Intelijensia Kuhusu Maandamano ya CHADEMA

huo ni ukweli lakini wao hawamuogopi Mungu,kwa maovu wanayofanya utadhani inchi wameumbiwa wao,mauaji ya watu wasio na hatia yanafanyika,nadhani sasa CCM imefurahia POLISI WANAVYOFANYA VURUGU KWA WANAINCHI,AU WANATAKA YA KENYA YAJE HAPA?Serikali jiulize.CHADEMA WAPO SAHIHI HEBU TUWATIE MOYO WA KUENDELEA NA KUPIGANIA MABADILIKO TUMECHOKA NA HALI HII MARA GHARAMA ZA USAFIRI KUPANDA 100 ASILIMIA,WATANZANIA HEBU AMKENI TUUNGANE MPAKA LINI TUTAENDELEA KUWA HALI HII YA UOGAWALIOKUFA ARUSHA WAMEKUFA KISHUJAA KWA KUPIGANIA INCHIYAO.SALUTI KWAO.VYAMA VINGINE HEBU UNGANENI NA CHADEMA NASI TUPO PAMOJA NANYI,BIG,UP CUF.MWEMA VIP?AU NAWE MWANACCM/TUAMBIE:A S 100::mad2::playball: .Viongozi wa Chadema walilazimisha maandamano yafanyike licha ya kuombwa na Mkuu wa Polisi Tanzania kuwa yasifanyike kwa sababu tu:

Walikuwa na nia ya kuwatisha wawekezaji wakubwa duniani ambao wapo Tanzania, huko huko Arusha kwa sasa.

Wawekezaji hao, wakiongozwa na Dhirubhai Ambani walikuwa Tanzania kwa nia ya mapumziko na biashara na kutazama mandhari ya Tanzania na uwezekano mkubwa wa kuwekeza Tanzania.

Kwa roho mbaya tu na kwa nia isiyoyatakia mema Tanzania, viongozi wa Chadema wakahakikisha maandamano hayo yanafanyika kwa lazima na hata yangeruhusiwa na polisi basi fujo lazima zingetokea ili kuwatisha hao wawekezaji waone kuwa Tanzania si pa kuwekeza.
 
Hizo ndio sababu ambazo hazipingiki, kulikuwa kuna umuhimu gani wa kufanya maandamano wakati kuna wageni? tena ni wawekezaji muhimu? kama si kuwatisha?

wawekezaji kama dowans na richmond? au barrick gold?pambaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaf kabisa
 
Waliosababisha mauaji Arusha ambao wanapaswa kufikishwa kwenye mahakama ya kimataifa hawa hapa:
Mkurugenzi wa jiji la Arusha - huyu ndiye aliitisha uchaguzi kinyemela
Katibu wa Bunge - Aliyetoa barua kuidhinisha kuwa mbunge wa viti maalum Tanga anaruhusiwa kupiga kura katika uchaguzi wa meya Arusha.
Mbunge wa viti maalumu Tanga - huyu alipiga kura wakati akijua fika kuwa yeye hastahili.
RPC Arusha - Kwa kuidhinisha matumizi ya risasi za moto.
IGP - Kwa kuwa kigeugeu mara anaruhusu mkutano mara bila taarifa rasmi atauzuia na pia kuidhinisha polisi kutumia risasi za moto dhidi ya raia wasiokuwa hata na rungu.
Madiwani wote wa CCM Arusha - kwa kukubali kushiriki uchaguzi waliojua fika kuwa si halali (hapa namuondoa huyu aliyejitoa CCM baada ya mauaji maana ametambua na kujutia makosa yake; huyu ni shahidi muhimu na yabidi alindwe).
JK - Kwa` kuwa yeye ndiye kiongozi wa nchi na kwa vyovyote polisi hawawezi kutumia risasi kuwaua raia bila yeye kuafiki. Kama kweli hakuafiki, amfukuze kazi mara moja IGP na RPC Arusha.
Makamba - kwa uchochezi na kutosikiliza ushauri, Hakika naamini uchunguzi wa kina utakuja kuonyesha kuwa Makamba ndiye archtect wa uvurugaji wa uchaguzi wa meya wa Arusha, ndiye alitoa maelekezo namna CCM wataweza kutumia nguvu ya dola kufanya hivyo.
Kila mtu aongezee/au apunguze kwenye orodha na sababu.
Kaka mimi siongezi kitu ila nakusifia the way ulivyo weza kuwatambua wauwaji,ila hivi tuna waziri mkuu kweli!namkumbuka lowasa jamani saa hizi watu wemesha kosa kazi
 
Ama kweli hakuna umaskini mbaya kupita wote kama umaskini wa mawazo- alisema Nyerere haya maneno.

Wewe ndugu yangu una hali mbaya inabidi tukuombee, maana bado umelewa fikra potofu za kifisadi, lkn sikulaumu maana hii elimu tunayofundishwa mashuleni mwetu ni wajanja wachache sana ndo hushtuka kuwa ni upuuzi, ndugu yangu mpk leo unawaita wageni kama Ambari ni muhimu kwa nchi yetu??!! na hizo ndo taarifa gani za kiinteligensia sasa? nadhani hata hujui maana ya intelligency information.

Maskini Mungu akurehemu uamke kwa usingizi huo mzito ndugu yangu!
 
Na naibu Meya-TLP,kwa kukubali kuchaguliwa ili hali yeye mwenyewe alishasema sheria na kanuni zilivunjwa
 
Vitendo na mawazo ya kipumbavu vinavyosababishwa na ulevi wa madaraka kwa viongozi wa serikali wanaotumia jeshi la polisi kama mbwa wao na jeshi hilo kukubali kutumika kulinda uovu wa walevi hao badala ya kulinda raia na mali zao ndyo hasa chanzo cha mauaji hayo.
Ni muhimu kuunda tume huru kuchunguza chanzo cha vurugu hizo na kuhakikisha wote waliosabisha hali hiyo wanashughulikiwa kwa mujibu wa sheria , bila upendeleo wowote ili kujenga imani ya raia kwa serikali na vyombo vya dola.
Askari waliopiga raia badala ya kuwakamata hata kama walivunja sheria kwa kuandamana lazima waadhibiwe na wauaji lazima waadhibiwe ili iwe fundisho kwa wengine wenye mawazo na tabia kama hizo.
Lazima tuhakikishe kuwa watendaji wote wa vyombo vya dola wanaolipwa kutokana na kodi za wananchi, wanafuata maadili ya kazi zao kwa kuwatumikia wananchi na siyo kutumikia maadui wa uma ambao ni kundi dogo tu liloteka nafasi za utawala kifisadi kwa kutumia uelewa mdogo wa wananchi.
 
Hizo ndio sababu ambazo hazipingiki, kulikuwa kuna umuhimu gani wa kufanya maandamano wakati kuna wageni? tena ni wawekezaji muhimu? kama si kuwatisha?


wawekezaji au wanyonyaji.... we kuna muhindi muwekeaji... c washenzi tu hao..... ambani ambani... mfuate ww bac huyo ambani akawekeze kijijini kwenu
 
Mkuu,
Mbali na kuipamba vyema post yako, ya uwekezaji na biashara.
Serikali hapa kupitia jeshi la polisi ndio wamevunja amani ambayo walipaswa wailinde!
Wangetoa nusu tu askali waliotumika kulinda usalama wa maandamano na mkutano hakuna mtu angeumia wala mali yoyote ingeathirika.

After all, Serikali haiwezi kuamua lini watu wafanye mkutano na lini waandamane. Ni haki zao kikatiba. serikali ilipaswa kutoa ulinzi basi.
Vilivyobaki ni visingizio visivyo na maana yoyote.
watu wameuawa na mali zimeharibika.. Serikali na polisi haikutumia busara hata kidogo hapa na zenyewe ndio zinastahiki lawama juu ya yaliyotokea na wawajibike au wawajibishane.

wangeacha maandamano na mkutano ufanyike na kama kungetokea uvunjifu wa amani hapo serikali na jeshi la polisi wangewachukulia hatua kisheria watuhumiwa......hizi siasa za kipuuzi za CCM kushika hatamu zinatugharimu sana hapa TZ. wanapaswa kubadilika, mfumo wa chama kimoja umepitwa na wakati.

Serikali ina mkono mrefu na hawana sababu ya kutolea ufafanuzi wa kina wanapozuia kitu kisifanyike. Wana namna na njia nyingi za kupata habari, za kuaminika na kusadikika na zisozo hivyo. Maamuzi mengine yanateghemea muda na kuepusha fadhaa inayoweza kupatikana, na nilimsikia Mwema akisema yawachwe kwa sasa. Jee, huoni kuwa hawa viongozi wanao kaidi amri ya Serikali ndio wakorofi?

Na ukorofi huo wanaoufanya ni kwa faida ya nani? Raia wengi Tanzania hatuungi mkono ufedhuli kwa Serikali. Raia wengi Tanzania hutuungi mkono Maandamano haramu. Raia wengi Tanzania hatuungi mkono chama kisicho kuwa na maamuzi ya amani. Raia wengi wa Tanzania hatuungi mkono siasa za ubabe.
 
wawekezaji au wanyonyaji.... we kuna muhindi muwekeaji... c washenzi tu hao..... ambani ambani... mfuate ww bac huyo ambani akawekeze kijijini kwenu

Huo ni ubaguzi dhahiri shahiri, sina cha kuongezea.
 
Ama kweli hakuna umaskini mbaya kupita wote kama umaskini wa mawazo- alisema Nyerere haya maneno.

Wewe ndugu yangu una hali mbaya inabidi tukuombee, maana bado umelewa fikra potofu za kifisadi, lkn sikulaumu maana hii elimu tunayofundishwa mashuleni mwetu ni wajanja wachache sana ndo hushtuka kuwa ni upuuzi, ndugu yangu mpk leo unawaita wageni kama Ambari ni muhimu kwa nchi yetu??!! na hizo ndo taarifa gani za kiinteligensia sasa? nadhani hata hujui maana ya intelligency information.

Maskini Mungu akurehemu uamke kwa usingizi huo mzito ndugu yangu!

Leo hii huoni umuhimu wa waekezaji Tanzania?

Hayo ndio unaita mawazo?

Kumbuka hayo mawazo yako ni kama yaliokuwa ya Nyerere, jee unajuwa alitufikisha wapi?

Mwenyewe alikiri kukosea. Sasa na wewe kama unaona watu wote duniani wanaovutia matajiri wawekezaji ni wajinga basi wewe ndio bado umelala tena nusu kaputi.

Tanzania ya leo ina teknoloji ipi ya kukataa wawekezaji? Ina mtaji upi wa viwanda kwa kukataa wawekezaji?

Nchi zenye teknolojia, viwanda, biashara na bado zinahitaji wawekezaji wenye misingi mikubwa, seuse sisi.
 
............hawa ndio ccm bana, wapo tayari kulala sebuleni kwenye kochi ampishe 'mgeni' alale na mkewe chumbani na asubuhi asiulize amelalaje na anaondoka na nini kwenye bag yake. Hiyo sababu ya kiitelejensia aliisema ustaadh mwema masjid gani? Mbona hajatamka yeye binafsi?
 
HIVI huyu ni zomba au ZOBA! Ama kweli kazi ipo! Huyu bandugu Zoba ni MASKINI sana mbaya zaidi ni MFUNGWA! Umaskini wake ni ktk fikra na mawazo. Bora angekuwa maskini wa mali lakini tajiri wa fikra. Huyu bandugu ni MFUNGWA! hayupo huru tena kuna kazi nzito ya kufanyika kumkomboa huyu bandugu! Yupo usingizini mithili ya pono. Yaani bandugu zoba hujui kuwa kuandamana au kufanyika mikutano ya hadhara ni haki ya kikatiba ya kila chama cha siasa na kila raia? Na kwamba polisi hawaombwi kibali bali wanapewa taarifa ili kama wana mashaka na usalama wa mali na raia basi waweze kutoa ulinzi? Kwamba polisi kikatiba hawana mamlaka ya kutoa au kuzuia maandamano! Ndugu amka usingizini. Yaani wewe unazungumzia wawekezaji kwamba ni muhimu zaidi kuliko mapambano ya ukombozi wa kweli ya nchi yetu! Hakika unaumwa! Pole sana ila tafakari sana kabla ya kupost pumba zako huku
 
Hizo ndio sababu ambazo hazipingiki, kulikuwa kuna umuhimu gani wa kufanya maandamano wakati kuna wageni? tena ni wawekezaji muhimu? kama si kuwatisha?

Mara ya kwanza polisi walipokuwa wameruhusu hayo maandamano hawakujua kuwa kuna wageni? Naomba jibu plz.
 
jamani, jamani watanzania wenzangu wenye akili timamu. Ni dola au taifa gani chini ya jua hili limeendelea kwa kuwategemea hao mnaowaita wawekezaji, tuache kudai maswala yetu ya msing kisa kuna kajamaa kana fedha kama mchanga kamepanga kwenye hoteli zetu,kwamba tutawapigia kelele pingi wakiwa wanakula vinono vya nchi yetu.mnitajie ni mwekezaji gani ametunufaisha hadi now??? zaidi ya kutugeuza shamba la bibi,
MUNGU AWAREHEMU NA KUWALAZA MAHALI PEMA PEPONI WANAHARAKATI WALIOTANGULIZWA MBELE ZA HAKI NA HAWA VIBARAKA WA CCM, NAWAHAKIKISHIA DAMU ZAO HAZIJAMWAGIKA BURE, MAPAMBANO DHIDI YA UDHALIMU NA UFISADI SO SOON TUTAIKAMILISHA:A S 465::A S 465::A S 465::A S 465:
 
Wewe ni Zomba au ZOMBE? Maana ya Zombe tunayajua hayana tofauati sana na ya Arusha!
 
HIVI huyu ni zomba au ZOBA! Ama kweli kazi ipo! Huyu bandugu Zoba ni MASKINI sana mbaya zaidi ni MFUNGWA! Umaskini wake ni ktk fikra na mawazo. Bora angekuwa maskini wa mali lakini tajiri wa fikra. Huyu bandugu ni MFUNGWA! hayupo huru tena kuna kazi nzito ya kufanyika kumkomboa huyu bandugu! Yupo usingizini mithili ya pono. Yaani bandugu zoba hujui kuwa kuandamana au kufanyika mikutano ya hadhara ni haki ya kikatiba ya kila chama cha siasa na kila raia? Na kwamba polisi hawaombwi kibali bali wanapewa taarifa ili kama wana mashaka na usalama wa mali na raia basi waweze kutoa ulinzi? Kwamba polisi kikatiba hawana mamlaka ya kutoa au kuzuia maandamano! Ndugu amka usingizini. Yaani wewe unazungumzia wawekezaji kwamba ni muhimu zaidi kuliko mapambano ya ukombozi wa kweli ya nchi yetu! Hakika unaumwa! Pole sana ila tafakari sana kabla ya kupost pumba zako huku

Nakubaliana na wewe.... huyu ni ZOBA wa hali ya juuuuuuu!!!!!!!
 
Ahsante sana, lakini nadhani ukweli umeuelewa na utauzingatia.

Ni vizuri ieleweke wazi kwamba kulikuwa na mkanganyiko wa amri kutoka Polisi juu ya kukatazwa kwa maandamano. RPC na IGP wamejichanganya katika hili.
Ok, amri ya mkubwa ikawa ya mwisho na maandamano yakafanyika; Nguvu iliyotumika inatakiwa kupongezwa na kubeza uongozi wa Chadema?? Kumbuka ni uongozi wa chama chenye wafuasi wengi kwenye nchi hii na ni chama rasmi cha upinzani nchi hii, hakukuwa na staha ya kulifanya hili zaidi ya kupigana risasi na mauaji?????? Think twice???
 
Hakuna mantiki yoyote kwa wana siasa walio mahiri kulazimisha maandamano yafanyike wakati kuna wageni, tena wawekezaji muhimu ambao hakuna nchi katika hii dunia yetu ya sasa isiotaka wawepo au watembelee kwao.

Tatizo lenu mnatukuza wageni na kuwabeza watanzania
Mbuga za wanyama mumewaachia
Madini wanachimba na wanatuachia mashimo na ndugu zetu walifukiwa
Wanakuja kuchuma na tunaingia mikataba ya kijinga halafu tunawalipa kwa jasho la masikini wa TZ
Halafu unasema wawekezaji, wafe kabisa mimi sitaki hata kuwasikia.
Tujipange kwanza then tuwalete, kuleta wawekezaji na mikataba kama ya Dowans ni ujinga
Nyamongo kule watu wamekufa na wengine wamegeuka ngozi kama chura (wote tumeona) sababu ya wawekezaji na serikali yenu iko kimya
Masilahi na uhuru wa kweli wa nchi na watu wake vitangulie kabla ya wawekezaji
 
Serikali ina mkono mrefu na hawana sababu ya kutolea ufafanuzi wa kina wanapozuia kitu kisifanyike. Wana namna na njia nyingi za kupata habari, za kuaminika na kusadikika na zisozo hivyo. Maamuzi mengine yanateghemea muda na kuepusha fadhaa inayoweza kupatikana, na nilimsikia Mwema akisema yawachwe kwa sasa. Jee, huoni kuwa hawa viongozi wanao kaidi amri ya Serikali ndio wakorofi?

Na ukorofi huo wanaoufanya ni kwa faida ya nani? Raia wengi Tanzania hatuungi mkono ufedhuli kwa Serikali. Raia wengi Tanzania hutuungi mkono Maandamano haramu. Raia wengi Tanzania hatuungi mkono chama kisicho kuwa na maamuzi ya amani. Raia wengi wa Tanzania hatuungi mkono siasa za ubabe.

Bw Zomba, post yako umeituma ama kwa sababu hujui unamaanisha nini au unajua lakini kwa malengo ya kupotosha umma, kwa sababu kabla ya kusema kuwa CDM walikuwa na lengo la kuipaka matope nchi, ulipaswa ujiulize yafuatayo;

1) Wageni unaowaongelea walikuja lini Tz, kabla au baada ya kupigwa marufuku mkutano wa kwanza wa CDM hapo December?

2) Wageni unaowaongelea walikuja Tz, au waliomba kuja tz kabla au baada ya polisi kutoa kibali (kilichokuja kufutwa saa chache kabla) cha maandamano?

3) Je, maandamano ni haramu? Sio kwa mujibu wa sheria?, Je, sheria inazuia uwepo wa maandamano kama wapo wageni?

4) Pamoja na wanazoita taarifa za kiinteligensia kuwa maandamano yangeambatana na vurugu, je baada ya CDM 'kulazimisha' maandamano hayo, vurugu zilitokeaje? Ina maana inteligensia ilitabiri vurugu kwa kujua kuwa lazima polisi wangewakabili na kuwapiga waandamanaji?

5) Je, upo mfano wowote katika nchi hii ambapo maandamano halali yamewahi kusababisha vurugu ambazo hazikuchochewa na polisi?

Kumbe basi kwa taarifa yako, inaonyesha kuwa polisi walijua kuwa maandamano yatakuwa ya amani, lakini kwa kutaka kuwaonyesha 'wawekezaji' advertise, wakaamua kuyazuia maandamano hayo kwa nguvu kubwa (ingawa dhaifu), ili wawekezaji waamini kuwa watakuwa salama na serikali itakuwa hata tayari kuua watu ili kulinda maslahi ya wawekezaji.

Lakini wewe bw Zomba na serikali naomba mkumbuke kitu kimoja, hakuna serikali iliyowahi kubaki madarakani milele kwa kutumia ubabe na mabavu. Zaidi sana serikali inazidi kujiongezea chuki, kwa hiki ni kipindi ambacho ilitakiwa iwabembeleze wananchi kutokana na machungu ya ugumu wa maisha: Ukosefu wa umeme, bei ya umeme, nauli, dowans, wizi wa kura, ukosefu wa ajira, kushuka kwa thaamani ya shillingi, nk.

CCM inatakiwa ikumbike kuwa CDM hawakushindwa kwa kutopata kura nyingi zaidi mwaka jana bali kwa kushindwa kuzilinda kura walizopata. hivyo bas CCM wasidhani kuwa chance ya kuogelea kwenye same grace uchaguzi ujao ni kubwa, bali wanatakiwa wadelive, watekeleze ilani ya chama chao kwani kamwe, HAKI YA RAIA WA TZ HAITANYIMWA KWA RISASI.
 
zombe nakubaliana na wewe asimia mia, tena nadhani na tanesco inabidi wasikate umeme mpaka wageni waondoke....maana wageni wakiouna huu mgao wanaweza kubadili mawazo ya ku "invest" kwenye nchi hii.
 
Back
Top Bottom