Inawezekana Magufuli sio tatizo?

Yaani leo nimeshangazwa mno na sisi watanzania tulivyo

eti Magufuli anarudi pale pale kutoa ahadi ile ile na inakuwa ni 'new event'
yaani hata siku 100 hazijaisha....tushasahau
Mkuu The Boss, mimi nimeshangazwa sana na kushangaa kwako. Magufuli alikuwa serikalini miaka 20 akiwa Waziri lakini katika kampeni yake muda mwingi alionesha kushangaa kwa nini mambo mengi yalikuwa hayaendi. Kwa kawaida mtu wa aina yake ilitakiwa aogopwe kama ukoma lakini cha ajabu Watanzania walichukulia huko kushangaa kwake kama sifa ya kupewa Uraisi. Hebu soma hili jibu lililotolewa na anayejiita Barbarosa kama sababu ya wagonjwa ku"share" vitanda Muhimbili, nanukuu;
Barbarosa said:
...kumbuka Hospitali zote Dar zimejengwa wakati Dar ikiwa na wakazi chini ya milioni Moja leo hii tuko zaidi ya milioni 4.5...
Hapa tayari yupo Mtanzania, Barbarosa, anayeshangaa kama Magufuli alivyokuwa akishangaa kwenye kampeni kwa nini idadi ya watu Dar inaongezeka mwaka hadi mwaka (sijui alitegemea iweje!) Ni sawa na mtu anayeshangaa kwa nini leo tuko milioni 50 wakati tukipata Uhuru tulikuwa milioni 9 tu.

Bila shaka Magufuli mwenyewe alishangaa kuambiwa wako wagonjwa wanalala chini siku mia baada ya serikali yake kuwahakikishia wananchi kwamba tatizo hilo limetatuliwa. Hii ndiyo sababu nakushangaa wewe kuwashangaa Watanzania wanaposhangaa ahadi za kushangaza zinazotolewa kwa mshangao mkubwa!
 
Magufuli akitaka mambo yawe mazuri kwenye hospital zetu azuiye viongozi wote wa kiserikali kwenda kutibiwa Ulaya (nje ya nchi) hapo mambo yatakuwa mazuri lkn km sio hivyo, itakuwa changa la macho tu
 
images


Utazunguka we mwisho wa siku huko pale pale raisi awezi kuwa pahala pamoja kila siku kuna namna zake za kudhibiti hayo mambo tukisema aliowachagaua hawana uwezo ndio ukweli hawana sio majungu vingenevyo wangeshatatua hayo mambo na kesho akienda mwananyamala choo atakikuta kichafu tu vilevile.
 
Mkuu The Boss, mimi nimeshangazwa sana na kushangaa kwako. Magufuli alikuwa serikalini miaka 20 akiwa Waziri lakini katika kampeni yake muda mwingi alionesha kushangaa kwa nini mambo mengi yalikuwa hayaendi. Kwa kawaida mtu wa aina yake ilitakiwa aogopwe kama ukoma lakini cha ajabu Watanzania walichukulia huko kushangaa kwake kama sifa ya kupewa Uraisi. Hebu soma hili jibu lililotolewa na anayejiita Barbarosa kama sababu ya wagonjwa ku"share" vitanda Muhimbili, nanukuu;

Hapa tayari yupo Mtanzania, Barbarosa, anayeshangaa kama Magufuli alivyokuwa akishangaa kwenye kampeni kwa nini idadi ya watu Dar inaongezeka mwaka hadi mwaka (sijui alitegemea iweje!) Ni sawa na mtu anayeshangaa kwa nini leo tuko milioni 50 wakati tukipata Uhuru tulikuwa milioni 9 tu.

Bila shaka Magufuli mwenyewe alishangaa kuambiwa wako wagonjwa wanalala chini siku mia baada ya serikali yake kuwahakikishia wananchi kwamba tatizo hilo limetatuliwa. Hii ndiyo sababu nakushangaa wewe kuwashangaa Watanzania wanaposhangaa ahadi za kushangaza zinazotolewa kwa mshangao mkubwa!


Siku 100 zimeisha kwa kuanza upya yale yale aliyoyafanya siku ya kwanza
 
...haya sasa tuone kama atawafuta kazi kina kigwangala wanaofungia watumishi nje ya ofisi wakati Muhimbili kina mama zao wanalalal chini... Btw vile vitanda walivyonunua kwa mbwembwe waliveweka wapi?...
...alafu huyu rais anazuga kutembeatembea Muhimbili kila kukicha tena kuitumia media wakati anawakimbia mabalozi wanaotoa hisani na misaada..ikiwemo kuboresha hizo hospital...kwangu namwona huyu rais kuwa wa ajabu kabisa..
...wamejikuta kutimuatimua watumishi kama suluhisho la matatizo...sasa aanze na mawaziri wake wa afya...maana ni juzi tu alikuwa Muhimbili... Na walisema tatizo la vitanda limeisha....this is amazing...
 
Leo ukifuatilia taarifa ya habari Magufuli katembelea tena Muhimbili kwa kustukiza
kakuta matatizo tele hasa amewakuta wamama waki share vitanda hadi watu watano
na wengine wakilala chini.....

Utakumbuka few months ago tulitangaziwa kuwa baada ya Magufuli kwenda Muhimbili
vitanda vilipelekwa hadi vikakosa wagonjwa
kuna picha zilisambazwa paka kalalia kitanda kipya Muhimbili
na kwamba sasa mambo ni tofauti kabisa...vitanda tele na kila kitu saafi

Sasa binafsi siamini kabisa Muhimbili imewahi kuwa safi na matatizo yakaisha
ambacho najiuliza why 'maigizo yale ya kuwa mambo ni saafi' yaliruhusiwa
kuendelea ?

why sisi wananchi na waandishi wa habari hatukupinga kabisa habari za kuwa
mambo ni saafi muhimbili?
why habari ya leo iwe kama habari mpya
while in reality watu wameendelea kulala chini tu kama zamani?

Inawezekana kabisa tatizo haliko kwa wanasiasa?

tatizo liko kwetu wananchi na hasa media?
tumeletewa 'sanaa tukaishangilia huku ukweli tunaujua'?
sababu muhimbili hali yake sio siri
lakini tulipoambiwa mambo sasa ni saafi tuliruka ruka na kushangilia...
huku kiukweli hali ni ile ile tu.....

Na leo tena wananchi wamemlilia tena Magufuli bila kujiuliza
ni kweli Magufuli hali iliyopo haijui?si alikwenda juzi tu hapo hapo Muhimbili?
au haya matatizo ni mapya kabisa?
Mahitaji ya muhimbili yanaongezeka kila leo hivyo hilo si jambo la kushangaza...
 
K



Kikwete anataka kina Ester na wenzie walipwe
sasa nguvu kubwa na focus ya CCM na serikali yake
ni kuwa na watu wa kuitetea mitandaoni kuliko
kutazama namna ya ku fix matatizo for good....
Unakumbuka nilizungumzia sana suala la MFUMO.

Nikasema mkurugenzi hawezi kuwa tatizo peke yake, lazima mfumo mzima uliosababisha hali hiyo urekebishwe

Nikasema mbona watu waliopaswa kufanya kazi na mkurugenzi kama wizara ya afya, hazina n.k. hawakutumbuliwa?

Nikahoji, inakuwaje mkurugenzi mpya alipewa bilioni 3 on spot, je huyu wa zamani angefanyaje kazi kama hazikuwepo?

Leo majibu yanapatikana, wapo walikejeli 'mfumo' ni dudu gani!

Unajua the Boss, nafsi ni kitu kizuri sana na kibaya pia. Inaweza kukupa faraja na kukuhukumu

L46 ambao kwa maneno ya mwenyekiti hali zao dhofla, wanadhani tunaandika tu ilimradi.

Hawaangalii mantiki ya hoja.

Leo nafsi zinawasuta hawana namna. Nafsi zinawahukumu wakiona mama, dada, vichanga vimelezwa sakafuni mithili ya mahabusu. Kwamba, kwa Tanzania uzazi ni sero isiyo rasmi.

Wananarudi ili twende pamoja. Karibuni hatuna kejeli wala kashfa tuna hoja na mantiki
 
Sasa ngoja tusubiri tuone Ummy na Hamisi [Kigwangalla] watafanya nini kesho.
Nadhani wanapaswa kuisoma namba katika mtindo wa #Hapakazi
Kinyume chake, #Hapakazi imuombe radhi mkurugenzi aliyeondolewa huku L46 wakishangilia bila akiba ya maneno
 
Watu wa propaganda wa magufuli haziwatoshi eti magufli alikutana na wanawake sijui wodini kwa Mufti wakamuomba akaone maternityna yeye akakubali huyu baba anapenda kideo mpaka anajitoa ufahamu kwa hiyo wasingekuwa wanawake kumuomba kwake ilikuwa sawa
 
Ndani ya siku 100 mahitaji yameongezeka kupita kasi ya Rais?
Njia nzuri ni kukabiliana na changamoto si kukimbia hadi wageni !

Kukabiliana na changamoto ni kuangalia, mbona tatizo linajirudia miaka nenda rudi? Tufanyeje! ni watu au mfumo?
 
Nadhani wanapaswa kuisoma namba katika mtindo wa #Hapakazi
Kinyume chake, #Hapakazi imuombe radhi mkurugenzi aliyeondolewa huku L46 wakishangilia bila akiba ya maneno

Watu ambao wao wenyewe wakienda Muhimbili watalazwa chini
na wanaenda kuwaona ndugu zao wakiwa chini lakini wanakomaa humu kutetea yanayowaumiza hadi wao
 
Watu wa propaganda wa magufuli haziwatoshi eti magufli alikutana na wanawake sijui wodini kwa Mufti wakamuomba akaone maternityna yeye akakubali huyu baba anapenda kideo mpaka anajitoa ufahamu kwa hiyo wasingekuwa wanawake kumuomba kwake ilikuwa sawa


Kwa hiyo bila kuombwa alikuwa hajui kuna kina mama wanalala chini?
asingeombwa angebaki hajui?angekua anajua kila kitu saafi Muhimbili?
dah...
 
Watu ambao wao wenyewe wakienda Muhimbili watalazwa chini
na wanaenda kuwaona ndugu zao wakiwa chini lakini wanakomaa humu kutetea yanayowaumiza hadi wao
Ndio maana nasema nafsi zinawasuta wakikumbuka ndugu zao wapo sakafuni wakiugulia. Hapo hapo wanahitaji kuwemo jamvini kwani mwenyekiti amedokeza hali si nzuri, watazamwe! wamenyongea! fungu la uchaguzi alijojo

Walichofanikiwa leo ni kupooza mjadala wa kukimbia wageni! sad
Wageni wetu wa kutoka mataifa, inauma sana!
 
Unakumbuka nilizungumzia sana suala la MFUMO.

Nikasema mkurugenzi hawezi kuwa tatizo peke yake, lazima mfumo mzima uliosababisha hali hiyo urekebishwe

Nikasema mbona watu waliopaswa kufanya kazi na mkurugenzi kama wizara ya afya, hazina n.k. hawakutumbuliwa?

Nikahoji, inakuwaje mkurugenzi mpya alipewa bilioni 3 on spot, je huyu wa zamani angefanyaje kazi kama hazikuwepo?

Leo majibu yanapatikana, wapo walikejeli 'mfumo' ni dudu gani!

Unajua the Boss, nafsi ni kitu kizuri sana na kibaya pia. Inaweza kukupa faraja na kukuhukumu

L46 ambao kwa maneno ya mwenyekiti hali zao dhofla, wanadhani tunaandika tu ilimradi.

Hawaangalii mantiki ya hoja.

Leo nafsi zinawasuta hawana namna. Nafsi zinawahukumu wakiona mama, dada, vichanga vimelezwa sakafuni mithili ya mahabusu. Kwamba, kwa Tanzania uzazi ni sero isiyo rasmi.

Wananarudi ili twende pamoja. Karibuni hatuna kejeli wala kashfa tuna hoja na mantiki

Ipo siku watakuelewa tu!
 
Tatizo kubwa ni Media ambayo ilichukua hili swala kwa utashi wa kutaka kuuza (kasi ya awamu mpya) wakati wakitoa matumaini hewa kwa wananchi."Muhimbili ile ileee "..sababu hata CT scan iliyoletwa kumbe ilikuwa ni ya Morogoro wamefanya kuhamisha tu.


Morogoro? Dah watanzania kwa uongo!!! I salute you
 
Ongezeko la watu ndiyo tatizo nchini mwetu, na suluhisho ni kupunguza kuzaliana kwetu hovyo!
Idadi ya watu ikiongezeka hata productivity inaongezeka,,vivyo hivyo mapato ya nchi yataongezeka.,!!hivyo wingi wa watu sio shda.tatizo ccm wakati wote mpo 'location'!!
 
Back
Top Bottom