Kuna baadhi ya wanasiasa na wanaJF walibeza maandamano ya Chadema kuwa hayatakuwa na impact yeyote, wengine wakadiliki kusema Chadema hawatapata watu Mwanza, lakini kadili siku zilivyoendelea yakatikisa anga lote la Tanzania hadi rais pressure ikampanda akaanza kulalamika kuwa kuna mpango wa kupindua nchi. Impact hiyo iliendelea kuwatoa watu ambao hatukutegemea kama kina Sophia Simba, Wasirra, Tendwa. Wengine tuliowasikia ni Fredrick Sumaye, Mzindakaya, Sitta, Lowassa nk. Hadi leo hii hata baada ya maandamano kwisha bado mtikisiko unaendelea kutikisa. Jana Pinda alipokewa na mabango yaliyoongelea maandamano ya Chadema. Hamuoni kuwa lengo la maandamano ya Chadema kisiasa limefikiwa. Nawauliza waliokuwa wanabeza wako wapi mbona hawaonekani tena au na wao wamekumbwa na impact ya maandamano, wanaona aibu.