Inasikitisha sanaaaaa!

Mercy Clara

Member
Mar 11, 2010
16
0
Mtu kuangamiza familia yako sababu ya mapito ya dunia?

Nazungumzia suala la mtu mmoja kuchoma nyumba makusudi kwa nia ya kumwangamiza baba yake na mama yake wa kambo, Hii ishu ilitokea siku mbili zilizopita huku Mbeya, Soweto ambapo kijana mmoja alikuwa amekorofishana na baba yake ndio akaamua kuchoma nyumba moto kwa kumwagia Petrol then kuilipua. Sasa basi kabla hajafanya hivyo aliwakataza dada yake na mke wake kulala kwenye nyumba ile kwa siku ile ila watoto wake walilala na wamojawapo wa watu waliokufa. Sasa je binadamu kama binadamu mwenye akili yako timamu unaweza ukafanya kitu kama hicho?

Embu tulonge wana wa JF.
 
ukijawa na ibilisi moyoni waweza kufanya lolote ambalo hukutegemea kufanya.....

sasa kijana hautaka babake aoe mke mwingine kwa hofu ya kutopata urithi mara baba atakpofariki. sijui mwenzetu alikuwa na mktaba na Mungu kuwa yeye hata kufa kabla ya mzazi wake??
 
RIP family. Ni vizuri pia tukapata funzo kubwa katika suala hili kuhusu malezi tunayowapa watoto wetu.
 
Hawa ni aina ya vijana ambao ni wavivu wa kufikiria na wavivu wa kutafuta mali. Wanayalaza mawazo yao kwa kujikomboa kwa mali zilizokwisha tafutwa na wazazi wao. Hili ni tatizo kubwa, na kuna migogoro mingi of this kind within our communities. This should end immedietely
 
Hakuna cha Ibilisi wala nini ni kujiendekeza tu, hata mimi nafikiri malezi yanachangia pia. Ibilisi gani huyo akufanye uangamize familia yako bila hatia yeyote pamoja na watoto zako mwenyewe? Basi si angemwacha na mkewe ili naye awe mmoja wapo!
Sasa pamoja na kufanikiwa kumuua baba yake na mama yake je hizo mali atazipata zaidi ya kuozea jela?
 
Hakuna cha Ibilisi wala nini ni kujiendekeza tu, hata mimi nafikiri malezi yanachangia pia. Ibilisi gani huyo akufanye uangamize familia yako bila hatia yeyote pamoja na watoto zako mwenyewe? Basi si angemwacha na mkewe ili naye awe mmoja wapo!
Sasa pamoja na kufanikiwa kumuua baba yake na mama yake je hizo mali atazipata zaidi ya kuozea jela?

basi tufanye ni malaika!!!
 
Imenisikitisha sana hii habari nikaifananisha na ile ya Kigamboni iliyokula roho za watu watano kwasababu za kimapenzi. MUNGU atulinde na kutuokoa na balaa hili
 
Juzi Nilikuwa Mbeya. Jamaa aliyechoma aliamua kujisalimisha mwenyewe katika kituo cha polisi.
Raia wenye hasira kwa moyo mkunjufu wakawaomba askari wakabidhiwe mtuhumiwa waongee nae japo kwa dakika tano tu, lakini askari wakakataa kata kata.
 
Jamani au mganga wake alimwambia afanye hivyo kwa ajili ya yale mambo fulani nini?????????????
Maanaaaaaaaaaaaaaaa!
 
wajumbe mi niseme kwa kifupi tu kwanza, vijana tusome ,tuache uvivu na kutegemea urithi coz sio ishu..pili,kama kijana unaweza kuwa na roho nzito kiasi hicho, tunatengeneza kizazi cha aina gani nchi hii? TUSOME ILI TUONDOE UJINGA,VINGINEVYO HUKO NI KUJILAANISHA TU!
 
Back
Top Bottom