Ikulu ilizuia Vigogo 3 Kufikishwa Mahakamani

Ibrah

JF-Expert Member
Mar 22, 2007
2,729
528
Nimepata habari kutoka vyanzo vya kuaminika kuwa DPP alikuwa awafikishe Watuhumiwa wakubwa wa Ufisadi; wawili walikuwa Mawaziri waandamizi wa Awamu ya II na Katibu Mkuu 1 ambaye amekuwa Wizara moja nyeti kwa muda mrefu hadi sasa.

Habari zinapasha kuwa walishatinga kwenye Jengo la Mahakama lakini haijulikani ni namna gani habari zilimfikia Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu, Katibu Mkuu Kiongozi alipothibitishiwa kuwa ni kweli Watuhumiwa hao wako aliwang'akia PCCB "Mnataka Nchii hii istawalike?" naye akawasiliana na Mkuu wa nchi aliyekuwa ughaibuni ambaye aliagiza kuwa wasisomewe mashitaka!
Habari zinapasha kuwa ushahidi dhidi ya Watuhumiwa hao uko wazi kabisa ingawa habari zinasema kuwa hata Rais aliyepita wa awamu ya II angejikuta yuko implicated kwenye tuhuma hizo za Ufisadi.

Habari nyingine zinapasha kuwa Serikali mwakani 2009 itaustua umma wa WaTz kwa kumfikisha Mahakamani Kigogo mmoja naMwanamtandao mkubwa ikiwa ni mkakati wa kujiandaa na uchaguzi wa 2010 ili kuzima jaribio la kumfanya JK aenguliwe katika kinyang'anyiro cha Urais katika CCM.
 
Duh Makubwa..
Hii ishu yawezekana kweli.Sasa kwa nini wanasua sua mbona nchi imesha haribika.
Nani hajui kuwa viongozi wetu wengi ni mafisadi?Wangelipuliwa tu ili wajisafishe.
Huyu Luhanjo naye amekalia kuti kavu mwacheni tu siku zake zinahesabika tutamsahau kama ndugu yake Mangula yupo kijijini sasa analima viazi tu.
 
Nimepata habari kutoka vyanzo vya kuaminika kuwa DPP alikuwa awafikishe Watuhumiwa wakubwa wa Ufisadi; wawili walikuwa Mawaziri waandamizi wa Awamu ya II na Katibu Mkuu 1 ambaye amekuwa Wizara moja nyeti kwa muda mrefu hadi sasa.

Habari zinapasha kuwa walishatinga kwenye Jengo la Mahakama lakini haijulikani ni namna gani habari zilimfikia Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu, Katibu Mkuu Kiongozi alipothibitishiwa kuwa ni kweli Watuhumiwa hao wako aliwang'akia PCCB "Mnataka Nchii hii istawalike?" naye akawasiliana na Mkuu wa nchi aliyekuwa ughaibuni ambaye aliagiza kuwa wasisomewe mashitaka!
Habari zinapasha kuwa ushahidi dhidi ya Watuhumiwa hao uko wazi kabisa ingawa habari zinasema kuwa hata Rais aliyepita wa awamu ya II angejikuta yuko implicated kwenye tuhuma hizo za Ufisadi.

Habari nyingine zinapasha kuwa Serikali mwakani 2009 itaustua umma wa WaTz kwa kumfikisha Mahakamani Kigogo mmoja naMwanamtandao mkubwa ikiwa ni mkakati wa kujiandaa na uchaguzi wa 2010 ili kuzima jaribio la kumfanya JK aenguliwe katika kinyang'anyiro cha Urais katika CCM.


Makubwa hayo. Madogo yana nafuu. Yangu macho na masikio. Mengi yamesemwa hatujaona matokeo. Labda hili la 2009 la kushtua umma kama litafanyiwa kazi itakuwa ni exceptional!!!!!
 
"mabangusilo" wanaandaliwa kwa ajili ya sympathy vote 2010.


Si mabangusilo Steve D ni kweli kuwa ni Mafisadi ila kinachofanyika ni kutaka kuwatumia Mafisadi hao kupata kibali cha kuendelea kuwadanganya watanzania ili waendelee kutuongoza tena 2010, na pia ni njia ya kuhakikisha kuwa wanawazima kwa kuwa ni wapinzania wao wa ndani kwa ndani na walishirikiana nao kwenye ufisadi wote isipokuwa kuwa sasa hawana nguvu ya kimadaraka tu.
 
taja majina... this is the forum where we dare to talk openly remember!!!
 
Nadhani tumwambie JK, kuwa kesi zote atakazofungua kuanzia mwakani hatutazitambua -Hizo itakuwa ni mbinu za kifisadi za kushinda uchaguzi! Kama kweli atakuwa anamaanisha basi azifungue na ziishe ndani ya mwaka huohuo ili tuone kama kutakuwa convictions! Safari hii wataishiwa tricks! Miti yote itateleza!
 
NImekupata

Hapo inamaana kuwa huo mtikisiko utakuwa hivi:
LOWASSA au CHENGE atapelekwa mahakamani 2009, HALAFU UMA WA WATZ UTADANGANYIKA MWAKA 2010 watamchagua tena Joti aka Muuza sura JK halafu baada ya uchaguzi mshtakiwa atashinda kesi maana serikali ndio inamiliki mahakama, umaendesha nchi kimabavu + mwanasheria mkono na wengine toka NJE watamtetea mashtakiwa+ hakima atapewa mabilioni kama rushwa na serikali na mshtakiwa binafsi

TZ ZAIDI UIJUAVYO
 
Nimepata habari kutoka vyanzo vya kuaminika kuwa DPP alikuwa awafikishe Watuhumiwa wakubwa wa Ufisadi; wawili walikuwa Mawaziri waandamizi wa Awamu ya II na Katibu Mkuu 1 ambaye amekuwa Wizara moja nyeti kwa muda mrefu hadi sasa.

Habari zinapasha kuwa walishatinga kwenye Jengo la Mahakama lakini haijulikani ni namna gani habari zilimfikia Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu, Katibu Mkuu Kiongozi alipothibitishiwa kuwa ni kweli Watuhumiwa hao wako aliwang'akia PCCB "Mnataka Nchii hii istawalike?" naye akawasiliana na Mkuu wa nchi aliyekuwa ughaibuni ambaye aliagiza kuwa wasisomewe mashitaka!
Habari zinapasha kuwa ushahidi dhidi ya Watuhumiwa hao uko wazi kabisa ingawa habari zinasema kuwa hata Rais aliyepita wa awamu ya II angejikuta yuko implicated kwenye tuhuma hizo za Ufisadi.

Habari nyingine zinapasha kuwa Serikali mwakani 2009 itaustua umma wa WaTz kwa kumfikisha Mahakamani Kigogo mmoja naMwanamtandao mkubwa ikiwa ni mkakati wa kujiandaa na uchaguzi wa 2010 ili kuzima jaribio la kumfanya JK aenguliwe katika kinyang'anyiro cha Urais katika CCM.


Mkuu nakupa tano: Vigogo hao ni: Mawaziri wa zamani, Daniel Yona kwa kesi ya Kiwira, Basil Mramba kwa kesi ya exemption ya Corporate Tax katika kampuni ya Alex Stewarts na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Gray Mgonja.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...ia-mashtaka-dhidi-ya-vigogo-kesi-za-pccb.html

Raia Mwema - Mawaziri kushitakiwa kwa tuhuma za ufisadi

Mramba na Yona kushitakiwa!! | Jambo Blog Network

Kwa ujumla ni kwamba kisingizio cha KAtibu Mkuu Kiongozi, P.Luhanjo ni kwamba, siku waliyokuwa wakitaka kupelekwa mahakamani Mgonja alikuwa akutane na wafadhili ambao wangepoteza imani na serikali kwa hiyo akaomba waahirishe kesi hadi muda wake wa kustaafu utakapofika. Inasemekana atastaafu kati ya mwezi huu na Novembe 08.

Kimsingi Luhanjo naye ni fisadi mkubwa, data zake tutaziweka wakati mwafaka.
 
Nimepata habari kutoka vyanzo vya kuaminika kuwa DPP alikuwa awafikishe Watuhumiwa wakubwa wa Ufisadi; wawili walikuwa Mawaziri waandamizi wa Awamu ya II na Katibu Mkuu 1 ambaye amekuwa Wizara moja nyeti kwa muda mrefu hadi sasa.

Habari zinapasha kuwa walishatinga kwenye Jengo la Mahakama lakini haijulikani ni namna gani habari zilimfikia Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu, Katibu Mkuu Kiongozi alipothibitishiwa kuwa ni kweli Watuhumiwa hao wako aliwang'akia PCCB "Mnataka Nchii hii istawalike?" naye akawasiliana na Mkuu wa nchi aliyekuwa ughaibuni ambaye aliagiza kuwa wasisomewe mashitaka!
Habari zinapasha kuwa ushahidi dhidi ya Watuhumiwa hao uko wazi kabisa ingawa habari zinasema kuwa hata Rais aliyepita wa awamu ya II angejikuta yuko implicated kwenye tuhuma hizo za Ufisadi.

Habari nyingine zinapasha kuwa Serikali mwakani 2009 itaustua umma wa WaTz kwa kumfikisha Mahakamani Kigogo mmoja naMwanamtandao mkubwa ikiwa ni mkakati wa kujiandaa na uchaguzi wa 2010 ili kuzima jaribio la kumfanya JK aenguliwe katika kinyang'anyiro cha Urais katika CCM.

...........No doubt............... Daniel Yona na Gray Mgonja ndani
 
NImekupata

Hapo inamaana kuwa huo mtikisiko utakuwa hivi:
LOWASSA au CHENGE atapelekwa mahakamani 2009, HALAFU UMA WA WATZ UTADANGANYIKA MWAKA 2010 watamchagua tena Joti aka Muuza sura JK halafu baada ya uchaguzi mshtakiwa atashinda kesi maana serikali ndio inamiliki mahakama, umaendesha nchi kimabavu + mwanasheria mkono na wengine toka NJE watamtetea mashtakiwa+ hakima atapewa mabilioni kama rushwa na serikali na mshtakiwa binafsi

TZ ZAIDI UIJUAVYO

Duh, haya anayobashiri Tuandamane tyaweza kutokea kweli siku moja. Na si mbali sana.
 
Nimepata habari kutoka vyanzo vya kuaminika kuwa DPP alikuwa awafikishe Watuhumiwa wakubwa wa Ufisadi; wawili walikuwa Mawaziri waandamizi wa Awamu ya II na Katibu Mkuu 1 ambaye amekuwa Wizara moja nyeti kwa muda mrefu hadi sasa.

Habari zinapasha kuwa walishatinga kwenye Jengo la Mahakama lakini haijulikani ni namna gani habari zilimfikia Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu, Katibu Mkuu Kiongozi alipothibitishiwa kuwa ni kweli Watuhumiwa hao wako aliwang'akia PCCB "Mnataka Nchii hii istawalike?" naye akawasiliana na Mkuu wa nchi aliyekuwa ughaibuni ambaye aliagiza kuwa wasisomewe mashitaka!
Habari zinapasha kuwa ushahidi dhidi ya Watuhumiwa hao uko wazi kabisa ingawa habari zinasema kuwa hata Rais aliyepita wa awamu ya II angejikuta yuko implicated kwenye tuhuma hizo za Ufisadi.

Habari nyingine zinapasha kuwa Serikali mwakani 2009 itaustua umma wa WaTz kwa kumfikisha Mahakamani Kigogo mmoja naMwanamtandao mkubwa ikiwa ni mkakati wa kujiandaa na uchaguzi wa 2010 ili kuzima jaribio la kumfanya JK aenguliwe katika kinyang'anyiro cha Urais katika CCM.

Hizi nyepesi nyepesi za mafisadi wakitaka kutuhadaa ili tuamini kuna progress. Nadhani kwa kuwa wameamua kuwadharau watanzania kwa kuamua kuulinda ufisadi kwa gharama yeyote basi wanaweka mazingira magumu ya nchi kutawalika hapo mbeleni. I mean tutawanyima kura zetu hata wakiamua kuziiba wataiba mapaka wataona aibu wenyewe...
Hakimu ni Fisi na mtuhumiwa ni Fisi je swala ahatapa haki yake??
 
Nimepata habari kutoka vyanzo vya kuaminika kuwa DPP alikuwa awafikishe Watuhumiwa wakubwa wa Ufisadi; wawili walikuwa Mawaziri waandamizi wa Awamu ya II na Katibu Mkuu 1 ambaye amekuwa Wizara moja nyeti kwa muda mrefu hadi sasa.

Habari zinapasha kuwa walishatinga kwenye Jengo la Mahakama lakini haijulikani ni namna gani habari zilimfikia Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu, Katibu Mkuu Kiongozi alipothibitishiwa kuwa ni kweli Watuhumiwa hao wako aliwang'akia PCCB "Mnataka Nchii hii istawalike?" naye akawasiliana na Mkuu wa nchi aliyekuwa ughaibuni ambaye aliagiza kuwa wasisomewe mashitaka!
Habari zinapasha kuwa ushahidi dhidi ya Watuhumiwa hao uko wazi kabisa ingawa habari zinasema kuwa hata Rais aliyepita wa awamu ya II angejikuta yuko implicated kwenye tuhuma hizo za Ufisadi.

Habari nyingine zinapasha kuwa Serikali mwakani 2009 itaustua umma wa WaTz kwa kumfikisha Mahakamani Kigogo mmoja naMwanamtandao mkubwa ikiwa ni mkakati wa kujiandaa na uchaguzi wa 2010 ili kuzima jaribio la kumfanya JK aenguliwe katika kinyang'anyiro cha Urais katika CCM.

Haya ndiyo matatizo ya kuwa na kiongozi wa nchi aliyeingia madarakani kwa kuwatumia mafisadi na kutoa rushwa kwa wapiga kura wa chama chake ili wampitishe kama mgombea wa chama chao. Hao mafisadi waliokuwa wafikishwe mahakamani wanajua fika aliyoyafanya Kikwete ili aingie Ikulu na kamwe hawatakuwa tayari kuadhirika pekee yao. Kuna uwezekano mkubwa wakaamua kuongea yaliyofanywa na mkuu pale Dodoma na hatimaye kuibuka kidedea na hili litamfanya mkuu aombe kuachia ngazi. Hivyo alivyosema kwamba nchi inaweza kushindwa kutawalika ni kweli kabisa. Lakini je tutalinda maslahi ya viongozi uchwara na mafisadi mpaka lini? Nchi sasa hivi inateketea kama kiongozi ni fisadi basi ni lazima aanikwe ili aachie ngazi na tupate kiongozi atakayeweka maslahi ya Watanzania mbele badala ya kwake binafsi.
 
Ibrah,



Hii habari yako inaonekana wazi kuwa sio ya kweli maana
  1. Haitaji jina la mhusika yeyote ingawa imeshaelezwa kuwa walionekana mahakamani.
  2. Either umeitunga kutokana na yale tunayoyafahamu juu ya mafisadi au umedanganywa maana kila kilichoandikwa ni cha kufikirika, including majina.
  3. Inaelekea aliyeitunga hii habari nia yake ilikuwa ni hilo hitimisho la kuwa CCM wana njama za kutumia ufisadi kuwafaa wao wenyewe kama ulivyoandika otherwise utueleze zaidi conclussion ilivyofikiwa;
Habari nyingine zinapasha kuwa Serikali mwakani 2009 itaustua umma wa WaTz kwa kumfikisha Mahakamani Kigogo mmoja naMwanamtandao mkubwa ikiwa ni mkakati wa kujiandaa na uchaguzi wa 2010 ili kuzima jaribio la kumfanya JK aenguliwe katika kinyang'anyiro cha Urais katika CCM.

Kama wahusika walikuwa wameshafikishwa mahakamani kama ulivyosema, ina maana hakuna aliyewaona huko mahakamani mpaka ikawa siri hadi leo? Ina maana hata huyo aliyekupa hizo 'nyeti' na yeye pia kayafanya hayo majina yao kuwa ni siri? Nanukuu ulivyoripoti hapa chini;
Nimepata habari kutoka vyanzo vya kuaminika kuwa DPP alikuwa awafikishe Watuhumiwa wakubwa wa Ufisadi; wawili walikuwa Mawaziri waandamizi wa Awamu ya II na Katibu Mkuu 1 ambaye amekuwa Wizara moja nyeti kwa muda mrefu hadi sasa.

Habari zinapasha kuwa walishatinga kwenye Jengo la Mahakama lakini haijulikani ni namna gani habari zilimfikia Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu, Katibu Mkuu Kiongozi alipothibitishiwa kuwa ni kweli Watuhumiwa hao wako aliwang'akia PCCB "Mnataka Nchii hii istawalike?" naye akawasiliana na Mkuu wa nchi aliyekuwa ughaibuni ambaye aliagiza kuwa wasisomewe mashitaka!

Ingawa tungependa hawa mabwana wafikishwe mbele ya kaisari, lakini nafikiri hilo halijafanyika kama ilivyosimuliwa, ila hii ni nyepesi ilitungwa kwa sababu anazojua mtungaji na haifai kuendelea kukaa katika jukwaa la siasa.

Mod hii ipelekwe kwenye nyepesi.
 
taja majina... this is the forum where we dare to talk openly remember!!!


Sitataja, lakini ni Mawaziri 2 wa awamu ya II na walishatajwaga sana huko nyuma, na katibu mkuu mmoja wa wizara nyeti (ileile ) tangu awamu ya ii hadi leo.
 
sitataja, lakini ni mawaziri 2 wa awamu ya ii na walishatajwaga sana huko nyuma, na katibu mkuu mmoja wa wizara nyeti (ileile ) tangu awamu ya ii hadi leo.

vipi mkuu!!! Umeshikiwa bunduki wakati unaandika hii taarifa maana una mis lead kwa makusudi, awamu ya pili mgonja alikuwa bot na si katibu mkuu pengine uniambie rutabanziba hapo nitakuelewa ila tayari jf ime doubt credibility ya story hii mkuu.

Tusubiri kuona pccb wakifanya kweli na si taarifa ya kughushi kama hii.
 
Ni habari nzuri kwa masikio, lakini katibu mkuu wa wizara kuandaliwa mashitaka hadi hatua ya kufika mahakamani bila Luhanjo (Mkuu wa utumishi serikalini) kujua basi kutakuwa na tatizo kubwa sana kiutendaji kuliko tunavyojua!
 
Back
Top Bottom