Ingekuwa vipi kama mkeo naye akakugeuzia kibao

WomanOfSubstance

JF-Expert Member
May 30, 2008
5,457
956
Kumekuwepo na majadiliano ya kutosha sana humu jamvini kuhusu matatizo ya wanawake na waume au wapenzi wao - Kutelekezwa, kuletewa nyumba ndogo,kuachiwa mzigo wa kulea familia, kutumiwa n.k.Pia tumejadili kuhusu kwanini wanaume hawapendi ushirika kwenye mapenzi.

Tunajua kabisa kuwa tamaduni, mila, desturi, dini vyote vinaamrisha wanandoa kuheshimu ndoa zao.Pamoja na hayo ukweli unabakia kuwa wanandoa hutetereka katika kuheshimu viapo vyao.Msisitizo zaidi uko katika kuwataka wanawake wajiheshimu na inashangaza kuwa msisitizo hauko zaidi katika kuwabana wanaume.Kutokana na hili, wanaume nao wamekuwa wakilega zaidi katika kuheshimu ndoa au mahusiano yao.

Matokeo yake ni kuwa watu wamekuwa wakifumbia macho suala zima la kutoka nje ya ndoa.Hakuna mwanamke anakubali kuwa wanawake nao wanatetereka , na hata wanaume nao wanajidanganya kuwa wapenzi wao au hata wake zao hawatoki nje ya ndoa.Ila hapohapo tunasikia ati vipimo vya DNA vimethibisha kuwa idadi kubwa ya watoto waliozaliwa na wazazi waliokuwa na mabishano kuhusu nani baba wa mtoto - wameonekana siyo wa akina baba hao walengwa.

Je, Mwanaume anayetoka nje ya ndoa na mke wa mtu au mpenzi wa mtu mwingine anajisikia vipi pale mkewe akichukuliwa na mwanaume mwingine?
 
Last edited:
...WoS, atayeanza ku cheat ndiye anayepaswa kulaumiwa, lakini kwa jinsi ulivyoliweka swali;


...tayari ushatoa 'dira' jibu liwe; Mwanaume, au?

Hii mada nataka kuchokoza kupata mawazo ya wanaume maana assumption ni kuwa wanawake hawatoki nje ya ndoa ( japo inajulikana kuwa wanatoka)lakini hapo hapo inajulikana kuwa wanaume wanatoka tena wakati mwingine na wake za watu au wapenzi wa watu wengine.
 
Dada wa kulaumiwa hapo ni anayetoka nje ya ndoa wa kwanza ingawa mie siamini katika kutoka nje nawe kama njia ya kulipiza kisasi. Ni kweli kuwa wapo wanawake wanaoanza na ukakuta mumewe yuko msafi but vyovyote vile hata kama utatoka nje baada ya mumeo kutoka nawe pia wastahili lawama.

Niaminivyo mie katika ulimwengu huu wa magonjwa mumeo akitoka nje ya ndoa huyo hakufai kwani si mwaminifu tena (si wanasema akishaonja kutoka nje hawezi acha?) sasa hii toka toka mwisho ataingia na maradhi muache watoto wakiteseka bila wazazi.

Mimi bado nafikiri kuwa kama huwa kuna adhabu ya mtu anayeambukiza virusi vya UKIMWI kwa makusudi basi hata mume/mke atakayeleta UKIMWI ndani ya familia anapaswa aadhibiwe iwapo itathibitika kuwa aliupata kutokana na mahusiano ndani ya ndoa badala ya kukaa na kupozana kuwa tulieni muishi kwa matumaini. Kwa sababu alipokuwa anatoka nje then anakuja back na kutotumia kinga maana yake ni nini? Si kukuua makusudi? Ah sijui hata kama nimeongea ndivyo.
 
Mimi bado nafikiri kuwa kama huwa kuna adhabu ya mtu anayeambukiza virusi vya UKIMWI kwa makusudi basi hata mume/mke atakayeleta UKIMWI ndani ya familia anapaswa aadhibiwe iwapo itathibitika kuwa aliupata kutokana na mahusiano ndani ya ndoa badala ya kukaa na kupozana kuwa tulieni muishi kwa matumaini. Kwa sababu alipokuwa anatoka nje then anakuja back na kutotumia kinga maana yake ni nini? Si kukuua makusudi? Ah sijui hata kama nimeongea ndivyo.
Mj1,
UKIMWI unapoingia kwenye familia mara nyingi siyo rahisi kujua umeingia lini...mpaka uje uhisi au hata kujua kuwa mwenzio hayuko mwaminifu, labda virusi vilishaingia siku nyingi sana. Na suala la kuvaa kinga, hivi ndugu yangu ushasikia mwanaume akakubali kuambiwa avae kinga hata kama mke anamhisi?
Nimeshuhudia ugomvi wa ajabu kisa mke kaenda kupima afya yake kwa vile alikuwa anajua mumewe ana mwanamke mwingine, majibu yaka +ve na alipoenda kumwambia mumewe - mume akawa mkali kama nyati aliyejeruhiwa akimlaumu mke kwa nini alienda kupima!
 
Dada wa kulaumiwa hapo ni anayetoka nje ya ndoa wa kwanza ingawa mie siamini katika kutoka nje nawe kama njia ya kulipiza kisasi. Ni kweli kuwa wapo wanawake wanaoanza na ukakuta mumewe yuko msafi but vyovyote vile hata kama utatoka nje baada ya mumeo kutoka nawe pia wastahili lawama.

Niaminivyo mie katika ulimwengu huu wa magonjwa mumeo akitoka nje ya ndoa huyo hakufai kwani si mwaminifu tena (si wanasema akishaonja kutoka nje hawezi acha?) sasa hii toka toka mwisho ataingia na maradhi muache watoto wakiteseka bila wazazi.

Mimi bado nafikiri kuwa kama huwa kuna adhabu ya mtu anayeambukiza virusi vya UKIMWI kwa makusudi basi hata mume/mke atakayeleta UKIMWI ndani ya familia anapaswa aadhibiwe iwapo itathibitika kuwa aliupata kutokana na mahusiano ndani ya ndoa badala ya kukaa na kupozana kuwa tulieni muishi kwa matumaini. Kwa sababu alipokuwa anatoka nje then anakuja back na kutotumia kinga maana yake ni nini? Si kukuua makusudi? Ah sijui hata kama nimeongea ndivyo.

Unajua ukweli ni kuwa mume au mke kutoka nje ya ndoa kunakuwa kumesababiswa na mmoja kati yao. Unakuta kila mtu alimzoea mwenzake kwa tabia fulani mara mambo yanabadilika either kutokana na kuzoena sana heshima inapungua ndani ya nyumba, sasa hii inapelekea mmoja kati yao kuweza kujaribu kutoka nje ya ndoa yao!
 
Sidhani kama assumption yako ya kusema wanawake hawatoki nje ya ndoa ni ya ukweli.

Kutoka nje ya ndoa ni tabia ya mtu (anaweza kuwa mwanaume au mwanamke). Tabia hii yaweza kuanza ndani ya ndoa au kabla ya ndoa, kutegemeana na mazingira yalivyo. Assumption yako yaweza kuwa ni ya uvumilivu, namanisha kwamba wanawake wengi (si wote) ni wavumilivu. Ndio maana ndoa nyingi zinazovunjika hutokana na wanaume, yaani mwanaume ndio chanzo ama ametengeneza mazingira ambayo mke kajibu au yeye mwenyewe mwanaume anatenda.

Ninaamini kuna ndoa ambazo ni imara, yaani wanandoa hawatoki nje. Uimara hutengenezwa na pande zote mbili (yaani mume na mke). Ndoa za namna hii ni chache sana. Sijajuwa ndoa yangu itakuwaje? Ninamuomba Mungu iwe kama hii (nzuri).

Ushirikiano baina ya mke na mume ni muhimu sana, asilimia kubwa mume huwa wa kwanza kualibu. Si ndoa zote zinazoharibika (mf kuvunjika, watu kutembea nje ya ndoa) husababishwa na mume. Binafsi nadiliki kusema mwanaume ndio chanzo maana familia nyingi sana huamini mume ni kichwa. Hapa nisieleweke vibaya, kwamba mke hana umuhimu. Mke anaumuhimu kama mume ILA imezoweleka kuwa mume ndio dereva. Sasa, kwanini tumraumu abiria kuanguka kwa gari na si dereva wakati abiria alikuwa ametulia kama maji ya mtungini kule kijijini? Kwa definition ya mume ni kichwa, Lawama zote ni kwa mume.
 
Maadam hakuna mwanaume anayependa ku share, na hapo hapo tunaambiwa wao mara nyingi ndiyo wanaanzisha hayo makasheshe, hatuoni kuwa wao ndiyo wana mchango mkubwa sana kufanya familia zisimame imara? kwanini basi wasitumie nafasi yao kama kichwa na pia ile hulka yao ya wivu na kuchukia ushirika ili kuzuia kuharibu mahusiano ya ndoa?
Kwa wanaume tu: Hivi mnadhani kuna mwanamke anayependa kuchukuliwa mumewe?
 
Hii mada nataka kuchokoza kupata mawazo ya wanaume maana assumption ni kuwa wanawake hawatoki nje ya ndoa ( japo inajulikana kuwa wanatoka) lakini hapo hapo inajulikana kuwa wanaume wanatoka tena wakati mwingine na wake za watu....

...Duuuh, WoS kwa 'ufafanuzi' wako :) wakulaumiwa ni hao wake za watu!
 
WoS
Asante sana kwa mada yako.
Ni ukweli usiopingika kuwa aslimia kubwa ya wanawake nao wanatoka nje ya NDOA zao. Hili halina ubishi! Ni nini kinasababisha haya,
1. Ni matatizo yanayosababishwa na wanandoa wenyewe, kmf, kumhisi mwenzako kuwa ana mahusiano na mtu fulani na bila kufanya uchunguzi basi hutaka kulipiza kisasi. Hili huchangia sana kwa akina mama kuamua tu na mimi wacha nimkomoe.
2. Kuna wale ambao hawatosheki na walichonacho. Nasema hawatosheki kwa sababu hawapati kile wanachokitegemea toka kwa mwenzie. Niliwahi kusema katika mada nyingine kuwa wengi huwa hatuweki mambo hadharani kabla ya kuona. Mathalani, utakuta kipindi fulani pale Jangwani wengi wa mabinti zetu pale walikuwa wanaliwa hii mnayoita T*Go. Sasa mtu kama huyu akiolewa na bahati mbaya mwoaji asigundue kuwa bibie anapenda hii kitu, basi lazima akamtafute mtaalamu. Hali kdhalika mwanaume akiyekwisha onjeshwa haka ka mchezo lazima atafute mwanamama wa kujalia hii hali.
Hapo ni lazima wote walaumiwe kwa kutojua mwenzako anataka nini. Nilikuwa na rafiki yangu fulani alikuwa na gf wake, akawa anampa shughuli kweli kweli, bahati mbaya walipomaliza shule jamaa akaingia mjini kusaka pesa na demu akaendelea na chuo. Huko chuoni akampata msomi mwenzake, mwisho wakaoana kabisa. Lakini baadae bibie akagundua anakosa raha, raha fulani hivi, inapatikana wapi? Flash back! Akaanza kufanya uchunguzi wa jamaa yake wa shuleni. Alipogundua alipo zikaanza safari uongo na fikiria kuwa anapanda ndege toka dar to arusha, just to have fun na jamaa over weekend then jumapili jioni huyoooo anarudi dar kwa mumewe. Someni alama za nyakati mtagundua tu!
3. Tamaa,,,, bbadhi ya wanawake huwa na tamaa ya hivi ama vile. Kwa kutizama kuwa Kidawa kila siku ana kanga mpya basi nao hujiingiza kwenye kamchezo kabovu. Huku pia utakuta kuna majanaume ambayo yamekolezwa na mijimama kwa kununuliwa vitu mbalimbali na hivyo kujenga tabia tegemezi. Kwa hili hata Wos utakuwa ushasikia huko bongo list flani hivi nilisoma ya RED CARS.
4. Hili la kuwa na watoto ambao si wa mme uliyenaye halikuanza leo. Mila na tamaduni za wazee wetu zilitaka hivyo. Wakati wa unyago kwa baadhi ya makabila yetu yalimfunda mwali kuwa anatakiwa kuwa na angalao mtoto mmoja wa mwanaume mwingine ili hata kama kutatokea laana kwenye ukoo wa huyu baba aliye naye basi huyo wa nje ya ndoa atabaki kuendeleza jina la huyu baba mwenye familia. Hivyo nayo jamii inatakiwa kulaumiwa kwa mafunzo hayo
Kimsingi niseme kuwa mengi ya matatizo haya husababishwa na wanandoa wenyewe.
Hauwezi kila siku unamsema mwezako,,, we malaya, we hivi halafu utegemee kuwa hali itabakia hiyo hiyo. Huyo unayemwita malaya basi iko siku ataamua kujua umalaya ni nini!
Njia bora ni pale unapogundua tatizo la mwenzako na ukawa na uhakika na tuhuma zako ukaamua kuvaa moyo ya kijasiri na kumweleza a-z halafu mkakubaliana kwa amani na upendo. Ni ngumu mtuhumiwa kukubali lakini ujumbe unakuwa umeshafika kwa mtuhumiwa.
 
Je, Mwanaume anayetoka nje ya ndoa na mke wa mtu au mpenzi wa mtu mwingine anajisikia vipi pale mkewe akichukuliwa na mwanaume mwingine?

Hapo talaka 3 na kuondoka na rambo mkononi kwenu.
 
hakuna mwanaume anaetakaga ku share mpenzi/mke wake na mwanaume mwenzie, hakutakalika! akikuhic tu ni tabu ijekuwa kujua ukweli?

WoS
Asante sana kwa mada yako.
Ni ukweli usiopingika kuwa aslimia kubwa ya wanawake nao wanatoka nje ya NDOA zao. Hili halina ubishi! Ni nini kinasababisha haya,
1. Ni matatizo yanayosababishwa na wanandoa wenyewe, kmf, kumhisi mwenzako kuwa ana mahusiano na mtu fulani na bila kufanya uchunguzi basi hutaka kulipiza kisasi. Hili huchangia sana kwa akina mama kuamua tu na mimi wacha nimkomoe.
2. Kuna wale ambao hawatosheki na walichonacho. Nasema hawatosheki kwa sababu hawapati kile wanachokitegemea toka kwa mwenzie. Niliwahi kusema katika mada nyingine kuwa wengi huwa hatuweki mambo hadharani kabla ya kuona. Mathalani, utakuta kipindi fulani pale Jangwani wengi wa mabinti zetu pale walikuwa wanaliwa hii mnayoita T*Go. Sasa mtu kama huyu akiolewa na bahati mbaya mwoaji asigundue kuwa bibie anapenda hii kitu, basi lazima akamtafute mtaalamu. Hali kdhalika mwanaume akiyekwisha onjeshwa haka ka mchezo lazima atafute mwanamama wa kujalia hii hali.
Hapo ni lazima wote walaumiwe kwa kutojua mwenzako anataka nini. Nilikuwa na rafiki yangu fulani alikuwa na gf wake, akawa anampa shughuli kweli kweli, bahati mbaya walipomaliza shule jamaa akaingia mjini kusaka pesa na demu akaendelea na chuo. Huko chuoni akampata msomi mwenzake, mwisho wakaoana kabisa. Lakini baadae bibie akagundua anakosa raha, raha fulani hivi, inapatikana wapi? Flash back! Akaanza kufanya uchunguzi wa jamaa yake wa shuleni. Alipogundua alipo zikaanza safari uongo na fikiria kuwa anapanda ndege toka dar to arusha, just to have fun na jamaa over weekend then jumapili jioni huyoooo anarudi dar kwa mumewe. Someni alama za nyakati mtagundua tu!
3. Tamaa,,,, bbadhi ya wanawake huwa na tamaa ya hivi ama vile. Kwa kutizama kuwa Kidawa kila siku ana kanga mpya basi nao hujiingiza kwenye kamchezo kabovu. Huku pia utakuta kuna majanaume ambayo yamekolezwa na mijimama kwa kununuliwa vitu mbalimbali na hivyo kujenga tabia tegemezi. Kwa hili hata Wos utakuwa ushasikia huko bongo list flani hivi nilisoma ya RED CARS.
4. Hili la kuwa na watoto ambao si wa mme uliyenaye halikuanza leo. Mila na tamaduni za wazee wetu zilitaka hivyo. Wakati wa unyago kwa baadhi ya makabila yetu yalimfunda mwali kuwa anatakiwa kuwa na angalao mtoto mmoja wa mwanaume mwingine ili hata kama kutatokea laana kwenye ukoo wa huyu baba aliye naye basi huyo wa nje ya ndoa atabaki kuendeleza jina la huyu baba mwenye familia. Hivyo nayo jamii inatakiwa kulaumiwa kwa mafunzo hayo
Kimsingi niseme kuwa mengi ya matatizo haya husababishwa na wanandoa wenyewe.
Hauwezi kila siku unamsema mwezako,,, we malaya, we hivi halafu utegemee kuwa hali itabakia hiyo hiyo. Huyo unayemwita malaya basi iko siku ataamua kujua umalaya ni nini!
Njia bora ni pale unapogundua tatizo la mwenzako na ukawa na uhakika na tuhuma zako ukaamua kuvaa moyo ya kijasiri na kumweleza a-z halafu mkakubaliana kwa amani na upendo. Ni ngumu mtuhumiwa kukubali lakini ujumbe unakuwa umeshafika kwa mtuhumiwa.


YAANI!Eeka Mangi umezoza kimwaukwelini kabisa!
Uliyoyaainisha ndiyo hasa matatizo ya ndoa nyingi...mchanganyiko wa matatizo yaletwayo na akina baba, yale ya akina mama na yale yakimfumo ( mila na desturi).Nadhani wandoa wengi wanaingia kwenye ndoa bila kujua uzito wa suala zima la kufunga pingu.Wengi huoana kama fashion tu na ndiyo maana inapofikia mahali vishawishi havikwepeki maana uzito wa kile kiapo cha uaminifu haupo mioyoni.

Hili la mila, ni kweli - jamii nyingi zina hayo mafundisho - kuna mafiga matatu, kuna jamii nyingine humwambia bibi harusi " asishangae shemeji akimtaka, ni kitu cha kawaida ila asimwambie mumewe! Sasa kama shemeji naruhusiwa ni kwa vipi mtu atamkataa mwanaume mwingine? halafu kuna hili la kuambiwa usiweke mayai yako yote kikapu kimoja - kwa maana ujaribu kupata ujauzito wa mtu mwingine asiye mumeo just in case mumeo ana hitilafu za kinasaba.Jamani ni vizuri tukazungumzia haya masuala maana inatusaidia kujua chanzo cha tatizo na hata kupata ufumbuzi.Je akina baba mlikuwa mnayajua haya?
 
Maadam hakuna mwanaume anayependa ku share, na hapo hapo tunaambiwa wao mara nyingi ndiyo wanaanzisha hayo makasheshe, hatuoni kuwa wao ndiyo wana mchango mkubwa sana kufanya familia zisimame imara? kwanini basi wasitumie nafasi yao kama kichwa na pia ile hulka yao ya wivu na kuchukia ushirika ili kuzuia kuharibu mahusiano ya ndoa?
Kwa wanaume tu: Hivi mnadhani kuna mwanamke anayependa kuchukuliwa mumewe?

Kwani wewe hujui kuwa wanawake wako too emotional, sasa mwanamke akitoka nje ya ndoa ndio ujue ataendelea tu!
 
Hili la mila, ni kweli - jamii nyingi zina hayo mafundisho - kuna mafiga matatu, kuna jamii nyingine humwambia bibi harusi " asishangae shemeji akimtaka, ni kitu cha kawaida ila asimwambie mumewe! Sasa kama shemeji naruhusiwa ni kwa vipi mtu atamkataa mwanaume mwingine? halafu kuna hili la kuambiwa usiweke mayai yako yote kikapu kimoja - kwa maana ujaribu kupata ujauzito wa mtu mwingine asiye mumeo just in case mumeo ana hitilafu za kinasaba.Jamani ni vizuri tukazungumzia haya masuala maana inatusaidia kujua chanzo cha tatizo na hata kupata ufumbuzi.Je akina baba mlikuwa mnayajua haya?

Si kwamba hatuyajui Wos, tunayajua sana ndo maana huwa tukimbilia kwenye hukumu bila kutafakari kosa ni la nani. Kama tungekuwa tunajiuliza kabla ya maamuzi basi tungefanikiwa angalao kidogo kupunguza.
Ila pia kuna mahali ambapo hatuwezi kupunguza. Hili ni tatizo lisiloisha, kwa mwanamume na mwanamke pia. Mfano kuna dada anapenda wanaume wenye maumbile makubwa,,,, hii ndo raha yake na ameolewa na ndoa ya kanisani. Bwana amesema amechoka naye kaamua kujitafutia ka small house kake na mama amnajua lakini hajali na anaraha ka nini, tena anamsifia mumewe kwa kuwa na kabinti kadogo. Mara utamsikia anasema aah baba nanii kwa kulenga shabaha hajambo ila wala hata simsikii akiingia anantia shombo tu, lakini nikistuka nna mimba. Hadi saa ingine utamsikia akiwaambia shoga zake hii mimba sijua na ya mume wangu? Maana kama sikumbuki siku nilolala naye hivi.
Bahati nzuri huwa anatoa kidogo copy ya jamaa sijui huko kwa DNA.
 
"MEN FALL IN LOVE THRU SEX, WOMEN FALL IN SEX THRU LOVE...." Nyamayao

Hiyo signature ya Nyamayao inaelezea kwa kiasi kikubwa tofauti ya mwanaume na mwanamke linapokuja suala la kutoka nje ya ndoa.

Ili mwanamke aweze ku-enjoy tendo la ndoa, ni lazima kwanza ampende mwanaume anayefanya nae tendo la ndoa. Mwanaume ni tofauti. Anaweza ku-enjoy tendo la ndoa hata kama hajampenda huyo mwanamke. Kwa mantiki hii, tafsiri ya mwanamke kutoka nje ya ndoa ni tofauti na mwanaume kutoka nje ya ndoa.

Kama mwanamke ametoka nje ya ndoa na ana-enjoy tendo la ndoa huko nje basi lazima mapenzi yake yatakuwa yameshift kwa kiasi kikubwa ukulinganisha na mwanaume anayetoka nje ya ndoa.

Hata hivyo kutoka nje ya ndoa ni tendo baya na lisilofaa iwe kwa mwanamke au mwanaume.
 
Hiyo signature ya Nyamayao inaelezea kwa kiasi kikubwa tofauti ya mwanaume na mwanamke linapokuja suala la kutoka nje ya ndoa.

Anaweza ku-enjoy tendo la ndoa hata kama hajampenda huyo mwanamke. Kwa mantiki hii, tafsiri ya mwanamke kutoka nje ya ndoa ni tofauti na mwanaume kutoka nje ya ndoa.
Kama mwanamke ametoka nje ya ndoa na ana-enjoy tendo la ndoa huko nje basi lazima mapenzi yake yatakuwa yameshift kwa kiasi kikubwa ukulinganisha na mwanaume anayetoka nje ya ndoa.
Kwani ni lazima mwanamke ampende huyo mtu wa nje? na kwani akimpenda kuna ubaya gani assuming kuwa na mwanamme wake ana nyumba ndogo na kahamishia majeshi yote na huduma zote kule.( just playing the devil's advocate)
 
Back
Top Bottom