Intelijensia Kuhusu Maandamano ya CHADEMA

Mh. Makamba ( Katibu Mkuu wa CCM) naomba unijibu hata kupitia kwa January Makamba ambaye huwa humu JF kwa jina jingine.

Ulisema CHADEMA hawakutii amri halali.
1. Je ukiwa na barua ya kukuruhusu kuandamana, kisha pakatokeo taarifa kwa mdomo kuwa umezuiwa kuandamana bila maandishi. Utatii amri ipi?

2. Kama polisi walikuwa na taarifa za kiitelijensia kuwa kuna shida itatokea na ndio maana wakawa wengi mno hata kutoka mikoa mingine kuzuia maandamano. Kwa nini wingi huo usitumike kuzuia yaliyokusudiwa katika taarifa hizo za kiitelijensia?

3. Unadhani kama kweli kuna taarifa za kweli zilizoonyesha kusudio lolote baya, je kwa nguvu iliyotumika na maisha yaliyoondolewa na waliojeruhiwa ( waliokuwamo na wasiokuwamo) imesaidia kugeuza ubaya wa yeyote aliyekusudia mabaya au mmewaongezea mashabaki hao waliokusudia mabaya?( kama kweli wapo waliokusudia mabaya)

4. Ni kwa nini vurugu haikutokea kabla ya polisi kuanza kuzuia maandamano?

5. Hata kama umezuiliwa kuandamana lakini ukapewa kibali cha mkutano wa hadhara. Je watu waende kwenye huo mkutano kwa Helkopta ili wasikamatwe kwa kuandamana? Je unaweza kuwawekea watu muda maalum wa kwenda kwenye mkutano mtu moja mmoja ili wasiende kwa pamoja au kwa makundi?

6. Kama kinacholindwa ni UMEYA na siyo wananchi wanaohudumiwa na meya huyo, ukishawaua utawasimamiaje?

7. Je CCM inaiheshimu mamlaka iliyo kuu (katiba) ambayo ndiyo mamlaka kuu kuliko zote?

TAFADHALI NIJIBU.
 
Zomba nadhani unaanza tena ugonjwa ule wa kipindi kile wa kupoteza fahamu. Usilete usisiem humu ndani kwa kufikiria kuuza samaki.
 
Mikutano ya UN inakuwaga na viongozi toka karibia kila taifa na watu huandamana NYC.USA kuna maandamano kila kukicha ila hakuna vurugu,nani anasema maandamano ni vurugu,polisi kazi yao nn? Nguvu zilizotumika kuua zingeweza tumia kuhakikisha amani kwenye maandamano
 
Demokrasi ni kuingia mitaani na kuanza fujo? Demokrasia ni kukaidi amri ya jeshi la polisi?

Kama mngekuwa mnaijuwa demokrasia msingeyafanya yote hayo. Kwa kipi kikubwa kilichowafanya muingie mitaani na kusababisha umwagikaji wa damu? kama si roho mbaya na fitna na uzabizabina?

It is better to be silent because you may speak and clear our doubt.
 
Shida yako haswa ni nini? kama kura mmeshindwa, tena vibaya sana. Wabunge hata nusu ya CCM hamjafikia, si msubiri muda wenu ukifika, na siasa zenu hizi za fujo, sasa wa Tanzania ndio kabisaaaaaaa wameshawashtukia. Hata wale wachache waliokuwa wakiwaung mkono, sasa mnawakosa.
You sound like that fisadi bootlicker in state house. Salva someone!
 
Ndugu zangu wanaJF,
Kila wakati polisi inapofanya unyanyasaji dhidi ya raia wasio na hatia imekuwa ikijitetea kuwa taarifa za kiintelijinsia zilionyesha uwezekano wa kutishiwa kwa amani ndiyo maana waliamua kuchukua hatua ya kutumia nguvu. Hata katika mauaji yaliyofanywa na polisi Arusha, IGP mwema ametoa sababu hiyohiyo ya taarifa za kiintelijinsia.

Hizo taarifa za kiintelijinsia kwa nini zinafichwa!! Kwa nini zisiwekwe hadharani. Mtizamo wangu ni kuwa hicho ni kichaka cha watawala kuficha nia zao mbaya dhidi ya wapinzani.
 
Mh. Makamba ( Katibu Mkuu wa CCM) naomba unijibu hata kupitia kwa January Makamba ambaye huwa humu JF kwa jina jingine.

Ulisema CHADEMA hawakutii amri halali.
1. Je ukiwa na barua ya kukuruhusu kuandamana, kisha pakatokeo taarifa kwa mdomo kuwa umezuiwa kuandamana bila maandishi. Utatii amri ipi?

2. Kama polisi walikuwa na taarifa za kiitelijensia kuwa kuna shida itatokea na ndio maana wakawa wengi mno hata kutoka mikoa mingine kuzuia maandamano. Kwa nini wingi huo usitumike kuzuia yaliyokusudiwa katika taarifa hizo za kiitelijensia?

3. Unadhani kama kweli kuna taarifa za kweli zilizoonyesha kusudio lolote baya, je kwa nguvu iliyotumika na maisha yaliyoondolewa na waliojeruhiwa ( waliokuwamo na wasiokuwamo) imesaidia kugeuza ubaya wa yeyote aliyekusudia mabaya au mmewaongezea mashabaki hao waliokusudia mabaya?( kama kweli wapo waliokusudia mabaya)

4. Ni kwa nini vurugu haikutokea kabla ya polisi kuanza kuzuia maandamano?

5. Hata kama umezuiliwa kuandamana lakini ukapewa kibali cha mkutano wa hadhara. Je watu waende kwenye huo mkutano kwa Helkopta ili wasikamatwe kwa kuandamana? Je unaweza kuwawekea watu muda maalum wa kwenda kwenye mkutano mtu moja mmoja ili wasiende kwa pamoja au kwa makundi?

6. Kama kinacholindwa ni UMEYA na siyo wananchi wanaohudumiwa na meya huyo, ukishawaua utawasimamiaje?

7. Je CCM inaiheshimu mamlaka iliyo kuu (katiba) ambayo ndiyo mamlaka kuu kuliko zote?

TAFADHALI NIJIBU.

Okampo akija, watu watajipanga tu. Enyi wanasheria mwandikieni Okampo kuwa kuna watu wanajifanya wanamiliki maisha ya watu na kwamba wao wataishi milele.....

Wengine bila aibu wanatumia biblia kuhalalisha uovu wao.....
 
Polisi wa tz, ni upepo. Amri ikitoka juu chini hakuna mjadala. Tatizo hapa ni upeofinyu wa maamuzi katika kufuatiria issue kamili atimae kudhibiti kwa amani. Na hii inakula kuanzia ngazi za juu kiutawala. Unaruhusu bunduki kwani wale walikuwa majambazi? SM SM! na mashaka bana wewe si mtz haya sasa watu wawili wamekufa kwa maamuzi wako.
 
Huyo zomba ni ***** hawezi kutetea ujinga unaofanywa na ndugu zako CCM kama huna kitu cha kuandika acha waandike wengine. Zomba nenda kijijini ukakae huna jipya baba
 
Viongozi wa Chadema walilazimisha maandamano yafanyike licha ya kuombwa na Mkuu wa Polisi Tanzania kuwa yasifanyike kwa sababu tu:

Walikuwa na nia ya kuwatisha wawekezaji wakubwa duniani ambao wapo Tanzania, huko huko Arusha kwa sasa.

Wawekezaji hao, wakiongozwa na Dhirubhai Ambani walikuwa Tanzania kwa nia ya mapumziko na biashara na kutazama mandhari ya Tanzania na uwezekano mkubwa wa kuwekeza Tanzania.

Kwa roho mbaya tu na kwa nia isiyoyatakia mema Tanzania, viongozi wa Chadema wakahakikisha maandamano hayo yanafanyika kwa lazima na hata yangeruhusiwa na polisi basi fujo lazima zingetokea ili kuwatisha hao wawekezaji waone kuwa Tanzania si pa kuwekeza.

Yote hiyo, ni kwa sababu tu, ya chuki zao binafsi walizozijenga baada ya kuangushwa vibaya kwenye uchaguzi uliopita.

Hakuna mantiki yoyote kwa wana siasa walio mahiri kulazimisha maandamano yafanyike wakati kuna wageni, tena wawekezaji muhimu ambao hakuna nchi katika hii dunia yetu ya sasa isiotaka wawepo au watembelee kwao.

Viongozi wa Chgadema kwa ajili tu ya chuki zao binafsi, wakaona hii ndio fursa ya kuipakaza matope (kama si m*v*) Tanzania. Walijuwa kuwa wawekezaji wakubwa kama hawa wanapokuja tena kwa idadi kubwa kama iliowasili hapa, lazima kuna waandishi wa habari wa kimataifa hususan wa mambo ya kibiashara na pia kuna watu wa intelijensia za kibiashara ambao misafara kama hiyo huwa hawakosekani.

Kwa namna ya maisha tunayoishi wa Tanzania au kwa mpenda amani yoyote, hata kama mna ugomvi wenu wa ndani, ajapo mgeni, tena ambae anaweza kuleta manufaa nyumbani kwenu, huwa mnasitisha ugomvi kwa siku mbili tatu mpaka mgeni aondoke. Haya hutokea hata majumbani mwetu, tukipapurana na bahati nzuri au mbaya mgeni akibisha hodi basi mara nyingi kwa wenye akili husitisha kupapurana kwao, wakamhudumia mgenina ikibidi kupapurana, wataendelea mgeni akisha ondoka.

Leo Chadema wameonyesha sura gani ya nchi yetu, kwa kulazimisha maandamano yaliyositishwa na Mkuu wa Polisi, mbele ya hawa wageni?

Nna uhakika, sura walioionyesha si nzuri, lakini, ni matumaini yangu kuwa wenyeji, waliowaalika hawa wageni, wataweza kuwafahamisha ukweli ulivyo na wataridhia si tu kuja tena kutembelea Tanzania, bali na kuwekeza kwa wingi, kwani kwa sasa bado tunahitaji mitaji ya nje.

Nawaomba wa Tanzania walaani kitendo cha viongozi wa Chadema baada ya kuuelewa huu ukweli wa kwanini hawa viongozi walilazimisha maandamano yafanyike.

Mungu awalaze popote apendapo Marehemu waliofarik.

Kweli Zomba wewe ni fisadi mkubwa sana..
WAGENI WAPI HAO AMBAO WANATAKA WANAJAMII WAKANDAMIZWE??? WEWE SURA YA NCHI IMEOZA NI KWAMBA HUJUI TU.. ANGALIA

KASHFA YA WIKELEAKS
KASHFA YA DOWANS
KASHFA YA RICHMONDS
KASHFA YA ATCL
KASHFA YA MINOFU YA SAMAKI
KASHFA YA MADINI MALIPO KIDOGO
KASHFA YA WIZI MEREMETA
KASHFA YA KUIBIWA URANIUM
KASHFA YA BARABARA YA SERENGETI
KASHFA YA EPA NA BOT
KASHFA YA BARABARA KUJENGWA CHINI YA KIWANGO.
KASHFA YA TANESCO KUPANDISHA BEI
KASHFA YA WIZI WA KURA WAKATI WA UCHAGUNI.

HIVI WEWE UONI HIZI NI SHIDA??????????
 
Hizo ndio sababu ambazo hazipingiki, kulikuwa kuna umuhimu gani wa kufanya maandamano wakati kuna wageni? tena ni wawekezaji muhimu? kama si kuwatisha?


mtajuta. na bado.

maeneo potential yote yapo chini ya waasi wa fikra.

mtakoma! mtakoma! mtakoma! mtakoma!
 
Zomba
Wageni/Wawekezaji hapa Tanzania??. Hapana sema labda waporaji wa maliasili zetu!. Na sidhani pia kama tunatakiwa kuwaabudu kwa kiwango cha kushindwa kutimiza haki yetu ya kidemokrasia kwa sababu tu wapo hapa kupanga jinsi ya kukwapua Asset zetu. Hili halikubaliki. Labda wewe- Zomba a.k.a Syatem at work.
 
Viongozi wa Chadema walilazimisha maandamano yafanyike licha ya kuombwa na Mkuu wa Polisi Tanzania kuwa yasifanyike kwa sababu tu:

Walikuwa na nia ya kuwatisha wawekezaji wakubwa duniani ambao wapo Tanzania, huko huko Arusha kwa sasa.

Wawekezaji hao, wakiongozwa na Dhirubhai Ambani walikuwa Tanzania kwa nia ya mapumziko na biashara na kutazama mandhari ya Tanzania na uwezekano mkubwa wa kuwekeza Tanzania.

Kwa roho mbaya tu na kwa nia isiyoyatakia mema Tanzania, viongozi wa Chadema wakahakikisha maandamano hayo yanafanyika kwa lazima na hata yangeruhusiwa na polisi basi fujo lazima zingetokea ili kuwatisha hao wawekezaji waone kuwa Tanzania si pa kuwekeza.

Yote hiyo, ni kwa sababu tu, ya chuki zao binafsi walizozijenga baada ya kuangushwa vibaya kwenye uchaguzi uliopita.

Hakuna mantiki yoyote kwa wana siasa walio mahiri kulazimisha maandamano yafanyike wakati kuna wageni, tena wawekezaji muhimu ambao hakuna nchi katika hii dunia yetu ya sasa isiotaka wawepo au watembelee kwao.

Viongozi wa Chgadema kwa ajili tu ya chuki zao binafsi, wakaona hii ndio fursa ya kuipakaza matope (kama si m*v*) Tanzania. Walijuwa kuwa wawekezaji wakubwa kama hawa wanapokuja tena kwa idadi kubwa kama iliowasili hapa, lazima kuna waandishi wa habari wa kimataifa hususan wa mambo ya kibiashara na pia kuna watu wa intelijensia za kibiashara ambao misafara kama hiyo huwa hawakosekani.

Kwa namna ya maisha tunayoishi wa Tanzania au kwa mpenda amani yoyote, hata kama mna ugomvi wenu wa ndani, ajapo mgeni, tena ambae anaweza kuleta manufaa nyumbani kwenu, huwa mnasitisha ugomvi kwa siku mbili tatu mpaka mgeni aondoke. Haya hutokea hata majumbani mwetu, tukipapurana na bahati nzuri au mbaya mgeni akibisha hodi basi mara nyingi kwa wenye akili husitisha kupapurana kwao, wakamhudumia mgenina ikibidi kupapurana, wataendelea mgeni akisha ondoka.

Leo Chadema wameonyesha sura gani ya nchi yetu, kwa kulazimisha maandamano yaliyositishwa na Mkuu wa Polisi, mbele ya hawa wageni?

Nna uhakika, sura walioionyesha si nzuri, lakini, ni matumaini yangu kuwa wenyeji, waliowaalika hawa wageni, wataweza kuwafahamisha ukweli ulivyo na wataridhia si tu kuja tena kutembelea Tanzania, bali na kuwekeza kwa wingi, kwani kwa sasa bado tunahitaji mitaji ya nje.

Nawaomba wa Tanzania walaani kitendo cha viongozi wa Chadema baada ya kuuelewa huu ukweli wa kwanini hawa viongozi walilazimisha maandamano yafanyike.

Mungu awalaze popote apendapo Marehemu waliofarik.
wageni wanahusika nini na maandamano.
 
Waliosababisha mauaji Arusha ambao wanapaswa kufikishwa kwenye mahakama ya kimataifa hawa hapa:
Mkurugenzi wa jiji la Arusha - huyu ndiye aliitisha uchaguzi kinyemela
Katibu wa Bunge - Aliyetoa barua kuidhinisha kuwa mbunge wa viti maalum Tanga anaruhusiwa kupiga kura katika uchaguzi wa meya Arusha.
Mbunge wa viti maalumu Tanga - huyu alipiga kura wakati akijua fika kuwa yeye hastahili.
RPC Arusha - Kwa kuidhinisha matumizi ya risasi za moto.
IGP - Kwa kuwa kigeugeu mara anaruhusu mkutano mara bila taarifa rasmi atauzuia na pia kuidhinisha polisi kutumia risasi za moto dhidi ya raia wasiokuwa hata na rungu.
Madiwani wote wa CCM Arusha - kwa kukubali kushiriki uchaguzi waliojua fika kuwa si halali (hapa namuondoa huyu aliyejitoa CCM baada ya mauaji maana ametambua na kujutia makosa yake; huyu ni shahidi muhimu na yabidi alindwe).
JK - Kwa` kuwa yeye ndiye kiongozi wa nchi na kwa vyovyote polisi hawawezi kutumia risasi kuwaua raia bila yeye kuafiki. Kama kweli hakuafiki, amfukuze kazi mara moja IGP na RPC Arusha.
Makamba - kwa uchochezi na kutosikiliza ushauri, Hakika naamini uchunguzi wa kina utakuja kuonyesha kuwa Makamba ndiye archtect wa uvurugaji wa uchaguzi wa meya wa Arusha, ndiye alitoa maelekezo namna CCM wataweza kutumia nguvu ya dola kufanya hivyo.
Kila mtu aongezee/au apunguze kwenye orodha na sababu.
 
Waziri wa mambo ya ndani( shamsi vuai nahodha) Kwa kuwa jeshi la polisi liko chini yake na alimruhusu mwema kufanya alichofanya.
 
Back
Top Bottom