Inatia Hasira!

Ndugu zangu wanaJF,
Nipo hapo Afrika kusini kwa muda sasa. Huwa najiuliza maswali mengi bila kupata majibu ninapokuwa nakatiza mitaa hasa ya Capetown. Miundo mbinu yao hasa barabara flyovers utashangaa.

Najua makaburu wamefanya kazi kubwa hapa lakini najaribu kulinganisha na kujifargua kwa makufuli na km 11,000 za barabara. Kusema ukweli tanzania hatuna barabara, ni mzaha mtupu!! yaani miaka hamsini ya uhuru rumeshindwa kuweka hata kaflyover kamoja hapo ubungo? miaka hamsini..! Kaflyover Kamoja tu! imekuwa ni siasa tuuu...!

Fikiria labda kila baada ya miaka kumi tungekuwa tunajenga kaflyover kamoja kwenye makutano ya barabara zetu, tungekuwa mbali sana? Inatia hasira na ni aibu kujisifia bila kufanya ulinganisho hata wa mbali tu na wenzetu! Hata Ethiopia wanatushinda? Kwanza kusema awamu ya nne wamejenga km11,000 kulinganisha na awamu nyingine, ina maana hizo awamu nyingine waliokuwepo madarakani ni CUF au CHADEMA? Si ni nyie nyie CCM? Au mnakubali sera zenu za huko nyuma hazikuwa na mashiko?

Tunapoitazama CCM tunaitazama kwa ujumla wake tangu uhuru sio katika vipindivipindi. Tunaangalia continuity ya sera na mipango ya CCM katika kutufikisha hapa tulipo! We cannot compartmentalize development!

Mawaziri wa Kikwete wanajua udhaifu wake ndio maana kila wanapozungumza wanasisitiza yale yaliyoyofanywa na serikali ya awamu ya nne kwa kumtaja Kikwete, bila kuzungumzia yana connection gani na yaliyofanywa na awamu nyingine! Kwa sababu wanajua mengi yaliyoahidiwa hayakutelezwa.

Kwa hiyo ni muda muafaka sasa CCM na serikali yake iache kujilinganisha na awamu zilizotangulia (thye are the same people) bali wajilinganishe na majirani zetu na nchi nyingine tulizopata uhuru pamoja. Kwamba wao wako wapi na sisi tupo wapi! Hapo ndipo wanaweza kujifaragua kwamba tunaongoza kwa miundo ya barabara. Sio kumlinganisha Kiwete na Mkapa au mwinyi huo ni upuuzi na udhaifu!
Rudini Bongo kuziendesha hizo wizara.
Mnafikiri mkikaa kwenye viota vya wenzenu nani atawaendeshea nji hii kama mnavyotaka?
 
Hahahaaa si bora hizo? Huku wamewekz taa za barabarani uhasibu na chang'ombe, zimewaka kwa muda wa wiki moja tu.....

Wanatuacha tugongane wenyewe tufe wapunguze population



...Mkuu mambo yameanza kigoma...Wameweka taa za barabarani zinawashwa pale anapokuja baba Riz tu otherwise zipo tu kama minazi ya kilwa!!....
 
Ndugu zangu wanaJF,
Nipo hapo Afrika kusini kwa muda sasa. Huwa najiuliza maswali mengi bila kupata majibu ninapokuwa nakatiza mitaa hasa ya Capetown. Miundo mbinu yao hasa barabara flyovers utashangaa.

Najua makaburu wamefanya kazi kubwa hapa lakini najaribu kulinganisha na kujifargua kwa makufuli na km 11,000 za barabara. Kusema ukweli tanzania hatuna barabara, ni mzaha mtupu!! yaani miaka hamsini ya uhuru rumeshindwa kuweka hata kaflyover kamoja hapo ubungo? miaka hamsini..! Kaflyover Kamoja tu! imekuwa ni siasa tuuu...!

Fikiria labda kila baada ya miaka kumi tungekuwa tunajenga kaflyover kamoja kwenye makutano ya barabara zetu, tungekuwa mbali sana? Inatia hasira na ni aibu kujisifia bila kufanya ulinganisho hata wa mbali tu na wenzetu! Hata Ethiopia wanatushinda? Kwanza kusema awamu ya nne wamejenga km11,000 kulinganisha na awamu nyingine, ina maana hizo awamu nyingine waliokuwepo madarakani ni CUF au CHADEMA? Si ni nyie nyie CCM? Au mnakubali sera zenu za huko nyuma hazikuwa na mashiko?

Tunapoitazama CCM tunaitazama kwa ujumla wake tangu uhuru sio katika vipindivipindi. Tunaangalia continuity ya sera na mipango ya CCM katika kutufikisha hapa tulipo! We cannot compartmentalize development!

Mawaziri wa Kikwete wanajua udhaifu wake ndio maana kila wanapozungumza wanasisitiza yale yaliyoyofanywa na serikali ya awamu ya nne kwa kumtaja Kikwete, bila kuzungumzia yana connection gani na yaliyofanywa na awamu nyingine! Kwa sababu wanajua mengi yaliyoahidiwa hayakutelezwa.

Kwa hiyo ni muda muafaka sasa CCM na serikali yake iache kujilinganisha na awamu zilizotangulia (thye are the same people) bali wajilinganishe na majirani zetu na nchi nyingine tulizopata uhuru pamoja. Kwamba wao wako wapi na sisi tupo wapi! Hapo ndipo wanaweza kujifaragua kwamba tunaongoza kwa miundo ya barabara. Sio kumlinganisha Kiwete na Mkapa au mwinyi huo ni upuuzi na udhaifu!
Ndugu mpendwa unachokiona SA kimetolewa hapa hapa Tanzania. Tanzanite inapatikana Tanzania tu. Haya ni madini ambayo yanauzwa ghali ile mbaya nje ya Africa na yako femous sana. SA inachimba inabeba na udogo wetu inauza kwa jina lake then wanajenga taifa lao. Vilaza Watanzania tunaambulia kilio, huku rais wetu DHAIFU akiwachekea na kuwa ghaia bure. Kweli ipo siku hii CCM tutaizika na manyoya yake na huyu chekacheka anayejidai kuingoza huku taifa letu likiangamia mchana wa jua. Watanzania tumeonewa, tumaibiwa, tumenyanyaswa na ujinga wetu wenyewe ya kutosha. Tunalia huku madini yetu yakinyanyuliwa na udongo. Bandari zetu zinauzwa na walafi hatuwezi kusema kitu eti serikali. Kwa nini tusijiundie serikali inayowajibika? Matumbo tu na ma V-8? We can do better than that!
 
Tunawachagua wajinga kwa asilimia kubwa watuongoze kuanzia ngazi ya mtaa hadi taifa, na matokeo yake ndiyo hayo. Ukiwasikiliza viongozi walio wengi utagundua tu kuwa mawazo yao ni ya kipuuzi tu lakini wanashangiliwa na kuheshimiwa kwa ushabiki wa kizuzu (mfano mzuri unapatikana bungeni).
Tunahitaji kuwa na mawazo yanayolenga maendeleo kuanzia ngazi ya chini hadi juu na kuyatekeleza kivitendo vinginevyo tutakuwa tunatamani na kujilaumu wakati wenzetu wanazidi kusonga mbele.
Dunia ya leo siyo ya maneno ila ni ya vitendo na wakati mwingine waweza kutoa maneno yanayowafurahisha watu lakini matendo yako yakawa kinyume chake kwa kuwa matendo ndiyo yanayokuletea faida halisi na ya moja kwa moja!
 
Haaa, unasema hakuna fly over hata moja? Kwani ile ya manzese hujaiona? Usitushushe hivyo bwana. By the way, wewe tatizo lako ni fly over tu? Wanafunzi kukaa chini hilo hujaona tatizo? Na why fly over? Tunahitaji barabara zaidi maeneo ya vijijini ambako ndiko vinakotoka vyakula, sasa wewe unaiangalia Dar es salaam tu na kusahau kwamba kuna majiji mengine kama Mwanza na kuna maeneo ya vijijini ambako hakupitiki kabisa wakati wa kifuku na hivyo tunahitaji kujenga huko pia? Maybe fly over iwe ni last option, tufikirie juu ya kutumia trein, na pia tufocus zaidi katika kujenga barabara vijijini.
Nimependa sana argument yako Mku.
 
Mkuu
ungetusaidia zaidi kwa kuchana ganda lako chooni fasta...ningeona usemi huu mzito na umeuchukulia hatua
 
Back
Top Bottom