Inawezekana kweli Kikwete ni chaguo la Mungu

Mwigamba Mungu hakuwachagulia Israel mfalme bali aliwaacha wafuate mawazo yao ya kuwa na mfalme kama mataifa meingine.Israel hapakuwa na mfalme bali Mungu mwenyewe alikuwa akiwaongoza Israel kupitia watumishi wake kama akina Samuel. Mungu hajipingi mtu wa Mungu atakuwa anaonekana ( mtawatmbua kwa matunda yao).


1Sam9:15-17 Basi Bwana alikuwa amemfunulia Samweli, siku moja kabla Sauli hajamwendea, akisema,

Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mtu kutoka nchi ya Benyamini, nawe mtie mafuta ili awe mkuu juu ya watu wangu Israeli, naye atawaokoa watu wangu na mikono ya Wafilisti; maana nimewaangalia watu wangu, kwa sababu kilio chao kimenifikilia.

Hata Samweli alipomwona Sauli, Bwana akamwambia, Huyu ndiye niliyekuambia habari zake; huyu ndiye atakayewamiliki watu wangu.
 
Kumbe hata Marasi waliopita Mawazri wao walikuwa wakifanya madudu? Kumbe tofauti kati ya JK na Marais walimtangulia ni kuchelewa kuchukua hatua? Binafsi naona JK ni bora kuliko waliomtangulia kwa sababu kwanza anaona, anatafakari, anajiridhisha na kuchukua hatua. Lakini pia Mwigamba hakusema iliwachukua muda gani Marais waliotangulia kuwachukulia hatua mawaziri wake. Naona kama bwana Mwigamba ana chuki zake binafsi na Serikali ya Jk na hana jipya kabisa. Kama kiongozi, huwezi kuwa mtu wa kukurupuka kuchukua hatua kama ambavyo Mwandishi wa habari anavyofanyakazi ya kuandika kile alichokisia kabla hata hajakifanyia kazi na kujiridhisha na uhalali wake.

eh! kumbe watu kama wewe bado wapo?
 
Kinachonishangaza habari za Mwigamba kuiba pesa huko CHADEMA huwa zinazungumzwa na watu wawili tu humu kwenye JF. Hatujawahi kusikia taarifa rasmi kwenye chama huko kwamba Mwigamba kafukuzwa kazi kwa sababu ya wizi wa fedha za umma. Maana ruzuku inayotolewa na serikali kwa CHADEMA ni mali ya umma na imetokana na kodi zetu. Kwa nini kama Mwigamba ni mwizi asitimuliwe kazi officially na apelekwe mahakamani kama ambavyo CHADEMA mnadai mawaziri wenye tuhuma wafikishwe mahakamani? Nakumbuka David Kafulila alipowakashfu viongozi wakuu wa chama kwamba walikuwa na kikao cha geto, mara moja alifukuzwa uofisa wa makao makuu ya CHADEMA na ikatangazwa vilivyo kwenye media. Kwa nini Miwigamba naye asifanyiwe hivyo. Kama hilo halitokei basi tuna kila sababu ya kuamini kwamba watu hawa wanaomwandika vibaya Mwigamba humu JF ni kati ya wale ambao alipokuwa Mhasibu wa chama aliwawekea vigingi kwenye matumizi mabaya ya fedha za chama. Kwa kuwa aliwazuia kufuja fedha za chama sasa hivi wanataka kumchafua lakini sidhani kama watamweza yule kijana. Kama wana jeuri wajitokeze hadharani kwa majina yao halisi tuone ukweli wao na Mwigamba atoe ukweli wake.
 
Hivi kwa nini hamtaki kuvua magamba ili yaache kuwafunika akili zenu za kuzaliwa, hivi wewe na akili zako kamili kabisa unaamini kwamba wewe ukishutumiwa kwa ubadhirifu pamoja na watu wengine kama watano au sita hivi halafu watatu kati yenu wakashughurikiwa na wengine wakaachwa tena kwenye ulaji zaidi, hivi kweli hilo ni jambo la kupongeza mtu au kiongozi kwamba eti amewajibisha watu? Ndg yangu hatuwajibishi watu na kuwaacha wengine kwa makosa yaleyale kwa sababu za kiurafiki na uswahiba tulionao, huko si kuwajibisha bali ni kukomoana na kujenga mizizi ya wizi na ubadhirifu wa mali za umma. Pia unatakiwa kujua kwamba serikali yenye kusimamia uwajibikaji haisubiri shinikizo la umma, wabunge na makundi mbalimbali ya kijamii. Serikali na kuwajibika katika utumishi si kwa mawaziri tu kuna wakurugenzi, waandisi, makatibu, maofisa mbalimbali, waalimu, madakita, manesi, ma-ward officers, n.k. utumishi wa umma una uwajibikaji wa kila siku tena kiofisi (yaani internal administrative disciplinary procedures) ambazo serikali inatakiwa kuzitumia bila kusubiri shinikizo na kama serikali ikifanya hivyo output itaonekana kwa wananchi na hakutakuwepo mashinikizo, mashinikizo ni kwa serikali iliyoshindwa sio ufanisi. Wewe katika viongozi waliopita ni nani umeona akiongoza nchi kwa mashinikizo ya kila kukicha kama iliovyo sasa, halafu wewe eti unasema hili ni jambo la kupongezwa. Ajabu hii!!!


VUA GAMBA NA VAA GAMBA WEWE ACHA LONGOLONGO HAPA HAZITAUSAIDIA WEWE WALA MTANZANIA YEYOTE!!!!

Kumbe hata Marasi waliopita Mawazri wao walikuwa wakifanya madudu? Kumbe tofauti kati ya JK na Marais walimtangulia ni kuchelewa kuchukua hatua? Binafsi naona JK ni bora kuliko waliomtangulia kwa sababu kwanza anaona, anatafakari, anajiridhisha na kuchukua hatua. Lakini pia Mwigamba hakusema iliwachukua muda gani Marais waliotangulia kuwachukulia hatua mawaziri wake. Naona kama bwana Mwigamba ana chuki zake binafsi na Serikali ya Jk na hana jipya kabisa. Kama kiongozi, huwezi kuwa mtu wa kukurupuka kuchukua hatua kama ambavyo Mwandishi wa habari anavyofanyakazi ya kuandika kile alichokisia kabla hata hajakifanyia kazi na kujiridhisha na uhalali wake.
 
WARAKA WA MWIGAMBA KWA WALALAHOI WA NCHI HII:
UJUMBE KUU NI KUSEMA KILA MMOJA WETU LEO HII VUA GAMBA HADI MOYONI, VAA GWANDA HADI MIGUUNI ILI TAIFA LETU LIPATE KUKOMBOLEWA BILA KUCHELEWA


Ewe Ndugu yetu Mhe Kamanda Mwigamba, nakusalimu katika jina la Mungu aliye hai, Mungu mmoja kwa Waislamu, Wahindu, Wakristo na hata wale wasiokua na dini.

Mheshimiwa mlalahoi mwenzetu, hakika NIMEGUSWA SANA TENA SANA na waraka huu ulioniandikia mimi kama sehemu ya UMMA WA TANZANIA na kunikumbusha wajibu wangu kama raia ni nini pindi ninapoona taifa langu linatafunwa bila huruma na ndugu zetu wachache waliojichagulia kugeuka mafisi kati kati yetu.

Ndio, kwa wale wanaodhani kuwa ni kitu sifa hapa watashangaa na roho zao wenyewe: Naseme mtu USIOMBE KUONA MWENZAKO ANAPOCHAGUA KUKISIMAMIA KIDETE NA KUENDELEA KUTETEA kwanguvu zote KILE ANACHOKIAMINI.

Jamani kitu 'KUTETEA KILE UNACHOKIAMINI' ni zaidi ya kilevi chochote kilichowahi kugundulika duniani kwa kuwa chenyewe tu kinakuimarisha mwilini wakati pombe inakudhoofisha, kinakulisha shibe ya kuona ushindi u karibu wakati bangi inakufanya uwe mharibifu, nasema kwamba pindi ntu unapotekeleza sehemu ya kile unachokiamini ndipo unapojihisi kwamba KAMA MUNGU MUUMBA WANGU HAPENDEZWI NA UFISADI, DHULUMA, MAUAJI sasa mimi nilie kiumbe chake tu nimekua nani kuhiari kuunga mikono machafu yote haya ya CCM?

Ni kweli kwamba hadi dakika hii mara baada ya kusoma waraka huu hakika ninaendelea kusikiliza hadi mapigo ya mioyo ya walalahoi wenzetu wengine huko madongo kuinama na jinsi gani wanavyoomba kama sisi hapa kwamba WATESI WETU HATA MMOJA ASIFE LEO WALA KESHO ili nao waje wakauonje utamu wa maisha huru bila dhuluma, ufisadi wala udhalilishaji wa HAKI NA UTU WA KILA MTANZANIA.

CHONDE USILIE KWA HAYA YOTE TUNAYOFANYIWA NDANI YA NCHI HII NA HAWA NDUGU ZETU WALIOGEUKA MAFISADI NA MANYANG'AU HUKO CCM, mwenzetu unapolia wengine ndio kwaaaanza unatupandisha mori ya MABADILIKO KWA NGUVU YA UMMA na kubakia tu kutama turuke vichwa vyetu viguse dari la huko mbinguni ili tunaporudi kukanyaga ardhini na watesi wetu wooooote wawe wamezama kwa nguvu moja hiyo hiyo tutakaotua na hapa chi.

Naam, Ndugu yetu mwigamba kwa kweli moyo inakwenda mbio sana lakini imani yangu inaimarika ajabu huku nikiendelea kuhimiza kila mmoja wetu ndani ya nchi hii atambue wazi kwamba sisi Umma wa Tanzania wengi wetu tulio masikini wa kutupwa UWEZO TUNAO kwa namna ya ajabu mno ambapo hata mdhalimu angekuja na nini mbele yetu KAMWE HAWEZI HATA DAKIKA MOJA kuzuia azma yetu kama taifa kuamua kukaa upande sahihi wa historia kwa kujichagulia MWANGA NA KUONDOKANA NA GIZA kimoja.

Hakika hadi hivi sasa WaTanzania TUMESHAAMUA KWA YETU SAFARI YA KUJIKOMBOA NI MBELE DAIMA BILA FUJO NA KWAMBA KATU NYUMA hakuridiki tena. Bai bai Mafisadi, bai bai CCM huku tukitumia fursa hii hii hapa kukaribisha HAKI, HESHIMA, na UTUNZAJI WA UTU NA HADHI YA MTANZANIA kwa ajili ya kujiletea maendeleo zaidi, kujijengea zaidi upendo wa kweli, amani na utulivu usiolazimishwa katika shingo yetu.

Hivyo kwa kila mlalahoi wa nchi hii bila kujali chama chako, dini yako, kabila wala kanda, hebu kaseme maneno haya mara tatu kisha ukayaweke katika dau kwa Mwenyezi Mungu ili yakapate kibali na baraka zake:

KASEME MANENO HAYA KISHA UKAYAOMBEE DUA YA KHERI:

a. JUKUMU LA KULIKOMBOA TAIFA LETU NI JUU YETU BILA KUBEMBELEZWA NA MTU,
b. UTETEZI WA HAKI NA UTU WA KILA MTANZANIA NI MILIKI YETU NA
c. AZMA YA KUUNG'O MFUMO FISADI KWA NJIA ZA KIDEMOKRASIA NI WAJIBU WETU,


na ukamalizie kwa kuliambia moyo wako mwenyewe kwamba UKOMBOZI WA TAIFA kuondokana na mfumo FISADI tangu sasa ni LAZIMA UANZE NA MIMI HAPA NA KUKAMILISHWA NA MIMI MWENYEWE kwa kucheza sehemu yangu ipasavyo!!!

EWE MUNGU WA MBINGUNI TUSAIDIE KWANI KATIKA WEWE WATANZANIA TUNAYAWEZA YOTE KWA KUWA UWEZO TUNAO KATIKA WEWE USIEPENDEZWA NA KITU DHULUMA.

Utaifa mbeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeele kama tai lakini katika haki kwa wote ndani ya taifa hili bila kubaguliwa kitu!!!!!
 
Mbona haueleweki, wewe mwenyewe unashangaa kuona kwamba ni watu wawili humu ndo wanaongelea wizi wa mwigamba, hilo ndo unataka CDM iache kazi mahususi ya ukombozi wa taifa ishughurike na umbeya wa watu wawili? Ok tuseme mwigamba kweli aliiba fine, je tunashiataki na kuwakilisha tuhuma au ushahidi wa wizi JF, hao wawili uliowashangaa hawajui ofisi za CDM zilipo, kwa nini wasiwakilishe tuhuma zao na ushahidi walio nao ili achukuliwe hatua? ACHA KUJAZA UMBEA WA KIGAMBA KICHWANI MWAKO, VAA GWANDA UPATE AKILI11

Kinachonishangaza habari za Mwigamba kuiba pesa huko CHADEMA huwa zinazungumzwa na watu wawili tu humu kwenye JF. Hatujawahi kusikia taarifa rasmi kwenye chama huko kwamba Mwigamba kafukuzwa kazi kwa sababu ya wizi wa fedha za umma. Maana ruzuku inayotolewa na serikali kwa CHADEMA ni mali ya umma na imetokana na kodi zetu. Kwa nini kama Mwigamba ni mwizi asitimuliwe kazi officially na apelekwe mahakamani kama ambavyo CHADEMA mnadai mawaziri wenye tuhuma wafikishwe mahakamani? Nakumbuka David Kafulila alipowakashfu viongozi wakuu wa chama kwamba walikuwa na kikao cha geto, mara moja alifukuzwa uofisa wa makao makuu ya CHADEMA na ikatangazwa vilivyo kwenye media. Kwa nini Miwigamba naye asifanyiwe hivyo. Kama hilo halitokei basi tuna kila sababu ya kuamini kwamba watu hawa wanaomwandika vibaya Mwigamba humu JF ni kati ya wale ambao alipokuwa Mhasibu wa chama aliwawekea vigingi kwenye matumizi mabaya ya fedha za chama. Kwa kuwa aliwazuia kufuja fedha za chama sasa hivi wanataka kumchafua lakini sidhani kama watamweza yule kijana. Kama wana jeuri wajitokeze hadharani kwa majina yao halisi tuone ukweli wao na Mwigamba atoe ukweli wake.
 
Maandamano ya wana-CCM Dodoma wala tusisahau kwamba hata shetani naye anao watetezi wake hapa hapa duniani.
 
Kumbe hata Marasi waliopita Mawazri wao walikuwa wakifanya madudu? Kumbe tofauti kati ya JK na Marais walimtangulia ni kuchelewa kuchukua hatua? Binafsi naona JK ni bora kuliko waliomtangulia kwa sababu kwanza anaona, anatafakari, anajiridhisha na kuchukua hatua. Lakini pia Mwigamba hakusema iliwachukua muda gani Marais waliotangulia kuwachukulia hatua mawaziri wake. Naona kama bwana Mwigamba ana chuki zake binafsi na Serikali ya Jk na hana jipya kabisa. Kama kiongozi, huwezi kuwa mtu wa kukurupuka kuchukua hatua kama ambavyo Mwandishi wa habari anavyofanyakazi ya kuandika kile alichokisia kabla hata hajakifanyia kazi na kujiridhisha na uhalali wake.



Na we ni Kenge kweli,nimeuona Ukenge wako haswaaaa kupitia Mchango wako!!
 
Samson Mwigamba
NAJUA msomaji unajiuliza maswali
mengi ndani ya sekunde chache
za kusoma kichwa cha habari cha
makala yangu ya leo.
Mojawapo ya swali muhimu
unalojiuliza ni kama hii kweli ni
Kalamu ya Mwigamba ndiyo
inamshukuru Mungu kwa
kutupatia Kikwete kuwa rais wetu
ama mhariri amechanganya
kurasa akachapa makala ya Nape
Nnauye kwenye ukurasa wa
Kalamu ya Mwigamba.
Lakini kama msomaji ni mfuatiliaji
wa karibu wa makala zangu na
kama utakuwa na kumbukumbu
nzuri utakumbuka kuna siku huko
nyuma niliwahi kuandika makala
nzima ya kukubali kwamba ni
kweli JK alikuwa chaguo la Mungu.
Niliwahi kukubaliana na Baba
Askofu Methodias Kilaini
aliyetamka mwaka 2005 kuelekea
kwenye uchaguzi mkuu kwamba
Kikwete alikuwa ni chaguo la
Mungu. Nilisema huenda mwaka
2005 hatukumwelewa Baba
Askofu Kilaini.
Nikasema kwamba nakubaliana
naye kama alisema JK ni chaguo la
Mungu akimaanisha ni tatizo
lililoletwa kwa watanzania ili
wajifunze kubadilika. Tunasoma
katika Biblia kwamba pale wana
wa Israel walipoamua kwamba
sasa hawataki kuchaguliwa
mfalme na Mungu wanataka
wachague wenyewe, Mungu
aliwaongoza kumchagua mfalme
aliyeitwa Sauli.
Sauli hakuwa kiongozi mzuri,
akalipotosha taifa na kutenda
maovu mbele za Bwana na
wananchi wakaingia katika shida
kubwa mpaka wakajuta
kumchagua.
Bwana akamchagua JK ili aje
kumtumia kuwaokoa Watanzania
hawa maskini. Biblia inasema
“akawauza kwa adui zao” nao
wakazama na kummwagia JK
ushindi wa asilimia 80 ambayo
haijapata kupatikana katika
uchaguzi wa vyama vingi siyo
hapa kwetu tu bali hata katika
nchi nyingi zenye demokrasia
inayoeleweka.
Wapo waliosema huyu ndiye
tuliyemsubiri. Kina Prince Bagenda
waliofikia kuandika kitabu
kwamba ‘JK ni tumaini lililorejea’
hawakukosekana.
Lakini alipoanza kutawala
haikuchukua muda kugundua
kwamba Watanzania tumechagua
Sauli kuongoza nchi. JK ameprove
kuwa rais dhaifu kuliko wote
waliopita kiasi cha kufikia
wanasiasa na wachambuzi wa
masuala ya kisiasa kusema nchi
ina ombwe la uongozi. Si maneno
yangu ya wazee wenye maono
kama kina Joseph Butiku na
Joseph Warioba.
Ni rais pekee ambaye
ameonyesha kwamba Waziri
Mkuu wake anaweza kutuhumiwa
kila kona ya nchi lakini akasubiri
mpaka ripoti ya kamati teule ya
Bunge ije imuumbue ndipo
amshauri kujiuzulu na si
kumtimua.
Mzee Mwinyi aliposoma tu kitabu
cha Nyerere kilichomtuhumu
Malecela akiwa waziri mkuu
wakati huo na mzee Kolimba
akiwa katibu mkuu wa chama
wakati huo, alichukua hatua mara
moja akavunja Baraza la Mawaziri
na kumtangaza Msuya kuwa
waziri mkuu mpya.
Mzee Mkapa aliwashauri mawaziri
wake wenye tuhuma wajiuzulu
mara moja akina Simon Mbirinyi,
Hans Kitine, Idd Simba, nk. pale
walipotuhumiwa. Lakini hilo
huwezi kulisikia wakati wa
Kikwete badala yake utasiki waziri
kwa jeuri akisema siwezi
kujiuzulu kamwe labda rais
anifukuze. Naye rais hutasikia
akimfukuza waziri.
Tumeyasikia maneno hayo kwa
Hussein Mwinyi wakati akiwa
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la
Kujenga Taifa, baada ya mabomu
ya jeshi kuangamiza watu
Mbagala na Gongo la Mboto,
tumeyasikia mara kadhaa kwa
Maige, tumeyasikia kwa Ngeleja,
na wengineo wengi na juzi hapa
tumeyasikia mpaka yakawa
yanakereketa masikioni kutoka
kwa Omary Nundu.
Maskini wakati huu wa Kikwete
wameongezeka kuliko kawaida,
rushwa ya kupindukia imeanza
kusikika wakati huu wa Kikwete
na ni wakati huu wa Kikwete
ambapo msamiati wa ufisadi
tuliokuwa tunausikia tu huko
Kenya, umeshika kasi hapa kwetu.
Mauaji ya raia kwa vyombo vya
dola yameongezeka sana wakati
huu wa Kikwete. Huko nyuma
tulizoea kutangaziwa mara kwa
mara majambazi yameua watu
wangapi. Siku hizi ni kawaida
kusikia polisi wameua watu
wangapi.
Nchi wakati huu wa JK imepoteza
mwelekeo. Wazee wa CCM, wala si
wa upinzani, wanapiga kelele kila
kukicha. Akina Warioba, Kaduma,
Butiku, Kitine na wengineo lakini
wanajibiwa kwa kejeli na serikali
ya Kikwete na awamu mpya ya
secretariat aliyoiweka kwenye
chama chake.
Ni vigumu leo kujua nini kitatokea
kesho kwenye serikali hii ya
Kikwete. Kila mtu ni gamba, kila
mtu ni fisadi na kila mtu ni
mpiganaji dhidi ya ufisadi.
Sasa wananchi wameshtuka.
Wametambua kwamba anapwaya
na siyo yeye peke yake bali wote
waliobaki ndani ya chama hicho
kikuukuu.
Ni Kikwete alipambwa
akapambika, akaonyeshwa kama
masalia pekee aliyebaki ndani ya
CCM mwenye uwezo wa
kulinyoosha taifa kuelekea
tunakotaka. Watanzania
waliaminishwa wakati ule
kwamba hakuna aliyebaki ndani
ya chama hicho anayestahili
kuchukua uongozi wa nchi zaidi
yake yeye.
Kwa hiyo alipokuja kuvurunda
wananchi wakasema basi inabidi
CCM iondoke madarakani. Kwa
sababu waliambiwa ni JK peke
yake aliyebaki kwenye CCM, sasa
kama amechemsha tena vibaya
kiasi hiki CCM itasema nini
kuwashawishi Watanzania
kwamba kuna mwingine tena
zaidi ya Kikwete? Najua
waliotengeneza huo mkakati
walikuwa na mawazo yao
kichwani lakini nawaambia
imekula kwao.
Nawapongeza sana CHADEMA. Ni
chama kinachojua nini kinafanya
na nini lengo lao. Wako tayari
muda wote kutumia kila nafasi
itakayojitokeza mbele yao kuzidi
kuisogelea Ikulu. Huko nyuma
niliwahi kusema maneno haya na
leo nayarudia. Mwaka 2005
Mungu alifanya machaguo mawili.
Alimchagua JK kuiangamiza CCM
na akamchagua Slaa kuinyanyua
CHADEMA. Ndiyo maana wakati
fulani nikasema, wote, JK na Slaa,
ni machaguo ya Mungu.
Saa ya ukombozi imewadia.
Wakati wa kuiondoa CCM
madarakani umewadia.
Wanaohusika na kuiondoa CCM
madarakani ni Watanzania wote
wakiwamo Wana CCM wengi.
Operesheni inayokuja kumaliza
kazi ni hii ambayo CHADEMA
wameipachika jina la M4C, kwa
kirefu ikiwa ni “Movement For
Change” yaani “Vuguvugu la
Mabadiliko”.
Kupitia M4C Watanzania
wanafikishiwa elimu ya uraia na
kufumbuliwa macho wajue haki
zao za kidemokrasia, wajue
nguvu waliyonayo kama chanzo
pekee kwa mujibu wa katiba yetu
cha mamlaka wanayopewa
serikali.
Wananchi wa kawaida
wanafundishwa kuelewa
kwamba wana nguvu kubwa mno
iitwayo nguvu ya umma ambayo
wakiitumia vizuri hakuna mtawala
wala mwanasiasa wala vyombo
vya dola vitakavyoweza
kuwanyanyasa.
Wananchi wanajua kupitia M4C
kwamba hatupaswi kuchukua
silaha za jadi kupambana
kuiangusha serikali, kwamba
hatuna haja ya kuipigia magoti
CCM kila kukicha na kuiomba
iisimamie serikali yake iwatumikie
wazawa na si wageni.
Si lazima tuibembeleze serikali ya
CCM itujengee barabara na
zahanati nasi tuishukuru kama
vile wametoa msaada wa
wahisani. Kwamba si lazima
tukakae vikao na wenye migodi
kuwaomba kwenye matrilioni ya
pesa wanayoyapata kwenye
dhahabu yetu, almasi yetu,
tanzanite yetu na madini mengine
mengi, eti watoe kwa mwaka
vimilioni 200 tu kwa halmashauri
ya wilaya ama mji inayopakana na
mgodi ambayo mgodi umo kwa
ajili ya kutengeneza madawati ya
kukalia watoto wetu.
Nguvu tuliyonayo twaweza
kuisubirisha siku ya kuandikisha
kupiga kura na siku ya kupiga
kura. Tujiandikishe kwa wingi na
siku ya kura tupige kwa wingi
kuiondoa CCM madarakani.
Tufanye kama Arumeru Mashariki.
Mpaka CCM wanapigia CHADEMA
wanapigia mabadiliko lakini
wakiwa ndani ya CCM.
M4C inalenga kukusanya pesa
kwa viwango vya mia mia, elfu
elfu, elfu kumi kumi, elfu hamsini
hamsini, laki laki na kadhalika. Hizi
hela ni kidogo sana lakini
tukichanga sisi maskini tulio
wengi zitatutosha kujenga chama
mbadala nchi nzima na
kukiwezesha kufanya kampeni za
kistaarabu lakini kabambe hapo
mwaka 2014 na 2015 kuchukua
dola.
M4C inalenga kujenga mtandao
wa chama nchi nzima. Mwaka huu
mwezi wa ujao utaanza uchaguzi
kwenye ngazi za misingi na
mabalozi wa nyumba kumi. Shiriki
kutandaza chama kote nchini.
Arusha kama kawaida yetu
tutaset mfano hivi karibuni.
Tunawasihi watakaoona mkakati
wetu unafaa wauige lengo ni
kufikia mabadiliko na si nani
alianzisha nini.
M4C inalenga kuwaleta nyumbani
makamanda waliopotea
jangwani. Wakati fulani palikuwa
na jangwa tupu (CCM), hamkuona
malisho mabichi. Kwa hiyo miaka
yote mmekuwa mkijua hamna
zaidi ya majani makavu. Mlipoanza
kuona majani mabichi mlidhani
yana sumu, haiwezekani nchi hii
kukawa na malisho mazuri kiasi
hiki.
Hapana, msimsikilize shetani
ambaye kazi yake ni kuwakatisha
tu tamaa. Njooni ndani ya zizi
lenye mchungaji mwema. Mkono
wa kuume wa M4C ni operation
ndogo inayoitwa “Vua gamba, vaa
gwanda”. Mpaka sasa karibia
makamanda elfu 20 wamejiengua
kwenye magamba na kuvalia
magwanda.
Hilo nalipongeza sana na
hatimaye unabii unaelekea
kutimia. Lakini naipenda sana
operation ndogo nyingine ya M4C
ambayo naweza kuiita mkono wa
kushoto wa M4C. Hii ni operesheni
ya kimya na kwa kweli naipenda
kwa kuwa iko effective kuliko
zote. Nayo ni “Toa gamba moyoni,
valia gwanda moyoni”.
Hii kwa sasa imefikisha mamilioni
ya Watanzania. Hawa ni wana CCM
ambao wanaendelea kuvalia
magamba kwa nje lakini mioyoni
mwao wamevalia magwanda na
kila wakati wanaitika kimoyo
kimoyo “Peopleeeeeeeees!
Poweeeeeeeeeeer!
Katika kundi hili wamo watumishi
wa umma. Hawa kwa miaka yote
wamekuwa hawana magamba
kwa nje lakini kwa ndani
wamevalia magamba hata kama
ni kwa kulazimishwa na
mazingira.
Ushauri wa bure kwa CCM ni
kwamba mafuriko hayajawahi
kuzuiwa na kitu chochote. Acheni
kujisumbua. Naona kama
mmeanzisha M4K (Movement for
Killing), wameuawa watu wengi
sana Igunga baada ya uchaguzi
mdogo wa Oktoba mwaka jana
na sasa Arumeru Mashariki, pia
wameanza kuuawa na wote ni
viongozi na makada wa CHADEMA.
Na vitisho vinaendelea, hivi sasa
vimefika kwa viongozi wetu wa
wilaya na wabunge wetu kina
Nassari na mwenzake aliye likizo,
Lema. Mbona mnaniacha
Kamanda mkuu wa mkoa
mnaelekea kwa walio chini yangu
tu? Njoni kwangu basi, mimi niko
tayari kuingia kwenye orodha ya
wafia nchi hii, kwa sababu najua
baada ya kifo changu wako
wengi watakaokombolewa!
Hivi hamjui damu ya Dennis
Shirima, Ismail na wenzao wengi
waliokufa wakati wa
maandamano ya Januari 5 mwaka
jana ndiyo imezidi kuleta
mapinduzi Arusha mpaka kufikia
hapa ilipo!? Tulieni muone damu
ya Msafiri Mbwambo inavyoigeuza
Arumeru Mashariki na Tanzania
nzima.
Eee Mungu wajalie uhai kina
Kikwete, Lowassa, Mangula,
Mkapa, Msekwa, Malecela, Mkama,
Nnauye, Sitta, na wenzao wote ili
siku nchi hii itakapokombolewa
washuhudie kwa macho yao, hata
kama sijui siku hiyo watazificha
wapi nyuso zao.
 
Samson Mwigamba

NAJUA msomaji unajiuliza maswali mengi ndani ya sekundechache za kusoma kichwa cha habari cha makala yangu ya leo.

Mojawapo ya swalimuhimu unalojiuliza ni kama hii kweli ni Kalamu ya Mwigamba ndiyo inamshukuruMungu kwa kutupatia Kikwete kuwa rais wetu ama mhariri amechanganya kurasaakachapa makala ya Nape Nnauye kwenye ukurasa wa Kalamu ya Mwigamba.

Lakini kama msomajini mfuatiliaji wa karibu wa makala zangu na kama utakuwa na kumbukumbu nzuriutakumbuka kuna siku huko nyuma niliwahi kuandika makala nzima ya kukubalikwamba ni kweli JK alikuwa chaguo la Mungu.

Niliwahi kukubalianana Baba Askofu Methodias Kilaini aliyetamka mwaka 2005 kuelekea kwenye uchaguzimkuu kwamba Kikwete alikuwa ni chaguo la Mungu. Nilisema huenda mwaka 2005hatukumwelewa Baba Askofu Kilaini.

Nikasema kwambanakubaliana naye kama alisema JK ni chaguo la Mungu akimaanisha ni tatizo lililoletwakwa watanzania ili wajifunze kubadilika. Tunasoma katika Biblia kwamba palewana wa Israel walipoamua kwamba sasa hawataki kuchaguliwa mfalme na Munguwanataka wachague wenyewe, Mungu aliwaongoza kumchagua mfalme aliyeitwa Sauli.

Sauli hakuwa kiongozimzuri, akalipotosha taifa na kutenda maovu mbele za Bwana na wananchi wakaingiakatika shida kubwa mpaka wakajuta kumchagua.

Bwana akamchagua JKili aje kumtumia kuwaokoa Watanzania hawa maskini. Biblia inasema “akawauza kwaadui zao” nao wakazama na kummwagia JK ushindi wa asilimia 80 ambayo haijapatakupatikana katika uchaguzi wa vyama vingi siyo hapa kwetu tu bali hata katikanchi nyingi zenye demokrasia inayoeleweka.

Wapo waliosema huyundiye tuliyemsubiri. Kina Prince Bagenda waliofikia kuandika kitabu kwamba ‘JKni tumaini lililorejea’ hawakukosekana.

Lakini alipoanzakutawala haikuchukua muda kugundua kwamba Watanzania tumechagua Sauli kuongozanchi. JK ameprove kuwa rais dhaifu kuliko wote waliopita kiasi cha kufikiawanasiasa na wachambuzi wa masuala ya kisiasa kusema nchi ina ombwe la uongozi.Si maneno yangu ya wazee wenye maono kama kina Joseph Butiku na Joseph Warioba.

Ni rais pekee ambayeameonyesha kwamba Waziri Mkuu wake anaweza kutuhumiwa kila kona ya nchi lakiniakasubiri mpaka ripoti ya kamati teule ya Bunge ije imuumbue ndipo amshaurikujiuzulu na si kumtimua.

Mzee Mwinyi aliposomatu kitabu cha Nyerere kilichomtuhumu Malecela akiwa waziri mkuu wakati huo namzee Kolimba akiwa katibu mkuu wa chama wakati huo, alichukua hatua mara mojaakavunja Baraza la Mawaziri na kumtangaza Msuya kuwa waziri mkuu mpya.

Mzee Mkapaaliwashauri mawaziri wake wenye tuhuma wajiuzulu mara moja akina SimonMbirinyi, Hans Kitine, Idd Simba, nk. pale walipotuhumiwa. Lakini hilo huwezikulisikia wakati wa Kikwete badala yake utasiki waziri kwa jeuri akisema siwezikujiuzulu kamwe labda rais anifukuze. Naye rais hutasikia akimfukuza waziri.

Tumeyasikia manenohayo kwa Hussein Mwinyi wakati akiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la KujengaTaifa, baada ya mabomu ya jeshi kuangamiza watu Mbagala na Gongo la Mboto,tumeyasikia mara kadhaa kwa Maige, tumeyasikia kwa Ngeleja, na wengineo wengina juzi hapa tumeyasikia mpaka yakawa yanakereketa masikioni kutoka kwa OmaryNundu.

Maskini wakati huu waKikwete wameongezeka kuliko kawaida, rushwa ya kupindukia imeanza kusikikawakati huu wa Kikwete na ni wakati huu wa Kikwete ambapo msamiati wa ufisadituliokuwa tunausikia tu huko Kenya, umeshika kasi hapa kwetu.

Mauaji ya raia kwavyombo vya dola yameongezeka sana wakati huu wa Kikwete. Huko nyuma tulizoeakutangaziwa mara kwa mara majambazi yameua watu wangapi. Siku hizi ni kawaidakusikia polisi wameua watu wangapi.

Nchi wakati huu wa JKimepoteza mwelekeo. Wazee wa CCM, wala si wa upinzani, wanapiga kelele kilakukicha. Akina Warioba, Kaduma, Butiku, Kitine na wengineo lakini wanajibiwa kwakejeli na serikali ya Kikwete na awamu mpya ya secretariat aliyoiweka kwenyechama chake.

Ni vigumu leo kujuanini kitatokea kesho kwenye serikali hii ya Kikwete. Kila mtu ni gamba, kilamtu ni fisadi na kila mtu ni mpiganaji dhidi ya ufisadi.

Sasa wananchiwameshtuka. Wametambua kwamba anapwaya na siyo yeye peke yake bali wotewaliobaki ndani ya chama hicho kikuukuu.

Ni Kikwete alipambwaakapambika, akaonyeshwa kama masalia pekee aliyebaki ndani ya CCM mwenye uwezowa kulinyoosha taifa kuelekea tunakotaka. Watanzania waliaminishwa wakati ulekwamba hakuna aliyebaki ndani ya chama hicho anayestahili kuchukua uongozi wanchi zaidi yake yeye.

Kwa hiyo alipokujakuvurunda wananchi wakasema basi inabidi CCM iondoke madarakani. Kwa sababuwaliambiwa ni JK peke yake aliyebaki kwenye CCM, sasa kama amechemsha tenavibaya kiasi hiki CCM itasema nini kuwashawishi Watanzania kwamba kuna mwinginetena zaidi ya Kikwete? Najua waliotengeneza huo mkakati walikuwa na mawazo yaokichwani lakini nawaambia imekula kwao.

Nawapongeza sanaCHADEMA. Ni chama kinachojua nini kinafanya na nini lengo lao. Wako tayari mudawote kutumia kila nafasi itakayojitokeza mbele yao kuzidi kuisogelea Ikulu.Huko nyuma niliwahi kusema maneno haya na leo nayarudia. Mwaka 2005 Mungu alifanyamachaguo mawili.

Alimchagua JKkuiangamiza CCM na akamchagua Slaa kuinyanyua CHADEMA. Ndiyo maana wakatifulani nikasema, wote, JK na Slaa, ni machaguo ya Mungu.

Saa ya ukomboziimewadia. Wakati wa kuiondoa CCM madarakani umewadia. Wanaohusika na kuiondoaCCM madarakani ni Watanzania wote wakiwamo Wana CCM wengi.

Operesheni inayokujakumaliza kazi ni hii ambayo CHADEMA wameipachika jina la M4C, kwa kirefu ikiwani “Movement For Change” yaani “Vuguvugu la Mabadiliko”.

Kupitia M4CWatanzania wanafikishiwa elimu ya uraia na kufumbuliwa macho wajue haki zao zakidemokrasia, wajue nguvu waliyonayo kama chanzo pekee kwa mujibu wa katibayetu cha mamlaka wanayopewa serikali.

Wananchi wa kawaidawanafundishwa kuelewa kwamba wana nguvu kubwa mno iitwayo nguvu ya umma ambayowakiitumia vizuri hakuna mtawala wala mwanasiasa wala vyombo vya dolavitakavyoweza kuwanyanyasa.

Wananchi wanajuakupitia M4C kwamba hatupaswi kuchukua silaha za jadi kupambana kuiangushaserikali, kwamba hatuna haja ya kuipigia magoti CCM kila kukicha na kuiombaiisimamie serikali yake iwatumikie wazawa na si wageni.

Si lazimatuibembeleze serikali ya CCM itujengee barabara na zahanati nasi tuishukuru kamavile wametoa msaada wa wahisani. Kwamba si lazima tukakae vikao na wenye migodikuwaomba kwenye matrilioni ya pesa wanayoyapata kwenye dhahabu yetu, almasiyetu, tanzanite yetu na madini mengine mengi, eti watoe kwa mwaka vimilioni 200tu kwa halmashauri ya wilaya ama mji inayopakana na mgodi ambayo mgodi umo kwaajili ya kutengeneza madawati ya kukalia watoto wetu.

Nguvu tuliyonayotwaweza kuisubirisha siku ya kuandikisha kupiga kura na siku ya kupiga kura.Tujiandikishe kwa wingi na siku ya kura tupige kwa wingi kuiondoa CCMmadarakani. Tufanye kama Arumeru Mashariki. Mpaka CCM wanapigia CHADEMAwanapigia mabadiliko lakini wakiwa ndani ya CCM.

M4C inalengakukusanya pesa kwa viwango vya mia mia, elfu elfu, elfu kumi kumi, elfu hamsinihamsini, laki laki na kadhalika. Hizi hela ni kidogo sana lakini tukichangasisi maskini tulio wengi zitatutosha kujenga chama mbadala nchi nzima nakukiwezesha kufanya kampeni za kistaarabu lakini kabambe hapo mwaka 2014 na2015 kuchukua dola.

M4C inalenga kujengamtandao wa chama nchi nzima. Mwaka huu mwezi wa ujao utaanza uchaguzi kwenyengazi za misingi na mabalozi wa nyumba kumi. Shiriki kutandaza chama kotenchini. Arusha kama kawaida yetu tutaset mfano hivi karibuni. Tunawasihiwatakaoona mkakati wetu unafaa wauige lengo ni kufikia mabadiliko na si nanialianzisha nini.

M4C inalenga kuwaletanyumbani makamanda waliopotea jangwani. Wakati fulani palikuwa na jangwa tupu(CCM), hamkuona malisho mabichi. Kwa hiyo miaka yote mmekuwa mkijua hamna zaidiya majani makavu. Mlipoanza kuona majani mabichi mlidhani yana sumu,haiwezekani nchi hii kukawa na malisho mazuri kiasi hiki.

Hapana, msimsikilizeshetani ambaye kazi yake ni kuwakatisha tu tamaa. Njooni ndani ya zizi lenyemchungaji mwema. Mkono wa kuume wa M4C ni operation ndogo inayoitwa “Vua gamba,vaa gwanda”. Mpaka sasa karibia makamanda elfu 20 wamejiengua kwenye magamba nakuvalia magwanda.

Hilo nalipongeza sanana hatimaye unabii unaelekea kutimia. Lakini naipenda sana operation ndogonyingine ya M4C ambayo naweza kuiita mkono wa kushoto wa M4C. Hii ni operesheniya kimya na kwa kweli naipenda kwa kuwa iko effective kuliko zote. Nayo ni “Toagamba moyoni, valia gwanda moyoni”.

Hii kwa sasaimefikisha mamilioni ya Watanzania. Hawa ni wana CCM ambao wanaendelea kuvaliamagamba kwa nje lakini mioyoni mwao wamevalia magwanda na kila wakati wanaitikakimoyo kimoyo “Peopleeeeeeeees! Poweeeeeeeeeeer!

Katika kundi hiliwamo watumishi wa umma. Hawa kwa miaka yote wamekuwa hawana magamba kwa njelakini kwa ndani wamevalia magamba hata kama ni kwa kulazimishwa na mazingira.

Ushauri wa bure kwaCCM ni kwamba mafuriko hayajawahi kuzuiwa na kitu chochote. Acheni kujisumbua.Naona kama mmeanzisha M4K (Movement for Killing), wameuawa watu wengi sanaIgunga baada ya uchaguzi mdogo wa Oktoba mwaka jana na sasa Arumeru Mashariki,pia wameanza kuuawa na wote ni viongozi na makada wa CHADEMA.

Na vitishovinaendelea, hivi sasa vimefika kwa viongozi wetu wa wilaya na wabunge wetukina Nassari na mwenzake aliye likizo, Lema. Mbona mnaniacha Kamanda mkuu wamkoa mnaelekea kwa walio chini yangu tu? Njoni kwangu basi, mimi niko tayarikuingia kwenye orodha ya wafia nchi hii, kwa sababu najua baada ya kifo changuwako wengi watakaokombolewa!

Hivi hamjui damu yaDennis Shirima, Ismail na wenzao wengi waliokufa wakati wa maandamano yaJanuari 5 mwaka jana ndiyo imezidi kuleta mapinduzi Arusha mpaka kufikia hapailipo!? Tulieni muone damu ya Msafiri Mbwambo inavyoigeuza Arumeru Mashariki naTanzania nzima.

Eee Mungu wajalieuhai kina Kikwete, Lowassa, Mangula, Mkapa, Msekwa, Malecela, Mkama, Nnauye,Sitta, na wenzao wote ili siku nchi hii itakapokombolewa washuhudie kwa machoyao, hata kama sijui siku hiyo watazificha wapi nyuso zao.

source; kalamu ya mwigamba - Tanzania daima.
 
Imeandikwa katika Biblia mamlaka zote hutoka kwa Mungu. Na Mungu humchagua mtu kupitia wanadamu na Mungu yupo juu ya yote asingeweza kuruhusu mamlaka bila kusudio,kwa msingi huo hata mamlaka dhalimu Mungu huziacha kwa madhumuni fulani vinginevyo angeweza kuziondoa kwa jinsi atakavyo.

Watu wengi sasa wamechoka CCM na ni ukweli na imedhihirika kuwa kuwa nchi hii haiwezi kwenda mbele tena kwa CCM ikiwa madarakani wengi mitaani na ofisini wanasema lazima chama kingine kichukue nchi kikate minyororo ya ufisadi na kujenga uzalendo na ili iwe hivyo ni lazima hii CCM ife kibudu. Dalili na wala hakuna ubishi tena hasa kwa mtu anayefikiri vizuri na asiyetumia masaburi kufikiri ataona CCM kupona hakupo tena ni suala la muda tuu sasa nani anapinga kuwa JK SI CHAGUO LA MUNGU.
 
Imeandikwa katika Biblia mamlaka zote hutoka kwa Mungu. Na Mungu humchagua mtu kupitia wanadamu na Mungu yupo juu ya yote asingeweza kuruhusu mamlaka bila kusudio,kwa msingi huo hata mamlaka dhalimu Mungu huziacha kwa madhumuni fulani vinginevyo angeweza kuziondoa kwa jinsi atakavyo.

Watu wengi sasa wamechoka CCM na ni ukweli na imedhihirika kuwa kuwa nchi hii haiwezi kwenda mbele tena kwa CCM ikiwa madarakani wengi mitaani na ofisini wanasema lazima chama kingine kichukue nchi kikate minyororo ya ufisadi na kujenga uzalendo na ili iwe hivyo ni lazima hii CCM ife kibudu. Dalili na wala hakuna ubishi tena hasa kwa mtu anayefikiri vizuri na asiyetumia masaburi kufikiri ataona CCM kupona hakupo tena ni suala la muda tuu sasa nani anapinga kuwa JK SI CHAGUO LA MUNGU.

Habari yako umeichanganya changanya kiasi kwamba inatia kinyaa.

Kwanza elewa hii kauli ya chaguo la Mungu ni unafiki wa wanandamu katika lugha ya kisiasa.
 
Mkubwa!..mimi nasema JK NI CHAGUO LA MUNGU kwa malengo ya kuua CCM,ule wakati wa MUNGU kiokoa tanzania ulianza mapema kwa kumuweka kiongozi ambaye nchi itamshinda alafu ndio CHADEMA wachukue....vitabu vya dini vinaeleza kuwa "mateso yakizidi ujue wokovu umekalibia"watanzania tunateseka sasa lakin wokovu ni 2015.nasema tena kusudio la Mungu kuiokoa nchi lilianza kwa kumuweka JK madarakani.JK NI CHAGUO LA MUNGU
 
Back
Top Bottom