kande kavu
JF-Expert Member
- Sep 17, 2011
- 234
- 86
Kumbe inawezekana Waungwana.
Mpaka miaka miwili iliyopita nilikuwa Fataki hasa. Namaanisha niliwabinua kweli kweli wa kila sampuli. Ilikuwa ni kama laana fulani kwani kila nilipomuona wa kike akili yangu ilirukia kwenye kumbinua.Hata kabinti kamoja kazini kalikaribia kabisa kuvunja ndoa yangu.Na hapo ndo nilipojua wamama wanaweza kuua kwa mapenzi, maana wife ghafla akawa si yeye tena.Hata hivyo niliendelea "kutengeneza CV" kwenye fani.
Ikaja wakati nikaanza kutafakari hasa ninachokipata kwenye hilo game.Nimetafuta mpaka kwenye uvungu lakini sikupata nilichopata kwa kuwekeza kwenye ngono. NIKAAMUA HIVI HIVI kuacha.Na NIMEACHA.Hivi naandika niko lunch time na kuna kabinti kako hapa kazuri kwa viwango vya nje.Naamini nimeishinda hiyo dhambi, kwani ingekuwa enzi zangu mpaka nywele za kwapa zingenisimama kwa mikakati ya kumbinua huyo mdada.Kwa hivi sasa wala, kwani hata meza nimebadili na nimemepa mgongo asinitege.
Sijaacha uzinzi kwa sababu za kiafya wala kiuchumi na nashukuru MUNGU nimetoka na afya yangu safi kwenye hilo balaa. Hayo maeneo niko poa.Je wewe unayesoma hapa,je unafanya uzinzi? kwa sababu gani hasa? Je ni kwa sababu umeambiwa ni kawaida ya mwanaume? Je ni kwa vile unaona haiwezekani kuacha? Hebu fikiri hizo gharama za "uwezeshaji wa uzinzi" zingefaa vipi maeneo mengine bora kwenye maisha yako!
INAWEZEKANA KUACHA UZINZI.ACHANA NA ILE SAUTI YA PILI KCHWANI MWAKO.
Nimetimiza wajibu.
Mpaka miaka miwili iliyopita nilikuwa Fataki hasa. Namaanisha niliwabinua kweli kweli wa kila sampuli. Ilikuwa ni kama laana fulani kwani kila nilipomuona wa kike akili yangu ilirukia kwenye kumbinua.Hata kabinti kamoja kazini kalikaribia kabisa kuvunja ndoa yangu.Na hapo ndo nilipojua wamama wanaweza kuua kwa mapenzi, maana wife ghafla akawa si yeye tena.Hata hivyo niliendelea "kutengeneza CV" kwenye fani.
Ikaja wakati nikaanza kutafakari hasa ninachokipata kwenye hilo game.Nimetafuta mpaka kwenye uvungu lakini sikupata nilichopata kwa kuwekeza kwenye ngono. NIKAAMUA HIVI HIVI kuacha.Na NIMEACHA.Hivi naandika niko lunch time na kuna kabinti kako hapa kazuri kwa viwango vya nje.Naamini nimeishinda hiyo dhambi, kwani ingekuwa enzi zangu mpaka nywele za kwapa zingenisimama kwa mikakati ya kumbinua huyo mdada.Kwa hivi sasa wala, kwani hata meza nimebadili na nimemepa mgongo asinitege.
Sijaacha uzinzi kwa sababu za kiafya wala kiuchumi na nashukuru MUNGU nimetoka na afya yangu safi kwenye hilo balaa. Hayo maeneo niko poa.Je wewe unayesoma hapa,je unafanya uzinzi? kwa sababu gani hasa? Je ni kwa sababu umeambiwa ni kawaida ya mwanaume? Je ni kwa vile unaona haiwezekani kuacha? Hebu fikiri hizo gharama za "uwezeshaji wa uzinzi" zingefaa vipi maeneo mengine bora kwenye maisha yako!
INAWEZEKANA KUACHA UZINZI.ACHANA NA ILE SAUTI YA PILI KCHWANI MWAKO.
Nimetimiza wajibu.