bornagain
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 3,383
- 1,354
Jamani ifike mahali sasa hili suala la kupitisha bajeti kwa mwenyekiti wa bunge kusema eti wanaokubali waseme ndiyo na wasiokubali waseme siyo iishe kabisa. Huu ni udikteta, jana kwenye bajeti ya wizara ya maji sauti za wanaosema sio zilikuwa nyingi kuliko waliosema siyo lakini kwa sababu ya usanii wa Jenesta Mhagama akasema eti waliosema ndiyo wameshinda eti na kwa hiyo bajeti imepitiswa. Ni upuuzi wa hali ya juu sana maana wabunge wengi walichangia kwa hisia na walikua wameshaapa kutoipitisha bujeti ya huyu Prof. Jumanne Maghembe mzee wa bodi ya Kahawa