Ingekuwa ma-rais wanaazimwa kwa muda, mi ningempendekeza kagame aje tz

Atleast umetueleza wadau kile ambacho mtoa mada amekificha kwa makusudi, kwa nyongeza tu ni kuwa anamiliki jet mbili zilizonunuliwa kwa fedha ya serikali, zinatumika kwenda kusalimia familia yake ulaya, ana ukabila kupita rais yeyote: washitakiwa na wahanga wengi wa kisiasa ni wahutu. Sasa hivi hapendi kutoka nje kwani unyanyasaji anaowafanyia raia wake unaweza mtokea puani...............:......................................
Mkuu naona unajichanganya hapo kwenye red, benz sio gari la kifahari? na hapo kwenye blue jaribu kuandika vizuri hii thread yako, Paul Kagame the new Hitler
 
Bongo tuna rais mwimbaji taarabu,mpaka Ambi usoni na kuweka kanta kichwani,mvivu kusoma na anaongea chochote ilimradi siku zinakwenda.
 
Mkuu umenichekesha sana Reference zako za maendeleo, facebook na Google sio maendeleo Google ni search engine wachina wanazo kibao, na facebook ni mtandao wa kijamii kama vile JF wachina wanayo mingi tu, kingine hiyo data ya watu tillioni kadhaa sijui umeitoa wapi dunia mpaka sasa ina watu 7 billion, China ina watu 1,341 billion, turudi Rwanda wapo wachache ina watu 11 million tu

Unataka kusema watu wa china ni wengi kuliko watu wa duniani? Embu weka sawa hizo takwimu zako. Ni watu 1.341 billion na sio 1,341 billion hapo kuna nukta sio mkato.
 
CPA kweli umekua mateka wa propaganda za kagame akisaidiwa na marekani na nchi za magharibi! Pole sana mdogo wangu! Kwa taarifa yako hakuna kiongozi balaa kwa mustakabali wa taifa lake kama kagame! Kwanza uliyoongea mengi sio kweli!,

Nikianza na kubwa la kukomesha ukabila hajafanya la maana! Anakandamiza sana wahutu na anajaribu kuweka chuki zaidi kwa kuhubili na kuonesha mafuvu kwamba wahutu ni wauaji wakati yeye ndio muuaji mkubwa! Kwenye safu ya uongozi wa juu na jeshini hakuna wahutu na mhutu yeyote mwenye pesa atazushiwa lolote ili afilisiwe na kufungwa ikibidi! Kagame ni mkabila kwa vitendo ndio maana hawezi kukomesha ukabila kwa maneno!

Mpango wa miaka hamsini umeusoma?, ni mzuri? Au kwako kuwepo mpango tu hata kama ni mpango kandamizi ni jambo la kusifiwa?

Kuhusu reli nakuomba CPA acha uzushi!, kwa haijaanza kujengwa pili sio yeye bali ni jumuia ya africa mashariki!, ni mpango wa nchi zote husika. Hata umeme utazalishwa rusumo kwa mpango huo huo!

Kwenye kikao kilichopita hakuja kwa sababu mwenyekiti alikua mhutu, rais wa burundi!

Pili, maendeleo yanayosemwa sio sawa na hali halisi wala hayajazidi yaliyokuwepo wakati wa Habyarimana! Kagame amewekwa na marekani kama mlango wa kuingilia kongo. Si unajua kipindi cha habyarimana rwanda na mobutu congo, marekani ilikua haifaidiki sana congo? Jamaa ni bonge la kibaraka!

Mji wa kigali ni mji mdogo sana, unaweza kutembea kwa miguu ukafika kila kona ndani ya siku moja! Haufikii hata robo ya Dar!, ni kama singida au kahama vile kwa ukubwa!

Mimi nilikuwepo wakati wa majeshi ya Rwanda yaliyomsaidia marehemu Kabila ....Nenda Katanga province na wacongo watakuambia jeshi la Kagame lilileta nidhamu kabisa na kuweza kusimamisha ufisadi uliokithiri RDC...

Rwanda ya leo bana ni toafauti kabisa na ya Habariyamana hakuna ujinga wa kuhongana kama bongo sheria ni msumeno bana mafisadi wanaogopa Rwanda bana na hiyo ni fact.

Unaweza kuhonga polisi Burundi,DRC au bongo lakini sio Rwanda.....nasema hivyo kwa sababu nemeenda Rawnda kabla ya Kagame na baada ya Kagame.

Naamini udikteta wa uzalendo Africa tunauhitaji......Jiulize watu wanatumia mapesa mengi mno kwenye kampeni mafano mmoja Nigeria Million Dollar 200 kutafuta u -Rais..ili iweje?

Kwa kifupi kila kiongozi anweza kuwa na mapungufu lakini jiulize amefanya nini kwa maendeleo ya nchi....Kama sio Kagame Rwanda ingekuwa kama Somalia...hata hivyo kunwa Watusi wa siasa kali hawamtaki wanadai anawakumbatia Wahutu.....Na kuna wahutu ambao ni matajiri wa kupita kiasi ambao wako DRC wanatafuta kila mbinu kumwondoa.

Mnaomwita Kagame dikteta ni wasaniii tu.
 
labda na sie tukipigana ndo tutaheshimiana. si unaona kenya sasa hivi wanaheshimiana sana.
Ndio tunapoelekea!.
Wewe chunguza kila sehemu kuanzia ngazi ya kaya hadi viongozi wakuu duniani bila vurugu hasa inapokua hakuna maelewano....suluhisho ndio hilo hilo unaloomba litokee Tz.
Japo sipendi vurugu ...pia nachukia sana war.
 
CPA hapo kwenye blue kuwa makini na kiswahili chako samahani lakini, Kagame muuaji mkubwa wapinzani wake wengi wamekimbia nchi
Bora kagame kaka!
Wananchi wanakula bata! Hata tz wapinzani wakimbie ni bora....kuliko wananchi kua kama walivyo sasa!.
Usichafue hewa kwenye thread hii...
Kagame akitawala Rwanda miaka 27 itakua nchi yake kama ......
Sio Tz ...wazee wanalazimishe kuiongoza nchi...mbaya zaidi wanasema kwa sasa na haya matatizo yote eti wao ndio maendeleo. Sijui wakoje?
 
Back
Top Bottom