Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
[SIZE="3"]Ikulu haijampa onyo Bw Reginal Mengi
Haitoi matamko kupitia kwmye simu za mkononi
Ikitoa tamko huita vyombo mbali mbali vya habari
Taarifa katika Tanzania Daima si tamko halali
Mwandishi alikurupuka bila kufuata utaratibu
Yeye wala si Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu
Taarifa zilizotolewa
Na Mwandishi Wetu, SEMA USIKIKE
Juni 8, 2009
TAARIFA zilizotolewa na mwandishi wa habari katika kitengo cha Mawasiliano Ikulu, Premy Kibanga, kuwa Ikulu imemuonya Mengi, si tamko la Ikulu bali ni mawazo yake mwenyewem SEMA Usikike limegundua.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari kutoka ndani ya kitengo hicho, zimesema kuwa kwa kawaida Ikulu ikitoa matamko huita vyombo vya habari vyote na kutoa taarifa zake kwa kufuata utaratibu uliowekwa jambo ambalo mwandishi huyu hakulifuata.
Vyanzo vyetu pia vimebainisha kuwa taarifa zilizoandikwa katika gazeti la Tanzania Daima zikimnukuu mwandishi wa Ikulu Premy Kibanga zinadaiwa kuwa hilo si tamko la Ikulu.
Katika sehemu ya tamko ambalo mwandishi huyo, Premy Kibanga alisema limetolewa na iIkulu linasema kuwa Bw Mengi ametakiwa aviheshimu vyombo vya dola na kwamba Ikulu imekanusha madai ya Mengi kuwa anaandamwa na baadhi ya viongozi wa kiserikali pamoja na taasisi zake.
Watu waliohojiwa na gazeti hili wanasema kama kweli mwandishi huyo aliongea na gazeti hilo, alifanya kosa kubwa ambalo halijawahi kufanywa na mwandishi yeyote wa kawaida aliyewahi kufanya kazi katika kitengo huicho cha mawasiliano.
Wamesema kuwa tokea enzi za Mwalimu, hakuna tamko la Ikulu lililowahi kutolewa kwa simu na kwa chombo kimoja kama ilivyotokea sasa, tena chombo binafsi. Kwa mfano, walisema, katika enzi za awamu ya kwanza, msemaji wa Ikulu alikuwa ni Katibu Mkuu Kiongozi Timothy Apiyo ambaye alitumia utaratibu wa kutoa taarifa kwa vyombo vya habari vyote ama kutoa tamko kupitia Idara ya Habari Maelezo ambayo ilikuwa ikisambaza habari hizi kwa wahariri wakuu.
Utaratibu ambao Rais wa awamu ya pili, Mzee Ruksa aliutumia kwa kumteua Balozi Patrick Chokala kuwa msemaji wa Ikulu, waandishi walikuwa wanaitwa pale Ikulu na kuongea na Chokala, kuuliza maswali kisha kurudi kuandika habari. Hata siku moja mtu huwezi kutoa tamko la Ikulu kupitia chombo kimoja cha habari tena si cha serikali. Tena mtu hyo akiwa siyo msemaji wa Rais.
Katika utawala wa awamu ya tatu, kama kawaida utaratibu wa kutoa matamko ya ofisi ya Rais ulifuatwa pia. Mheshimiwa Benjamin Mkapa naye akamteua Geoffrey Nkurlu naye akawa anatoa taarifa kwa vyombo vyote ya habari, na si kutoa tamko kupitia simu ya mkononi tena kwa jambo nyeti kama alivyofanya mwandishi huyu Premy Kibanga .
..Habari kamili Ukurasa wa pili katika SEMA Usikike la leo [/SIZE]
Haitoi matamko kupitia kwmye simu za mkononi
Ikitoa tamko huita vyombo mbali mbali vya habari
Taarifa katika Tanzania Daima si tamko halali
Mwandishi alikurupuka bila kufuata utaratibu
Yeye wala si Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu
Taarifa zilizotolewa
Na Mwandishi Wetu, SEMA USIKIKE
Juni 8, 2009
TAARIFA zilizotolewa na mwandishi wa habari katika kitengo cha Mawasiliano Ikulu, Premy Kibanga, kuwa Ikulu imemuonya Mengi, si tamko la Ikulu bali ni mawazo yake mwenyewem SEMA Usikike limegundua.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari kutoka ndani ya kitengo hicho, zimesema kuwa kwa kawaida Ikulu ikitoa matamko huita vyombo vya habari vyote na kutoa taarifa zake kwa kufuata utaratibu uliowekwa jambo ambalo mwandishi huyu hakulifuata.
Vyanzo vyetu pia vimebainisha kuwa taarifa zilizoandikwa katika gazeti la Tanzania Daima zikimnukuu mwandishi wa Ikulu Premy Kibanga zinadaiwa kuwa hilo si tamko la Ikulu.
Katika sehemu ya tamko ambalo mwandishi huyo, Premy Kibanga alisema limetolewa na iIkulu linasema kuwa Bw Mengi ametakiwa aviheshimu vyombo vya dola na kwamba Ikulu imekanusha madai ya Mengi kuwa anaandamwa na baadhi ya viongozi wa kiserikali pamoja na taasisi zake.
Watu waliohojiwa na gazeti hili wanasema kama kweli mwandishi huyo aliongea na gazeti hilo, alifanya kosa kubwa ambalo halijawahi kufanywa na mwandishi yeyote wa kawaida aliyewahi kufanya kazi katika kitengo huicho cha mawasiliano.
Wamesema kuwa tokea enzi za Mwalimu, hakuna tamko la Ikulu lililowahi kutolewa kwa simu na kwa chombo kimoja kama ilivyotokea sasa, tena chombo binafsi. Kwa mfano, walisema, katika enzi za awamu ya kwanza, msemaji wa Ikulu alikuwa ni Katibu Mkuu Kiongozi Timothy Apiyo ambaye alitumia utaratibu wa kutoa taarifa kwa vyombo vya habari vyote ama kutoa tamko kupitia Idara ya Habari Maelezo ambayo ilikuwa ikisambaza habari hizi kwa wahariri wakuu.
Utaratibu ambao Rais wa awamu ya pili, Mzee Ruksa aliutumia kwa kumteua Balozi Patrick Chokala kuwa msemaji wa Ikulu, waandishi walikuwa wanaitwa pale Ikulu na kuongea na Chokala, kuuliza maswali kisha kurudi kuandika habari. Hata siku moja mtu huwezi kutoa tamko la Ikulu kupitia chombo kimoja cha habari tena si cha serikali. Tena mtu hyo akiwa siyo msemaji wa Rais.
Katika utawala wa awamu ya tatu, kama kawaida utaratibu wa kutoa matamko ya ofisi ya Rais ulifuatwa pia. Mheshimiwa Benjamin Mkapa naye akamteua Geoffrey Nkurlu naye akawa anatoa taarifa kwa vyombo vyote ya habari, na si kutoa tamko kupitia simu ya mkononi tena kwa jambo nyeti kama alivyofanya mwandishi huyu Premy Kibanga .
..Habari kamili Ukurasa wa pili katika SEMA Usikike la leo [/SIZE]