Ikulu inamhitaji zaidi Jairo kuliko inavyomhitaji Pinda?

pinda ajue sasa kuwa yuko kwenye gari amablo anasafiri nalo yeye ni dereva lakini hajui destination ya safari hiyo anaelekezwa na kina mkw ere, Jeuri na Mihanjo. Aachie ngazi ili kulinda adabu yake vinginevyo anaprove beyond doubt kuwa yeye ni ziro mtanzania
 
Ndugai '' huko huko (ikulu) na sio hapa (bungeni) ''
bunge 0-1 ikulu
dakika ni ya 89 na bunge wameamua kufanya sabu ya tume ya mashambulizi na tuone kama watarudisha na kuongeza bao la ushindi
 
serikali ya JK ni upuuzi mtupu.. hakuna msafi kiakili mpaka wizi shenzyyyyyyyyyyyyyyyyy...! ipo siku
 
<b>Pinda is an accidental prime minister cheo kakipata kibahati na haikutokana na nguvu yoyote aliyo nayo ndani ya chama. Jairo inajulikana wazi ni mtu wa JK tokea zamani. Pinda kaukwa tu kwa vile EL alijiuzuru na serikali ilihitaji mtu asie na makundi wala nguvu kujaza nafasi. Huo ndiyo ukweli.</b>
<br />
<br />I agree with you, and that is the truth.
 
Jamani Jairo ni rafiki sana wa JK na asingekubali rafiki yake adharirishwe na serikali yake pia iendelee kupata aibu hivyo ilikuwa ni lazima Jairo asafishwe kupitia kwa CAG. Pia JK aliona Pinda hafai kwa vile amezielewa vizuri ukweli wa tuhuma na alikuwa tayari kumwadhibisha Jairo. Hivyo aliona Luhanjo ambaye ni mdogo kwa ranking apewa kazi ya kusimamia kumsafisha jairo, mawaziri wa wizara hiyo na serikali yake, baada ya kutoa maelekezo kwa Luhanjo na CAG, JK kama kawaida akanyamaza kama vile yeye si Rais wa Jamhuri ya Tanzania.

Sasa kusafishwa kumekamilika vizuri sana, wabunge na Pinda wameonekana ni waongo na wapika majungu. Ama kweli Watanzania tumekuwa kuku wa kizungu bandani.
 
Waziri Mkuu angejitengenezea mazingira mazuri sana na ya kuheshimika kama hapo ijumaa wakati wa hotuba yale ya kuhairisha bunge la kumi angetamka pia kwamba anajiuzulu rasmi nafasi yake ya uwaziri mkuu. Pengine atafanya hivyo, tusubiri.
 
Waziri Mkuu angejitengenezea mazingira mazuri sana na ya kuheshimika kama hapo ijumaa wakati wa hotuba yale ya kuhairisha bunge la kumi angetamka pia kwamba anajiuzulu rasmi nafasi yake ya uwaziri mkuu. Pengine atafanya hivyo, tusubiri.

Jamani kujiuzuli ccm wapi mliona???? si jambo la kawaida kwa ccm, he can't do that coz siyo culture yao na je mafao yake na miposhoposho nani ataila??? wanatamaa, hawezi pia kiprotocali wanamautaratibu mengi, sioni ajabu ktk hili. wananchi ndo mnaoumia
 
Wabunge- Bunge limedhalilishwa, Pinda kafedheheshwa
BUNGE limesema, Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo amelidhalilisha na pia amemdhalilisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwa kumuamuru Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo arudi kazini. Wabunge wamesema, taarifa ya uchunguzi ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG) kuhusu tuhuma kwamba, Jairo alichangisha shilingi bilioni moja ili kuwezesha bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini ipitishwe bungeni ilistahili kupelekwa bungeni waijadili kabla Serikali kutoa uamuzi.

Wabunge leo wamejadili kauli ya Luhanjo kama jambo la dharura baada ya wabunge kukubali hoja ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto aliyoitoa asubuhi kabla ya kipindi maswali na majibu na kuifafanua baada ya Kamati ya Bunge ya Uongozi kukutana katika ukumbi wa Spika.

Spika wa Bunge, Anne Makinda aliongoza kikao hicho cha dharura wakati wa kipindi cha maswali na majibu.

Kabla ya kamati hiyo kukutana, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, alisema, kwa kutumia kifungu cha 51 cha Kanuni za Bunge alichotumia Zitto kuwasilisha hoja yake, inamtaka Mbunge aiwasilishe mapema kwa Spika wa Bunge ili atoe uamuzi. Naibu Spika Spika wa Bunge, Job Ndugai, alimjibu Lukuvi kwamba, kabla ya kuanza kwa kikao cha leo, Zitto alipeleka taarifa fupi kwa Spika wa Bunge kuhusu hoja hiyo kwa hiyo utaratibu umefuatwa.

“Hoja hii nzito kweli…na ndiyo hoja iliyoungwa mkono” amesema Ndugai baada ya Zitto kuiwasilisha kwa mara ya kwanza kabla ya.

Zaidi ya robo tatu ya wabunge waliokuwa ukumbini wakiwemo kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) wameunga mkono hoja ya Zitto. Ndugai, amesema bungeni kuwa, hoja ya Zitto ni ya msingi kwa kuwa Bunge limedharauliwa.

“Kwa sababu Bunge ni mhimili, hatuwezi kudharauliwa kirahisi”amesema Ndugai na kusisitiza kwamba,Wabunge hawawezi kukaa kimya wakati Waziri Mkuu anadhalilishwa. “Kama dharau inaweza ikatokea basi huko huko lakini sio ndani ya Bunge hili” amesema Ndugai baada ya wabunge kuijadili hoja ya Zitto na kusisitiza kwamba, kwa kuwa suala hilo lilianzia bungeni, taarifa ya CAG ingepelekwa kwanza kwenye mamlaka hiyo kabla ya uamuzi wa Serikali.

Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Zainab Vullu, wabunge wamepewa jukumu la kuisimamia na kuishauri Serikali kwa niaba ya wananchi hivyo kauli ya Luhanjo imewadhalilisha, na limepokwa mamlaka yake.

Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka, amesema, suala hilo lina maslahi kwa Taifa, taarifa ya CAG ingepelekwa kwanza bungeni itendewe haki. Sendeka amesema bungeni kuwa, Waziri Mkuu amefedheheshwa kwa kuwa Kiongozi huyo wa Shughuli za Serikali Bungeni alisema, kama angekuwa yeye angemchukilia hatua Jairo, na pia Bunge limedhalilishwa. Kwa mujibu wa Sendeka, kauli ya Luhanjo imelilidhalilisha Bunge na imekiuka Sheria ya Kinga na Madaraka ya Bunge na ibara ya 100 ya Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.

Mbunge huyo ametumia Kanuni 117 ya Bunge kuomba iundwe kamati teule ya Bunge kuchunguza jambo hilo ukiwemo utaratibu wa Jairo kukusanya fedha za kupitishia bajeti hasa ikizingatiwa kuwa, kila Waziri huwa na fungu la kugharamia bajeti kila idara zikiwemo fedha za kununulia mafuta. Sendeka aliomba Bunge liunge mkono hoja yake ili kulinda hadhi ya Bunge, takribani wabunge wote walikubali isipokuwa mawaziri na manaibu mawaziri.

Wakati anatoa hoja hiyo, Zitto amesema, kwa kuwa jambo hilo lilianzia bungeni wakati Mbunge wa Kilindi, Beatrice Shelukindo (CCM) alipolieleza Bunge kuwa ana barua ya Jairo kuzitaka idara katika Wizara za Nishati na Madini zichangie shilingi milioni 50 kila moja, wabunge walistahili kuijadili ripoti ya CAG kabla ya Serikali kufanya uamuzi.

Zitto amelieleza Bunge kuwa, kauli ya Luhanjo ni dharau kwa Waziri Mkuu, na imeingilia hadhi, kinga na madaraka ya Bunge kwa kuwa wabunge ndiyo wana mamlaka ya kuisimamia Serikali. Zitto alipendekeza kwamba, shughuli na hoja zote za Serikali bungeni zisitishwe, kwanza wabunge waijadili taarifa za CAG kwa kuwa Bunge limepokwa nafasi yake.

Ndugai amewaeleza wabunge kuwa, Spika wa Bunge, Makinda, ataunda tume kuchunguza kudharauliwa kwa Bunge, na kukusanywa kwa fedha kwa ajili ya kupitishwa bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2011/2012. Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa Bunge, tume hiyo itapaswa kufanya kazi haraka ili taarifa yake ijadiliwe katika mkutano ujao wa Bunge.

Luhanjo jana alimuagiza Jairo arudi kazini leo aendelee na madaraka yake katika Wizara ya Nishati na Madini kwa kuwa tuhuma zilizotolewa dhidi yake hazikuthibitika. Leo asubuhi, Jairo alikwenda ofisini kwake wizarani jijini Dar es Salaam, wafanyakazi wakampokea kwa shangwe na vigelegele huku wakiimba kwamba wana imani naye.

Source: Habari Leo
 
Nchi zinazoongozwa kwa mujibu wa sheria kitendo cha Ikulu kuteka hoja iliyoibuliwa na Bunge na kuchukulia uamuzi bila kufikisha matokeo ya uchunguzi maana yake ni kudharau mhimili wa Bunge. Papo hapo ni dharau kubwa kwa waziri mkuu aliyeonyesha kutoridhishwa na Jairo na hata kuwa tayari kutolea uamuzi papo kwa papo lakini alichelea kuheshimu mamlaka yaliyo juu yake yaari Rais.

Katibu mkuu wa Rais ni mdogo kimadaraka kwa Waziri Mkuu, ingawa anaweza kuchukua maamuzi kwa kuelekezwa na Rais, swali linalojitokeza inawezekanaje uamuzi huo ukafikiwa na Ikulu bila kumhusisha Waziri mkuu aliyekaribu na kujua zaidi kilichojilia ndani ya Bunge. Kwa mtazamo wa jumla inaonekana serikali haifanyi kazi kwa ushirikiano, na hivyo kila chombo, idara na mhimili hujitolea kauli na utekelezaji usio na mshikamano wa kuwajibika pamoja.

Tofauti ya kutoheshimu Bunge pamoja na baadhi ya matuzi ya rejareja ambayo wahusika na kashfa wamewatukana wabunge au Bunge na hivyo kuonekana kutojali shughuli ya bunge kusimamia serikali, Sitashangaa kuona kuna siku Bunge kwa dhamira ya uwajibikaji na uchungu kwa nchi yetu ikapiga kura ya kutokuwa na imani na serikali iliyopo kikatiba.
 
Inavyoonekana shida inaanzia juu. Yaani mpaka nawahurumia watendaji wachache waadilifu wanaofanya kazi kwenye system kama hii. Yaani hawa jamaa kwao nyeupe ni nyeusi na nyekundu ni njano. Aah! Basi tu!
 
Wakati mwingine nabaki kucheka tu na sina la kusema. Hii nchi ni wenda wazimu mtupu. Hivi whats wrong with Tanzanians? How low can we get?

Someone has to be very stupid kusikiliza maneno ya kikwete na hii serikali. Really kuna watu wanakaa chini na kusikiliza akisema kitu, its .....and crap again and again.
 
Waziri Mkuu alisema kama angekuwa na mamlaka angemuwajibisha Katibu Mkuu Nishati na Madini siku ileile iliposomwa ile barua bungeni.

Baada ya ripoti ya CAG Katibu Mkuu Kiongozi Luhanjo anasema alichofanya Jairo ni utaratibu wa kawaida kabisa ...na kama Jairo ataweza kuwashtaki waliomdhalilisha ni yeye tu.

Nini implication ya haya kama sio kumdhalilisha na kumshusha Pinda na kumnyanyua Jairo ni nn?

Ndo maana mi nasema IKULU INAMHITAJI ZAIDI JAIRO KULIKO PINDA
Hii ilifahamika tangu mwanzo ya kua katika swala la kuwahonga wabunge ili wapitishe bajeti ya wizara ya nishati na madini ulikua ni mpango wa JK na serikali na ulipata baraka zote toka kwa JK na serikali kwa ujumla.Na hii imekua inafanyika kwa muda mrefu na hii ndio siri ya mikataba feki.Jairo alikua mtekelezaji tu.Kwa madai ya Katibu Mkuu Kiongozi, Phillemon Luhanjo ya kua wafanyakazi waliovujisha siri watachukuliwa hatua kimenishanagaza!Kama utaratibu huo ni halali kwanini uwe siri!
 
Jamani Jairo ni rafiki sana wa JK na asingekubali rafiki yake adharirishwe na serikali yake pia iendelee kupata aibu hivyo ilikuwa ni lazima Jairo asafishwe kupitia kwa CAG. Pia JK aliona Pinda hafai kwa vile amezielewa vizuri ukweli wa tuhuma na alikuwa tayari kumwadhibisha Jairo. Hivyo aliona Luhanjo ambaye ni mdogo kwa ranking apewa kazi ya kusimamia kumsafisha jairo, mawaziri wa wizara hiyo na serikali yake, baada ya kutoa maelekezo kwa Luhanjo na CAG, JK kama kawaida akanyamaza kama vile yeye si Rais wa Jamhuri ya Tanzania.

Sasa kusafishwa kumekamilika vizuri sana, wabunge na Pinda wameonekana ni waongo na wapika majungu. Ama kweli Watanzania tumekuwa kuku wa kizungu bandani.
Kwenye nyekundu hapo, hiyo ndiyo stahili ya Utawala ya JK, Yeye anawasha Moto halafu anakaa kimya pembeni akijifanya kama hajui lolote linaloendelea, kwamba yeye hausiki.
 
Luhanjo huyu huyu aliyepigana vikumbo na waziri wa mambo ya ndani 2008/9, sasa na na wziri mkuu, next atapigana vikumbo na Rais.
Jeuri anaitoa wapi?
 
Back
Top Bottom