DSN
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 2,837
- 1,674
Purukushani za hao wanaofanya michakato,mbinu maarifa na mengineyo ya kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 2015,wajue moja Watanzania wa leo,bila viatu vya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere watachemka na piga uwa itakula kwao kwa sana.Watanzania wameona tawala tatu zenye viongozi tofauti tofautikwa karibu miaka ishirini na saba [27] bado wote kwa ujumla wao wanakili kuwa kiongozi aliyelitumikia Taifa la Watanzania kwa moyo wake wote ni Mwalimu Julius K Nyerere.
Raisi ajae Watanzania wanataka kumuona Nyerere wa Vitendo,aijalishi atatoka chama gani? Mfumo [System] ujipange kuanzia sasa kuwa tayari kukubali kufanya kazi na mtu yoyote toka chama chochote. Ukweli aijalishi lawama za kujitetea kuwa hawajajitayarisha wakubali ukweli ili daima dhambi hii ya kuepuka ukweli ifike mwisho.
Muda mfumo [System] ulionao ni mrefu ni vyema wajipange kuanzia sasa kujipanga kwa lolote manake mwendelezo huu,usije ukachelewa tena yakaja yale ya kujitetea mfumo haujajipanga kufanya kazi na mtu aliyekuwa nje ya Serikali.Ndio wananchi hawajui hasara za kukurupuka na kufanya kazi na mtu aliye nje ya mfumo,lakini ni haki yao kuongozwa na Kiongozi wanayemtaka wao.Hivyo kujitetea huko kwa mfumo kufike mwisho mwanzo ni leo kwa kuangalia hali ya muamko wa kuelewa wa wananchi juu ya viongozi wanaowataka.
Raisi ajae Watanzania wanataka kumuona Nyerere wa Vitendo,aijalishi atatoka chama gani? Mfumo [System] ujipange kuanzia sasa kuwa tayari kukubali kufanya kazi na mtu yoyote toka chama chochote. Ukweli aijalishi lawama za kujitetea kuwa hawajajitayarisha wakubali ukweli ili daima dhambi hii ya kuepuka ukweli ifike mwisho.
Muda mfumo [System] ulionao ni mrefu ni vyema wajipange kuanzia sasa kujipanga kwa lolote manake mwendelezo huu,usije ukachelewa tena yakaja yale ya kujitetea mfumo haujajipanga kufanya kazi na mtu aliyekuwa nje ya Serikali.Ndio wananchi hawajui hasara za kukurupuka na kufanya kazi na mtu aliye nje ya mfumo,lakini ni haki yao kuongozwa na Kiongozi wanayemtaka wao.Hivyo kujitetea huko kwa mfumo kufike mwisho mwanzo ni leo kwa kuangalia hali ya muamko wa kuelewa wa wananchi juu ya viongozi wanaowataka.