Tutor B
JF-Expert Member
- Jun 11, 2011
- 9,025
- 6,554
Alinitamkia kuwa ananipenda, kipindi penzi likiwa motomoto, kwa mdomo wake tukiwa kwenye mtoko beach tumejiachia alinambia hivi "Sweety ninavyokupenda hivi, ikitokea ukaniacha nitaumia sana, kwa hali hiyo nitajitahidi mi ndo nitangulie kukuacha" Nilimwangalia sikupata kumwelewa, badala yake nilihama mada tukaendelea na mambo mengine hadi mda ulipofika tukaagana. Tangu siku hiyo nimekuwa nakaa naye tu ila akidemand mambo fulani namwambia bado natafakari maneno alonambia tukiwa kwenye mtoko. Amekuwa akiwatumia marafiki zangu wanibembeleze niweze kumsamehe kwa kosa la kauli yake . . . . ukweli nami naogopa kuendelea naye. Marafiki wanasema nimtamkie, wengine wanasema niache hivyohivyo. Ipi ni sahihi? Nimwambie basi au niendelee kumyuti hadi kieleweke?