Zipuwawa
JF-Expert Member
- Nov 28, 2010
- 3,053
- 653
Hili limetokea sasa hivi naomba ushauri wako ili angalau maamuzi yangu yasiwe mabaya.
Mimi nina ndugu yangu amabaye ni mtoto wa Mama yangu mdogo yeye kwa sasa ni marehemu ambaye alijaliwa kuzaa watoto wanne wakike wawili na wakiume wawili, sasa nilipokwenda liziko mwezi uliopita nilikuta yule mtoto wa mwisho yupo darasa la saba. Nilipomuona hali waliyokuwa nayo hao watoto mimi niliona ni bora nimuhaidi kuwa atakapomaliza darasa la saba nitamsomesha hadi hapo atakapopata mafanikio na kuwa mkombozi wa familia yao.
Niliona kwa kipindi atakachomaliza elimu ya darasa la saba basi aje nyumbani kwangu Morogoro ili aweze kujiandaa na mitihani ya shule mbalimbali kwa kusoma pre form one ili atakapoanza mipango ya kupata shule basi yeye interview iwe rahisi kwake na aweze kupata shule.
Jana amekuja kwa kusafirishwa toka Dodoma alipofika mimi kutokana na mihangaiko sikuweza kukaa nae nakumueleza cha kufanya na nini nimemuandalia kwaajili ya masomo yake. Basi leo nilitembelea shule mbili na kuchukua form kwaajili ya kupata nafasi.
Niliporudi mchana baada ya kupata chakula cha mchana na familia yangu basi walikwenda kulala wote mimi nikiwa nachat alinifuata sebuleni na kuniambia kuwa yeye hawezi kukaa kwangu kwani maisha haya hatoyaweza. Nikamuuliza kunatatizo gani? akasema yeye hawezi kukaa nilishtushwa sana kwani huyu mtoto ni mdogo ana umri wa miaka kumi 13 sasa. Mimi nilijiuliza maswali mengi na kukosa majibu ndipo nikampigia dada yake ambaye mimi ni mdogo wangu na kumueleza yeye alianza kwa kulia na kusema nimwambie akirudi yeye si ndugu yake. Kumbuka huyu mtoto hakuwa anaishi na dada yake yeye ndio anajua maisha anayoishi huko aliko kwa mama yake mkubwa.
Dada yake akasema nisimruhusu nikae nae mimi naona kama huyu mdogo wangu anaweza kuniletea matatizo mbeleni kwani ameonesha picha mbaya mapema sana.
Mimi baada ya kufanya mawasiliano na baadhi ya ndugu niliamua kumwambia kesho nitakusafirisha na urudi huko utakakoishi maisha unayotaka . Baadae baada ya kuongea na dada yake akaja na kuniomba msamaha eti anaomba aendelee kubaki mimi nikamuuliza kwanini? hana jibu sasa mimi uamuzi wangu ni kumruhusu aende ili asije leta matatizo katika familia yangu. Mimi hapa ninaishi na mke mtoto mmoja pamoja na mtoto wa kazi hakika Mungu ametujalia maisha ya kuweza hata kubadilisha mboga mara moja moja. Na hata makazi yetu yanaridhisha . Naomba ushuri wako ili niondokane na hili jambo au kwa kusaidia au kutokusaidia kwani mimi naona bora hata nikatafuta mtu baki na mkumsaidia sasa hivi hapa namuangalia yupo mezani anapata chakula.
Mimi nina ndugu yangu amabaye ni mtoto wa Mama yangu mdogo yeye kwa sasa ni marehemu ambaye alijaliwa kuzaa watoto wanne wakike wawili na wakiume wawili, sasa nilipokwenda liziko mwezi uliopita nilikuta yule mtoto wa mwisho yupo darasa la saba. Nilipomuona hali waliyokuwa nayo hao watoto mimi niliona ni bora nimuhaidi kuwa atakapomaliza darasa la saba nitamsomesha hadi hapo atakapopata mafanikio na kuwa mkombozi wa familia yao.
Niliona kwa kipindi atakachomaliza elimu ya darasa la saba basi aje nyumbani kwangu Morogoro ili aweze kujiandaa na mitihani ya shule mbalimbali kwa kusoma pre form one ili atakapoanza mipango ya kupata shule basi yeye interview iwe rahisi kwake na aweze kupata shule.
Jana amekuja kwa kusafirishwa toka Dodoma alipofika mimi kutokana na mihangaiko sikuweza kukaa nae nakumueleza cha kufanya na nini nimemuandalia kwaajili ya masomo yake. Basi leo nilitembelea shule mbili na kuchukua form kwaajili ya kupata nafasi.
Niliporudi mchana baada ya kupata chakula cha mchana na familia yangu basi walikwenda kulala wote mimi nikiwa nachat alinifuata sebuleni na kuniambia kuwa yeye hawezi kukaa kwangu kwani maisha haya hatoyaweza. Nikamuuliza kunatatizo gani? akasema yeye hawezi kukaa nilishtushwa sana kwani huyu mtoto ni mdogo ana umri wa miaka kumi 13 sasa. Mimi nilijiuliza maswali mengi na kukosa majibu ndipo nikampigia dada yake ambaye mimi ni mdogo wangu na kumueleza yeye alianza kwa kulia na kusema nimwambie akirudi yeye si ndugu yake. Kumbuka huyu mtoto hakuwa anaishi na dada yake yeye ndio anajua maisha anayoishi huko aliko kwa mama yake mkubwa.
Dada yake akasema nisimruhusu nikae nae mimi naona kama huyu mdogo wangu anaweza kuniletea matatizo mbeleni kwani ameonesha picha mbaya mapema sana.
Mimi baada ya kufanya mawasiliano na baadhi ya ndugu niliamua kumwambia kesho nitakusafirisha na urudi huko utakakoishi maisha unayotaka . Baadae baada ya kuongea na dada yake akaja na kuniomba msamaha eti anaomba aendelee kubaki mimi nikamuuliza kwanini? hana jibu sasa mimi uamuzi wangu ni kumruhusu aende ili asije leta matatizo katika familia yangu. Mimi hapa ninaishi na mke mtoto mmoja pamoja na mtoto wa kazi hakika Mungu ametujalia maisha ya kuweza hata kubadilisha mboga mara moja moja. Na hata makazi yetu yanaridhisha . Naomba ushuri wako ili niondokane na hili jambo au kwa kusaidia au kutokusaidia kwani mimi naona bora hata nikatafuta mtu baki na mkumsaidia sasa hivi hapa namuangalia yupo mezani anapata chakula.