Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,721
- 21,778
Inspekta wa polisi auawa kwa kudhaniwa mwizi
Na Suzy Butondo, Shinyanga
INSPEKTA mkaguzi wa polisi, George Libenti, 36, ameshambuliwa kwa kipigo na wananchi wenye hasira kali kwa kudhaniwa kuwa ni mwizi na kusababishiwa maumivu makali na baadaye kufariki siku iliyofuata.
Tukio hilo lilitokea Novemba 13, majira ya saa 1.30 usiku katika eneo la Ndembezi lililo kwenye manispaa ya Shinyanga baada ya askari huyo kudaiwa ingia kwenye makazi ya watu kwa nguvu na kulazimisha kuingia ndani ya nyumba.
Kuona hivyo, wakazi hao walianza kupiga kelele za kuomba msaada na ndipo watu walipokusanyika na kuanza kumshambulia kabla ya kutoa taarifa polisi za kuomba msaada. Polisi walifika eneo hilo muda mfupi baadaye.
Kamanda wa polisi wa mkoani hapa, Daudi Siasi alisema kuwa askari walivyopigiwa simu, walienda eneo la tukio lakini walipofika waligundua kuwa mtu aliyedhaniwa kuwa mwizi ni inspekta wa polisi ambaye walimkuta akiwa amelewa na kumpeleka kituoni.
Kamanda Siasi alisema inspekta huyo alikuwa na matatizo ya akili na kwamba alikuwa hapangiwa kazi za kipolisi kutokana na matatizo hayo ingawa alikuwa akiendelea kutambuliwa kuwa mfanyakazi wa jeshi hilo. Alisema chanzo cha kifo cha Inspekta huyo bado kinautata kama kilitokana na maumivu aliyoyapata kutokana na kipigo cha wananchi ama ni matatizo mengine. Tayari mwili wa marehemu umesafirishwa kwenda Bukoba kwa ajili ya mazishi ambayo yatafanyika leo.
INSPEKTA mkaguzi wa polisi, George Libenti, 36, ameshambuliwa kwa kipigo na wananchi wenye hasira kali kwa kudhaniwa kuwa ni mwizi na kusababishiwa maumivu makali na baadaye kufariki siku iliyofuata.
Tukio hilo lilitokea Novemba 13, majira ya saa 1.30 usiku katika eneo la Ndembezi lililo kwenye manispaa ya Shinyanga baada ya askari huyo kudaiwa ingia kwenye makazi ya watu kwa nguvu na kulazimisha kuingia ndani ya nyumba.
Kuona hivyo, wakazi hao walianza kupiga kelele za kuomba msaada na ndipo watu walipokusanyika na kuanza kumshambulia kabla ya kutoa taarifa polisi za kuomba msaada. Polisi walifika eneo hilo muda mfupi baadaye.
Kamanda wa polisi wa mkoani hapa, Daudi Siasi alisema kuwa askari walivyopigiwa simu, walienda eneo la tukio lakini walipofika waligundua kuwa mtu aliyedhaniwa kuwa mwizi ni inspekta wa polisi ambaye walimkuta akiwa amelewa na kumpeleka kituoni.
Kamanda Siasi alisema inspekta huyo alikuwa na matatizo ya akili na kwamba alikuwa hapangiwa kazi za kipolisi kutokana na matatizo hayo ingawa alikuwa akiendelea kutambuliwa kuwa mfanyakazi wa jeshi hilo. Alisema chanzo cha kifo cha Inspekta huyo bado kinautata kama kilitokana na maumivu aliyoyapata kutokana na kipigo cha wananchi ama ni matatizo mengine. Tayari mwili wa marehemu umesafirishwa kwenda Bukoba kwa ajili ya mazishi ambayo yatafanyika leo.