Deejay nasmile
JF-Expert Member
- Nov 8, 2011
- 5,759
- 5,289
basi bwana kongosho akaendelea kunitumia sms kuwa yupo mbagala pale mission,hivyo niende kukutana nae,kwa kuwa nilikuwa na shauku ya kujua ni mvurana au msichana nikachukua pikipiki yangu mpaka mbagala kwa kuwa muda huo nilikuwa mitaa ya keko pale.nikafika pale nikampigia simu kwa ile namba aliyonibip lakini kama kawaida hakupokea ili nisiisikie sauti yake ila akani sms,kuwa nimsubili dakika mbili.mzee mzima nikaamua kutulia sehemu nikiwa na shauku kubwa ya kukutana na kongosho alafu miwajuze watu humu jf kuwa kongosho ni jinsia flani,baadae kidogo sms ikaingia katika simu yangu ikasema hivi "nipo hapa karibu na internet cafe,njoo". SASA ile nataka niende tu ndipo kwa mbali nikasikia sauti ya mwenye nyumba ananigongea mlango kwa nguvu.Duh NDOTO yangu ikakata hapo hapo.nikaamka,nikatoka nje kufungua mlango nikakutana na mzee mwenye nyumba akitaka kodi yake.Ndio hivyo tena wakuu sikufanikiwa kukutanana na kongosho....