Imani ya Ushirikina na Maisha ya Mwananchi

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
Ndugu msomaji,

Napenda kuuliza yafuatayo ili kuweza kujadiliana kuhusu haya mambo yanayo zingira jamii zetu.

--Je, unaamini nini kuhusu uchawi? Upo au haupo?
--Je,ulisha shuhudia mtu aliye logwa (rogwa) na kuamini kuwa amelogwa?
--Je, uchawi unapingana vipi na imani yako nyingeneyo kama unayo?
--Uchawi unachukuliwa vipi mbele ya vyombo vya sheria?
--Je, mazingaombwe ni aina ya uchawi?...majini nayo?

Ahsanteni.


SteveD.
 
Last edited by a moderator:
Kila siku naona issues za dini zikikatwa hapa za ukristo na uislamu lakini leo ningependa nitoke kitofauti kidogo. Siku hizi ukiamini kwenye imani zetu zetu za asili unaitwa 'mshirikina' lakini kwa wale tuliokulia bush, mtakumbuka viji imani vingi tulivyokua tukivipata toka kwa bibi na mama zetu kama-

-"Usipige mlunzi usiku, utamwita shetani",
-"Usitoe au kuomba chumvi kwa jirani usiku",(cant remember the
reason!)
-"Usishone nguo wakati umeivaa, utakua maskini wa kutupwa!"
-"Usishone chupi iliyochanika", (sababu???)
-"Usimpige mwenzio kwa nguo, na kama umefanya hivyo uitemee
mate."(sababu??)
-"Usimruke mwenzako miguu, kama umefanya hivyo-kusahihisha
inabidi umruke tena." (Sababu??)
-"Usifagie usiku." (Sikumbuki sababu)
-"Usimpige mwenzako kwa fagio." (Sababu?)

Ukiachilia mbali 'makatazo' hayo, pia kilikua na imani nyingine kuhusiana na matukio- kama vile ukimsikia bundi ama Paka mweusi analia ni ishara kwamba kutatokea msiba, Kakakuona akionekana anawekewa maji(ukame), unga(njaa) na bunduki(vita)- atakachokifuata kwanza ndio kinatoa picha halisi ya utabiri kama ilivyo kwenye mabano.

Je kuna anayejua sababu za imani hizi kuwepo? na naomba kama kuna mwenye mpya zaidi ya hizo hapo juu atupatie hapa na sababu zake, najua kila kabila lina almost imani zake tofauti na mengine.
 
"Usipige mlunzi usiku, utamwita shetani"
Hii ni kati ya imani ambayo imeanza kipindi kile ambacho machifu ambao walikuwan wakishirikiana na walowezi (Wazungu)kukamata watumwa, upigaji wa mruzi ilikuwa ni njia mojawapo ya kuwahatarisha au kuwataarifu watu kuwa kuna hatari kwa hali hiyo wajihadhari.
Sababu nyingine ni kuwa kipindi cha usiku kuna baadhi ya wadudu hatari kama vile nyoka, ambao wanafutiwa na sauti za miruzi. Kwa wale wanaotoka mikoa ya Tabora, Shinyanga na Mwanza nadhani wana maelezo ya kutosha kuhusiana na upigaji wa miruzi usiku.



"Usitoe au kuomba chumvi kwa jirani usiku",(cant remember the reason!).

Chumvi ni bidhaa ambayo rahisi kupatikana, Kipindi hicho kwa mwanamke kupika chakula bila chumvi ilihesabika kama dharau na kutojari kile anacho kifanya. kwa hali hiyo kuishiwa na chumvi kulihesabika kama kutokuwa makini na jiko lako. Ndio maana wanawake kwa kuona hivyo wakatengeneza baadhi ya misamiati ya kuombea chumvi ili waume zao wasitambaue kuwa wameishiwa chumvi Ex: chumvi iliitwa kwa jina la Mkuu wa Jiko, au kwa jina la asili Munyu.


-"Usishone nguo wakati umeivaa, utakua maskini wa kutupwa!"

Kushona nguo wakati umeivaa kulihesabiwa kama ni kujichulia kifo chako. hii ilionekana kama unajishonea sanda mwenyewe. Hii ilikuwa kuwatisha haswa watoto wadogo kwani kushona nguo huku ukiwa umeivaa ni hatari kwao kwani kunaweza kusababisha kujichoma kwa sindano hizo.


-"Usishone chupi iliyochanika", (sababu???)
Kushona chupi iliyo chanika kulihesabiwa kama umaskini, kwani chupi ni kati ya nguo ambayo ni bei rahisi, sasa ikitokea kwa mwanamke au mwanaume kushona chupi iliyo chanika kulihesabiwa kama dalili ya Ubahiri.


-"Usimpige mwenzio kwa nguo, na kama umefanya hivyo uitemee mate." (sababu??)
Kumpiga mwenzio kwa nguo kuna weza kusababisha nguo yako kuchanika, ukizingatia nguo ilikuwa ni bidhaa ghali kidogo. Si mnajuwa tena yaani Msimu hadi Msimu.


-"Usimruke mwenzako miguu, kama umefanya hivyo-kusahihisha inabidi umruke tena." (Sababu??).

Watoto walikuwa wakiambiwa si heshima kumruka mtu mzima, ki ukweli si adabu njema, na hata kurukana watoto kwa watoto kulihesabika kama yule aliye rukwa kuwa mfupi yaani kutamsababishia kuwa Andunje. Lakini sababu mojawapo kubwa ilikuwa Kumruka mwenzio miguu ni hatari kwani wakati wewe unataka kumruka mwenzio na yeye wakati huo huo akakunja miguu kunaweza kusababisha mrukaji kudondoka na kuumia.


-"Usifagie usiku." (Sikumbuki sababu).

Kipindi hicho cha zamani ilikuwa kufagia usiku si kwamba kulikatwazwa ila ukifagia usiku haswa chumbani usitupe taka nje, kwa sababu nyumba zilikuwa zinatumia Vibatari na mwanga wa kibatari haukuwa kama huu wa taa za umeme, kwa hali hiyo ilikuwa rahisi kwa mtu kufagia KITO au KIPURI au kitu chochote cha thamani na kukitupa nje bila kujuwa. kwa hivyo basi unapofagia ndani au chumbani usiku takataka unazikusanya pembeni ya chumba na asubuhi yake inakubidi kuzichambua kuangalia kama kuna KITO au kitu chochote cha thamani kabla ya kutupa takataka nje.


-"Usimpige mwenzako kwa fagio." (Sababu?).
Fagio ni kifaa ambacho ni cha kufagilia uchafu, kumpiga mwenzio kwa fagio kunaweza kumletea madhara, kwani utakapo mpiga mwenzio na ukamdhuru aidha kwa kumjeruhi kunaweza kupelekea kupata bakteria au vijidudu vywa maradhi kama vile Pepopunda au Tetenasi

Ukiachilia mbali 'makatazo' hayo, pia kilikua na imani nyingine kuhusiana na matukio- kama vile ukimsikia bundi ama Paka mweusi analia ni ishara kwamba kutatokea msiba, Kakakuona akionekana anawekewa maji(ukame), unga(njaa) na bunduki(vita)- atakachokifuata kwanza ndio kinatoa picha halisi ya utabiri...

Wanyama ni viumbe ambao M'Mungu amewajaalia kuwa na sense kubwa wakati mwingine kushinda binadamu. Bundi, Paka, Fisi au Tai ni wanyama ambao wanauwezo wa kunusa harufu ya mtu au kiumbe ambacho kinakaribia kufa, kwao inawajia kama harufu ya mzoga. Binadamua au wanyama wanapokasirika au kukaribia kufa au wakiwa na furaha, au wakitaka kufanya mapenzi kuna harufu wanatoa ambayo kitaalamu inaitwa Pheromones.(The term "pheromone" was based on the Greek pherein (to transport) and hormon (to stimulate).) Hali hii ni mabadiriko ya kikemikali ambayo utolewa na viumbe hususani wanyama na wadudu.

Vile vile wanyama wanauwezo wa kuhisi majanga ya kiasiri kama vile Vimbunga, mafuriko na matetemeko ya ardhi, majanga ambayo binadamu si rahisi kuyahisi au kuyajuwa mpaka kwa kutumia vyombo vya uchunguzi
.
 
Ni kweli sheria haitambui uchawi?


Na Majaliwa Mohamed.
Posted Date::12/13/2007


Katika jamii nyingi duniani hasa za kiafrika, imani za kichawi zimejikita na kuota mizizi kiasi cha baadhi ya jamii au wanajamii fulani kutukuza imani hizo wakiamini ni sehemu ya mila zao.


Na pia katika jamii hizo zenye imani ya uchawi, imedhihirika ili uwe maarufu na mwenye kuheshimiwa katika jamii hiyo husika, uwezo wako katika kumiliki na pia kutumia nguvu zinazoaminika ni za kichawi huwa ni kigezo kikuu na muhimu.


Kwa maneno mengine ni kuwa heshima na ukubwa wa mtu hupimwa kwa kuangalia uwezo wake wa kichawi alionao.


Zaidi katika jamii za aina hii, watu wake huamini kuwa kwa mafanikio katika maisha, hutokana na jitihada katika matumizi ya nguvu za kichawi, hii hujumuisha kuhusisha kuhusisha imani hizo katika nyanja mbalimbali za maisha kama vile biashara, elimu, kazi, michezo na hata uongozi (siasa).


Lakini ni ukweli usiofichika kuwa kuna baadhi ya watu ambao hutumia nguvu za kichawi kudhuru wenzao katika miili yao au hata katika mali zao.

Kimsingi katika sheria, kumdhuru mtu kwa makusudi kwa namna yoyote ile ni kosa chini ya sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai.


Sasa je, utambuzi huu wa sheria juu ya makosa yanayohusu kumdhuru mtu katika mwili wake, hufika hata kwa makosa kama hayo yanayoaminika kutendeka kwa njia ya kichawi?


Swali hili litatusaidia kutambua kama mashitaka au malalamiko yanayohusiana na uchawi yanapokelewa au kutambulika na sheria.


Ni siku za hivi karibuni tu katika maeneo ya kanda ya ziwa , hasa katika mikoa ya Shinyanga na Mwanza, kulizuka mfululizo wa matukio ya mauaji yanayofanywa zidi ya vikongwe kwa imani kuwa vikongwe hao walikuwa na nguvu za kichawi wanazozitumia kuwadhuru watu wengine.


Baada ya uchunguzi rasharasha, sababu zilizoelezwa kuchochea mauaji hayo ni ukweli kuwa hata ukiamua kumchukulia hatua za kisheria mtu unayeamini kuwa ndiye mchawi wako, haitosaidia kitu kutokana na ukweli kuwa serikali au sheria haitambui uchawi.


Hivyo wauaji waliamini hata wakiwapelekwa katika vyombo vya dola, bibi vizee hao ambao ndio hasa waathirika katika mauaji hayo, wataachiwa huru kutokana na kukosekana kwa ushahidi kuthibitisha malalamiko yao ya uchawi.


Kwa mujibu wa sheria ya uchawi ya mwaka 1920 toleo la 18, sheria imejidhihirisha kutambua baadhi ya makosa yanayotokana na imani za kichawi, hii ni pamoja na mtu kutengeneza au kumiliki vifaa vinavyoaminika kuwa ni zana za kichawi.


Kwa mashitaka kama haya huwa ni utata katika kuyaendesha hasa kwa upande wa mashitaka ambao ndio wenye jukumu la kuthibitisha madai hayo zidi ya mshitakiwa.


Hii inatokana na ukweli kuwa ni vigumu kuthibitisha kuwa vitu au vifaa alivyokutwa navyo mshitakiwa ni kweli vinanguvu inayoaminiwa kuwa ni ya kichawi.


Katika hili pia kuna wanaharakati wengine hujenga hoja kuwa iweje sheria imuadhibu mtu kwa kosa la kudhania tu.


Ukweli ni kuwa ni vigumu kama siyo haiwezekani kabisa kuthibitisha uwezo wa nguvu za kichawi wa vitu husika mbele ya mahakama.


Lakini kwa upande mwingine vifaa ambavyo hudhaniwa ni vya kichawi hujieleza vyenyewe kutokana na asili yake na hasa baada ya mshitakiwa kushindwa kujitetea kwa kueleza matumizi ya vifaa hiyo na jinsi alivyovipata.


Hii inatokana na ukweli kuwa mara kadhaa imetokea watu kukamatwa na viungo vya binaadamu kama vile sehemu za siri za watoto wadogo na vingine vinavyofanana na hivyo.


Na hili pia si rahisi kuthibitisha kuwa viungo hivyo vina nguvu za kichawi. Endapo upande wa mashitaka ukiweza kuthibitisha kuwa vifaa hivyo vina nguvu au inaaminika kuwa na nguvu za kichawi, mtuhumiwa atashitakiwa na kuadhibiwa kwa mujibu wa sheria hii ya uchawi, lakini pia mshitakiwa anaweza kufunguliwa kosa lingine kwa kukutwa na viungo vya binaadamu chini ya sheria ya makosa ya jinai.


Kosa jingine na ambalo ni maarufu sana linalotambuliwa na sheria ya uchawi ni lile la kutishia watu kuwaumiza au kuwadhuru kwa kutumia nguvu za kichawi.


Kutishia katika sheria ni kosa hata pasipo kuhusisha imani ya kichawi. Japo ni agharabu kutokea, lakini imetokea mara kadhaa baadhi ya wanafamilia wa familia moja au mtaani kutishiana kulogana kutokana na uhasama uliopo kati yao.


Vitisho vya kichawi ni kosa kwa mujibu wa sheria hii ya uchawi, kosa hili linaweza kufanywa aidha kwa maneno ya mdomo au maandishi. Vitisho peke yake vinatosha kuthibitisha kosa hilo.


Vitisho hivi vinaweza kuwa vya kuondoa maisha ya mtu, yaani kifo, kumbebesha ugonjwa au kumdhuru vinginevyo kwa nguvu za kichawi, na adhabu ambayo imewekwa na sheria hii juu ya kosa hili ni kifungo kisichopungua miaka saba, lakini pia mahakama ina nguvu ya kisheria kubadilisha adhabu hii pindi ikiona inafaa kufanya hivyo.

Source link: Mwananchi.co.tz

SteveD.
 
Story by AMINA KIBIRIGE


Those who dont believe in 'kamuti' as the kamba call it or witchcraft and protection, read this....soooo hilarious!!!!!!



Publication Date: 1/8/2008

Mombasa residents were on Sunday night treated to comical drama as people who had looted property during the chaos started returning the stolen goods.

A hardware dealer in Mwandoni, Kisauni constituency who lost timber worth thousands of shillings, had on Friday issued a one-week ultimatum to all those who had stolen from his associate’s hardware to return the wood planks. He had vowed at the end of the ultimatum to invoke a special Islamic prayer.

The prayer, known as halbadiri in Kiswahili, is said to be invoked by people who are wronged to seek justice from God. It is one of the most feared curses at the Coast as it is believed that it brings calamities to those it is directed at.

Suffering as a consequence

One self-confessed thief said he returned 20 planks of wood he had stolen after learning of the ultimatum.

“Despite the fact that I was turning myself into a laughing stock, I returned the planks that I had stolen for fear of what might befall me,” said the man who identified himself as John Josh.

“What drove us to this point is a rumour doing rounds that one man dropped dead as he carried away a stolen TV set from an electronic shop in Magongo,” said the thief.

“Why wait for such fate to befall me yet there is a deadline I can beat?” he said as of dozens others returned the timber. Some hired handcarts to return the loot.

According to local residents, such prayers, probably already resorted to by many others, were actually working as some suffered in the privacy of their homes.

“It is not a joke! Many people are suffering as a consequence of their actions,” said one woman who did not give her name.

“I have seen with my own eyes several people who are now complaining that they cannot go the toilet anymore, just a few days after looting,” she said.

Speaking to the Nation, Sylvester Wainaina, a worker at the hardware shop explained that the timber had been bought from Tanzania last year for sale.

“The timber dealer approached the hardware owner and told him that he wanted to invoke the prayer so that those who stole the wood would be punished if they did not return the property in seven days,” said Mr Wainaina.

Curious residents

Word spread quickly and the thieves started returning the timber.

“They started coming in from Sunday at 11pm and have not stopped till now,” he added.

Mr Wainaina and other curious residents sacrificed their sleep and spent the night at the premises to watch the unfolding scenario.

He says several other looters have confessed saying the items they stole like beds and sofa sets had caused them to “see people they did not know”sharing their beds with them.

In a call for peace, Kisauni chief, Mohammed Nzaro asked all those who had taken what did not belong to them to return them even if it meant dropping the goods at the village elder’s home.

“Nobody is going to persecute them. All we ask is they return what does not belong to them so as to save themselves from any unforeseen calamities,” said the chief.

Uphold peace

In Malindi, religious leaders yesterday met district commissioner Anne Ng’etich to chart the way forward for peace.

The leaders from the National Council of Churches of Kenya (NCCK), Supreme Council of Kenya Muslims (Supkem), Council of Imams and Preachers of Kenya (CIPK), Muslims for Human Rights (Muhuri) and other organisations held a two-hour meeting with the DC over the issue and asked for the participation of the provincial administration.

Addressing the Press after their meeting, CIPK Malindi branch treasurer Ustadh Shamy Athman appealed to leaders at the national level to uphold peace.

“We have lived peacefully as brothers and sisters for 44 years. We can’t now start killing one another unless somebody incites us. We must stop this,” he said in a statement on behalf of the other leaders.

He said truth, justice and people’s rights should be upheld and violence shunned. Top leaders should consider the future generations of the country and come together to cultivate peace, he said.

The Rev Diane Kawira of the Methodist Church of Kenya urged President Kibaki and Mr Raila Odinga to visit clash torn areas and meet the victims to restore peace in the country.

She urged district commissioners, district officers and chiefs to start peace campaigns throughout the country to sensitise the people against violence.

The Rev Kawira said the religious leader’s visit to Mrs Rotich was to ask her to coordinate peace programmes with Non-Governmental Organisations and all stakeholders in the area to end the chaos.

NCCK’s Hosea Shikuku appealed to the leaders to make sacrifices and compromise their hard-line positions for the sake of bringing peace to the country.

“The only way to bring peace is for one or both of you to make a sacrifice, otherwise the curse of all Kenyans will fall upon you,” he warned the leaders.

Meanwhile, Supkem Coast branch has formed a committee to sensitise the public on the importance of peace and effects of violence. The Upendo Peace Committee will go to all districts in Coast Province targeting the youth, parents, and religious leaders preaching the message of peace.

Speaking by telephone, the council’s Coast chairman, Sheikh Juma Ngao, said the committee aimed to offer guidance and counselling to avoid a repeat of what happened during the Islamic Party of Kenya (IPK) wave in the early ‘90s where many youths were misused by political leaders.
 
Ni katika tukio linalohusishwa na ushirikina


Na Irene Lipende


MTOTO wa miaka mitatu Halima Said, amefariki dunia baada ya kuchunwa ngozi na kunyofolewa baadhi ya viungo vya mwili.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala Masindoki Masindoki aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa mtoto huyo alikutwa amefariki dunia eneo la Tabata Darajani jijini Dar es Salaam.


Alisema alikutwa akiwa amechunwa ngozi, kanyofolewa macho, katolewa utumbo na kukatwa sehemu za siri.


Akielezea tukio hilo Kamanda Masindoki alisema kuwa lilitokea juzi saa 4:00 asubuhi eneo la Tabata Darajani ambapo ndiko kulikopatikana mwili wa marehemu.


Alisema mtoto huyo alipotea nyumbani kwao katika mazingira ya kutatanisha Desemba 29 mwaka jana katika ukumbi wa sherehe wa Mama Karolo ulioko Vingunguti jijini Dar es Salaam


Alisema alienda huku pamoja na mama yake Editha Valentino katika sherehe za harusi za ndugu yao zilizofanyika ukumbini hapo.


Alisema pamoja na jitihada za wazazi wake kumtafuta mtoto huyo hakuonekana na ndipo wazazi hao walipoamua kutoa taarifa katika kituo cha polisi cha Buguruni.


Alisema katika tukio hilo ambalo wazazi wa mtoto huyo wamelihusisha na mambo ya ushirikina, lilileta mgongano baina ya baba mzazi wa mtoto huyo Said Ramadhani (28) kumtuhumu mama mkubwa wa mtoto huyo Aulelia Thomas (65) kuwa ndiye aliyehusika na mauaji hayo.


Alisema baada ya maiti ya mtoto huyo kukutwa mama mkubwa wa mtoto huyo alifika katika eneo la tukio ambako wananchi wenye asira walimvamia na kutaka kumpiga na aliokolewa na askari aliyekuwapo katika tukio hilo.


Kamanda Masindoki alisema askari katika kuokoa maisha ya Aulelia walimpeleka kituo cha polisi Buguruni ndipo wananchi pia walipotaka kuvamia kituo hicho lakini kwa ulinzi hawakufanikiwa na kuamua kwenda kufanya fujo nyumbani kwake ambapo waliharibi mali mbalimbali.


Kuna information nyingi zime miss kwenye hii habari,sijui ni kwa sababu ya kimaadili au ndio mwundelezo ulele wa "baadha ya mambo ya natakiwa yasisemwe,sababu selikari aiamini ushilikina"

Kwa habari nilizo nazo zinasema kwamba huyu Bibi Aulelia Thobias alipo banwa alikubari kwamba hicho kiumbe kilicho onekana kimechunwa ngozi si mtoto bali ni 'mdoli' tu wa kimazingira na nikweli kwani baada ya kusema hivyo wakazi wa maeneo yale waliongozana na polisi mpaka makaburini kilipozikwa kiumbe kile na kufukua kaburi ambako walikuta kaburi walimozika HAMNA KITU.
Sasa kama haya mambo yapo na yanaonekana live,nasisi hasa vyombo vya habari na serikali bado wana fumbia macho maswala haya ya Ulozi kweli tutafika!!??
kuna kitu gani hasa hapa ambocho hakizungumziki?kama ni kweli nyinyi wenyewe mnashiliki kwenye mambo hayo ndio maana mnapata nafasi za uongozi ndio.. mnafichaa...!?
Sasa kam mnaona mambo hayo mazuri kwa kurahisisha mabo kwanini yasiwekwe wazi kiasi ambacho kita tuwezesha kusafiri na hizo NYUNGO mpaka china kwa bei rahisi kuliko kuwatajirisha makampuni ya ndege.
WHY........jamani embu wekeni wazi hizi kamati za ufundi.....
 
Naililia nchi yangu! Namlilia Halima! Badala ya watu kukemea hizi imani chafu zilizotanda katika jamii yetu tunaanza kukamatana wenyewe! mambo haya yanatokana na imani hizi na ndizo zinazowapelekea watu kufanya unyama kama huu. Huyo mama yake mkubwa inawezekana kabisa kuwa hahusiki lakini kwa vile jamii imeishamhukumu ndiyo basi. Mtu yeyote akibanwa vizuri atakiri kwa jambo lolote ndiyo maana torture si njia ya kutafuta ukweli! Inatakiwa watafutwe wahusika wote (sio kwa kutumia mibano) kisayansi na pale watakapopatikana wapelekwe mahakamani na watolewe mfano kwa jamii. Ati kiumbe kile ni doli!!!!! Na hii ni karne ya 21. Njia moja ya kumuenzi malaika huyu ni kwa kukemea kwa nguvu zote imani chafu kama hizi. Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu.
 
Naililia nchi yangu! Namlilia Halima! Badala ya watu kukemea hizi imani chafu zilizotanda katika jamii yetu tunaanza kukamatana wenyewe! mambo haya yanatokana na imani hizi na ndizo zinazowapelekea watu kufanya unyama kama huu. Huyo mama yake mkubwa inawezekana kabisa kuwa hahusiki lakini kwa vile jamii imeishamhukumu ndiyo basi. Mtu yeyote akibanwa vizuri atakiri kwa jambo lolote ndiyo maana torture si njia ya kutafuta ukweli! Inatakiwa watafutwe wahusika wote (sio kwa kutumia mibano) kisayansi na pale watakapopatikana wapelekwe mahakamani na watolewe mfano kwa jamii. Ati kiumbe kile ni doli!!!!! Na hii ni karne ya 21. Njia moja ya kumuenzi malaika huyu ni kwa kukemea kwa nguvu zote imani chafu kama hizi. Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu.


Ni kweli uyasemayo FM,
Tatizo langu wana jamii wamekaa kimya kwenye jambo hili wakati kwa inavyo semekana Mama huyu Huu ndio mchezo wake na amesema WAKO wengi hapao mtaani kwao ila yeye ni kinara wao an Kuharibu nyumba ya HUYU mama watu walikua katika harakati za kuwatafuta watoto wengine waliopotea katika mtaa wao.Chakushangaza hawakuona kitu.
Ila kwa mujibu wa mjukuu mwingine wahuyo BIBI alipoulizwa maisha hapo nyumbani alisema,"Bibi anachumba ambacho hakifunguliwi ovyo ila ananipa chakula kila siku nipeleke lakini mimi sioni watu humo"
 
Inasikitisha sana!
Ndio imani kama hizi zinawafanya wazungu watutukane na kutuaminisha kwamba Waafrika tuna akili pungufu.
Mungu amweke pema Halima.
 
Inasikitisha sana!
Ndio imani kama hizi zinawafanya wazungu watutukane na kutuaminisha kwamba Waafrika tuna akili pungufu.
Mungu amweke pema Halima.

Yatupasa kubadilika,nakumbuka kusoma mahara fulani ,kwamba huko ulaya miaka ya 1400 wachawi walikuwa wakichomwa moto hasa U.K na ilisaidia kupunguza vitendo vya kilozi
 
Fundi Mchundo Niko Nyuma Yako Kabisa,,tukemee Huu Uchafu Jamani
Hizi Imani Zitatufanya Hata Mjini Hakupitiki
 
Yatupasa kubadilika,nakumbuka kusoma mahara fulani ,kwamba huko ulaya miaka ya 1400 wachawi walikuwa wakichomwa moto hasa U.K na ilisaidia kupunguza vitendo vya kilozi

Na ilisaidia sana nadhani, kwani imani hizi za kishirikina kwa Ulaya hazipo kabisa kwa sasa, kumetulia sana.
Kinachohitajika kwa Waafrika ni elimu, kwani watu walioelimika na kupata sayansi ya kutosha hawawezi kuamini katika ushirikina.
 
Ni kweli uyasemayo FM,
Tatizo langu wana jamii wamekaa kimya kwenye jambo hili wakati kwa inavyo semekana Mama huyu Huu ndio mchezo wake na amesema WAKO wengi hapao mtaani kwao ila yeye ni kinara wao an Kuharibu nyumba ya HUYU mama watu walikua katika harakati za kuwatafuta watoto wengine waliopotea katika mtaa wao.Chakushangaza hawakuona kitu.
Ila kwa mujibu wa mjukuu mwingine wahuyo BIBI alipoulizwa maisha hapo nyumbani alisema,"Bibi anachumba ambacho hakifunguliwi ovyo ila ananipa chakula kila siku nipeleke lakini mimi sioni watu humo"

Mkuu Matuta, kwa nini unashangaa? Haiwezekani kuwa kweli HAMNA kitu pale? Ni imani tuu za watu? Watoto wadogo wanajulikana kwa kusema chochote ambacho wanajua kitawafurahisha wakubwa zao. sasa hicho chumba walishindwa kuvunja mlango wake? Huyu bibi atafaidika vipi na kuwafuga hao ndondocha? Mbona bado inaelekea hali yake ni duni? Ni imani kama hizi ambazo zinafanya bibi vizee wauawe ati kwa sababu wana macho mekundu bila kuangalia kuwa hao vibibi wameishi maisha yao yote wakipilizia moto wa kuni! Inabidi tutoke kwenye imani kama hizi. Tutaendelea kuua wasio na hatia bure.
 
Hali ya ushirikina inaonyesha ishara kuwa kwenye jamii kuna matatizo mengi zaidi! Shinikizo mbalimbali katika jamii zinaleta hali ya watu kutafuta suluhisho au jawabu la matatizo yao kwa njia mbalimbali, nyingi ambazo si nzuri. Ni muhimu wana jamii kutafuta chanzo cha matatizo hayo na kuyatafiti kwa undani.
 
Siku chache baada ya Rais Kikwete kukemea tabia za kuua watu kwa kuwashuku uchawi mama mmoja amenusurika kuuawa lakini akapoteza nyumba na mali yake yote kwa kushukiwa uchawihuko Vingunguti, Ilala jijini Dar-es-Salaam.

Tarehe 29 Disemba 2007 binti mdoto wa kama miaka 12 hivi aitwaye Rehema Said alitoweka nyumbani kwao huko Vingunguti jijini Dar-es-Salaam. Baada ya kila jitihada kufanyika za kumtafuta watu walikuwa hawajui wafanye nini. Juzi hata hivyo, mwili wake ukiwa umeharibika ulikutwa pembezoni mwa mto wa Msimbazi.

Mara baada ya habari za mwili huo kupatikana tetesi za imani za kishirikina zilizokuwa zimeanza zikazagaa na mara moja watu wakahusisha kifo cha binti huyo na mama mmoja hapo mtaani. Bi. Aurelia Thomas. Bi. Aurelia Thomas bila kujua hili wala lile na yeye alikuwa ni miongoni mwa watu waliotoka kwenda kuushuhudia huo mwili matokeo yake yeye akawa ndiyo mtuhumiwa namba moja.

Siku ile ya Jumatatu watu wakaanza kumzonga mama huyo na wakawa tayari kumfanyizia. Bahati nzuri Polisi walifika mahali hapo na wakirusha risasi za moto wakaweza kuwatawanya watu hao wenye hasira na kumuokoa mama huyo. Watu wakazihamishia hasira zao kwenye nyumba ya mama huyo wakijaribu kurusha mawe na kuivunja vunja. Viongozi wa mtaa wakafika na kuingia hadi ndani ya nyumba hiyo bila kukuta ushahidi wowote ule.

Kiongozi mmoja wa mtaa akiwatuliwa wananchi akawaambia kuwa huko ndani "hakuna mtoto mwingine"; kana kwamba mtoto Rehema ambaye hakuwahi kuonekana nyumba hiyo aliwahi kuwemo! Watu hawakuridhika na matokeo yake wakaendelea kuijaribu kuivunja nyumba ya Bi. Thomas aliyojitahidi kuijenga kwa miaka mingi na kulelea watoto wake ambao ni watu wazima na wengine wameshaolewa! Polisi wakaweka ulinzi pale na watu wakatawanyika lakini siku hiyo ya Jumatatu jioni Polisi wakaondoa ulinzi wao na kutokomea!
Wananchi wakawa wamepewa kibali cha ufisadi. Wakaipangusa nyumba ile kila kitu, wakang'oa madirisha na milango, kuvunja choo na kukwapua kila walichoweza kwa kisingizio cha "kumuadhibu mchawi".! Mama Thomas na familia yake wakajikuta hawana mahala pa kuishi na hakuna wa wa kuwatetea! Kisa na mkasa ni kwa sababu wao wametuhumiwa uchawi. Mwanae wa kiume akizungumza na televisheni moja akasikika kusema "kama angekuwa mtu mmoja ningelipiza kisasi ili wajue jinsi kitendo hiki kinavyotuuma!, hata kama kunyongwa niko tayari kunyongwa"!

Cha kusikitisha ni kuwa hakuna wa kumtetea mama huyo na familia yake au kiongozi yeyote kuonesha anajali kwa ajili ya hofu ya "ushirikina". NInafahamu wengi tuna imani hizi na sisi wengine ambao tumekulia pwani na hata wale wa bara imani za kulogana, misukule, n.k ni za kawaida. Hata hivyo siku hizi kama ilivyo hasa mkoani Shinyanga, kina mama wazee hawatakiwi kuzeeka! wanaitwa wachawi! Wenye macho yaliyopoteza rangi kwa kupulizia moto wa moshi na kushinda juani, wanaambiwa ni macho ya uchawi! Kina mama wazee wanaoishi kama wajane wamekuwa ndiyo kondoo wa kafara inapotokea misiba, ajali n.k!

Imani hizi za kilozi ambazo mwanzoni zilikuwa zinapuuziwa sasa zimefikia pabaya kwani katika TAnzania mtu hafi kwa ajali, kwa mapenzi ya Mungu au kwa sababu za kawaida. Kila anayekufa hata aliyegonwa na gari atatafutwa mchawi. Kinachosikitisha kwenye kesi ya Rehema Said ni Polisi kushindwa kutoa maelezo ya kitaalamu ili kuzuia tetesi hizi. Kwa jinsi mwili ulivyokuwa haiwezekani binti yule awe amekufa juzi au jana.

Binafsi nimeumizwa moyoni na kitendo hiki ambacho siyo cha kibidamu, cha kinyama na ambacho kinatishia kuivunja jamii hasa pale ambapo watoto wadogo wanaachwa kuvunja nyumba za watu na kuoneshwa kwenye televisheni kama jambo la kuonea fahari. Jinsi Channel 10 ilivyoripoti habari hiyo binafsi nimeona aibu kwa sababu ilikuwa na lengo la kuhamasishwa watu katika imani za kishirikina!

Wakati serikali imekurupuka kwa haraka na kwenda kumsaidia mwandishi mwenzetu Saed Kubenea kwa vile ni mtu maarufu na impact yake kwa jamii ni kubwa, je serikali hiyo hiyo itaweza kujitokeza na kumsaidia mama Aurelia Thomas? Au na serikali yetu inaamini ushirikina kiasi kwamba inaogopa kujitokeza na kutoa msaada na kuwakamata wale wote waliohusika na uvunjaji na uharibifu wa mali ya Mtanzania mwenzetu huyu? HIvi mtu ukituhumiwa uchawi unapoteza utu wako? Je mjane anayeishi peke yake au anayefanya jitihada za kuishi kwa kujitegemea yeye mwenyewe ni raia nusu ambaye hastahili kulindwa uhai na mali yake! Wako wapi viongozi wetu walio na haraka ya kusafirisha mtu India ambaye tayari amegharimiwa na watu wengine na kumfumbia macho mama huyu na familia yake? Ni nani basi atakuwa sauti ya wasio na sauti katika nchi yetu kama siyo serikali yao?
 
Sanda, sikuona posti yako hapo.. maana na miye nimelifuatilia suala hili tangu jumatatu na nimelitolea maoni leo. Itakuwa vizuri ma MoD wakaunganisha ile ya kwangu na hii ya kwako..
 
TAnzania mtu hafi kwa ajali, kwa mapenzi ya Mungu au kwa sababu za kawaida.

Nimeguswa kuandika yanayojiri nyumbani kuhusu imani za kishirikina. Awali ya yote napingana na hii kauli 'ya kufa kwa mapenzi ya mungu'. Haiwezekani kuwa huyu muumba atupendelee sisi tulio masikini kufa haraka na lundo la sababu na awaache walio na maisha bora wakaendelea kuishi hadi miaka 80/100.

Kwa wanaotumia biblia sina uhakika katika quran, lakini Biblia inautambua uchawi japo kuwa serikali ni kinyume chake.

Unajua watu huwa hawakurupuki tuu na kumtuhumu mtu! kunakuwa na sababu au tabia fulani ambazo huwa zinaonyeshwa na hao wanaotuhumiwa. Kabla ya kutoa hitimisho/hukumu ni vema 'background informations' zikaangaliwa ili kujua ni kwa nini yeye na si wengine!

Kwa nini kasi ya ushirikina inazidi kushika hatamu? Hali duni ya maisha, watu wameshakata tamaa na njia halali za kuboresha hali zao, hivyo wanaopt hiyo shortcut.

Nini kifanyike, kuondoa matawi peke yake hakutoshi(kutumia dola), ni lazima tuondoe mizizi yake (umasikini.
 
Kenyans hand back 'cursed' loot

Looters in Kenya took advantage of the mayhem to raid shops
The threat of witchcraft has scared looters into returning goods they stole during unrest which followed last month's disputed Kenyan elections.
TV stations broadcast pictures of people returning to places they robbed in the coastal city of Mombasa carrying beds, sofas and other items.

A police commander confirmed the reports and said the rumours of witchcraft had made his job "easy".

One woman said the curse had prevented people from going to the toilet.

"I am telling the truth. I am not lying. There are some people who are not able to pass urine nor faeces," she told Kenyan broadcaster NTV.

Other looters attributed "mystery" illnesses to the curse.

Whether ghosts exist or not, our work has been made easy

Mombasa police commander
Widespread looting followed a breakdown in law and order after President Mwai Kibaki was sworn in after being declared the winner of the disputed poll.

But word spread around Mombasa that a timber merchant had brought in a community elder to place a curse on the thieves.

"He gave us 10 days to return the timber. I will return them at night because people really laugh at us when we do so during the day," an unidentified man told the TV station.

Other victims of looters have also reportedly followed suit.

John Joash confessed to stealing a bed during the mayhem.

"I am fearful for my life because of the ghosts, that is why I decided to return the property," the AFP news agency quotes him as saying.

A local police commander welcomed the looters' second thoughts.

"Whether ghosts exist or not, our work has been made easy. I wish there were ghosts all over the country," he said.

The BBC's Odhiambo Joseph in Mombasa says people turned to witchcraft when they realised the police were powerless to prevent their livelihoods being destroyed
 
Back
Top Bottom