Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,778
- 59,133
Hivi inakuaje mwanamke anaondoka nyumbani kwake anamuaga mume wake ambae ni mzuri as in hamnyanyasi na anajitahidi siku zote kumfanyia mke yaliyo mema..alafu anaenda kukutana na kimada wake ambae nae ni mume wa mtu ambae nae mke wake anajitahidi kumfanyia yaliyo mema?Yani wote wanavunja ahadi zao kwanza kwa kutoka nje ya ndoa zao alafu wanafikia kutamani mpaka kutembea na mume/mke wa mwingine!Watu hawa ambao kuna watu wanawaangalia kama 'rolemodels' kwenye maswala ya maisha tuwachukulieje?