Inamaanisha nini?

MwanajamiiOne

Platinum Member
Jul 24, 2008
10,470
6,562
Wapendwa habari zenu?

Hebu ninaomba msaada wenu ili nimsaidie huyu shogaangu hapa maana anasema hajui afanyeje... Ilikuwa namna hii

Asubuhi ya leo katika kuzungumza mawili matatu, bi shost akawa anamwuliza mwenzake (mume wake) kama anamfahamu dada mmoja anayefanya naye kazi ambaye shosti alisikia watu wakimsema vibaya huyo dada. Yaani swali lilikuwa " Eti mume wangu unamfahamu vizuri flani?" Anasema badala ya kujibiwa ndio namfahamu au hapana simfahamu- alipokea matusi ya ajabu, mume karukia kumsema shost kuwa anamfanya yeye (mume) mhuni wa kutembea na kila changu, tena kamtaka akome kabisa kumshuku mambo ya kipuuzi kama hayo!! Shoga kabaki mdomo wazi maana anasema yeye hakuwa na wazo lolote baya na wala hakuwahi kumwambia mumewe kuwa anamshuku na mtu yeyote achilia mbali huyo mwanamke!

Mdada wa watu analia tu hapa kwani anahisi mwenzie ana jambo na huyo mdada na mbaya zaidi anasema huyo mdada inasemekana ni HIV + siku nyingi kwani mumewe alishakufa kwa ugonjwa huo.

Sasa nimshaurije?
 
"acha kulia shida za duia Mungu yupo atakusaidia"kila jambo lina mwanzo na mwisho,moyo wa binadam ni msitu mnene
 
walianzaje mpka huyo shost wako akamuulizia huyo mdada? yani alimuulizia tu ili mradi au kuna alilotaka kujua? wengine hata hawajuagi kuiba, wakianza kuingizza mkono tu wanakamatwa, ndio huyo mkaka sasa, anaulizwa be anasema che.
 
....

Sasa nimshaurije?


Mwache alie hadi machozi yake yaishe, usimbembeleze.

Akishanyamaza mshauri ajiweke tayari kufanya maamuzi mazito na magumu.

Katika kufanya maamuzi hayo, hatua ya kwanza, akapime ngoma. Majibu yatampa mwanga wa nini afanye next.

One step at a time.
 
Hii kwa kibongo bongo tunaita defence mekanizimu jamaa alikuwa anajaribu kujilinda kwa nafsi yake alijua kuwa huyo shost wako anataka kumtega si unajua nyie kwa maswali yenu ya kimtego mtego je angesema anamjua na si kumfahamu hapo ingekuwa kasheshe zaidi.
 
analia nini sasa huyo dada!

hiyo ndume imejistukia ikaamua kuweka selfdefence

kwa kuporomosha matusi

watayamaliza wao wenyewe maana mambo ya ndoa.......!
 
walianzaje mpka huyo shost wako akamuulizia huyo mdada? yani alimuulizia tu ili mradi au kuna alilotaka kujua? wengine hata hawajuagi kuiba, wakianza kuingizza mkono tu wanakamatwa, ndio huyo mkaka sasa, anaulizwa be anasema che.

Dada yeye mwenyewe anasema jana jioni ofcn kwake secretary wao alikuwa anasimulia habari ya dada mmoja ambaye anafanya kazi ofc flani (ambako mumewe naye anafanya) vituko vya huyo dada ni vikubwa si ndio akaona amwulize mumewe kama anamfahamu huyo mdada akiwa anataka kujua kama kweli ofc hiyo kuna mtu wa jina hilo. Hayo majibu alopata kabadki kaduwaa.
 
Mwache alie hadi machozi yake yaishe, usimbembeleze.

Akishanyamaza mshauri ajiweke tayari kufanya maamuzi mazito na magumu.

Katika kufanya maamuzi hayo, hatua ya kwanza, akapime ngoma. Majibu yatampa mwanga wa nini afanye next.

One step at a time.
Aksante Ama nitafanya kama ulivyonishauri. Hivi inawezekana jamaa (shem) anamega ?? Maana mbona kareact kihivyo??
 
DADA ZANGU,
maswala ya wanaume muyachukulie ''kawaida''!kinyume na hilo mtakufa mapema kwa stroke
 
Hii kwa kibongo bongo tunaita defence mekanizimu jamaa alikuwa anajaribu kujilinda kwa nafsi yake alijua kuwa huyo shost wako anataka kumtega si unajua nyie kwa maswali yenu ya kimtego mtego je angesema anamjua na si kumfahamu hapo ingekuwa kasheshe zaidi.

Aksante Fidel ah yaani hawa watu wengine kwa kujishuku!! Sasa kaambiwa kuwa yeye alikuwa anauliza kwa nia njema tu kwa kuwa alitaka kujua kama yupo ndo jamaa kawa mdogo kama piriton hajasema kitu zaidi ya kukauka lakini ndo keshachemka tena. Ngoja dada akacheck afya
 
Dada yeye mwenyewe anasema jana jioni ofcn kwake secretary wao alikuwa anasimulia habari ya dada mmoja ambaye anafanya kazi ofc flani (ambako mumewe naye anafanya) vituko vya huyo dada ni vikubwa si ndio akaona amwulize mumewe kama anamfahamu huyo mdada akiwa anataka kujua kama kweli ofc hiyo kuna mtu wa jina hilo. Hayo majibu alopata kabadki kaduwaa.

eeh ngoja kwanza nimpe pole, mie ndio ningembania hapo hapo mpaka kieleweke...sasa hapo janaume ndio litanuna kukwepa kuhojiwa...haaa cjui kwanini ckuwaga sista mie.
 
Unauliza makofi polithi na wewe? Au unauliza vilungu kwa mgambo wa city hapo pigia mstari.
Eh MUNGU tunusuru waja wako !! Kumbe ndo maana shem anamzuiaga shost kwenda kuangazwa!! Au anajihisi kaukwaa? Jamani wanaume wengine wauaji!!!
 
DADA ZANGU,
maswala ya wanaume muyachukulie ''kawaida''!kinyume na hilo mtakufa mapema kwa stroke

Tatizo mashost wa M1 wanapenda uzungu uzungu ishu ndogo kama hii tayari uwe unawaambia wanakuwa fair tu mambo mengine ni ya kumezea mate tu siku akirudi shirt linanukia dawa za nywele za kike itakuwaje?
 
Aksante Fidel ah yaani hawa watu wengine kwa kujishuku!! Sasa kaambiwa kuwa yeye alikuwa anauliza kwa nia njema tu kwa kuwa alitaka kujua kama yupo ndo jamaa kawa mdogo kama piriton hajasema kitu zaidi ya kukauka lakini ndo keshachemka tena. Ngoja dada akacheck afya[/QUOTE]


ni vizuri lakini mhh, inauma sana ukijiona ulikuwa mtulivu/mwamnifu then lenzako likuletee magonjwa, yaani hapo ni anajifia pole pole kwa mawazo...yaani wacha tu.
 
eeh ngoja kwanza nimpe pole, mie ndio ningembania hapo hapo mpaka kieleweke...sasa hapo janaume ndio litanuna kukwepa kuhojiwa...haaa cjui kwanini ckuwaga sista mie.
Dada mie nimebakia kimya ila nimemshauri atulie kwanza wala asipanick na mume akisms kitu akae kimya kama si cha lazima kujibiwa lengo ni kumpa muda wa kutafakari na kuyapanga maswali ya kumbana baada ya kazi nyumbani. Hata mie imenishangaza sana nakwambia amenionyesha hizo sms alizoendelea kutumiwa na Mr wake nimechoka mwenyewe.
 
Sometimes wanawake mnakera, hata mie nimeshawahi ulizwa mtu ambaye simfahamu kabisa kisa huyo dada ni famous kwa kugawa uroda mtaani kwetu na hupenda kuchangamkia waume za watu. Nikaulizwa unamfahamu Fulani? nikauliza ndo nani huyo? nikaambiwa mh unajifanya humjui wakati ndo superstar hapa mtaani, aaaaaaaaaaaaagrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr kweli nilipandwa na hasira ya kulazimishwa kumjua mtu ambaye hata siku moja sikuwahi kumsikia wala kumwona, lkn nikaona omvi wa nini nikamwambia twende basi ukanioneshe, nikaambulia kuambiwa kumbe namtamani. ssa tokea hapo unajua hulka ya binadamu nikawa nataka nimwone huyo anayesujudiwa kuwa ni super star, JAMANI kuja kumwona huyo dada mwenyewe hata hamu sina, kwanza nahisi kila kitu cha kununua pale alipo, WEUPE wa dukani, Makalio ya kichina, yaani nahisi hata kutapika.halafu kila mtu ana type zake anazo penda jamani wake zetu, si kila mwanamke eti kisa kajichubua na ana makalio ya kichina basi eti ndo MZURI. Nilichokifanya baada ya hapo sasa, nikagundua wife confidence imemshuka nadhani huko saluni anakokwenda walimzungumzia huyo dada kuwa ni mwizi wa waume za watu akapata wasi wasi. Jmosi moja nikampeleka shopping kidogo, halafu jioni nikampeleka pale Girrafe Hotel just kupata kaupepo na wine ya kuzugia, akafurahi vibaya mno! lastly nikamwambia unajua wewe ndo MAMA YANGU UNAYENILEA? Na MTOTO HAKUI KWA MAMA so please take care of me. (Huwa anapenda sana kusema yeye ndo mama yangu kwa sasa) Basi everything ikarudi ikawa normal
 
Tatizo mashost wa M1 wanapenda uzungu uzungu ishu ndogo kama hii tayari uwe unawaambia wanakuwa fair tu mambo mengine ni ya kumezea mate tu siku akirudi shirt linanukia dawa za nywele za kike itakuwaje?

ishu ni kwamba mdada story alizopewa huko ndio zilimuwasha akitaka kumjua/kumfahamu zaidi huyo mtuhumiwa, alikuwa hana hili wala lile kuuliza mackini, majibu aliyopewa ndio hayo tena.
 
Tatizo mashost wa M1 wanapenda uzungu uzungu ishu ndogo kama hii tayari uwe unawaambia wanakuwa fair tu mambo mengine ni ya kumezea mate tu siku akirudi shirt linanukia dawa za nywele za kike itakuwaje?
Eti uzungu uzungu hata ningekuwa mie Fidel ningemaka kwa sababu huyo dada sifa zake si haba sasa nikiona Mr kareact hivyo nikaekimya na kufungulia magonjwa mlango? Nyie wanaume sijui mkoje yaani mnatake kila kitu simple tu!!
 
Eh MUNGU tunusuru waja wako !! Kumbe ndo maana shem anamzuiaga shost kwenda kuangazwa!! Au anajihisi kaukwaa? Jamani wanaume wengine wauaji!!!

Uzuri kama anamega kawaida kama anajiexpress hapo sasa msiba mwingine huo.
Wanaume bana we tuangalie tu kama tulivyo tunajua nn kilichopo moyoni mwetu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom