Mimi ni shabiki wa Arsenal!
Ilikuwa ni miaka kadhaa iliyopita wakati nikiwa kijana mdogo ambae nahisi hata kidato cha kwanza nilikuwa sijaanza! Nakiri, wakati huo sikuwa na uwezo mkubwa wa kuchambua ama kudadisi mambo critically, hususani yale ya magazetini!
Hata hivyo, jambo ambalo sina shaka nalo ni kwamba nilikuwa ni bonge la shabiki la Dar es salaam Young Africans a.k.a YANGA! Nilikuwa ***** sana enzi hizo! Nilikuwa nashindwa hata kula kisa tu eti Yanga imefungwa! Acha tu baadhi ya Masheikh waseme kwamba kabumbu nalo ni haramu!
Basi bana! Siku moja nikiwa kwenye viunga wa Uwanja wa Taifa (siku hizi wa Uhuru) niliokota kipande cha gazeti! Hata hivyo, bado sifahamu kilikuwa ni kipande cha gazeti gani ingawaje nahisi ilikuwa ni ama gazeti la Majira au Uhuru. Kwenye kipande hicho cha gazeti kulikuwa na habari eti Uingereza kuna timu inayoitwa Arsenal ambayo ni marafiki wakubwa wa timu ya Yanga na kwamba Yanga wamekuwa wakipata misaada mbalimbali toka timu hiyo ya kwa Malkia!
Nakiri kwamba, hiyo ilikuwa ndio siku yangu ya kwanza kusikia kuwapo kwa timu ya Arsenal kwani kabla ya hapo nilikuwa naifahamu Man U na Liverpool peke yake! Mwandishi wa habari hiyo aliendelea kudai kwamba, kutokana na urafiki huo wa karibu kati ya Arsenal na Yanga, timu hiyo ya Uingereza ilikuwa na mpango wa kuja Dar kucheza mechi za kirafiki na wana wa Jangwani!
Dah! Mzee kichwakichwa nikajikuta nikianza kuipenda Arsenal!
Na hata pale Ligi Kuu ya Uingereza ilipoanza kuoneshwa kupitia ITV katikati ya 1990's nilikuwa tayari nimeshaoza kwa Arsenal!
Hivi sasa, nikiwa mtu mzima mwenye uwezo wa ku-reason mambo ndipo naanza kushituka na kujiuliza ukweli wa habari ile (kwamba Arsenal ma Yanga ni marafiki)! Nahisi, ilikuwa ni habari ambayo iliandikwa siku ya Wajinga (April 01) ambayo nami niliimeza kama ilivyokuwa na kuathiri kabisa maisha yangu!
Je, mwenzangu wewe ilikuwaje hata ukawa mpenzi wa ama Arsenal, Man U, Liverpool , Chelsea au timu yoyote ile ya Ulaya?
Ilikuwa ni miaka kadhaa iliyopita wakati nikiwa kijana mdogo ambae nahisi hata kidato cha kwanza nilikuwa sijaanza! Nakiri, wakati huo sikuwa na uwezo mkubwa wa kuchambua ama kudadisi mambo critically, hususani yale ya magazetini!
Hata hivyo, jambo ambalo sina shaka nalo ni kwamba nilikuwa ni bonge la shabiki la Dar es salaam Young Africans a.k.a YANGA! Nilikuwa ***** sana enzi hizo! Nilikuwa nashindwa hata kula kisa tu eti Yanga imefungwa! Acha tu baadhi ya Masheikh waseme kwamba kabumbu nalo ni haramu!
Basi bana! Siku moja nikiwa kwenye viunga wa Uwanja wa Taifa (siku hizi wa Uhuru) niliokota kipande cha gazeti! Hata hivyo, bado sifahamu kilikuwa ni kipande cha gazeti gani ingawaje nahisi ilikuwa ni ama gazeti la Majira au Uhuru. Kwenye kipande hicho cha gazeti kulikuwa na habari eti Uingereza kuna timu inayoitwa Arsenal ambayo ni marafiki wakubwa wa timu ya Yanga na kwamba Yanga wamekuwa wakipata misaada mbalimbali toka timu hiyo ya kwa Malkia!
Nakiri kwamba, hiyo ilikuwa ndio siku yangu ya kwanza kusikia kuwapo kwa timu ya Arsenal kwani kabla ya hapo nilikuwa naifahamu Man U na Liverpool peke yake! Mwandishi wa habari hiyo aliendelea kudai kwamba, kutokana na urafiki huo wa karibu kati ya Arsenal na Yanga, timu hiyo ya Uingereza ilikuwa na mpango wa kuja Dar kucheza mechi za kirafiki na wana wa Jangwani!
Dah! Mzee kichwakichwa nikajikuta nikianza kuipenda Arsenal!
Na hata pale Ligi Kuu ya Uingereza ilipoanza kuoneshwa kupitia ITV katikati ya 1990's nilikuwa tayari nimeshaoza kwa Arsenal!
Hivi sasa, nikiwa mtu mzima mwenye uwezo wa ku-reason mambo ndipo naanza kushituka na kujiuliza ukweli wa habari ile (kwamba Arsenal ma Yanga ni marafiki)! Nahisi, ilikuwa ni habari ambayo iliandikwa siku ya Wajinga (April 01) ambayo nami niliimeza kama ilivyokuwa na kuathiri kabisa maisha yangu!
Je, mwenzangu wewe ilikuwaje hata ukawa mpenzi wa ama Arsenal, Man U, Liverpool , Chelsea au timu yoyote ile ya Ulaya?