Nduka
JF-Expert Member
- Dec 3, 2008
- 8,552
- 2,359
Nasikitika sintoweza kuweka sehemu yote ya shairi hili kwa sababu za zilizo ndani ya uwezo wangu ukizingatia hali ya mijadala ya kisiasa na upepo dhoruba ndani ya CHADEMA. Enjoy!!
Ikiwa chungu tema Zitto.
Natanguliza salamu, kwako kamaradi Zitto,
Natumai utimamu, wewe na mama mtoto,
Kitabu na majukumu, si haba ni kazi nzito,
Donge ulilolimeza, likiwa chungu uteme.
Likiwa chungu uteme, nduguyo nakushauri,
Watakuvika utume, sifa na umashuhuri,
Vyote hivyo uvipime, visije kupa kiburi,
Donge walilokunywesha, likiwa chungu uteme
Taifa lakuhitaji, kupinga hao fisadi,
Wasikufanye mtaji, siasa kwao mradi,
Wakufunike theluji, kukukinga na baridi,
Ukishindwa kulimeza, donge chungu uliteme.
Na pia uwe makini, na hao zako rafiki,
Wa nje na pia kundini, wapo pia wanafiki,
Watakuja kurubuni, kwa mbinu za kifataki
Usije jilazimisha, donge chungu uliteme.
Kwa njaa na zao shida, taifa wameliuza,
Wamechokonoa donda, madini kuya maliza,
Wajifanya wakupenda, gutuka wanakuchuza,
Usijitwishe machungu, kama hauwezi tema.
Ikiwa chungu tema Zitto.
Natanguliza salamu, kwako kamaradi Zitto,
Natumai utimamu, wewe na mama mtoto,
Kitabu na majukumu, si haba ni kazi nzito,
Donge ulilolimeza, likiwa chungu uteme.
Likiwa chungu uteme, nduguyo nakushauri,
Watakuvika utume, sifa na umashuhuri,
Vyote hivyo uvipime, visije kupa kiburi,
Donge walilokunywesha, likiwa chungu uteme
Taifa lakuhitaji, kupinga hao fisadi,
Wasikufanye mtaji, siasa kwao mradi,
Wakufunike theluji, kukukinga na baridi,
Ukishindwa kulimeza, donge chungu uliteme.
Na pia uwe makini, na hao zako rafiki,
Wa nje na pia kundini, wapo pia wanafiki,
Watakuja kurubuni, kwa mbinu za kifataki
Usije jilazimisha, donge chungu uliteme.
Kwa njaa na zao shida, taifa wameliuza,
Wamechokonoa donda, madini kuya maliza,
Wajifanya wakupenda, gutuka wanakuchuza,
Usijitwishe machungu, kama hauwezi tema.