MwanajamiiOne
Platinum Member
- Jul 24, 2008
- 10,470
- 6,562
Wapendwa habari zenu?
Hebu ninaomba msaada wenu ili nimsaidie huyu shogaangu hapa maana anasema hajui afanyeje... Ilikuwa namna hii
Asubuhi ya leo katika kuzungumza mawili matatu, bi shost akawa anamwuliza mwenzake (mume wake) kama anamfahamu dada mmoja anayefanya naye kazi ambaye shosti alisikia watu wakimsema vibaya huyo dada. Yaani swali lilikuwa " Eti mume wangu unamfahamu vizuri flani?" Anasema badala ya kujibiwa ndio namfahamu au hapana simfahamu- alipokea matusi ya ajabu, mume karukia kumsema shost kuwa anamfanya yeye (mume) mhuni wa kutembea na kila changu, tena kamtaka akome kabisa kumshuku mambo ya kipuuzi kama hayo!! Shoga kabaki mdomo wazi maana anasema yeye hakuwa na wazo lolote baya na wala hakuwahi kumwambia mumewe kuwa anamshuku na mtu yeyote achilia mbali huyo mwanamke!
Mdada wa watu analia tu hapa kwani anahisi mwenzie ana jambo na huyo mdada na mbaya zaidi anasema huyo mdada inasemekana ni HIV + siku nyingi kwani mumewe alishakufa kwa ugonjwa huo.
Sasa nimshaurije?
Hebu ninaomba msaada wenu ili nimsaidie huyu shogaangu hapa maana anasema hajui afanyeje... Ilikuwa namna hii
Asubuhi ya leo katika kuzungumza mawili matatu, bi shost akawa anamwuliza mwenzake (mume wake) kama anamfahamu dada mmoja anayefanya naye kazi ambaye shosti alisikia watu wakimsema vibaya huyo dada. Yaani swali lilikuwa " Eti mume wangu unamfahamu vizuri flani?" Anasema badala ya kujibiwa ndio namfahamu au hapana simfahamu- alipokea matusi ya ajabu, mume karukia kumsema shost kuwa anamfanya yeye (mume) mhuni wa kutembea na kila changu, tena kamtaka akome kabisa kumshuku mambo ya kipuuzi kama hayo!! Shoga kabaki mdomo wazi maana anasema yeye hakuwa na wazo lolote baya na wala hakuwahi kumwambia mumewe kuwa anamshuku na mtu yeyote achilia mbali huyo mwanamke!
Mdada wa watu analia tu hapa kwani anahisi mwenzie ana jambo na huyo mdada na mbaya zaidi anasema huyo mdada inasemekana ni HIV + siku nyingi kwani mumewe alishakufa kwa ugonjwa huo.
Sasa nimshaurije?