Ijue Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2010 - 2015

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
301
ILANI YA UCHAGUZI YA CCM YA MWAKA 2010 – 2015

UTANGULIZI
1. Katika Uchaguzi wa kushindanisha vyama vingi vya siasa ili kutwaa Dola na kuunda Serikali kila Chama hutarajiwa kuandaa Ilani ya Uchaguzi. Ilani hutafsiri na huelezea Sera za Chama kuhusu maeneo muhimu ya siasa, uchumi na jamii na hutoa maelezo fasaha kuhusu mikakati ya utekelezaji wa sera zinazonadiwa pindi wagombea wake wakifanikiwa kushinda.

Aidha hutoa ahadi kwa Wananchi kuhusu mambo ambayo Chama kitaelekeza na kusimamia Serikali kutekeleza. Kwa hiyo Ilani ya Uchaguzi ni Maelezo ya Sera katika kipindi husika, na inalenga kuwaeleza Wananchi ni mambo gani Chama kitafanya iwapo kitashinda Uchaguzi na kuunda Serikali. Ilani hii ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2010 hadi 2015 inalengo hilo hilo…………..

Hali ya Nchi yetu
Pamoja na mafanikio mengi tuliyopata na changamoto zilizojitokeza, tuna fursa kubwa ya kuendelea kujenga uchumi wa kisasa ili kumudu ushindani katika mazingira ya utandawazi na kuongeza tija kwa kasi zaidi…………

Pata
Ilani ya CCM 2005 - 2010 na
Ilani ya CCM 2010 - 2015........Attached below
 

Attachments

  • Ilani ya CCM 2010 - 2015.pdf
    629.3 KB · Views: 3,989
Mwandishi atakuwa hajui maana ya 15%... maana asilimia 15% ya 2005 haiwezi kuwa the same kama ya 2015... b'se hiyo asilimia ina-take base ya sasa. ... siasa bwana... I bet they won't meet that.... 15% is that huge....
 
Luteni, tunashukuru sana kwa Ilani. Maswali uliyouliza ni ya msingi. Lakini hiyo ilani tunayebahatika kuiona ni mimi na wewe, ambao yumkini wengi wetu hatupigi kura.

Wapiga kura kule vijijini hawapewi kabisa hiyo nafasi ya kuiona ilani ya uchaguzi. Na hata wakiiona, hawawezi kuchambua mambo kama haya.

Ndiyo maana siku zote huwa naamini kwamba CCM haitakaa iwakomboe watanzania kutoka katika dibwi la umaskini kwa kuwa umaskini na ujinga wa Watanzania ndiyo mtaji wa CCM kisiasa.
 
Hawa jamaa kwa kuahidi ni kiboko, yaani wangekuwa wanatekeleza hizi ilani zao tungekuwa mbali sana.
Kuna maeneo yanayonikera kwa kurudia rudia katika ilani zao zote bila kutekelezwa kila mwaka yanatajwa hivyo hivyo mfano:-
- kukamilisha maandalizi na kuanza ujenzi wa daraja la kigamboni
- kuanzia mabasi ya kasi dar es salaam (DART)
- kupanua mtandao wa barabara DSM
- Kuunganisha umeme wa grid ya Taifa Makambako - Songea
- kujenga daraja la mto kilombero

haya yamekuwa ni maneno tu katika ilani zote pasipo utekelezaji.

Jambo la pili hivi kweli tunauwezo wa kujenga international airports zote hizo kwa wakati mmoja?
JNIA (kujenga jengo jipya la abiria na majengo ya huduma) Songwe Mbeya (kukamilisha ujenzi), Bagamoyo (upembuzi), Msalato Modoma (kuanza ujenzi), Mwanza na Mtwara (ukarabati na ujenzi) na ukarabati wa viwanja Mafia, Arusha, Mpanda, Sumbawanga Bukoba, Kigoma, Tabora na Shinyanga.
Haya yote yanaweza kufanyika katika miaka mitano? kwanini tusitoe kibaumbele katika viwanja vichache na tukaanzisha shirika jipya la ndege? forget about ATCL
 
Hawa jamaa kwa kuahidi ni kiboko, yaani wangekuwa wanatekeleza hizi ilani zao tungekuwa mbali sana.
Kuna maeneo yanayonikera kwa kurudia rudia katika ilani zao zote bila kutekelezwa kila mwaka yanatajwa hivyo hivyo mfano:-
- kukamilisha maandalizi na kuanza ujenzi wa daraja la kigamboni
- kuanzia mabasi ya kasi dar es salaam (DART)
- kupanua mtandao wa barabara DSM
- Kuunganisha umeme wa grid ya Taifa Makambako - Songea
- kujenga daraja la mto kilombero

haya yamekuwa ni maneno tu katika ilani zote pasipo utekelezaji.

Jambo la pili hivi kweli tunauwezo wa kujenga international airports zote hizo kwa wakati mmoja?
JNIA (kujenga jengo jipya la abiria na majengo ya huduma) Songwe Mbeya (kukamilisha ujenzi), Bagamoyo (upembuzi), Msalato Modoma (kuanza ujenzi), Mwanza na Mtwara (ukarabati na ujenzi) na ukarabati wa viwanja Mafia, Arusha, Mpanda, Sumbawanga Bukoba, Kigoma, Tabora na Shinyanga.
Haya yote yanaweza kufanyika katika miaka mitano? kwanini tusitoe kibaumbele katika viwanja vichache na tukaanzisha shirika jipya la ndege? forget about ATCL
Unachosema Nemesis ni kweli kuna mambo mengi sana wamerudia au wamekopi Ilani zilizopita sijui huwa hawana muda wa kuandaa mpya wanakopi and paste tu.

Ukiipitia vizuri kuna kitu kimenifurahisha sana wanasema baadhi ya mafanikio ya Ilani iliyopinta ni pamoja na kuhamishia makao makuu ya Chama cha mapinduzi Dodoma. Sina uhakika kama kweli yametoka pale Lumumba, hata ikiwa kweli makao ya chama yanaingiaje hapo kinachotakiwa ni shughuli za serikali kuhamia Dodoma si chama.
 
Naomba kuwaomba wana JF tujitokeze kwa wingi 31 Oct 2010 tujibu hizi kejeli za CCM kwa kuchagua wabunge wa upinzani angalau wafikie 60% ya wabunge wote.

Nilikuwa nasikiliza wakati Pinda akieleza utekelezaji wa ilani iliyopita sikuamini aliyokuwa anasema. Nilijaribu kuwauliza watu wengine juu ya utekelezaji wa ahadi za 2005-2010 wote tukawa na maoni yale yale kuwa hawajafikia hata 40% ya malengo lakini wao wanajinadi ile mbaya na kwa maoni yao (CCM) wamefikia zaidi ya 95% ya malengo.
Kwa maana hiyo kama tunataka maendeleo lazima tubadilishe serikali, maoni yangu ni kwamba tufanye mabadiliko haya kwa awamu mbili ya kwanza iwe 2010 ambapo wabunge wengi wawe wa upinzani na 2015 rais atoke chama kingine, lakini siyo CCM.

Nawakilisha
 
Mwenye ya mwaka 2005 atuwekee hapa tuweze kuoanisha. Muda wa kuchezeana umekwisha!
 
Kupanua mafunzo ya VETA yaweze kuchukua vijana wengi zaidi
wanaofuzu elimu ya msingi ili waandaliwe kujiajiri wenyewe

Nikinukuu hapa lengo la kuwapeleka hawa sekondari limekwisha wanajichanganya wenyewe? Hizi bla bla tulikwisha choka nazo.
 
10. Kwa kutekeleza haya, Chama cha Mapinduzi kitakuwa kimeandaa mazingira ya kuondoa unyonge na shida zinazowasibu wananchi wake zinazotokana na umaskini na uchumi ulioduni. Aidha Ilani hii itakuwa kielelezo cha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Nne ya kuhakikisha kuwa inaitoa Tanzania kutoka uchumi ulio nyuma na tegemezi na kupambana na umaskini kwa hamasa, dhamira na kasi kubwa.

Naota, naota nadanganywa hooooo Mbaraka Mwishehe
 
Naomba kuwaomba wana JF tujitokeze kwa wingi 31 Oct 2010 tujibu hizi kejeli za CCM kwa kuchagua wabunge wa upinzani angalau wafikie 60% ya wabunge wote.

Nilikuwa nasikiliza wakati Pinda akieleza utekelezaji wa ilani iliyopita sikuamini aliyokuwa anasema. Nilijaribu kuwauliza watu wengine juu ya utekelezaji wa ahadi za 2005-2010 wote tukawa na maoni yale yale kuwa hawajafikia hata 40% ya malengo lakini wao wanajinadi ile mbaya na kwa maoni yao (CCM) wamefikia zaidi ya 95% ya malengo.
Kwa maana hiyo kama tunataka maendeleo lazima tubadilishe serikali, maoni yangu ni kwamba tufanye mabadiliko haya kwa awamu mbili ya kwanza iwe 2010 ambapo wabunge wengi wawe wa upinzani na 2015 rais atoke chama kingine, lakini siyo CCM.

Nawakilisha

Ni swali tuu la kijinga, mnapokataa kuwa hawakufikia 95% mnatumia vigezo gani? Mfano mimi binafsi ofisi yangu nimefungua January 2006, nina jumla ya wafanyakazi watano (5) hivyo katika ajira milioni moja(1,000,000) zitakuwa zimebakia 999,995; Jee mbali na ofisi yangu ni biashara ngapi mpya zimefunguliwa kati ya January 2006 hadi leo? Kwa nini lengo la ajira 1,000,000 lisiwe limefikiwa.

Ni mawazo yangu wala sipo kwenye politics, hata class monitor sijawahi kupata cheo hicho, sana sana kusimamia kanisani.
 
Nimefurahi sana kuwa mambo ya Sheria hayahusiani na dini yoyote bali hapa yanalengwa maslahi ya umma, maana Serikali haina dini!
Sekta ya Sheria
186. Katika kipindi cha utekelezaji wa Ilani hii ya 2010-2015, Chama kitaitaka Serikali
iendelee kuimarisha Sekta ya Sheria kwa kuchukua hatua zifuatazo:-
(a) Pamoja na kuipongeza Serikali ya Awamu ya Nne kwa kuteua Majaji wengi
wakiwemo Wanawake, jitihada hizo za Serikali ziendelee pamoja na kuona
kwamba Mahakama zote zinajengewa mazingira yatakayowawezesha
kutimiza majukumu yake kwa ufanisi.
(b) Kuhakikisha kuwa wanakuwepo pia wataalamu waliobobea katika Sheria
za Mikataba na kwamba wanatumika ipasavyo wakati Serikali inapoandaa
mikataba mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.
(c) Kuyatafutia ufumbuzi endelevu masuala ya mlundikano wa kesi
mahakamani na la msongamano wa wafungwa magerezani.
(d) Kupanua mafunzo ya Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo na kuwapangia
kazi ili utoaji wa haki katika ngazi za chini usicheleweshwe.
117
(e) Kuboresha posho za Wazee wa Mahakama na kuhakikisha kwamba
zinatolewa kwa wazee wote kwa wakati unaotakiwa.
(f) Kuzifanyia marekebisho sheria za mirathi na zile zinazoonekana
kuwakandamiza wanawake.
(g) Kuanzisha na Kutekeleza Mpango maalum wa kuanzisha Ofisi za
Mahakama Kuu katika kila Mkoa ili kusogeza huduma kwa wananchi.
(h) Kukamilisha Mchakato wa kutenganisha shughuli za upelelezi na
uendeshaji mashtaka.
(i) Kutekeleza Mpango wa Uboreshaji wa Mfuko wa Sheria hususan ujenzi wa
majengo ya Mahakama ya ngazi zote na kuajiri Majaji na Mahakimu wa
kutosha. Mfumo wa elektroniki katika kuendesha mashauri na kuhifadhi
nyaraka za mashauri utaanzishwa.
(j) Kuweka mfumo wa Kuwasaidia wananchi wasiojiweza kupata msaada wa
Kisheria.
(k) Kupeleka huduma za Mahakama karibu na wananchi ikiwa ni pamoja na
kujenga masjala ya Mahakama ya Biashara Dodoma.
(l) Kuendelea kuimarisha na kuongeza kasi ya usikilizaji wa migogoro ya
nyumba na Ardhi ili kuwezesha wananchi kuendelea na shughuli za
uchumi.
(m) Kuyawekea mfumo wa sheria maagizo mbalimbali ambayo hutolewa kama
amri halali na viongozi wakuu wa nchi yetu kuhusu maendeleo yetu ili
utekelezaji wa maagizo hayo upate nguvu ya sheria.
(n) Kuendelea kupunguza mlundikano wa mahabusu katika magereza.
 
Ni swali tuu la kijinga, mnapokataa kuwa hawakufikia 95% mnatumia vigezo gani? Mfano mimi binafsi ofisi yangu nimefungua January 2006, nina jumla ya wafanyakazi watano (5) hivyo katika ajira milioni moja(1,000,000) zitakuwa zimebakia 999,995; Jee mbali na ofisi yangu ni biashara ngapi mpya zimefunguliwa kati ya January 2006 hadi leo? Kwa nini lengo la ajira 1,000,000 lisiwe limefikiwa.

Ni mawazo yangu wala sipo kwenye politics, hata class monitor sijawahi kupata cheo hicho, sana sana kusimamia kanisani.

Hongera.

Kama hiyo 95% ndiyo imetufikisha hapa tulipo tuna kazi ya kufanya....

Niambie kitu kingine ambacho unadhani kimetekelezwa kwa zaidi ya 50% with hard reality siyo hizi bla blah za takwimu zisizo na mashiko
 
Naomba msaada wa Tafsri ya Katiba ya CCM Toleo la 2010: Sehemu ya Kwanza: Malengo ya Chama

12) Kuona kwamba Dola inakuwa Mhimili wa Uchumi wa Taifa.
 
Wakuu.... samahani kama hii mada imejadiliwa

NImeambiwa kwamba CCM wameondoa kigamboni bridge kwenye ilani yao!!! Je ni kweli? na kama ni kweli, hii ina maana gani kwa multibillion cosmopolitan City plan that is circulating around the country adn some potential investors community?

Na hii ina maana gani kwenye suala la ahadi na utekelezaji?

what about land grabbing ?
 
Mbezi (Morogoro road)-Malambamawili-Kinyerezi-Banana (Km
14.0); Ubungo Bus Termanial-Mabibo-Kigogo Round about (Km 6.4)

barabara hizi tayari iko kwenye ujenzi au hatua zaq mwisho kukamilika sasa sijui hii ilikuwa ilani ya 2005-2010 au 2010-2015 nilitegemea kuwe na bara bara zingine
 
Mbezi (Morogoro road)-Malambamawili-Kinyerezi-Banana (Km
14.0); Ubungo Bus Termanial-Mabibo-Kigogo Round about (Km 6.4)

barabara hizi tayari iko kwenye ujenzi au hatua zaq mwisho kukamilika sasa sijui hii ilikuwa ilani ya 2005-2010 au 2010-2015 nilitegemea kuwe na bara bara zingine

Kuanzisha mradi wa mabasi yaendayo kasi (DART).

huu mradi si ulishaanza zamani nachelea kusema kuwa watu hawafanyi kazi zaidi ya kukopy na paste
 
Kutenga kila mwaka kiasi kisichopungua asilimia 1.0 ya pato ghafi la Taifa
(GDP) kwa ajili ya Utafiti, Maendeleo na Maonyesho ya Matokeo ya Utafiti
(R,D&D).

nchi hii itaendeleaje kama hawajatoa kipaumbele kwenye Utafiti, Maendeleo na Maonyesho ya Matokeo ya Utafiti (R,D&D). sipati jibu baaado tutabaki nyuma <=1% kweliiiiiiiiiiii????????!!!!!!!!!???
 
Back
Top Bottom