kunyanyaswa kijinsia kati ya Oktoba mwaka jana na Machi mwaka huu, mengi yakiwa ya kingono na kipigo.

Matukio hayo yameripotiwa kwenye Taasisi ya Maendeleo ya Wanawake na Watoto wa Vijijini (Tarwoc) kupitia kituo chake cha Family Drop in Centre cha mjini Iringa. Meneja Mradi wa kituo hicho, Amani Nduhise alisema juzi kuwa ili kurahisisha kazi yao, mradi wao wa kupambana na unyanyasaji wa kijinsia unafanya kazi kwa karibu na Polisi, Mahakama na Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake na Watoto.

Alisema ili kurahisisha upatikaji wa taarifa sahihi, mradi wao umepata mabalozi wa kujitolea kutoka katika kila kata watakaokuwa na wajibu wa kufuatilia matukio ya unyanyasaji wa kijinsia katika maeneo yote ya kata zao.

Alisema wakati mradi huo unafanya kazi katika kata zote 16 za Manispaa ya Iringa, Iringa vijijini kata zilizoingizwa katika mradi huo ni Ifunda, Mseke, Kihorogota na Kising’a. Kwa mujibu wa Nduhise, mabalozi 20 watakaofanya kazi katika kata hizo watapewa mafunzo ya kuwawezesha kushiriki kukabiliana na vitendo vyote vya unyanyasaji.

Meneja Utawala na Fedha wa mradi huo, Beatus Magoti alisema katika mafunzo hayo mabalozi hao watafanya kazi ya usuluhishi na utetezi na kuziwasilisha taarifa za vitendo hivyo katika ngazi za uongozi na mradi kabla ya kufikishwa kwenye vyombo vya Dola kama kutakuwa na haja.

HabariLeo | Iringa yavuka wastani ukatili wa kingono
Du!! Iringa is an issue!! pia ndio mkoa unaoongoza TZ kwa HIV/AIDS prevalence........currently at 15.7%..which is the highest compared to other regions in the country....nadhani pia wanaongoza kwa suicide rates.....lakini(on the other end) wako blessed kwa kuwa one of the big 4s...kwenye kilimo...
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Du!! Iringa is an issue!! pia ndio mkoa unaoongoza TZ kwa HIV/AIDS prevalence........currently at 15.7%..which is the highest compared to other regions in the country....nadhani pia wanaongoza kwa suicide rates.....lakini(on the other end) wako blessed kwa kuwa one of the big 4s...kwenye kilimo...

Hapo kwenye red, nilisoma somehwere nikadhani wamekosea.
 
Hapo kwenye red, nilisoma somehwere nikadhani wamekosea.
Hawajakosea mtu wangu....ni kweli kabisa na inatisha vibaya.....yaani mikoa mingine iko chini saana ukilinganisha...hata interventions nyingi za maswala ya ukimwi huwa zinaelekezwa Iringa kwa kipaumbele....kama umekaa Iringa usishangae kuona utitiri wa NGOs za Ukimwi kule...ndio hali halisi..Wilaya zoote.....soma hii survey ya uhakika hapa chini utapata majibu ya prevalence za HIV Tz nzima.......i was involved in this survey too...survey hii ilifanyika 2007/2008....inawezekana trend imeshuka sasa...kwasababu ya massive intervention campaigns......na inawezekana ikawa imepanda pia.......
http://www.measuredhs.com/pubs/pdf/HF28/HF28.pdf
 
Hawajakosea mtu wangu....ni kweli kabisa na inatisha vibaya.....yaani mikoa mingine iko chini saana ukilinganisha...hata interventions nyingi za maswala ya ukimwi huwa zinaelekezwa Iringa kwa kipaumbele....kama umekaa Iringa usishangae kuona utitiri wa NGOs za Ukimwi kule...ndio hali halisi..Wilaya zoote.....soma hii survey ya uhakika hapa chini utapata majibu ya prevalence za HIV Tz nzima.......i was involved in this survey too...survey hii ilifanyika 2007/2008....inawezekana trend imeshuka sasa...kwasababu ya massive intervention campaigns......na inawezekana ikawa imepanda pia.......
http://www.measuredhs.com/pubs/pdf/HF28/HF28.pdf
je hii inatokea kwa kuwa Iringa ni mkoa wenye watu wachache au?
 
Hawa jamaa wana hasira za papo kwa papo kweli. Wameacha kujiua siku hizi wananyanyasa?
 
Hawajakosea mtu wangu....ni kweli kabisa na inatisha vibaya.....yaani mikoa mingine iko chini saana ukilinganisha...hata interventions nyingi za maswala ya ukimwi huwa zinaelekezwa Iringa kwa kipaumbele....kama umekaa Iringa usishangae kuona utitiri wa NGOs za Ukimwi kule...ndio hali halisi..Wilaya zoote.....soma hii survey ya uhakika hapa chini utapata majibu ya prevalence za HIV Tz nzima.......i was involved in this survey too...survey hii ilifanyika 2007/2008....inawezekana trend imeshuka sasa...kwasababu ya massive intervention campaigns......na inawezekana ikawa imepanda pia.......
http://www.measuredhs.com/pubs/pdf/HF28/HF28.pdf

Nimesoma by mwaka jana bado inaongoza: Francis Godwin Mzee Wa Matukio Daima: MAADHIMISHO YA UKIMWI DUNIANI ,IRINGA BADO YAONGOZA KITAIFA. Pia inaongoza kwa mimba za wanafunzi.
 
And yet kuna watu wanaamini wanawake wote wamekomboka na hawahitaji kuwezeshwa.... This is sad. Juzi Mzee Dark City karusha uzi hapa kuelezea mwana mama kaburutwa na mumewe... na kuna mengi ambayo hayaongelewi na hatuna habari....
 
And yet kuna watu wanaamini wanawake wote wamekomboka na hawahitaji kuwezeshwa.... This is sad. Juzi Mzee Dark City karusha uzi hapa kuelezea mwana mama kaburutwa na mumewe... na kuna mengi ambayo hayaongelewi na hatuna habari....

Kwa hiyo viti vya ubunge vya kuwezeshwa viendelee kuwepo?
 
Viti maalum ni muhimu kuwepo?? NDIO...

Viendelee kuwepo? HAPANA....

Najaribu kupiga mahesabu ya haraka hapa NDIO + HAPANA = ?
Bado najiuliza kwa nini huu mkoa unongoze kwa kuwa na watu wenye Ukimwi?
 
Najaribu kupiga mahesabu ya haraka hapa NDIO + HAPANA = ?
Bado najiuliza kwa nini huu mkoa unongoze kwa kuwa na watu wenye Ukimwi?


I took it for granted utanielewa. Viti maalum Misingi yake ya kuanzishwa ilikua thabiti na tija sana kwa taifa tokana na kwamba it was believed it would be covered by Women who were qualified and of Potential output to the society. Tokana na kwamba vimechakachuliwa na vingi vimekaliwa na mahawara ama salient nyumba ndogo za wakubwa na wengi wenye hio nafasi kutoonekana Input yao mle ndani na output kwenye jamii HAPANA Havitakiwi viendelee kuwepo! Hopefully umenpata!

My theory kwanini Ukimwi uwepo zaidi hapo....

Katika eneo lililokua linaongoza kwa kutoa vijana wa kazi wake kwa waume wadogo wadogo maarufu kwa House gal na house boy Iringa ndio inayoongoza Tanzania. Ni wafanya kazi wenye adabu, wakarimu, sio wezi na wachapa kazi (hivo ndio sifa zao walizokua wanajulikana nazo); Wanakua ni wadogo na wanasambaa eneo kubwa la Tanzania. Wakienda hio mikoa kama Mbeya (Tunduma na Kyela zina UKIMWI Balaa sababu ya Boarders), Dar, Morogoro wanajenga mahusiano na wenyeji wa huko na ni rahisi kurubunika hasa wanawake.

Wengine wanapata mimba wanarudi majumbani... Wengine ile likizo kuja salimu homu vijana wanapapatikia kumpata for anakua amependeza (mabinti wengi ni maji ya kunde, hua wanarudi wamenawili na kua weupe walo wengi; na waelewa vilevi hivi kwa wanaume). Tokana na kwamba mji ni mdogo, yule binti akilala na vijana wawili tu ama hata mmoja.... Hio chain reaction itayokua hapo ni balaaa!
 
Lazima kutakuwa na sababu zinazosababisha haya matukio ya unyanyasaji na ukatili wa kijinsia yawe mengi Iringa. Nisingeshangaa mtu angesema haya kwa majirani zangu wa Mara!

Mwenye idea why atusaidie, please!

Babu DC!!
 
  • Thanks
Reactions: EMT
I took it for granted utanielewa. Viti maalum Misingi yake ya kuanzishwa ilikua thabiti na tija sana kwa taifa tokana na kwamba it was believed it would be covered by Women who were qualified and of Potential output to the society. Tokana na kwamba vimechakachuliwa na vingi vimekaliwa na mahawara ama salient nyumba ndogo za wakubwa na wengi wenye hio nafasi kutoonekana Input yao mle ndani na output kwenye jamii HAPANA Havitakiwi viendelee kuwepo! Hopefully umenpata!

My theory kwanini Ukimwi uwepo zaidi hapo....

Katika eneo lililokua linaongoza kwa kutoa vijana wa kazi wake kwa waume wadogo wadogo maarufu kwa House gal na house boy Iringa ndio inayoongoza Tanzania. Ni wafanya kazi wenye adabu, wakarimu, sio wezi na wachapa kazi (hivo ndio sifa zao walizokua wanajulikana nazo); Wanakua ni wadogo na wanasambaa eneo kubwa la Tanzania. Wakienda hio mikoa kama Mbeya (Tunduma na Kyela zina UKIMWI Balaa sababu ya Boarders), Dar, Morogoro wanajenga mahusiano na wenyeji wa huko na ni rahisi kurubunika hasa wanawake.

Wengine wanapata mimba wanarudi majumbani... Wengine ile likizo kuja salimu homu vijana wanapapatikia kumpata for anakua amependeza (mabinti wengi ni maji ya kunde, hua wanarudi wamenawili na kua weupe walo wengi; na waelewa vilevi hivi kwa wanaume). Tokana na kwamba mji ni mdogo, yule binti akilala na vijana wawili tu ama hata mmoja.... Hio chain reaction itayokua hapo ni balaaa!

Katika kutafuta chanzo nimekuta kuwa unywaji wa pombe ya ulanzi unadaiwa pia kuwa chanzo cha kuongezeka kwa maambukizi ya Ukimwi Iringa kama inavyosomeka hapo chini.

"KARIBU mchumba, karibu unywe ulanzi, unataka mtogwa (uliogemwa leo) au mkangafu (wa siku nyingi)? Njoo ukae nami hapa usiogope! Mama Anita, lete lita moja fanya haraka mrembo asije akaondoka," hivyo ndivyo nilivyopokewa katika klabu cha pombe cha Nyololo mufindi, Iringa.

Nilikwenda kufanyia kazi utafiti wa wataalamu unaosema kuwa moja ya sababu zinazochangia kasi ya maambukizi ya Ukimwi katika Mkoa wa Iringa ni ulevi hasa wa pombe za kienyeji.

Mmoja wa wauzaji wa pombe hiyo ambaye hakutaka jina lake liandikwe anasema wakati wa msimu wa pombe ya ulanzi, wanywaji wengi hushindwa kuzuia tamaa zao za ngono na kujikuta wakijiingiza katika vitendo hivyo bila kinga.

"Ulanzi ukiwa mwingi ngono pia huwa nje nje! Ndiyo maana msimu wa ulanzi ukiisha tu wanawake wengi huwa na mimba zisizotarajiwa. Ulanzi ni hatari, unasababisha watu washindwe kujizuia na hatuwezi kuuacha kwani ni asili yetu," anasema.

Pombe hiyo iligunduliwa wakati wa utawala wa machifu wa kabila la Wabena katika Wilaya ya Njombe baada ya mti mchanga wa mwanzi kukatika na kuanza kutoa maji matamu. Tangu wakati huo, pombe hiyo imekuwa ikithaminiwa na wakazi wa Mkoa wa Iringa na tayari imesambaa na kufika katika maeneo mengine mengi hasa kusini mwa Tanzania. Wanywaji wengi wa ulanzi wanasema bila shaka kwamba pombe hiyo inachangia kasi ya Ukimwi.

"Msimu wa ulanzi huwa unauzwa bei rahisi ambayo hakuna inayemshinda ndo maana watu wengi hulewa hivyo kuwa rahisi kwao kufanya ngono bila kujiandaa kwani wanawake wengi wakishanunuliwa kinywaji hicho huwa wepesi kukubali," anasema Richard Mwenda mkazi wa Nyololo.

Mtaalamu na afisa maendeleo ya jamii wilayani Mufindi mkoani Iringa, DEOGRASIA LIGANGA anasema pombe hiyo ndiyo kichocheo kikubwa cha ngono zembe hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa maambukizi ya Ukimwi.

"Ulevi hasa wa pombe ya ulanzi unachangia kuongeza hamu ya kufanya ngono zembe, wengi wamejikuta wakipata maambukizi kutoka na pombe hii ambayo inaheshimiwa na wenyeji," anasema LIGANGA.

Ulanzi siyo kichocheo pekee, Liganga anataja mila na desturi potofu ambazo jamii nyingi mkoani humo bado inaziendeleza. Miongoni mwazo ni kurithi wajane, kukosekana kwa usawa kijinsia, kutakasa wajane na wasichana, kuoa wake wengi, imani za kishirikina na kutotahiri.

Nyingine ni umaskini wa kipato. Maisha ya wananchi wengi ni duni. Anasema kutobadili tabia licha ya elimu ya ukimwi kuwafikia wananchi na wengine kuathiriwa kwa njia moja au nyingine na Ukimwi ni miongoni mwa sababu za kuenea kwa ugonjwa huo.

Anataja sababu nyingine kuwa ni muingiliano mkubwa wa watu kutokana na shughuli nyingi za biashara na ongezeko la taasisi mbalimbali mkoani humo.

Hali ya maambukizi ikoje?

Katika wilaya ya Mufindi hali ya maambukizi inazidi kutishia amani kwa kuwa na kiwango kikubwa cha maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI ambapo kwa takwimu za mwaka huu wilaya ya Mufindi pekee ina asilimia 15.9 ikilinganishwa na kiwango cha mkoa ambayo ni asilimia 13.5

Zaidi: McDONALD MASSE: ULANZI NOMA KWA UKIMWI MUFINDI
 
afu nyie kina kamwene mna balaa
siku hizi nikija huko, nabeba chakula tokea huku nilipo

asubuhi wanakupiga andazi lina ulanzi
mchana wanakupa ugali wa ulanzi
usiku wanakupiga wow wow wow.

Ila, ukitembelea Makete unasikitika sana, hawajui hapana kabisa. Ni niangusage tu.
 
afu nyie kina kamwene mna balaa
siku hizi nikija huko, nabeba chakula tokea huku nilipo

asubuhi wanakupiga andazi lina ulanzi
mchana wanakupa ugali wa ulanzi
usiku wanakupiga wow wow wow.

Ila, ukitembelea Makete unasikitika sana, hawajui hapana kabisa. Ni niangusage tu.

Usiwe unaenda huko wakati wa msimu wa ulanzi basi.
 
Back
Top Bottom