Ikulu sasa ni BMW kwa kwenda mbele

Status
Not open for further replies.

Fidel80

JF-Expert Member
May 3, 2008
21,947
4,444
*YAACHANA NA MERCEDES BENZI


Na Ramadhan Semtawa
AWAMU ya nne ya Serikali ya Jakaya Kikwete, imeamua kuachana na magari iliyotumia kwa muda mrefu ya Marcedes Benz na sasa inatumia magari mengine ya kifahari ya BMW kwa ajili ya msafara wa rais.

Mercedes Benz, gari ya kifahari inayotengenezwa nchini Ujerumani, imekuwa ikitumiwa na serikali zote tatu zilizopita zilizoongozwa na Mwalimu Julius K. Nyerere, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa. Gari iliyotumika mwanzoni mara baada ya kupata uhuru ilikuwa Rolls Royce.

Lakini kwa sasa, msafara wa Rais Kikwete unapambwa na magari matano ya BMW, mawili yakiwa ni X 5, ambayo ni mithili ya Toyota VX kwa ukubwa na matatu yakiwa Series Seven, Mwananchi imeshuhudia.

Hatua hiyo ya Ikulu imekuja wakati mpango wa wataalamu wa kutaka kupunguza magari ya kifahari ya serikali ukiwa umekwama katika meza ya Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo.

Wakati Luhanjo akiwa na ripoti ya mpango huo ambao unaonyesha serikali ina magari 40, 000 ya kifahari maarufu kama mashangingi Vx na Gx, yakiwa ni 15,000, Ikulu imeibuka na magari hayo mengine ambayo bei yake ni kati ya Sh200 milioni hadi Sh500 milioni.

Habari ambazo Mwananchi imezipata zinaeleza kuwa gari hizo ziliingizwa nchini kwa ndege kutoka Afrika Kusini na kwamba, lengo la kuhama Mercedes Benz ni kuimarisha zaidi usalama wa rais na msafara wake.

Lakini Katibu Mkuu Kiongozi, Luhanjo alipoulizwa sababu za Ikulu kuhamia BMW, hakutaka kueleza lolote.

Luhanjo alisema kwa kifupi: "Ahaa, bwana ee...!"

Wakati Luhanjo akiwa bubu, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Rais, Salva Rweyemamu, naye aliamua kuwa kimya.

Salva alipotafutwa kwa simu yake ya mkononi hakuipokea, lakini baadaye akiwa nje ya nchi kwenye msafara, ndipo alipotuma ujumbe mfupi wa simu (sms).

Mkurugenzi huyo, ambaye aliwahi kuwa mwandishi mahiri na mchambuzi mzuri wa sera za serikali, alituma ujumbe huo mfupi akisema: "Niko nje, siko nchini."

Katibu Mkuu Wizara ya Miundombinu ambayo ndiyo yenye dhamana ya ununuzi wa magari ya serikali, Omar Chambo, akionyesha ushirikiano kwa mwandishi, alisema kwa uwazi kwamba, hakuwa na taarifa na mpango huo.

Chambo, ambaye ni mtendaji na mmoja wa wateule wa rais mwenye uhusiano mzuri na vyombo vya habari, alisema: " kwa kweli kabisa sina taarifa kwani si mpango wa wizara, uliza Ikulu kama kuna kitu kama hicho maana mimi sijakisikia."

Mercedese Benz ndizo gari ambazo zimekuwa zikitumiwa na marais katika misafara yao.

Katika uchunguzi huo, Mwananchi imebaini kwamba uamuzi wa kuhama Mercedes Benz unatokana na ushauri wa timu ya usalama wa rais.

Pamoja na gari hizo kuwa na bei kati ya Sh200 milioni na Sh500 milioni, gari ambazo huagizwa kwa maelekezo maalum kutokana na mahitaji ya mteja (specifications) huwa na bei tofauti na zile zinazouzwa sokoni.

Kwa ujerumani, bei ya BMW ndogo ya 730d ni kati ya Euro 69,500 na euro 70,000, wakati kubwa kabisa, BMW 750Li ni Euro 94,000 kwa magari ambayo hayajaagizwa, au yale yaliyo sokoni.

Hata hivyo, magari hayo mawili-Merceds Benz na BMW hayana tofauti kubwa ya bei, ingawa Mercedes imekuwa ikionekana kuwa imara na inayodumu kwa muda mrefu.

Inaelezwa kuwa baada ya kuwasilishwa kwa mpango wa kuhama Mercedes, Rais Kikwete alipinga wazo hilo, lakini timu ya usalama ikashauri na kusisitiza kuwa gari hizo ni muhimu kwa sasa.

Ingawa inaonekana gari hizo ni za gharama, lakini timu hiyo ilisisitiza kwamba usalama wa rais ni jambo muhimu zaidi.

Hata hivyo, Rais Kikwete bado anatumia gari aina ya Mercedes Benz kwenye misafara yake na alitumia msafara wa Mercedes wakati alipokuwa Dodoma kuongoza kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM.

Akiwa Dodoma, Rais Kikwete alitumia Mercedes Benz kubwa ya milango sita, ambayo ilimchukua kutoka Uwanja wa Taifa mara baada ya kukabidhiwa nchi na rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa.

Source: Mwananchi


My take
Haya sasa ooh serikali haina pesa ooh nchi yetu maskini.
Mambo hayo magari haya tayari yamesha igharimu serikali si chini ya Bilioni 1.
Bado msafara wa Pinda,Shein,KArume na wengineo.
 
Nawashangaa waandishi wetu wa habari kwa kuchelewa kuripoti habari hii. Mboan msafara wa JK umekuwa ukitumia BMW kwa zaidi ya miezi mitatu sasa!
 
Hatuna fedha (serikali) za kuwakopesha wanafunzi 100% vyuo vikuu!! Tulizo nazo ni za kuhakikisha tu usalama wa viongozi hivyo kununua BMW customized/special order bulletproof.

Ama kwa hakika usalama wa kiongozi is a function of what he does, what he decide, what he defend, what he is, how his image is perceived, how he makes decision, how he talks or make speech, how he keep close to the people. If all is well kiongozi can walk even in the mid night on foot in Manzese suburbs, 1200 noon at Kariakoo, or going to mosque/church at 0500am on foot at Magomeni. I do not mean the president must risk but security should not cost us too much over the interest of the citizens. Mbona viongozi wetu wa vijiji hawahofu security? BUT Yes we are unique and we LOVE our president and our country too! Outside the box we need to have very well organised team to set priorities and prioritize when it comes to matters of high financial coughs.

CREDIT to our hon. President kwa kukubali kwa kutokubaliana na uamuzi huo wa usalama kununua BMW wakati duniani Mercedes inakubalika na tunazo za kutosha. Haya watueleze hizo walizo nazo Benz watazipeleka wapi au ndio minada ya kishikaji kimya kimya? Hata mimi ningependa kununua Benz walizoendeshwa marais wangu Dar es Salaam. Tena bado zitakuwa mma kabisa kwani hazijavuka Dar es Salaam. Barabara ni mkeka kama Nyu Yoku vile. Cha kubadilisha ni matairi tu.

Mungu ibariki Tanzania!
 
Aarrrggghhh...

Naona baadhi ya wadanganyika tayari wameshadanganyika tayari..Eti wanampongeza rais kwa 'kupinga' kununuliwa hizi BMW!! Sasa Mh. rais amekataa zisinunuliwe, mbona zipo barabarani? Kupinga huku kupinga gani wajameni?

Kweli wadanganyika hatustahili kuonewa huruma..
 
Lazima kuna cha juu hapo. Watu wamekaa chini, wametafuta pa kutokea, wakaamua kubadilisha magari ya msafara wa Rais.
 
Lazima kuna cha juu hapo. Watu wamekaa chini, wametafuta pa kutokea, wakaamua kubadilisha magari ya msafara wa Rais.

May be, just may be 'cause kama EPA, Richmond, etc happened, this one is no exemption!
 
Misalocation of resources. Tukiwauliza wahusika tunajibiwa "Wadanganyika mlitaka Mr Presidaa apande pikipiki?"
 
*YAACHANA NA MERCEDES BENZI


Na Ramadhan Semtawa


Source: Mwananchi


My take
Haya sasa ooh serikali haina pesa ooh nchi yetu maskini.
Mambo hayo magari haya tayari yamesha igharimu serikali si chini ya Bilioni 1.
Bado msafara wa Pinda,Shein,KArume na wengineo.

Kwani hujui kuwa tuna mfalme na siyo raisi???? mfalme lazima awe na maBMW,mabenzi,ndege ya gharama mno!!! na pia lazima aitalii dunia nzima ili ajitambulishe!!.na pia anahitaji helikopta ya kuzungukia mjini ili asichoke sana!
 
Sasa hamtaki kukubali kuwa nchi yenu ni maskini? Waziri Mkuu kasema sisi ni "maskini sana" halafu mnakataa; mnataka Rais atumie usafiri gani kuendana na hadhi yake kama Amiri Jeshi Mkuu, na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi. Hawezi kusafiria Corolla!
 
Nimesikitika kusoma kwenye magazeti kwamba Rais amesema sera ya mikopo haiwezi kubadilisha na kuwakopesha wanafunzi kwa asilimia 100. Halafu upungufu uliopo, kwa mujibu wa Prof Lipumba ni Shs 23 bilioni tu.

Hivi mnakumbuka kwamba serikali ilitoa Shs 20 bilioni kumsadia mwekezaji wa wa Shirika la reli kulipa mishahara ya wafanyakazi? Je mnakumbuka kwamba serikali itoa pia Shs 20 bilioni kulipa fidia ya wakazi wa Tabata waliobomolewa nyumba zao kwa makosa ya kizembe ya maafisa wa jiji? Wanashindwa nini kurekebisha bajeti na kuongeza hizo bilioni 23 kwa mwaka?

Leo hii, serikali inachezea sekta nyeti ya elimu kwa kufunga vyuo vikuu vyake saba, wahadhiri na wafanyakazi wengine wa vyuo hivyo bado wanaendelea kulipwa mishahara kama kawaida, na gharama zingine ziko pale pale (fixed costs). Siku wakipiga mahesabu watakuja kugundua wamepata hasara kubwa inayokaribiana na pesa hizo ambazo wangeweza kuongezea!
 
Sasa hamtaki kukubali kuwa nchi yenu ni maskini? Waziri Mkuu kasema sisi ni "maskini sana" halafu mnakataa; mnataka Rais atumie usafiri gani kuendana na hadhi yake kama Amiri Jeshi Mkuu, na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi. Hawezi kusafiria Corolla!
Mwanakijiji,

That's nice of you.

Namheshimu sana rais wa nchi, napenda sana awe salama wakati wote. Tena nipo tayari kujitolea kumwokoa pindi atapokuwa katika hataari.

Lakini mkuu kumbuka kuwa tupo ulimwengu wa tatu.
Adui yetu ni nani?

Nimesikitika kusoma kwenye magazeti kwamba Rais amesema sera ya mikopo haiwezi kubadilisha na kuwakopesha wanafunzi kwa asilimia 100. Halafu upungufu uliopo, kwa mujibu wa Prof Lipumba ni Shs 23 bilioni tu.

Hivi mnakumbuka kwamba serikali ilitoa Shs 20 bilioni kumsadia mwekezaji wa wa Shirika la reli kulipa mishahara ya wafanyakazi? Je mnakumbuka kwamba serikali itoa pia Shs 20 bilioni kulipa fidia ya wakazi wa Tabata waliobomolewa nyumba zao kwa makosa ya kizembe ya maafisa wa jiji? Wanashindwa nini kurekebisha bajeti na kuongeza hizo bilioni 23 kwa mwaka?

Leo hii, serikali inachezea sekta nyeti ya elimu kwa kufunga vyuo vikuu vyake saba, wahadhiri na wafanyakazi wengine wa vyuo hivyo bado wanaendelea kulipwa mishahara kama kawaida, na gharama zingine ziko pale pale (fixed costs). Siku wakipiga mahesabu watakuja kugundua wamepata hasara kubwa inayokaribiana na pesa hizo ambazo wangeweza kuongezea!
Masaki, observation yako mkuu iko sahihi. Ni vipaumbele vya taifa letu havieleweki tu.
 
Mimi nina wasi wasi na uamuzi huu wa ghafla kwamba wananunua gari hizo kwa ajili ya usalama wa Mh. Raisi.
  1. Rais wetu hayuko hatarini kiasi cha kununua gari aina nyingine.
  2. Kama Mh Rais alikataa kwanini walazimishe?
  3. Wana agenda gani?
  4. Tafakari
  5. Chukua hatua
 
Last edited:
Hmmm BMW gani ya $ 500,000 alafu hiyo gari ya milango sita alimaanisha stretched limo? lol
 
Hmmm BMW gani ya $ 500,000 alafu hiyo gari ya milango sita alimaanisha stretched limo? lol
Mkuu Icadon,

Kwenye masuala haya nakukubali sana tu. Hebu tupe ushauri, ni gari gani la gharama nafuu linaweza kumfaa rais wetu? Be frank, kama hawajakosea tusiwabebeshe mzigo wa lawama bure
 
Mkuu Icadon,

Kwenye masuala haya nakukubali sana tu. Hebu tupe ushauri, ni gari gani la gharama nafuu linaweza kumfaa rais wetu? Be frank, kama hawajakosea tusiwabebeshe mzigo wa lawama bure

Inategemea na aina ya BMW anayoitumia na security features zake
kama ni 760Li bei yake ni $ 124,000 bila vikorombwezo vya usalama....kuhusu X5 nadhani tulizungumzia kwenye ile thread.
 
Tuishi kwa matumaini tu, pengine Tanzania ipo siku itapata Rais aliye "humble" na mwenye akili kama yule wa Iran!!
 
Jamani,hapa JK tusimuonee.Haya magari wamepewa buree toka uarabuni.Tena hawa waarabu walileta mpaka mtaalamu wa haya magari toka Ujerumani kuja kuyafanyia service kabla hayaanza kutumiwa.Hata lile benzi alilotumia Mkapa wakati anamaliza muda wake nalo lilikuwa la chee toka hukohuko.
 
Jamani,hapa JK tusimuonee.Haya magari wamepewa buree toka uarabuni.Tena hawa waarabu walileta mpaka mtaalamu wa haya magari toka Ujerumani kuja kuyafanyia service kabla hayaanza kutumiwa.Hata lile benzi alilotumia Mkapa wakati anamaliza muda wake nalo lilikuwa la chee toka hukohuko.

acha kutudanganya bana, waarabu gani hao wanaoingia hadi kwenye usalama wa Rais? wewe umejuaje? isitoshe misaada huwa inatangazwa.
 
Ukiona mtu anakupa msaada mkubwa kama wa magari ya mamilioni ujue hapo kuna kupeana fadhira in return sasa kama ni kweli waarabu wametoa hayo magari kuna kitu nasi tunawanufaisha hakuna urafiki usio kuwa na manufaa lazima mmoja aumie mwingine anufaike huu ndo urafiki wote mkitaka kunufaika basi mifalakano huanza.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom