ITEGAMATWI
JF-Expert Member
- Jan 26, 2012
- 5,310
- 4,040
- Thread starter
- #21
Hii inatikana na wakati gani siku huanza kwa wenzetu. Kwa wao siku mpya huanza saa sita na dakika moja usiku (00:01) kwa hiyo saa moja asubuhi ni masaa saba (7.00 Anti Meridian) tangu siku ianze.
Kwasisi waswahili siku huanza jua linapochomoza, kwahiyo saa moja asubuhi ni lisaa limoja tangu jua lichomoze (saa 12 asubuhi). Tulifanya hivyo kwasababu katika ukanda wa ikweta tuna masaa 12 ya mwanga na 12 ya giza, mwaka mzima. Wenzetu wasinge weza kutumia kigezo cha jua kwakuwa muda wa jua kuchomoza na kuzama hubadilika kutokana na majira
Ok!Nimekusoma mkuu!Hii kitu inachanganya sana yaani huwa najichanganya sana sometimes!!