Ikulu vs Gazeti la Mwananchi: JK akana kuwasamehe waliomuua Lut Jen Kombe

Hata haiingii akilini, kama maamuzi yalifanyika toka mwaka 2005 (chini ya Mkapa) imekuwaje bado wafungwa hao bado walikuwa wamefungwa hadi leo?..

Mkuu hilo ndo swali la msingi ambalo salva alitakiwa kulijibu. Lakini kila mmoja anashangaa jinsi taarifa hii ya ikulu ilivyo kuwa fupi na yenye kuacha maswali mengi yanayohitaji majibu.
 
hii kurugenzi inamtetea rais kama mtu au taasisi ya urais? Fafanuzi zote za sasa na kabla yao tuite hao wastaafu? Sekta zote za umma ingekuwa hivi si balaa!
 
  • Thanks
Reactions: Ame
huu upuuz ndio huwa siupendi....kila mara wanasingizia utawala ulipita......
 
Haya sasa kama kawaida ya wazee wa kiduku, wanajibu kama siyo serikali. Kama maamuzi yalifanywa kabla ya JK na kama yalifanywa na Ikulu hiyohiyo kwanini wasitoe ufafanuzi wa swala hilo kuliko kutoa statement fupi tu inayoacha maswali zaidi ?
Hapo kwenye RED.....
Kumbe na ww mkuu umeliona nilitaka kuandika hivyo hivyo, halafu mbona hata hiyo statement haieleweki? Haielezi nani anahusika, haisemi kama walipunguziwa adhabu kweli yaani haikani na wala haikiri,

Statement yote ndo hii hapa yale mengine ya juu ni maelezo kuhusiana na gazeti la Mwananchi...

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, inapenda kufafanua kuwa Mheshimiwa Rais Kikwete hajawahi na hajapata kuhusika hata kidogo kutoa msamaha wa kirais kwa kupunguza adhabu ya wauaji hao wa Luteni Jenerali Kombe tokea kuingia madarakani.Masuala yote yanayohusu polisi hao waliohukumiwa kifo kwa mauaji ya Luteni Jenerali Kombe yalifanyiwa maamuzi kabla ya Rais Kikwete kuingia madarakani Desemba 21, 2005.


Ebu fikirieni huku ni kufafanua kweli? hii kurugenzi ya mawasiliano ikulu wanaumwa nin kiasi cha kuwa hata wavivu kueleza kitu kama hiki? Na ni kwanini wanaibuka kutoa maelezo kwenye issue ambazo sio za kitaifa wakiacha issues kubwa za kitaifa zikielea tu? Uchumi wetu una didimia hakua ufafanuzi, shilingi yetu inapoteza dhamani hakuna ufafanuzi, Kuna taarifa za serikali kupanga njama za mauaji kwa baadhi ya wabunge na mawaziri na raia wengine kurugenzi imekaa kimya... wengine tunaogopa BAN tu hapa lakini tunauwezo wa kufyatuka kwa maneno makali, Mungu apishe mbali!!!

Pambaf kabisa...
 
Mkuu hilo ndo swali la msingi ambalo salva alitakiwa kulijibu. Lakini kila mmoja anashangaa jinsi taarifa hii ya ikulu ilivyo kuwa fupi na yenye kuacha maswali mengi yanayohitaji majibu.
Halafu mwandishi wa ile habari alijitahidi kweli kueleza mpaka kifungu kinachompa mamlaka rais kusamehe, sasa nashangaa Ikulu inaweweseka nini? Jamaa wamewahoji mpaka hao ex - wafungwa na jamaa kuelezea jinsi walivyoishi maisha ya jela hadi kuachiwa kwao. Mimi naamini gazeti la mwananchi si wazushi, ila kuna aina fulani ya kutaka kumis lead watu. Halafu kwa jinsi Ikulu ilivyojibu ndiyo itaibua maswali mengi kuliko ile taarifa ilivyotoka kwenye gazeti.
 
Nasubiri ufafanuzi wa kipuuzi kama huu toka kwa waziri wa mambo ya ndani labda yy atatuambia ilikuaje tangu serikali ya Mkapa mpaka leo ndo taarifa hizi zinatolewa
 
Kimsingi gazeti la mwananchi wamekuwa wakiandika mengi hasa yahusuyo ikulu na hasahasa Jk mwenyewe..,bahati mbaya na nasema ni bahati mbaya kwa wananchi wapenda habari na kufuatilia mambo ni kuwa wamekuwa wakiandika habari ambazo ni za upande mmoja na hivyo kuibua maswali na hisia tofauti kwa sisi wafuatiliaji lakini pia mara nyingi ikulu inapojitokeza kujibu, kufafanua ama kukanusha baadhi ya hoja na habari zinazotolewa na mwananchi, huishia kwenye press release na hakuna hatua ya mbele zaidi kitu kinachoibua maswali mara nyingine tena.

Hivyo kwa maoni yangu ni kuwa zipo ajenda zilizojificha kwa pande mbili hizi zinazoonekana kujuana kiundani....!
 
Kizungumkuti.

Mwananchi iliwatafuta na kufanya mahojiano na Koplo Juma Mswa na Konstebo Mataba Matiku, na taarifa zipo za uhakika.

Salva na Premi wanafanya usanii tu.
 
Hapo kwenye RED.....
Kumbe na ww mkuu umeliona nilitaka kuandika hivyo hivyo, halafu mbona hata hiyo statement haieleweki? Haielezi nani anahusika, haisemi kama walipunguziwa adhabu kweli yaani haikani na wala haikiri,

Statement yote ndo hii hapa yale mengine ya juu ni maelezo kuhusiana na gazeti la Mwananchi...

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, inapenda kufafanua kuwa Mheshimiwa Rais Kikwete hajawahi na hajapata kuhusika hata kidogo kutoa msamaha wa kirais kwa kupunguza adhabu ya wauaji hao wa Luteni Jenerali Kombe tokea kuingia madarakani.Masuala yote yanayohusu polisi hao waliohukumiwa kifo kwa mauaji ya Luteni Jenerali Kombe yalifanyiwa maamuzi kabla ya Rais Kikwete kuingia madarakani Desemba 21, 2005.


Ebu fikirieni huku ni kufafanua kweli? hii kurugenzi ya mawasiliano ikulu wanaumwa nin kiasi cha kuwa hata wavivu kueleza kitu kama hiki? Na ni kwanini wanaibuka kutoa maelezo kwenye issue ambazo sio za kitaifa wakiacha issues kubwa za kitaifa zikielea tu? Uchumi wetu una didimia hakua ufafanuzi, shilingi yetu inapoteza dhamani hakuna ufafanuzi, Kuna taarifa za serikali kupanga njama za mauaji kwa baadhi ya wabunge na mawaziri na raia wengine kurugenzi imekaa kimya... wengine tunaogopa BAN tu hapa lakini tunauwezo wa kufyatuka kwa maneno makali, Mungu apishe mbali!!!

Pambaf kabisa...
Ufafanuzi upo kwenye kashfa tu, mambo mengine yanapotezewa.
 
Duh hii mpya hawajakanusha watuhumiwa hao kusamehewa ila wansema Mk we re hakuwasamehe. yalifanyika siku za nyuma
 
Inasikitisha sana kuona kurugenzi ya ikulu inafanya madudu ya kushangaza...! 'rais Kikwete hahusiki' kwani kunashida gani kama angehusika? Kwanini anapenda kujikosha? Huo ni upungufu mkubwa sana. Hii ni kudhalilisha Taasisi ya Ikulu. Ikulu haimaanishi mtu kama individual, inasimama kama taasisi, kwanini kujikosha? Huo ni ubinafsi wa hali ya juu haipendezi hata kidogo ni fedheha isiyo na kifani nakosa pa kuficha uso wangu.
 
Wale walipwa msamaha na ikulu ya kikwete wala hao akina salavva wasipindishe ukweli.....
 
Wakati mwingine taarifa ya ufafanuzi inaweza nayo ikahitaji kufafanuliwa zaidi
 
Hatimaye Ikulu yetu imegeuzwa kuwa Kitengo cha Propaganda cha kukanusha habari za Fisadi Kikwete na genge lake la Kufilisi Nchi. Haya endeleeni kukanusha kila kitu msije mkajikanusha wenyewe kwa wenyewe huko Ikulu Propaganda
 
Back
Top Bottom