Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Wadadisi wengi wa habari niliozungumza nao, wanatafsiri kitendo cha baadhi ya viongozi waandamizi serikalini, kutamka wazi hata kabla ya mahakama kuu kuridhia, kwamba serikali haina budi kuilipa Dowans fidia iliyotolewa na jopo la upatanishi, kuwa kina lengo la kuishinikiza mahakama kuu kuridhia fidia hiyo. Je hayo yana ukweli wowote? Nakaribisha maoni.