Ikiwa CDM inataka kushinda Arumeru...

Losambo

JF-Expert Member
Nov 8, 2011
2,613
864
Napenda niwakumbushe wanaCDM na wana Arumeru juu ya principle moja muhimu sana katika kuishinda CCM. Ikiwa CDM inataka kushinda Arumeru basi ihakikishe inashinda kwa tofauti ya kura nyingi. Uzoefu unaonyesha kuanzia uchaguzi 2010 majimbo yote yaliyokuwa na upinzani mkubwa na matokeo yake kuwa na tofauti ndogo CCM walitumia nafasi hiyo kujinufaisha. Unaweza kuona jinsi jimbo la Rukwa Mjini n.k

Tukiacha hapo rudi Igunga, karibu tofauti ilikuwa ni kura chache na alipokuja kutangaza matokeo Novatus Makunga ambayo ilionyesha CDM ipo nyuma kwa karibu kura 3000 ndiyo yaliyopelekea ushindi wa CCM.

Hivyo katika kuelekea uchaguzi huu wa Arumeru, ni bora viongozi, wanachama na mashabiki wa CDM wakalielewa ikiwa wanataka kuishinda CCM basi wahakikishe wanapiga kampeni nyumba hadi nyumba, kichwa kwa kichwa ili matokeo yakavyoanza kutoka tayari kuwe na tofauti kubwa hali itayowafanya wajiulize waanzie wapi kuchakachua. Ni kilio hiki cha uchakachuaji ambacho kinatumika kama kigezo cha kujitetea, kumbe wakati mwingine tunamkaribisha adui mlangoni bila sababu.

Mwisho, chama saizi kimekomaa ni lazima kijue fitna za siasa. Na bila ya shaka uchaguzi huu utatawaliwa na "irregularities" nyingi siyo kwa bahati mbaya lakini kwa makusudi kabisa ya kuzua vurugu ili ionekane vurugu ndiyo jadi ya CDM.

Moja ya technique kubwa itakutumika ni kuhakikisha P17 hazipo za kutosha na zikiwepo basi matumizi yake yanabaki mikononi mwa msimamizi ambaye anaweza kupima upepo na kuamua zisitumike.

Hitimisho ya yote hayo, ni kuhakikisha katika kipindi hiki cha lala salama viongozi, wanachama na mashabiki wanatoa hamasisho kwa rika zote kwenda kupiga kura na si kupiga kura tu bali kupiga kura ya kuing'oa CCM ambao ndiyo waliogawa ardhi yako kwa walowezi, walioshindwa kuwapa maji, walionyanyasa akina mama katika biashara zao ndogo ndogo n.k

I stand to be corrected,

Nawasilisha.
 
Yes mkuu I salute you. mimi naafikiana na wewe kaasilimia 100%, mimi nipo A mashariki kwakazi hiyo. natoa elimu ya uraia watu waelewe madhara ya sisiem nakwanini wanahitaji mtu m badala amaye ni joshua.
nawaelimisha iliwatapike sumu mbaya waliopewa kuwa cdm nichama cha vurugu. kwani wengi wao hawajui tafsiri ya rangi zilizo kwenye bendera.
Hakuna kulala , pamoja sana
 
Yes mkuu I salute you. mimi naafikiana na wewe kaasilimia 100%, mimi nipo A mashariki kwakazi hiyo. natoa elimu ya uraia watu waelewe madhara ya sisiem nakwanini wanahitaji mtu m badala amaye ni joshua.
nawaelimisha iliwatapike sumu mbaya waliopewa kuwa cdm nichama cha vurugu. kwani wengi wao hawajui tafsiri ya rangi zilizo kwenye bendera.
Hakuna kulala , pamoja sana

Tukifakiwa la kuwashawishi watu kupiga kura CDM basi kazi ya kulinda inakuwa nyepesi sana. Nadhani hapo ndipo pa kutilia mkazo.
 
Nadhani mtanisupport wanaJF wenzangu ikiwa CCM imediriki kuongeza vituo 55 hewa basi ni wazi kuishinda CCM kuna hitaji kazi ya ziada.

Yenyewe ina dola, tume zote zipo upande wao. CDM yenyewe inajitahidi kuringia nguvu ya umma ambayo haina hakina kama angalau 75% ina support kwa kumananisha.

Ni bora angalizo hili likafanyiwa kazi ipasavyo. Na katika vita kitu pekee ambacho ni muhimu kuliko vyote ni data. Pls katika kila tukio we need to ne reastic.
 
chadema itashinda kwa 28% pamoja na chopa..siyo mbaya sana..mtakuwa mmeongeza kura, mmetangaza chama, na zaidi mmefanya harambee kuchangisha ..good try..
 
Napenda niwakumbushe wanaCDM na wana Arumeru juu ya principle moja muhimu sana katika kuishinda CCM. Ikiwa CDM inataka kushinda Arumeru basi ihakikishe inashinda kwa tofauti ya kura nyingi. Uzoefu unaonyesha kuanzia uchaguzi 2010 majimbo yote yaliyokuwa na upinzani mkubwa na matokeo yake kuwa na tofauti ndogo CCM walitumia nafasi hiyo kujinufaisha. Unaweza kuona jinsi jimbo la Rukwa Mjini n.k

Tukiacha hapo rudi Igunga, karibu tofauti ilikuwa ni kura chache na alipokuja kutangaza matokeo Novatus Makunga ambayo ilionyesha CDM ipo nyuma kwa karibu kura 3000 ndiyo yaliyopelekea ushindi wa CCM.

Hivyo katika kuelekea uchaguzi huu wa Arumeru, ni bora viongozi, wanachama na mashabiki wa CDM wakalielewa ikiwa wanataka kuishinda CCM basi wahakikishe wanapiga kampeni nyumba hadi nyumba, kichwa kwa kichwa ili matokeo yakavyoanza kutoka tayari kuwe na tofauti kubwa hali itayowafanya wajiulize waanzie wapi kuchakachua. Ni kilio hiki cha uchakachuaji ambacho kinatumika kama kigezo cha kujitetea, kumbe wakati mwingine tunamkaribisha adui mlangoni bila sababu.

Mwisho, chama saizi kimekomaa ni lazima kijue fitna za siasa. Na bila ya shaka uchaguzi huu utatawaliwa na "irregularities" nyingi siyo kwa bahati mbaya lakini kwa makusudi kabisa ya kuzua vurugu ili ionekane vurugu ndiyo jadi ya CDM.

Moja ya technique kubwa itakutumika ni kuhakikisha P17 hazipo za kutosha na zikiwepo basi matumizi yake yanabaki mikononi mwa msimamizi ambaye anaweza kupima upepo na kuamua zisitumike.

Hitimisho ya yote hayo, ni kuhakikisha katika kipindi hiki cha lala salama viongozi, wanachama na mashabiki wanatoa hamasisho kwa rika zote kwenda kupiga kura na si kupiga kura tu bali kupiga kura ya kuing'oa CCM ambao ndiyo waliogawa ardhi yako kwa walowezi, walioshindwa kuwapa maji, walionyanyasa akina mama katika biashara zao ndogo ndogo n.k

I stand to be corrected,

Nawasilisha.

Mtaweweseka sana ! ila kuinamishwa ni lazima kwa cdm
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom