Ilikuwaje Portugal kwa kiswahili ikaitwa Ureno?

Hii inatikana na wakati gani siku huanza kwa wenzetu. Kwa wao siku mpya huanza saa sita na dakika moja usiku (00:01) kwa hiyo saa moja asubuhi ni masaa saba (7.00 Anti Meridian) tangu siku ianze.

Kwasisi waswahili siku huanza jua linapochomoza, kwahiyo saa moja asubuhi ni lisaa limoja tangu jua lichomoze (saa 12 asubuhi). Tulifanya hivyo kwasababu katika ukanda wa ikweta tuna masaa 12 ya mwanga na 12 ya giza, mwaka mzima. Wenzetu wasinge weza kutumia kigezo cha jua kwakuwa muda wa jua kuchomoza na kuzama hubadilika kutokana na majira


Ok!Nimekusoma mkuu!Hii kitu inachanganya sana yaani huwa najichanganya sana sometimes!!
 
Sahihisho........gari ni neno linalojitegemea na tumekopa kwa wahindi...just like baba
Asante sana Mkuu kwa mafahamisho. Bado kuna uwezekano kuwa neno *gari limetokana na *car, hasa ikiwa gari limeingia katika Kiswahili kutoka Wahindi ambao wao kama sisi tulikuwa makoloni ya Mwingereza. Maneno baba (papá) au mama (mamá) nilikuwa ninafikiri yametokana na kilatini.
*Ni dhana yangu tu, sina uhakika wowote.
 
Kiranga umetoa mwanga mahususi kuhusu sisi wabantu kutumia neno Ureno. Ikiwezekana kuwasiliana na mamlaka za kiswahili kubadilisha matumizi na kuacha kutumia neno Ureno maana kumbe haileti maana.
Reign=Ufalme=Ureno=Reigno
Regno de portugal= ufalme wa portugal

Thanks!
 
kuna vitu vyengine havizingatii sheria wala kufata nasaba...ila wazo hili la GOODRICH nalikubali .
waingereza na wafaransa wanaiita moroko ,ila wenyewe wanaiita MAGHRIB, Je pana uhusiano wa majina hayo ?? Zamani Uholanzi ilikuwa ikijulikana sana kwa jina la Udachi, ila wao wenyewe hawalifahamu neno hili kwani lina nasaba na ujerumani na sio wao.
 
Portugal ilizaliwa katika karne ya 12 baada ya kujitenga toka kwenye Kingdom ya Leon. Wazungumzaji wa lugha ya kiswahili wana tabia ya kuchanganya matamshi ya "r" na "l". Inawezekana jina la Ureno limetokana na Kingdom ya Leon ambayo ndiyo lililokuwa jina la Portugal kabla ya kujitenga.
 
kuna vitu vyengine havizingatii sheria wala kufata nasaba...ila wazo hili la GOODRICH nalikubali .
waingereza na wafaransa wanaiita moroko ,ila wenyewe wanaiita MAGHRIB, Je pana uhusiano wa majina hayo ?? Zamani Uholanzi ilikuwa ikijulikana sana kwa jina la Udachi, ila wao wenyewe hawalifahamu neno hili kwani lina nasaba na ujerumani na sio wao.


Hapo kwenye red unamaaana gani ndugu?. Mbona tuliohuku tunaona neno Dutch wanalitumia vizuri tu
 
@@@Jagermaster
Hoi ? Gaat het met je ? Ik heb noit DUTCH gehoord. Spreek je nederland ?maar niet DUTCH....
 
Ushauri wa bure. Kiswahili kimetokana na Kiarabu kwa kiasi kikubwa sana. Hebu tafuta hayo maneno yako ufahamu kwa kiarabu huitwaje. Nadhani utapata jibu sahihi na utaelewa nini namaanisha mkuu.
 
Back
Top Bottom