Ikulu yalijibu Gazeti la Dira ya Mtanzania: Yataka watoe majibu au wachukuliwe hatua...

Ikulu ndo wasemaji wa familia ya rais na si taasisi ya rais kazi ipo
 
Even the speculative part? Ikulu itasemaje kwamba gazeti lina nia ya kumchafua mfanyabiashara kama haina biashara yoyote na huyu mfanyabiashara? Itajuaje habari hii?

Vipi kama mfanyabiashara mwenyewe ka brag bila ukweli kwamba anafanya biashara na familia ya rais, ile kibongobongo kuwatisha watu?

Nadhani unazungumzia kipande hiki, sio?

Na, au vinginevyo unalenga kuchafua jina la Kampuni ya Home Shopping Centre. Kama nia ni kufanya hivyo tafadhali msilitumie jina la familia ya Rais.

Kama ni hicho basi mimi sioni ubaya wowote hapo kwani ni kuna mawili, mosi, Ikulu imekanusha na kusema habari si za kweli na zenye lengo la kumchafua Kikwete na familia yake, pili, kama lengo si hilo basi litakuwa ni kuchafua jina la Home Shopping Centre kwa kulihusisha na jina la rais.

Hakuna ubaya wowote hapo. Ikulu wameshakanusha and now the ball is in the weekly's court to back up its allegations with supporting evidence.

Sasa watu sijui mlitaka Ikulu waandikeje....
 
Rais mkulima mzuri wa mananasi Kurugenziya lkulu wanakanusha kuwa rais hajawahi fanya biashara sijui huwa anagawa bure kijijini msoga?
 
Ukiisoma hii Press Release utadhani imeandikwa na bibi yangu ambaye alijifunza kusoma kwenye miembe na ambaye hana muda wa kutosha kutafakari kabla ya kuandika kwa hadhara kubwa na namna hii kutoka na shuguli nyingi za shamba.

Pathetic! Jamani ina maana Ikulu imeshindwa kuwapata watànzania wenye weledi kutuepusha na aibu hizi?
 
NN matamko ya ikulu yanatakiwa kujikita ktk hoja and in this case they misfired.

Ila kama ni kimipasho kama huku uswahilini wako kwenye mstari!

Ulitaka waandike nini? Hebu niambie ingekuwa wewe unaandika kukanusha hiyo habari ya Dira ya Mtanzania ungeandikaje?
 
Ukiisoma hii Press Release utadhani imeandikwa na bibi yangu ambaye alijifunza kusoma kwenye miembe na ambaye hana muda wa kutosha kutafakari kabla ya kuandika kwa hadhara kubwa na namna hii kutoka na shuguli nyingi za shamba.

Pathetic! Jamani ina maana Ikulu imeshindwa kuwapata watànzania wenye weledi kutuepusha na aibu hizi?

Ulitaka watumie vocabulary gani ili uridhike nayo? Ulitaka waandikeje? Nionyeshe kwa utondoti ubaya wa walichoandika, tafadhali.
 
Nadhani unazungumzia kipande hiki, sio?



Kama ni hicho basi mimi sioni ubaya wowote hapo kwani ni kuna mawili, mosi, Ikulu imekanusha na kusema habari si za kweli na zenye lengo la kumchafua Kikwete na familia yake, pili, kama lengo si hilo basi litakuwa ni kuchafua jina la Home Shopping Centre kwa kulihusisha na jina la rais.

Hakuna ubaya wowote hapo. Ikulu wameshakanusha and now the ball is in the weekly's court to back up its allegations with supporting evidence.

Sasa watu sijui mlitaka Ikulu waandikeje....

Ikulu ishajiingiza katika speculations, na inaonekana kuanza kumtetea mfanyabiashara kabla hata ya kuwa na habari kamili.

Hili linaweza kuwafanya wengine waanze kujiuliza, kuna jambo hapa?

Mbona ikulu imejibu siku hiyo hiyo habari hii wakati kuna habari kemkem zinaandikwa kuhusu Kikwete kila siku hazijibiwi?

Mbona Ikulu inamtetea sana huyu mfanyabiashara kwamba anachafuliwa kabla hata ya kupata habari kamili na bila hata kutuonyesha kwamba mfanyabiashara mwenyewe ndiye aliyejitapa?

Au maneno haya yana ukweli na Ikulu inaona ni bora iyazime mapema yasije kulipuka baadaye?
 
Yaani siku hizi mdosimdosi akijitapa tu "ninafanya biashara na familia ya rais", gazeti likiandika "Mdosi kajitapa anafanya biashara na familia ya rais" Ikulu inakuja juu siku hiyo hiyo na communique kukanusha?

Methinks the lady protests too much!

Kwanza Ikulu wamejuaje kwamba gazeti linaipaka matope hiyo biashara?

I mean hata kama Ikulu haihusiki, imejuaje kwamba mdosi hajajitapa na kusema hivyo hata kwa uongo?

Kiranga, ukitaka kujua nguvu ya huyu bwana nenda Kariakoo! Haielezeki anapata wapi nguvu kubwa hivyo na nadhani watu wamevulia wakashindwa!

Mwaka jana Rais alihudhuria function (kama sikosei ilikuwa kufungua tawi) ya hawa hawa shopping centre na watu walijuliza sana inakuwaje? Rais?

Ni vizuri washauari wa Rais wakawa makini juu ya functions anazohudhuria Rais.
 
Ikulu ishajiingiza katika speculations, na inaonekana kuanza kumtetea mfanyabiashara kabla hata ya kuwa na habari kamili.

Hili linaweza kuwafanya wengine waanze kujiuliza, kuna jambo hapa?

Mbona ikulu imejibu siku hiyo hiyo habari hii wakati kuna habari kemkem zinaandikwa kuhusu Kikwete kila siku hazijibiwi?

Mbona Ikulu inamtetea sana huyu mfanyabiashara kwamba anachafuliwa kabla hata ya kupata habari kamili na bila hata kutuonyesha kwamba mfanyabiashara mwenyewe ndiye aliyejitapa?

Au maneno haya yana ukweli na Ikulu inaona ni bora iyazime mapema yasije kulipuka baadaye?

Wewe ndiyo una speculate like you are on steroids!

Ikulu wameshafanya walichokuwa wanatakiwa kufanya: kukanusha au kuthibitisha. Wao wamekanusha.

Watu kuongea na kujiuliza na kuja na tafsiri zao ni jambo la kawaida sana.

Mengi mno yamesemwa na bado yatasemwa. Na wao hawawezi kujibu kila lisemwalo au kuandikwa la sivyo hawatafanya kazi zingine zozote zaidi ya kujibu yasemwayo na watu.

Ikulu wameshafanya walichopaswa kufanya na kibao kimerudi kwa Dira ya Mtanzania. Tuone kama watathubutu kuthibitisha waliyoyachapisha.
 
Wewe ndiyo una speculate like you are on steroids!

Ikulu wameshafanya walichokuwa wanatakiwa kufanya: kukanusha au kuthibitisha. Wao wamekanusha.

Watu kuongea na kujiuliza na kuja na tafsiri zao ni jambo la kawaida sana.

Mengi mno yamesemwa na bado yatasemwa. Na wao hawawezi kujibu kila lisemwalo au kuandikwa la sivyo hawatafanya kazi zingine zozote zaidi ya kujibu yasemwayo na watu.

Ikulu wameshafanya walichopaswa kufanya na kibao kimerudi kwa Dira ya Mtanzania. Tuone kama watathubutu kuthibitisha waliyoyachapisha.

Ikulu ime speculate kwa kujiingiza kwenye habari na kusema gazeti linamchafua mfanyabiashara wakati gazeti linasema mfanyabiashara ndiye anayejitapa kwamba ana biashara na familia ya rais.

Kama Ikulu/ familia ya rais haina biashara na mfanyabiashara huyu, kurugenzi inachotakiwa inachotakiwa kusema ni kwamba familia ya rais haina biashara na huyu mtu. Hizi habari nyingine za kwa nini gazeti limeandika ni tofauti. Ikulu / familia ya rais inaweza isiwe na biashara na mfanyabiashara lakini ikakosea vile vile kusema gazeti linamchafua mfanyabiashara kwa sababu mfanyabiashara anaweza kuwa anajigamba openly kwamba ana biashara na familia ya rais, hata kama si ukweli.

Hizi habari za kujichomeka chomeka kumkingia kifua mfanyabiashara si kazi yao Ikulu, sanasana zitatupa maswali tu. Kwa nini Ikulu inamkingia mfanyabiashara kifua?

Ni kwa sababu waandishi wa Ikulu ni bongokamasi na hawakupata legal counsel kabla ya kufyatua huo utumbo wa speculations bila kujua ukweli?

Au ni kwa sababu habari ina ukweli fulani ndani yake wanataka kuizima mapema?
 
Mpaka ifike 2015 hii sehemu inayoitwa ikulu itakua imeshageuzwa ukumbi wa taarabu............ni utabiri tuu :car:
 
Hiyo Ndiyo kazi iliyobaki sasa kila siku kujibu magazeti!Mbona kuna issue nyingine huwa hazijibiwi au hazina majibu?!Dira wamejaribu kuwafahamisha watanzania wa pembezoni wasiyo litua hilo!Walisponsor Show ya Mabwepande mwanzo mwisho!Isije kuwa kama KIwira tu!Its just amatter of time mtakuwa watupu!
 
Safari hii kila mtu kinamnukia,habari ndio kwanza imeanza wataiona wengi watachangia mengi yatazuka mengi tutayajua na yale tusiyokuwa tukiyajua.
 
Hizi Sarakasi ya usiku sinashida sana.Hivi hili Gazeti DIRA ni la nani Vile?Mbona kama nao linahusiano ya watajwa na kurugenzi? Kwa kifupi vijana wa kitaa wanasema Mbwa kala mbwa!
 
Huyu mwarabu ana nguvu za ajabu. Madhambi yake mengi yameshawekwa hadharani mara chungu nzima na ushahidi wa wazi lakini bado anadunda. Ni nani yuko nyuma yake? si polisi si TRA si usalama wa taifa wanamlamba miguu. Ni nani yuko nyuma yake?
 
Ikulu ime speculate kwa kujiingiza kwenye habari na kusema gazeti linamchafua mfanyabiashara wakati gazeti linasema mfanyabiashara ndiye anayejitapa kwamba ana biashara na familia ya rais.

Kama Ikulu/ familia ya rais haina biashara na mfanyabiashara huyu, kurugenzi inachotakiwa inachotakiwa kusema ni kwamba familia ya rais haina biashara na huyu mtu. Hizi habari nyingine za kwa nini gazeti limeandika ni tofauti. Ikulu / familia ya rais inaweza isiwe na biashara na mfanyabiashara lakini ikakosea vile vile kusema gazeti linamchafua mfanyabiashara kwa sababu mfanyabiashara anaweza kuwa anajigamba openly kwamba ana biashara na familia ya rais, hata kama si ukweli.

Hizi habari za kujichomeka chomeka kumkingia kifua mfanyabiashara si kazi yao Ikulu, sanasana zitatupa maswali tu. Kwa nini Ikulu inamkingia mfanyabiashara kifua?

Ni kwa sababu waandishi wa Ikulu ni bongokamasi na hawakupata legal counsel kabla ya kufyatua huo utumbo wa speculations bila kujua ukweli?

Au ni kwa sababu habari ina ukweli fulani ndani yake wanataka kuizima mapema?

Ikulu wameandika hivi;

Na, au vinginevyo unalenga kuchafua jina la Kampuni ya Home Shopping Centre. Kama nia ni kufanya hivyo tafadhali msilitumie jina la familia ya Rais.

Hawataki jina la familia ya Rais litumiwe. Sasa kama ni mambo ya speculation, mtu yeyote yule anaweza aka-speculate chochote kile kutokana chochote kama ulivyofanya wewe.

It's fair to say speculations are subjective.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom