inflation, inflation, inflation

Igabiro

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
242
27
[h=6]Tanzania Shilling hits 1823 against US Dollar, Where R we going?[/h]
 
Na hapo ndiyo tujiulize wale wanaodai uchumi wa tz unakua kwa kasi, wanatumia vigezo vipi?
 
Kwakweli hali ni mbaya sana mimi mwenyewe leo nilitaka kununua dola lakini sikuamini rate niliyoikuta kwenye maduka coz juzi tu ilikuwa somewhere around 1730!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Hii maana yake hali itaendelea kuwa ngumu kwa masikini wa nchii hii kwasababu kila kitu kitazidi kupanda bei,please you guys up there who are using our sweat in public offices try to do something about this.
 
Kwa Tafasri ya haraka: Inflation is too much money chasing few goods. '' Pesa nyingi kwenye mzunguko zikikabiliana na uhaba wa bidhaa sokoni'' Sasa hapa ndo ninapokuja kwenye uchumi wetu wa bongo, pesa kwenye mzunguko hakuna, bidhaa kama sukari hakuna sasa inflation inatoka wapi au wamezishikila wao wachache? Napata shaka sana kama Tanzania inaelekea kunako salama. Sitashanga kama tutajikuta tunaipoteza hii amani ambayo tumekuwa tukiimaba kila kukicha. Wanasiasa vigeugeu angalieni sana, I think you have lost the direction so far. Its my opinion I stand to be collected.
 
Hii ndiyo tanzania dhamani ya fedha inashuka, umeme tatizo, inflation juu, wa2 hawana ajira asilimia za kutosha, high importation of china lakini at the end of the day takwimu zinaonyesha uchumi uko juu. Laha sana kuongoza taifa la asilimia kubwa la wa2 wasiojali mambo muhimu kama uchumi, politics etc
 
Kwa Tafasri ya haraka: Inflation is too much money chasing few goods. '' Pesa nyingi kwenye mzunguko zikikabiliana na uhaba wa bidhaa sokoni'' Sasa hapa ndo ninapokuja kwenye uchumi wetu wa bongo, pesa kwenye mzunguko hakuna, bidhaa kama sukari hakuna sasa inflation inatoka wapi au wamezishikila wao wachache? Napata shaka sana kama Tanzania inaelekea kunako salama. Sitashanga kama tutajikuta tunaipoteza hii amani ambayo tumekuwa tukiimaba kila kukicha. Wanasiasa vigeugeu angalieni sana, I think you have lost the direction so far. Its my opinion I stand to be collected.

I think you wanted to say "Corrected". You have a point mkuu, inshu kubwa hapa ni umeme!! kama viwanda havifanyi kazi, nchi haifanyi uzalishaji vya kutosha! Lazima uchumi uende alijojo!! Ngoja labda wabongo safari hii tutapata somo vizuri!
 
Hali ni mbaya yaweza kubadilika tu ikiwa mtanzania mimi nitaamua kubadilika,narudia kusema serikali yetu imeshindwa kukabiliana na hali hii hata kwa kutoa taarifa tu kwa wananchi kuwa hali ya uchumi ni mbaya ili angalau tuweze kutafuta njia mbadala(huku ni kushindwa kukubwa)

Ingekuwa kwa wenzetu hata Bunge lingeitishwa kujadili hali hii lakini hapa kwetu it is nothing but politics!naogopa tukianza kununua USD kwa 2000Tzs.

Hivi nani mwenye ufahamu atuambie shilingi yetu inawezaje kuwa na thamani?

FYI

Gharama za uzalishaji kwa kutumia Generator ni mara tano ya umeme wa Tanesco. Sasa fikiri ni kwa muda gani Nchi yetu inakuwa Gizani?yani namanisha gharama za uzalishaji zimekuwa kubwa mno thus bei nazo zitapanda tu,kuna jamaa mmoja pale Kenya ameamua ku import vitu kutoka China tu kwasababu gharama za uzalishaji ni kubwa kuliko ukiagiza na kuuza.

Mana yangu ni kwamba mimi yani wewe (sisi watanzania)tuanze kufanya vitu vyetu wenyewe ili kuondokana na hali hii, tatizo ni kwamba tunapenda mambo makubwa kuliko uwezo wetu yani tu kuanzia mavazi malazi hata magari yetu wote tunapenda vya nje yani mana yake ni kwamba watanzania tumeshindwa kufanya vya kwetu na hakuna cha kujivunia na kama hali hii ni ndiyo basi shilingi yetu itakuwaje na thamani?tufanye jambo watanzania wenzangu kwajili ya Nchi yetu wenyewe na wajukuu zetu wajao.

Fanya ulinagnifu kati ya maendeleo ya sekta ya kilimo na mifugo na sekta ya maendeleo ya uagizaji magari nchini uone ipi inakua kwa kasi na ipi ina tija kwa watanzania halafu discuss.

Hivi kweli miaka 50 ya uhuru watanzania tumeshindwa kupiga hatua kwenye kilimo?shilingi yetu ipate vp thamani kama hata mchele tuna nunua kwa USD kutoka nje?

Sipendi nichafue hali ya hewa lakini inaniudhi kuona wengi mliosoma kwa lodi za dungu zangu mnaendelea kuwa watumwa wa hindi kwenye viwanda na makampuni yao bila hat ubunifu wowote na mbaya zaidi tunaishia kulalamika bilakuchukua hatua hata za kufanya maandamo kuishinikaza serikali juu ya jambo fulani muhimi kwa Taifa. Nasema hivi wasomi wa nchi hii mna deni kubwa sana kwa watanzania,poleni sana kwa kutotimiza wajibu wenu.

Inaniuma kuona tunakuwa watumwa wa labtop na makampuni mikubwa ya sim za mikoni kwa kipindi kifupi tu cha kama miaka 15 hivi ukilinganisha na miaka 50 ya kilimo kisicho endelea,kama juhudi hizi za ku adapt haya mambo ya technology tunge apply kwenye kilimo hizi hadithi wala zisingekuwepo hakyanani mimi nawambia.

FYI

Kwa hali hii iliyopo wale tu watakao jihusisha na masula ya kilimo na mifugo ndio watakaoepuka mtikisiko wa uchumu uliokwisha piga hodi nchini,hujachelewa ndg yangu chukua hatua.

Vikao vingi vinavyoendela sasa vya watendaji wa makampuni ni namna gani wataongeza bei ya bidhaa zao ili kukidhi ghrama za uendeshaji naamini zoezi hili litaenda sambamba na kupunguza idadi ya watumiaji wa bidhaa hizo na hivyo bila shaka kupunguza idadi ya wafanyakazi kwani demand itakuwa ndogo(tupeane pole mapema jamani hali inayofuata sio nzuri)

Mwisho nauliza hiviiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!!!!!!

Kama tunaweza kuilipa dowans tunashindwa hata kununua mtambo wa kutengeneza furnitur za kisasa kuliko zile za kichina ambazo zimepamba maofisi ya Nchi yetu???????????????????????????????????????????????????????????tena tunaya nunua kwa USD????????????????????TATIZO LIKOWAPI NINYI MLIOSOMA HAPO MLIMANI????????????????????NA VYOU VINGINE DUNIANAI?????????????????????????????????????

Nifuteni machozi wapendwa

Enough is not enough until enough is enough
 
naungana na mwanaJF mwingine, mambo yanayoleta kuvurugika kwa amani ndiyo kama haya ya inflation...wakati BOT imelala kukabiliana na hili kutumia monetary policy za kueleweka, majizi yameweka hela kwenye assets kama mahoteli na wengine wana accounts nchi za nje...wewe umekuwa mwanasiasa au mfanyakazi wa serikali miaka 30, umetoa wapi $ milioni 900 (mfano tu!!)..biashara gani umefanya (na ujue kabisa maadili mengine hayaruhusu kufanya biashara ukiwa serikalini) bado hapo kiongozi anasomesha watoto nje ukiuliza mshahara ni Tsh. 3m ameweza kusave hela yote hiyo. Hapa ni hela za walipa kodi, unajitahidi na kaduka kako TRA wanachukua kodi then majizi yanachukua. Itafika mahali mwananchi hawezi kupata hata mlo mmoja hapo mtaona amani inatoweka.
 
Ni hatari kwa uchumi. Sijazipitia exchange rate kwa muda kidogo sasa lakini kama hali iko hivyo basi inatisha. Kama alivyosema mdau mmoja hapo juu tatizo kubwa ni umeme. Nionavyo mimi hakuna mipango ya maana na ya muda mrefu ya kutupa utatuzi wa kudumu wa tatizo la umeme, maana hata zile ahadi za Ngeleja katika bunge hazina ukweli wowote tutaingia mwaka 2012 tukiwa gizani. Labda maji ya mvua yatatuokoa kwa muda lakini mvua zikiisha tatizo liko pale pale na mipango mingine ya dharura.

Ukiondoa tatizo la umeme ni jambo ambalo liko wazi kwamba nchi kama Tanzania haiwezi kuwa na uchumi imara bila kuboresha kilimo. Nasema hivi kwa sababu hatuna viwanda vya kutosha kuubeba uchumi wetu na vile vya enzi ya Mwalimu vilishakufa au tumewapa wageni kwa bei ya kutupa. Maendeleo katika kilimo yatawainua wananchi walio wengi hasa wa vijijini na kuimarisha uchumi kwa ujumla na kutuondoa kwenye uchuuzi ambako hata mapeasi tunaletewa toka nje.
 
Back
Top Bottom