Hakuna kitu kinachokera kama kuona askari polisi wanaosimamia utekelezaji wa sheria wao wenywe ndio wa kwanza kuzivunja. Mara kadhaa nimekuwa nikiona askari polisi wakiendesha pikipiki bila helmet au askari polisi amempakia mtu asiye na helmet. Nchi nyingine ambako sheria zinasimamiwa vizuri kitu kama hiki kukioni. Lakini hapa kwetu kila siku kinaonekana na wakati huohuo askari wanasimama barabarani kuwakamata waendesha pikipiki bila helmet au kama wamempakia mtu asiye na helmet isipokuwa kama anayekamata ni askari mwenyewe - maana wao kwa wao wanasameheana. Kwa maneo mengine, wao wanaridhia kuvunja sheria kama askari!
Nikiona hivi huwa najiuliza: Hivi hawa askari wanatufundisha nini sisi wananchi! kwamba wao wako juu ya sheria? Kwamba hawajali sheria? Kwamba wana mamlaka ya kufanya watakavyo? Hali hii ni ulimbukeni!
Nikiona hivi huwa najiuliza: Hivi hawa askari wanatufundisha nini sisi wananchi! kwamba wao wako juu ya sheria? Kwamba hawajali sheria? Kwamba wana mamlaka ya kufanya watakavyo? Hali hii ni ulimbukeni!