Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 46,903
- 32,312
Wanabodi.
Chadema wanadai eti Intelijensia yao imenasa habari za kuwindwa na kuwawa wanasiasa watatu Slaa, Mnyika, Lema, pamoja na mtambo wa mawasiliano...madai ya aina hii mbali ya kuwa ya uwongo pia yanaonyesha kwamba hiyo Intelijensia wana tatizo kuu la kukosa uelewa na wamepotoka kwa kiasi kikubwa bila kujielewa.
Chadema wanadhani wanafanya makubwa kumbe wanajidanganya wenyewe wanaonyesha pia hawaelewi kabisa jukumu la Idara ya Usalama wa Taifa wanadhani ni chama cha siasa ni wapinzani wao wanaweza kurushiana vijembe na maneno mengine ya kipropaganda.
Intelijensia ya Chadema ndio ilimletea habari Dr Slaa na kuwa alishinda uchaguzi wa rais na kumwangusha Jakaya Kikwete hata hivyo shutuma zao dhidi ya Usalama wa Taifa hazikupokelewa kwa uzito maana matokeo waliyoyakubali ya ushindi wa wagombea Ubunge yaliifanya hoja yao ionekane dhaifu. Watanzania wale wale waliokuwa wakipiga kura za kumchagua rais, ndio hao waliopiga kura za kuchagua wabunge..
Intelijensia ya Chadema inashindwa kuelewa nchi yoyote duniani yenye usalama huwa ni kutokana na sera ya nchi hiyo ya Ulinzi na Usalama na utendaji kazi wa vyombo vya ulinzi...maantiki ya kawaida inasababisha liibuke swali la msingi kwamba ikiwa Chadema ina viongozi wengi inakuaje wanne tu watake kuuwawa.
Chadema mbinu zenu za kutaka kuonewa huruma na wananchi na kupitia Intelijensia yenu inazidi kukidhoofisha chama chenu.
Chadema wanadai eti Intelijensia yao imenasa habari za kuwindwa na kuwawa wanasiasa watatu Slaa, Mnyika, Lema, pamoja na mtambo wa mawasiliano...madai ya aina hii mbali ya kuwa ya uwongo pia yanaonyesha kwamba hiyo Intelijensia wana tatizo kuu la kukosa uelewa na wamepotoka kwa kiasi kikubwa bila kujielewa.
Chadema wanadhani wanafanya makubwa kumbe wanajidanganya wenyewe wanaonyesha pia hawaelewi kabisa jukumu la Idara ya Usalama wa Taifa wanadhani ni chama cha siasa ni wapinzani wao wanaweza kurushiana vijembe na maneno mengine ya kipropaganda.
Intelijensia ya Chadema ndio ilimletea habari Dr Slaa na kuwa alishinda uchaguzi wa rais na kumwangusha Jakaya Kikwete hata hivyo shutuma zao dhidi ya Usalama wa Taifa hazikupokelewa kwa uzito maana matokeo waliyoyakubali ya ushindi wa wagombea Ubunge yaliifanya hoja yao ionekane dhaifu. Watanzania wale wale waliokuwa wakipiga kura za kumchagua rais, ndio hao waliopiga kura za kuchagua wabunge..
Intelijensia ya Chadema inashindwa kuelewa nchi yoyote duniani yenye usalama huwa ni kutokana na sera ya nchi hiyo ya Ulinzi na Usalama na utendaji kazi wa vyombo vya ulinzi...maantiki ya kawaida inasababisha liibuke swali la msingi kwamba ikiwa Chadema ina viongozi wengi inakuaje wanne tu watake kuuwawa.
Chadema mbinu zenu za kutaka kuonewa huruma na wananchi na kupitia Intelijensia yenu inazidi kukidhoofisha chama chenu.