Asubuhi ya leo nimefika ofisini na kukaa chini kuanza kazi.
Kama kawaida ya siku za kawaida baada ya kupata kifungua kinywa katika mgawaha katikati ya jiji la Dar nikaona leo ni siku ya kuchapa kazi kwa nguvu zote. Ilipotimu mida ya saa nne asubuhi ameingia mfanyakazi mwenzangu wa kike na tumekuwa tukifahamiana kwa muda mrefu hapa kijiweni (kazini). Dada huyu mzuri na amejaaliwa kimaumbile na ni msomi tulisoma wote pale kwenye mlima wa dar. Kwa bahati mbaya au nzuri amekuwa katika mahusiano ya muda mrefu bila ya mafanikio ya kupata mtu aliyeserious katika maisha yake. Kwa bahati mbaya au nzuri mie sio katika hao waliobahatika kumpata ijapokuwa nilivutiwa naye sana chuoni.
Imepita miaka tumekutana ofisini na kufanya kazi pamoja na tumekuwa marafiki wa karibu sana. Mie binafsi nimepata mwenza na tunafurahia ndoa yetu kwa muda mrefu nashukuru mungu. Karibuni, kwa kipindi cha mwezi nyuma dada yangu huyu alinifuata kwa ushauri kuhusu mpenzi wake anayeishi naye muda mrefu ila hana shukrani na anamsaliti ijapokuwa anampenda sana. Binafsi nilichomshauri ni kwamba mimi siwezi kumshauri kuhusu jambo lililokuwa moyoni mwake isipokuwa ingelikuwa mie binafsi sitapendelea kuwa mtumwa wa kupenda kwasababu mapenzi ni sharing responsibility. Isitoshe, mwanaume au mwanamke anayemsaliti mkewe au mumewe hafai kuwa mumeo au mkeo. Ikiwa utaruhusu mtu akutawale kifikra utakuwa mtumwa wa mapenzi na inaweza kukuathiri kimaendeleo, kifikra na kiafya pia.
Nikasikia ofisini ameachana na mchumba wake (ijapokuwa hakunifuata kunitaarifu mwenyewe) na anatafuta mchumba wa kuishi nae maisha. Leo ndio amenifuata ofisini na kuniomba kitu sijapata kusikia maishani. Amenitaka radhi sana nisije kumuona muhuni ila ameniomba nizae nae tu halafu majukumu ya mtoto yeye atayamudu mwenyewe pasina kunisumbua. Kali ya yote ameniambia sina haja ya kufanya naye tendo la ndoa ila naweza kumpatia maji yangu ya uzazi kuna kliniki South Africa ataenda kuziweka katika mfuko wake wa uzazi.
Nikaona wacha nifikiri kwanza maana hii kali!!!!
a. Nikizaa naye atanihakikishia vp hatonisumbua katika malezi ya mtoto hata kama maisha yakibadilika baadae?
b. Mke wangu akisikia nimezaa nje ya ndoa (wanawake wa kiafrika na fikra zao tunawajua wenyewe) si itakuwa kasheshe la nguvu?
c. Je nikimkatalia urafiki wetu utaendelea au ndio utageuka kuwa uadui?
d. Je mtoto akitaka kumjua baba yake au baba akiwa anataka kumufahamu mtoto itakuwaje?
Naona ninapata masuali mengi kuliko majibu nawaulizeni nyie Je ingelikuwa wewe ungelifanyaje kwasababu ameumbika huyu dada na angelikuwa anataka za chap chap ningelimpa ila hili la mtoto mh?
Kama kawaida ya siku za kawaida baada ya kupata kifungua kinywa katika mgawaha katikati ya jiji la Dar nikaona leo ni siku ya kuchapa kazi kwa nguvu zote. Ilipotimu mida ya saa nne asubuhi ameingia mfanyakazi mwenzangu wa kike na tumekuwa tukifahamiana kwa muda mrefu hapa kijiweni (kazini). Dada huyu mzuri na amejaaliwa kimaumbile na ni msomi tulisoma wote pale kwenye mlima wa dar. Kwa bahati mbaya au nzuri amekuwa katika mahusiano ya muda mrefu bila ya mafanikio ya kupata mtu aliyeserious katika maisha yake. Kwa bahati mbaya au nzuri mie sio katika hao waliobahatika kumpata ijapokuwa nilivutiwa naye sana chuoni.
Imepita miaka tumekutana ofisini na kufanya kazi pamoja na tumekuwa marafiki wa karibu sana. Mie binafsi nimepata mwenza na tunafurahia ndoa yetu kwa muda mrefu nashukuru mungu. Karibuni, kwa kipindi cha mwezi nyuma dada yangu huyu alinifuata kwa ushauri kuhusu mpenzi wake anayeishi naye muda mrefu ila hana shukrani na anamsaliti ijapokuwa anampenda sana. Binafsi nilichomshauri ni kwamba mimi siwezi kumshauri kuhusu jambo lililokuwa moyoni mwake isipokuwa ingelikuwa mie binafsi sitapendelea kuwa mtumwa wa kupenda kwasababu mapenzi ni sharing responsibility. Isitoshe, mwanaume au mwanamke anayemsaliti mkewe au mumewe hafai kuwa mumeo au mkeo. Ikiwa utaruhusu mtu akutawale kifikra utakuwa mtumwa wa mapenzi na inaweza kukuathiri kimaendeleo, kifikra na kiafya pia.
Nikasikia ofisini ameachana na mchumba wake (ijapokuwa hakunifuata kunitaarifu mwenyewe) na anatafuta mchumba wa kuishi nae maisha. Leo ndio amenifuata ofisini na kuniomba kitu sijapata kusikia maishani. Amenitaka radhi sana nisije kumuona muhuni ila ameniomba nizae nae tu halafu majukumu ya mtoto yeye atayamudu mwenyewe pasina kunisumbua. Kali ya yote ameniambia sina haja ya kufanya naye tendo la ndoa ila naweza kumpatia maji yangu ya uzazi kuna kliniki South Africa ataenda kuziweka katika mfuko wake wa uzazi.
Nikaona wacha nifikiri kwanza maana hii kali!!!!
a. Nikizaa naye atanihakikishia vp hatonisumbua katika malezi ya mtoto hata kama maisha yakibadilika baadae?
b. Mke wangu akisikia nimezaa nje ya ndoa (wanawake wa kiafrika na fikra zao tunawajua wenyewe) si itakuwa kasheshe la nguvu?
c. Je nikimkatalia urafiki wetu utaendelea au ndio utageuka kuwa uadui?
d. Je mtoto akitaka kumjua baba yake au baba akiwa anataka kumufahamu mtoto itakuwaje?
Naona ninapata masuali mengi kuliko majibu nawaulizeni nyie Je ingelikuwa wewe ungelifanyaje kwasababu ameumbika huyu dada na angelikuwa anataka za chap chap ningelimpa ila hili la mtoto mh?