Mkuu!
Mimi siyo mtaalam wa kiswahili ila kula chungwa nahisi ni sahihi,katika kula ndo kuna kitendo cha kulinyonya.
Halafu unaweza kusema kunywa juisi ya chungwa siyo kunywa chungwa.
Hapo si mtaalam wa kiswahili ukaweza kupatia vizuri hivyo! Fikiria ungekuwa mtaalam..! Any way umemjibu vizuri ingawaje na mimi siyo mtaalam.
Tafadhali tuhifadhi roho ya kilugha tukitumia "maji ya chungwa" badala ya "juisi". Nakiri ndio "juisi" limeenea sana lakini ..... si lazima hata kidogo liwepo.
Mimi ninavyo ona yote matatu ni sahihi, inategemea na wakati na kitendo unchofanya.Kula chungwa,
kunywa chungwa,
kunyonya chungwa.Ipi lugha sahihi?