kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
MLEZI wa mtoto mwenye umri wa miaka minane anayedaiwa kunajisiwa, ameiomba Serikali na taasisi mbalimbali kumsaidia fedha za matibabu ili mtoto huyo akatibiwe.
Akizungumza na gazeti hili jana jijini Dar es Salaam, Marium Omary, shangazi wa mtoto huyo ambaye ni yatima anayesoma darasa la pili katika shule ya Msingi Buguruni, alisema tangu mtoto huyo aingiliwe kimwili na mwanaume wa miaka 25 na kuchanwa katika maumbile yake hajapata tiba ya kutosha.
Nalazimika kumvalisha vitambaa hasa anapokwenda shule kwa kuwa haja zinatoka mara kwa mara kupitia njia ya uzazi. Naomba msaada mtoto huyo ashonwe ili awe na maisha mazuri kama watoto wengine,amesema.
Amesema, mtoto huyo (jina limehifadhiwa) alinajisiwa, Agosti mosi mwaka jana saa 3 asubuhi katika eneo la Buguruni.
Mariam amesema, baada ya kufanyiwa kitendo hicho, mtoto huyo alipelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam, akalazwa lakini Daktari aliyekuwa akimtibu alisema hawezi kumshona kabla kidonda hakijakauka hivyo alimpa dawa za kutumia.
Amesema, walipokwenda mara ya pili waliambiwa daktari huyo aliyemtaja kwa jina la Mohamed aliondoka na kuhamishiwa katika hospitali nyingine na kumtaka aende huko alipo lakini alishindwa kwa kuwa hana fedha.
Kwa upande wake, mtoto huyo amesema, siku ya tukio kijana alimuita na kumuomba amsindikize kwenye duka la dawa ghafla akamuingiza kwenye nyumba mbovu na kumlisha pipi aliyoipaka dawa yenye rangi nyeupe akamziba mdomo na kumuingilia kimwili.
Omary amesema, mtoto huyo amepata madhara makubwa kwa kuwa njia yake ya haja kubwa na ndogo vimeunganika na kuwa wamefungua kesi namba 864 ya mwaka 2010 katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala na mshitakiwa, Mwarami Gumbo (25) yupo mahabusu.
Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Wilaya Ilala, Naima Mwanga amethibitisha kuwa kesi hiyo imefunguliwa mahakamani hapo.
Akizungumza na gazeti hili jana jijini Dar es Salaam, Marium Omary, shangazi wa mtoto huyo ambaye ni yatima anayesoma darasa la pili katika shule ya Msingi Buguruni, alisema tangu mtoto huyo aingiliwe kimwili na mwanaume wa miaka 25 na kuchanwa katika maumbile yake hajapata tiba ya kutosha.
Nalazimika kumvalisha vitambaa hasa anapokwenda shule kwa kuwa haja zinatoka mara kwa mara kupitia njia ya uzazi. Naomba msaada mtoto huyo ashonwe ili awe na maisha mazuri kama watoto wengine,amesema.
Amesema, mtoto huyo (jina limehifadhiwa) alinajisiwa, Agosti mosi mwaka jana saa 3 asubuhi katika eneo la Buguruni.
Mariam amesema, baada ya kufanyiwa kitendo hicho, mtoto huyo alipelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam, akalazwa lakini Daktari aliyekuwa akimtibu alisema hawezi kumshona kabla kidonda hakijakauka hivyo alimpa dawa za kutumia.
Amesema, walipokwenda mara ya pili waliambiwa daktari huyo aliyemtaja kwa jina la Mohamed aliondoka na kuhamishiwa katika hospitali nyingine na kumtaka aende huko alipo lakini alishindwa kwa kuwa hana fedha.
Kwa upande wake, mtoto huyo amesema, siku ya tukio kijana alimuita na kumuomba amsindikize kwenye duka la dawa ghafla akamuingiza kwenye nyumba mbovu na kumlisha pipi aliyoipaka dawa yenye rangi nyeupe akamziba mdomo na kumuingilia kimwili.
Omary amesema, mtoto huyo amepata madhara makubwa kwa kuwa njia yake ya haja kubwa na ndogo vimeunganika na kuwa wamefungua kesi namba 864 ya mwaka 2010 katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala na mshitakiwa, Mwarami Gumbo (25) yupo mahabusu.
Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Wilaya Ilala, Naima Mwanga amethibitisha kuwa kesi hiyo imefunguliwa mahakamani hapo.